Tuna uhakika juu ya jambo moja kuhusu kukamatwa kwa viongozi wa Upinzani mara kwa mara. Huenda mabadiliko chanya yako karibu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1593181610463.png
Kumekuwa na matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi wa upinzani kwa kipindi kirefu kidogo. Ijapokuwa kuna mazingira tofauti tofauti yanayotawala matukio hayo, angalau sasa tuna uhakika wa jambo moja muhimu.

Utaratibu wa kuwakamata viongozi hao unaonekana kutokuwa na faida kwa CCM, hauna faida kwa viongozi wanaokamatwa, hauna faida kwa viongozi ambao hawajakamatwa, hauna faida kwa viongozi wa upinzani, hauna faida kwa wananchi na hauna faida kwa taifa kwa ujumla.

Sana sana una mfululizo wa madhara ya hatari ambayo katika hatua fulani yanaweza kumuangukia yoyote. Yaani unazalisha tatizo kama ugonjwa wa kuambukiza ambapo haifahamiki atakayeambukizwa ni nani na mwisho wake ni nini. Nitataja madhara yake kwa uchache kwa minajili ya kufanya hoja yangu iwe na nguvu.

Kwanza, Kwa upande wa wanaokamatwa mara kwa mara wanakuwa na hisia za kudhulumiwa. Hisia hizo zikijenga mizizi, watu hao wanaandaliwa kuwa watu wabaya na hatari. Wanaandaliwa kuwa watu wa visasi, roho mbaya na dhuluma na haifahamiki madhara yatakayotokana na kujenga tabia hizo yatakuwa ni ya kiasi gani na kwa nani. Je! kama nchi, hii ndio aina ya watu ambao tungependa kuzalisha? Ikumbuke tabia ya binadamu (njema au mbaya ) hujengwa na mambo anayopitia “Experience”. Kwa maoni yangu, uamuzi wa kuamua kuzalisha watu kama hawa ni hatari kwetu sote kama taifa, hivyo ni vizuri kulitizama kwa umakini jambo hili.

Pili, Kwa upande wa vyama vya upinzani ambao kwa maoni yangu hawana hoja za maana kwenye mambo mengi, wanapata hoja ya bwerere, “Unaona sisi tunavyoonewa?” kwa hiyo wanavutia huruma badala ya kuegemea kwenye mambo ya msingi ‘Appeal for sympathy”, kwa hiyo matukio hayo yanatengeneza shida ambayo haikuwa na ulazima.

Tatu, Kwa upande wa CCM, wanapata madhara makubwa ya aina mbili. Kwanza kwa wapenzi wa CCM wanapata wakati mgumu kidogo kukitetea chama kwa hoja kwa sababu ya swali moja tu “kama mna hoja, kwa nini mnawakamata wapinzani badala ya kuwashughulikia kwa hoja?”Nje ya swali hilo, CCM wana mengi mazuri sana ya kujivunia. Pili, hali hiyo inaweza kuwapa wana CCM shida ya ndani ya kisaikolojia na kuwapelekea kupunguza kiwango cha kujiamini katika ujengaji hoja na kuzisimamia.

Nne, kwa upande wa jamii matukio ya namna hiyo yanasababisha taharuki isiyo lazima kwa jamii. Na ,

Tano, matukio ya namna hiyo huivuta jamii ya kimataifa kutuangalia kwa jicho lisilopendeza. Ikumbukwe, hata kama tuko vizuri kiasi gani, kwa kadiri tunavyokuwa na uhusiano mzuri zaidi na kuaminika kwenye jumuia za kimataifa ndivyo tunavyoweka mazingira ya kufanikiwa zaidi na kinyume chake tunajiweka kwenye changamoto ambazo pengine zingeepukika.

Kwa mantiki hiyo basi, nashauri yafuatayo;-

Kwanza, Pamoja na matatizo yote waliyonayo viongozi wa upinzani, bado ni watu, ni watanzania na binadamu huwa wana matatizo mbalimbali na tunapoamua kuwa viongozi, maana yake tunakuwa tumeamua kuongoza watu wenye matatizo. Kwa hiyo ni muhimu kuwa na namna bora ya kujadiliana na kwekeana misingi kwenye mambo muhimu.

