Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Jiji la Dar es Salaam limetajwa katika orodha ya majiji 20 hatari zaidi duniani kwa wageni kutembelea. Ripoti ya utafiti uliofanywa na shirika la WITNESS la nchini Marekani
(2017/18) inatahadharisha wageni wanaotaka kutembelea Tanzania (kibiashara au kwa shughuli za Utalii) wahakikishe hawafiki Dar es Salaam.
Dar imeingia kwa mara ya kwanza ktk orodha hiyo (ya majiji yasiyofaa kutembelewa), huku jiji la Aleppo (Syria) likishikilia nafasi ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo. Baadhi ya vigezo vilivyoiweka Dar kwenye orodha hiyo ni pamoja na matukio ya utekaji, watu kupotea, polisi kutumia nguvu kupita kiasi, kuminywa kwa demokrasia na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Kutekwa kwa Mo Dewji, mwandishi Azory Gwanda, kupotea kwa Ben Saanane, Polisi kumuua Aquilina bila hatia, na miili ya watu kuokotwa hovyo ufukweni mwa bahari ni miongoni mwa matukio yaliyotumika kwenye ripoti hiyo. Tukio jingine ni la kuvamiwa kwa afisa ubalozi wa Syria (H. Alfaouri) kupigwa na kuporwa zaidi ya Euro 93,000.
_
Ripoti hiyo inaeleza kuwa magenge ya watu wanaotenda uhalifu huo (kuteka raia, kupora, kupoteza) huenda yanalindwa na dola ndio maana licha ya matukio hayo kushamiri hakuna hatua za maana zilizochukuliwa.
Ripoti hiyo imependekeza wasafiri wanaounganisha ndege kupitia uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (Dar) kutafuta njia mbadal ili kuepuka kuhatarisha maisha yao.
Orodha kamili ya majiji 20 hatari zaidi kutembelea duniani ni:
1. Aleppo (Syria)
2. Kabul (Afghanistan)
3. Juba (South Sudan)
4. Cape town (South Africa)
5. Sanaa (Yemen)
6. Mexico city (Mexico)
7. Kinshasha (DRC)
8. Pyonyang (North Korea)
9. Khartoum (Sudan)
10. Acapulco (Mexico)
11. Islamabad (Pakistan)
12. Baghdad (Iraq)
13. Bogota (Colombia)
14. Bujumbura (Burundi)
15. Karachi (Pakistan)
16. Bangui (Central Africa Republic)
17. San Pedro (Honduras)
18. Tripoli (Libya)
19. Dhaka (Bangladesh)
20. Dar es Salaam (Tanzania)
(2017/18) inatahadharisha wageni wanaotaka kutembelea Tanzania (kibiashara au kwa shughuli za Utalii) wahakikishe hawafiki Dar es Salaam.
Dar imeingia kwa mara ya kwanza ktk orodha hiyo (ya majiji yasiyofaa kutembelewa), huku jiji la Aleppo (Syria) likishikilia nafasi ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo. Baadhi ya vigezo vilivyoiweka Dar kwenye orodha hiyo ni pamoja na matukio ya utekaji, watu kupotea, polisi kutumia nguvu kupita kiasi, kuminywa kwa demokrasia na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Kutekwa kwa Mo Dewji, mwandishi Azory Gwanda, kupotea kwa Ben Saanane, Polisi kumuua Aquilina bila hatia, na miili ya watu kuokotwa hovyo ufukweni mwa bahari ni miongoni mwa matukio yaliyotumika kwenye ripoti hiyo. Tukio jingine ni la kuvamiwa kwa afisa ubalozi wa Syria (H. Alfaouri) kupigwa na kuporwa zaidi ya Euro 93,000.
_
Ripoti hiyo inaeleza kuwa magenge ya watu wanaotenda uhalifu huo (kuteka raia, kupora, kupoteza) huenda yanalindwa na dola ndio maana licha ya matukio hayo kushamiri hakuna hatua za maana zilizochukuliwa.
Ripoti hiyo imependekeza wasafiri wanaounganisha ndege kupitia uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (Dar) kutafuta njia mbadal ili kuepuka kuhatarisha maisha yao.
Orodha kamili ya majiji 20 hatari zaidi kutembelea duniani ni:
1. Aleppo (Syria)
2. Kabul (Afghanistan)
3. Juba (South Sudan)
4. Cape town (South Africa)
5. Sanaa (Yemen)
6. Mexico city (Mexico)
7. Kinshasha (DRC)
8. Pyonyang (North Korea)
9. Khartoum (Sudan)
10. Acapulco (Mexico)
11. Islamabad (Pakistan)
12. Baghdad (Iraq)
13. Bogota (Colombia)
14. Bujumbura (Burundi)
15. Karachi (Pakistan)
16. Bangui (Central Africa Republic)
17. San Pedro (Honduras)
18. Tripoli (Libya)
19. Dhaka (Bangladesh)
20. Dar es Salaam (Tanzania)