Tuna uhakika gani na wimbi la uingizwaji nchini wa simu a Kichina???????????

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Mar 28, 2011
1,002
274
Habarini za jpili wanaJF wenzangu.nilikuwa natafakari peke yangu nikakoswa jibu hivyo nimelileta mbele yenu.Hivi ni mamlaka gani inayohusika na ubora wa uingizwaji wa simu nchini kati ya TBS na TCRA?.Kwa sababu nina wasiwasi mkubwa sana na ubora wa mionzi inayotumika katika simu za kichina kweli mionzi hiyo itaziacha afya zetu salama?????.Au ni bora mawasiliano masuala ya afya yako baadae!!!!!!!!!!
 
Hawa jamaa wanaohusika japokuwa siwajui lakini kiukweli hawapo makini, hata ubora wa bidhaa ni mbovu. Sema sasa ndio hivyo na sisi mazoea yetu wabongo..mtu anaona 75000 anapata simu ya mchina ina tv, redio, media player n.k tunaona ni poa kuliko kununua simu original ya bei hiyo hiyo ambayo ni vigumu kupata tv na sifa nyinginezo kwa bei rahisi.
 
Kila mbuz anakula kwa urefu wa kamba yake,mtu anawasiliana,anackiliza mzk,na cm za kichna smtyms zinakaa na chaj kwel! Na hata ikiharibika ni khasara yake! Hamtak watu wawe na cm kulingana na uwezo wao?ndo maana zikawepo RANGE ROVER na COROLLA! mtu kama cm inamtimizia mahitaj yake con tabu,to each their own!
 
Watu wanacho sahau ni kwamba components na dislays zinazotumika kwenye Iphone na motorola na PC nyingi zinaundwa u-China na kupelekwa Merikani na kwingineko Ulaya, wanachofanya ni kuweka nembo tu na ku-observe standards za nchi husika. Kwa hiyo si kweli kwamba kitu chochote kutoka u-China kina walakini, kuhusu mionzi: Hakuna mionzi ya Kichina au Ulaya/Merikani nchi zote hizo zinatumia mionzi(mawimbi ya radio yale yale) za kwenye vipimo vya microwave, cha muhimu hapa ni kuangalia kwamba transmitting power kwenye hand set hazizidi kiwango cha kimataifa bila kujali kama simu inatoka Uchina, Merikani au Ulaya vile vile na kuhakikisha kwamba simu zenyewe zianakuwa properly screened kupunguza hadhali za mionzi kupenya kutoka ndani ya simu wakati inapo tumika, simu za Kichina zinakuwa na bei nafuu kwa sababu ya cheap labour huko kwao.
 
mbona serikali ya India march mwaka huu iliBan importation ya fake Chinese mobile phones ambazo hazina valid imei numbers, nashangaa serikali yetu pamoja na kuelewa kwamba kuna vitu vingi feki vya kichina lakini bado ipo so reluctant katika hilo,,,,ni lazima serikali ya ccm iwe makini lasiivyo waTzania wengi wataumia kwa kupata hasara zisizo na maana'..
 
Back
Top Bottom