Pili, ikiwa viongozi wa vyama vya upinzani wanaokamatwa wanakuwa wanakosea mahali fulani; basi vyama husika vikutane vikubaliane juu ya utaratibu unaokubalika kwa wote na utaratibu huo uwe wazi, ili anayeuvunja kila mtu aone. Hili ni la maana zaidi na lina faida kwa watu wote ikiwemo CCM na vyama mbadala.

Tatu, ikiwa wanaokamatwa wanakuwa hawajavunja utaratibu, basi ni bora utaratibu huo ukafikiriwa upya kwa kuwa ni wazi kwamba una hasara nyingi kuliko faida, na hasara hizo katika hatua flani zinaweza kuathiri aliyekuwemo na asiyekuwemo. na,

Mwisho,Kwa mazingira ya Tanzania, CCM bado imevizidi vyama vingine kwenye mambo mbalimbali tena kwa mbali sana. CCM imefanya mambo mengi mazuri, kwa hiyo inaweza kujitangaza kwa mambo hayo na kueleweka. CCM ina rasilimali watu ya kutosha; inaweza kujibu hoja zote za vyama mbadala kiraia.

CCM ina karibu nguvu zote za msingi ili kujenga ushawishi na kukubalika kisiasa kwa mbinu za kiraia; kwa hiyo inaweza kushida kwenye uchaguzi huru na haki. Kwa hiyo ni vizuri kuhakikisha uwanja sawa wa kisiasa na kisha hawa jamaa tukawakabili kwa hoja ambazo kimsingi tunazo. Hiyo itakuwa na faida kwa Taifa, kwa CCM kwa vyama mbadala na kwa kila raia.

Ndugu zangu, tunapotathmini jambo na kubaini kuwa halina faida kwa yoyote, bila shaka si busara sana kuliendeleza, au ni nani anayedhani ipo haja ya kuendeleza jambo lisilomsaidia yeye mwenyewe wala kumsaidia yeyote? vinginevyo labda ajitokeze mtu na kuthibitisha kwamba yeye linamsaidia. Kama sivyo, ni vyema kuangalia njia bora zaidi ya kufanya siasa kwa maslahi ya wote na Taifa kwa ujumla, kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeamua kwa busara na hatutajuta kwa uamuzi huo.
 
Wote mlioelewa tunawashukuru sana kwa kuelewa na tunawatakia kila la heri kwenye kufanya uamuzi sahihi.
 
Peleka lumumba huko ndo kuna vichwa vigumu hawaelewi haya
Misingi ya kidemokrasia inataka kuwavumilia na kuwaelimisha watu wa jamii yako maana wakati mwingine hata wewe mwenyewe unakuwa hupendi kuwa ulivyo, ni changamoto tu .
 
Hoja yako kwa kiwango kikubwa sio mbaya, ila inakwepa ukweli mchungu. Kimsingi CCM ina hoja fulani fulani, lakini sio kweli kuwa ina hoja zinazoweza kuifanya ishinde, iwapo itashindana kwenye uwanja ulio sawa.

Ifahamike CCM sio chama cha kizazi hiki, bali ni chama cha kizazi kilichopita. Hivyo wafanyacho CCM sasa hivi ni kutumia shuruti kubaki madarakani, kisha hizo unazoita hoja, ndio wanazitumia kuhalalisha uwepo wao madarakani. Na iwapo ccm itafuata huu ushauri wako bila kutumia vyombo vya dola kwa namna hasi, basi ndio itakuwa mwisho wake.

Na ukweli ulio wazi japo unakwepa kuusema, CCM sio chama cha siasa tena, bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa. Na CCM ukiitazama kwa undani wake, hakiongozwi tena kwa itakadi, bali huendeshwa kwa tabia na utashi binafsi wa mwenyekiti wake, ambaye kimazoea huwa ndio rais wa nchi.

Linganisha enzi za JK, na sasa Magufuli. Magufuli ni mkomunisti, na ni mtu anayeamini kwenye matumizi ya nguvu na kujenga hofu ili kukubalika, kuliko kushawishi na kuheshimu demokrasia/box la kura. Hii ccm ya sasa hivi, inafuata tabia binafsi za mwenyekiti wake kwa kuwa ni rais, ndio hapo unapoona matumizi ya nguvu, shuruti, kutoheshimu box la kura na uchafu mwingine kama huo.
 
