bukoba boy
JF-Expert Member
- Jan 15, 2015
- 5,371
- 3,946
Phd na bado pocket money shida! Kweli elimu na pesa ni vitu vitatu tofauti
sisi wanafunzi wa kitanzania tunaosoma vyuo vikuu mbali mbali hapa ujerumani masomo ya Shahada ya Uzamivu kwa ufadhili wa wizara ya elimu, tunadhalilika kutokana na mfadhili (wizara ya elimu, TZ) kutokutulipa pesa ya kujikimu kwa muda wa miezi 4 sasa.
Huku tunadaiwa kodi za nyumba pamoja na pesa za chakula. kila tukifuatilia wizarani tunapigwa kalenda. Tunaishi kwa taabu na kukopa kopa maana hapa ngumu kupata vibarua ukiwa mwanafunzi. kwa kweli hata wenye nyumba wametishia kutufukuza kwenye nyumba kwa kulimbikiza kodi muda mrefu inafikia hatua mtu unakosa nauli ya kutoka nyumbani kwenda chuoni. wizara ya elimu liangalien hili suala kwa jicho la 3
Phd na bado pocket money shida! Kweli elimu na pesa ni vitu vitatu tofauti