Mambo mazuri unayodhani CCM wanaweza kupeleka kwa wananchi halafu wakubalike watasema tumejenga... tumejenga... tumejenga... wananchi watawauliza kwani mmejenga kwa pesa zenu? hilo ni jukumu lenu, kama mnataka kusifiwa kwa kutimiza wajibu wenu sio karne hii.

Suala la msingi kama ajira hapa CCM na serikali yake ndio ina prove failure every year, kila mwaka tatizo linazidi kuwa kubwa zaidi, msijitetee tatizo la ukosefu wa ajira ni la dunia nzima, basi atleast tuonesheni mipango yenu ya angalau kupunguza tatizo tuone kama inaeleweka, but hakuna, ni kelele tu.

Mnatudanganya mmejenga viwanda lakini mpaka leo tunaona bidhaa hasa matunda vikiharibika mashambani kwa kukosa viwanda vya usindikaji, mnajiita serikali ya viwanda, but hivyo viwanda hata havionekani, vilivyopo ni viwanda vile vile vya miaka yote.

Upande wa pili wataulizwa mbona wapinzani wanaonewa na vyombo vya dola, mfano wa hivi karibuni kauli ya Dr. Bashiru aliejitapa wanajua kuitumia dola kubaki madarakani hapo sijui watajibu nini?!

Maendeleo mliyotuletea kwa muda wote mlioko madarakani hayafanani na hali halisi ambavyo ingetakiwa kuwa, asilimia kubwa ya sera zenu mbovu zimelisababishia hili taifa makovu yatakayochukua muda mrefu sana kufutika, mf. sekta ya madini, kuna maeneo kumebaki mashimo tu madini yamemalizwa na mzungu na jamii inayoizunguka hayo maeneo ya uchimbaji bado imetawaliwa na umasikini wa kutisha, nyie mlishachukua 10% yenu.

Kwa ufupi, hoja zozote ambazo CCM watazileta zitajibiwa kwa urahisi sana, tofauti na mwandishi ulivyoandika hapa, lakini hoja za upande wa pili (upinzani) hazijibiki, na ole wenu CCM wajaribu kuwaambia polisi waache kuingilia mambo ya kwenye siasa, huo ndio utakuwa mwisho wenu, bahati yenu mnalijua hili ndio maana hamtaki kujaribu.
 
Mambo mazuri unayodhani CCM wanaweza kupeleka kwa wananchi halafu wakubalike watasema tumejenga... tumejenga... tumejenga... wananchi watawauliza kwani mmejenga kwa pesa zenu? hilo ni jukumu lenu, kama mnataka kusifiwa kwa kutimiza wajibu wenu sio karne hii.
Lakini mkuu kwani kwa kawaida chama si kinapaswa kutimiza wajibu wake? au ! na kama kinapaswa kutimiza wajibu, sasa kinapotimiza, kikisema kimetimiza wajibu, hilo ni kosa tena? wakati fulani tuwe wakweli na waaminifu pale penye ukweli na haki tuseme ili pia tukisema penye shida iwe rahisi kueleweka.

Hata wewe ukiwa na mtu ambaye kila unachofanya lazima akiponde hata kama ni sahihi, huwezi kumwamini mtu huyo hata pale anaposema kitu sahihi, na hili ndio hutokea kwa upinzani wa Tanzania. Mtu anayekuponda kwa kila kitu huyo ni tatizo, na hata ikitokea siku akishauri au kuponda kwenye jambo la msingi, hata kama ni mimi siwezi kumtilia manani; sio kwa sababu ya uzuri au ubaya wa anachosema bali nitahofia dhamira
 
Lakini mkuu kwani kwa kawaida chama si kinapaswa kutimiza wajibu wake? au ! na kama kinapaswa kutimiza wajibu, sasa kinapotimiza, kikisema kimetimiza wajibu, hilo ni kosa tena? wakati fulani tuwe wakweli na waaminifu pale penye ukweli na haki tuseme ili pia tukisema penye shida iwe rahisi kueleweka.

Hata wewe ukiwa na mtu ambaye kila unachofanya lazima akiponde hata kama ni sahihi, huwezi kumwamini mtu huyo hata pale anaposema kitu sahihi, na hili ndio hutokea kwa upinzani wa Tanzania. Mtu anayekuponda kwa kila kitu huyo ni tatizo, na hata ikitokea siku akishauri au kuponda kwenye jambo la msingi, hata kama ni mimi siwezi kumtilia manani; sio kwa sababu ya uzuri au ubaya wa anachosema bali nitahofia dhamira
Asante.

Kama nyie mnataka kusifiwa kwa kutimiza wajibu wenu, basi nanyi muwe tayari kuwasifia wapinzani ambao kimsingi ndio wanaowasukuma nyie kutimiza huo wajibu wenu, hapo tutaenda sawa. Lakini tusilazimishane kufanya mnachotaka nyie, haya mambo ni sawa na mbio usijisifu unajua kukimbia, msifu na aliekukimbiza, bila yeye usingejua kama unajua kukimbia.
 
Suala la msingi kama ajira hapa CCM na serikali yake ndio ina prove failure every year,
Kuhusu suala la ajira kwa mfano, mtizamo na sera ya ajira ya CCM ikoje na ya vyama vingine ikoje, na ubara wa sera ya vyama vingine kwenye hili la ajira ukoje? usikimbie tafadhali.

Kumbukumbu zangu zinaonesha tushawahi kuleta mijadala kadhaa humu kuhusu hili suala la ajira na hapo wanaoiponda CCM hawakuwa na solution zaidi ya kulalamika tu. Ukitaka naweza kukumbusha mijadala hiyo, halafu utuoneshe suluhu ya vyama mbadala kwenye hilo la ajira.
 
Asante.

Kama nyie mnataka kusifiwa kwa kutimiza wajibu wenu,
Narudia tena, ukitaka watu wawe waaminifu kwako, unapaswa kuwa mwaminifu kwanza, hii ni principle. Kulipuuza hili ni moja ya kitu kinachopoteza kabisa credibility ya vyama vya upinzani Tanzania. Hauwezi kwa mfano kusema eti mazuri ambayo CCM imefanya haistahili kupongezwa kwayo au kuomba kuungwa mkono kwayo kwa sababu ni wajibu wao, as if hawakutakiwa wafanye wajibu wao.

Sasa kama hawakutakiwa wafanye wajubu wao walitakiwa wafanye nini? kujenga hoja kama hiyo inaonesha kabisa kwamba ni hoja inayosimama juu ya msingi wa hila na kama hivyo ndivyo, inaharibu reputation ya hoja zingine zote, sio kwa sababu ya uzuri au ubaya wa hoja hizo, bali kwa sababu ya dhamira ya mleta hoja.

Kuna mada tulishawahi kuleta humu, kwamba moja ya tatizo linalosababisha demokrasia na vyama vingi iwe janga Tanzania badala ya kuwa neema ni unafiki. Yaani kila mtu kujifanya kwamba kile kinachomsaidia yeye na kundi lake ndio haki na kinyume chake. Mambo mengi tunayoona leo ni matokeo ya tabia hii ya kihuni, na tusipoiacha tutegemee mbegu itazalisha yatokanayo zaidi na zaidi.

Kwa lugha ningine; kama wewe mwenyewe mhuni, ukifanyiwa uhuni ni sawa, sio kwa sababu uhuni ni jambo zuri bali kwa kuwa ndio mchezo uliochagua. Sasa tatizo unakuta kila mmoja anataka afanyie wengine uhuni ila yeye afanyiwe fair.
 
Kuhusu suala la ajira kwa mfano, mtizamo na sera ya ajira ya CCM ikoje na ya vyama vingine ikoje, na ubara wa sera ya vyama vingine kwenye hili la ajira ukoje? usikimbie tafadhali.

Kumbukumbu zangu zinaonesha tushawahi kuleta mijadala kadhaa humu kuhusu hili suala la ajira na hapo wanaoiponda CCM hawakuwa na solution zaidi ya kulalamika tu. Ukitaka naweza kukumbusha mijadala hiyo, halafu utuoneshe suluhu ya vyama mbadala kwenye hilo la ajira.
Mkuu unataka kusema hujawahi kuona mipango ya upinzani kuhusu hilo suala la ajira, CCM si ndo huwa mnaiba ilani za wapinzani wakati wa uchaguzi, au kama unataka kuona implementation ya wapinzani kwenye suala la ajira kwani wao ndio wenye serikali? au unataka wakafanyie wapi vitendo vyao muone kama nyie bado mnalazimisha kuiba kura?

Suala la demokrasia ya vyama vingi iwe janga Tanzania, hata CCM kwa upande wao wamechangia kwa kiasi kikubwa sana, hamkuwa tayari toka mwanzo kuupokea huu mfumo, ni kama mlilazimishwa na Nyerere, ndio maana mmekuwa mkiwafanyia wapinzani vitimbi kama sio watanzania wenzenu, ubinafsi wenu uliopitiliza ndio unaosababisha huo unaoita unafiki.

Sikukimbii Aziz kuwa na amani, niko hapa vizuri tu.
 
Narudia tena, ukitaka watu wawe waaminifu kwako, unapaswa kuwa mwaminifu kwanza, hii ni principle. Kulipuuza hili ni moja ya kitu kinachopoteza kabisa credibility ya vyama vya upinzani Tanzania. Hauwezi kwa mfano kusema eti mazuri ambayo CCM imefanya haistahili kupongezwa kwayo au kuomba kuungwa mkono kwayo kwa sababu ni wajibu wao, as if hawakutakiwa wafanye wajibu wao...
Nakuelewa vizuri sana Aziz, relax.

Hebu niambie, hivi kati ya anaekwambia fanya hivi na wewe unaefanya kitendo, ni nani alieanza? tatizo lenu mnatumia hilo suala la kusifiwa na upinzani kama mtaji wa kisiasa, ndio maana mkiambiwa mbona nyie hamuwasifii wanaowasukuma kufanya mnachofanya hamtaki kujibu, mnalalamika tu wapinzani hawana shukrani, hivi nyie mnayo kwa muktadha huo?!
 
Mkuu unataka kusema hujawahi kuona mipango ya upinzani kuhusu hilo suala la ajira, CCM si ndo huwa mnaiba ilani za wapinzani wakati wa uchaguzi, au kama unataka kuona implementation ya wapinzani kwenye suala la ajira kwani wao ndio wenye serikali?
Sasa kama CCM imeona ilani ya upinzani ni nzuri na ikaifanyia kazi, hilo ni jambo zuri au baya? sio kwamba chama kizuri ni kile kinachofanyia kazi ilani yake na kuchukua mawazo mazuri pia kutoka kwenye vyama vingine? au wewe ulitaka CCM isichukue mawazo ya wengine hata kama ni mazuri?

Haya unasema CCM imeiba ilani za vyama vya upinzani kuhusu ajira, hapo hapo unasema CCM imeshindwa kwenye kuzalisha ajira, sasa huoni unatuambia ilani za vyama vya upinzani zimeshindwa kuzalisha ajira? huoni hiyo ni contradiction ya wazi kabisa?
 
Sasa kama CCM imeona ilani ya upinzani ni nzuri na ikaifanyia kazi, hilo ni jambo zuri au baya? sio kwamba chama kizuri ni kile kinachofanyia kazi ilani yake na kuchukua mawazo mazuri pia kutoka kwenye vyama vingine? au wewe ulitaka CCM isichukue mawazo ya wengine hata kama ni mazuri?

Haya unasema CCM imeiba ilani za vyama vya upinzani kuhusu ajira, hapo hapo unasema CCM imeshindwa kwenye kuzalisha ajira, sasa huoni unatuambia ilani za vyama vya upinzani zimeshindwa kuzalisha ajira? huoni hiyo ni contradiction ya wazi kabisa?
Hapo kwenye kuchukua ilani ya upinzani nilikuwa nakuonesha kwamba hata wapinzani huwa wanazo tofauti na ulivyosema kule juu, suala la kuchukua kizuri cha mwenzio sina tatizo nalo.

Kuhusu kinachofuatia baada ya nyie kuiba ilani, huwa mnashindwa kwenye implementation, sababu mnakuwa mmedandia kitu msichokijua mbele wala nyuma, ndio maana mnafeli kwenye utelekezaji, mfano elimu bure mliiba idea bila kujua how to perform mkafeli, wangekuwa wapinzani wanatekeleza mngefurahi wenyewe.
 
Nakuelewa vizuri sana Aziz, relax.

Hebu niambie, hivi kati ya anaekwambia fanya hivi na wewe unaefanya kitendo, ni nani alieanza? tatizo lenu mnatumia hilo suala la kusifiwa na upinzani kama mtaji wa kisiasa, ndio maana mkiambiwa mbona nyie hamuwasifii wanaowasukuma kufanya mnachofanya hamtaki kujibu, mnalalamika tu wapinzani hawana shukrani, hivi nyie mnayo kwa muktadha huo?!
Kwa mfano, unataka kusifiwa kwenye nini? hebu kuwa specific. Halafu mimi ninachosema hapa sio kusifiwa. Ninachosema ni kwamba mtu anapofanya kitu sahihi ni vyema ku appreciate ili anapokosoa uki criticise inakuwa na mantiki. Hiyo ndio hoja yangu, kabla hujasema mbona nyie! unatakiwa kwanza uelewe hoja. Binafsi naamini constructive criticism ndio kitu muhimu kinachomjenga mtu au taasisi kuliko kitu kingine chochote, lakini sio kila ukosoaji unalenga kujenga, mwingne unalenga kukatisha tamaa, mwingine kuudhi, mwinge kudhalilisha n.k. sasa suala ni kujua kipi ni kipi.

Kuhusu ni nani wa kwanza, kwenye mambo ya msingi kuwa wakwanza inasaidia nini? Ndio maana kuna kiongozi wa chama kimoja kila siku anakazana kuwa wakwanza kuripoti vitu mtandaoni kabla havijathibitishwa, mwishowe inabainika ni fake news, akishauriwa asifanye hivyo anadai kwenye chama chake hakuna protocol. Kwa hiyo ishu sio wa kwanza, ishu nini ni muhimu nini si muhimu, nini ni sahihi na nini si sahihi.
 
CCM imeshaishiwa ushawishi na mbinu za kutawala na walitakiwa kupumzishwa kwa muda mrefu!

Lakini kwa mtiririko wa matukio na matendo ya wanasiasa wa upinzani kunaonyesha kuwa utayari wao upo chini na hawajui wala kutambua ukubwa wa jukumu wanalopigania, hali hiyo imewajengea hofu wapiga kura juu ya mustakabali wa taifa hili kwenye mikono ya wapinzani!

Wapo waliozibaka katiba za vyama vyao ili waendelee kuwa wenyeviti wa kudumu!

Wapo wanaokinzana wenyewe kwa wenyewe na kuleta mivurugano ndani vyama vyao kwa uroho wa madaraka madogo ya chama!

Wapo wenye kashfa za kugawa nafasi za upendeleo kwa ndugu zao au vimada wao!

Hayo ni uchache wa matukio yanaoendelea kwenye vyama ambavyo vinapigania kuipumzisha CCM,

Kama wanashindwa kusimamia itikadi na misingi ya vyama vyao watawezaje kusimamia misingi na itikadi ya taifa hili ambalo limeshaliwa na kuoza na funza CCM!?

WATANZANIA WAPO NJIA PANDA NA HAKUNA WA KUWATOA NJIA PANDA KWA MIAKA YA HIVI KARIBUNI!
 
Kwa mfano, unataka kusifiwa kwenye nini? hebu kuwa specific. Halafu mimi ninachosema hapa sio kusifiwa. Ninachosema ni kwamba mtu anapofanya kitu sahihi ni vyema ku appreciate ili anapokosoa uki criticise inakuwa na mantiki. Hiyo ndio hoja yangu, kabla hujasema mbona nyie! unatakiwa kwanza uelewe hoja. Binafsi naamini constructive criticism ndio kitu muhimu kinachomjenga mtu au taasisi kuliko kitu kingine chochote, lakini sio kila ukosoaji unalenga kujenga, mwingne unalenga kukatisha tamaa, mwingine kuudhi, mwinge kudhalilisha n.k. sasa suala ni kujua kipi ni kipi.

Kuhusu ni nani wa kwanza, kwenye mambo ya msingi kuwa wakwanza inasaidia nini? Ndio maana kuna kiongozi wa chama kimoja kila siku anakazana kuwa wakwanza kuripoti vitu mtandaoni kabla havijathibitishwa, mwishowe inabainika ni fake news, akishauriwa asifanye hivyo anadai kwenye chama chake hakuna protocol. Kwa hiyo ishu sio wa kwanza, ishu nini ni muhimu nini si muhimu, nini ni sahihi na nini si sahihi.
Mambo mazuri ya wapinzani yapo mengi tu, kule bungeni kuna hoja nyingi tu za wapinzani huwa mnazikataa kwa sababu ya viburi vyenu vinavyochangiwa na wingi wenu mnaoutumia vibaya mkiongozwa na Spika wenu.

Halafu huwezi wewe kuwa ndio unaefanya kizuri kila siku usione zuri la jirani yako hata mara moja, mpinzani hana platform ya kutenda, yeye ni wakuongea zaidi, hivyo mnatakiwa kumpongeza kwa mawazo yake mazuri anayowapa kama serikali, sio kuzomea tu kisa kaongea mpinzani.
 
mnakuwa mmedandia kitu msichokijua mbele wala nyuma, ndio maana mnafeli kwenye utelekezaji, mfano elimu bure mliiba idea bila kujua how to perform mkafeli, wangekuwa wapinzani wanatekeleza mngefurahi wenyewe.
Hivi wewe kwa uelewa wako, unaamini kabisa kwamba kwa mfano mtu 'A' akaandika mahali 'nitatoa elimu bure' mtu B akisoma hapo haelewi? kwa hiyo unataka kusema Waitara anaelewa zaidi sera ya elimu bila kuchangia kuliko Jaffo? Kwenye hili hoja yako ni dhaifu sana.

Unasema elimu bure imefeli, unapimaje kufeli?na kama imefeli na unasema ni sera ya vyama mbadala sasa unataka kutuambia nini? unasema ingekuwa upinzani ungefurahi, sasa wewe unatumia kigezo gani kujua wao wangefanya vizuri kuliko inavyofanyika sasa! hebu toa viashiria. Nikuulize swali dogo tu, watu waliopewa nafasi za uongozi kutoka vyama vya upinzani CHADEMA mathalan, wanafanya vizuri kuliko wale waliopo CCM siku zote?
 
Hivi wewe kwa uelewa wako, unaamini kabisa kwamba kwa mfano mtu 'A' akaandika mahali 'nitatoa elimu bure' mtu B akisoma hapo haelewi? kwa hiyo unataka kusema Waitara anaelewa zaidi sera ya elimu bila kuchangia kuliko Jaffo? Kwenye hili hoja yako ni dhaifu sana.

Unasema elimu bure imefeli, unapimaje kufeli?na kama imefeli na unasema ni sera ya vyama mbadala sasa unataka kutuambia nini? unasema ingekuwa upinzani ungefurahi, sasa wewe unatumia kigezo gani kujua wao wangefanya vizuri kuliko inavyofanyika sasa! hebu toa viashiria. Nikuulize swali dogo tu, watu waliopewa nafasi za uongozi kutoka vyama vya upinzani CHADEMA mathalan, wanafanya vizuri kuliko wale waliopo CCM siku zote?
Azizi hilo sio suala la kujua kusoma tu, ni suala la kiutendaji zaidi, ujue ni mbinu gani utazotumia kufikia hilo lengo, nyie hamjui yote hayo zaidi mnajua kusoma tu.

Nasema mmefeli kwasababu kiasi kinachopelekwa kuzihudumia hizo shule ni kidogo sana hakitoshi kukidhi mahitaji hapa usibishe, nyie mnalazimisha tu bora msikike mnatoa elimu bure.

Hilo swali lako kuhusu kufanya vizuri kama wangekuwa hawafanyi vizuri msingewapa hizo nafasi, naamimi wanafanya vizuri kwa viwango vyenu ndio maana bado mnawachukua tu na kuwapa madaraka.
 
Back
Top Bottom