#COVID19 Tuna Serikali ya ajabu sana. Nchi inachafuliwa kwa COVID-19 huko India na mamlaka zimekaa kimya

Semahengere

JF-Expert Member
Nov 29, 2020
1,186
1,953
Hii nchi Ina laana kama balaa bluu.

Tangu juzi India inalalamika kupokea watu wao wanaorudi kutoka Tanzania wakiwa na Omicron the latest COVID-19 na walipimwa huku wakawa Negative. Nashangaa hakuna mwenye dhamana anayejibu chochote. Watu wamekaa kimya na kisheria ukinyamaza Ina maana umekubali

Inawezekana Waziri wa afya hajui Kingereza Kwa hiyo hana ujasiri wa kujibu. Au inawezekana hata hata hajui nini kinaendelea huko Duniani

Nikuombe Mama Samia hebu hebu ongoza nchi kisasa. Ongoza nchi kimataifa. Kaa na teamwork inayojielewa. Hawa mbwa wanaobwekea ndani tu sio wawindaji watatuchelewesha. Dunia siku hizi ni kama Kijiji. Taarifa inatakiwa ijibiwe punde tu inapotoka otherwise kuna nia ovu inakuja.

Nishauri tu jambo Moja Kwa kiongozi unaeona linamfaa achukue hili

Kwenye utalii Kuna kitu kinaitwa REVIEWS

Kila ukipata mgeni unajitahidi kumhudumia vizuri Ili kwenye TripAdvisor akuandikie review nzuri

Huwa wageni wakitaka kusafiri na Company yako wanaangalia waliokwisha kusafiri na wewe kwanza wameandika nini mtandaoni (reviews) wanashauri nini wenzao Ili wachague kusafiri na wewe.

Kama mgeni akisema nilisafiri na wewe mfano BAKARI TOURS lakini sikufanikiwa kuona rhino

Basi saa hiyo hiyo inatakiwa BAKARI TOURS ijibi Ile review Sababu ya mgeni kutokuona rhino kulisababishwa na nini

BAKARI TOURS akinyamaza ana kuwa amekubali kuwa mgeni hakuna rhino na ni Kosa la kampuni na guide alikuwa sio professional Kwa hiyo adhabu inakuja hutapokea booking

So ushauri wangu Kwa Waziri wa afya na utalii waache kukaa tu wakijua mambo yanakuja kirahisi

Hii taarifa inaenda kulaza chini utalii uliokuwa umechangamka tayari zaidi ya nchi yeyote Africa mashariki kama sio Africa nzima
Mambo yalishaanza kuwa mazuri

Tanzania has became alread the best destination of Tourism kipindi hiki hali ilivyotulia na hata wakati wa covid iliyopita

Ombila langu viongozi msibweteke namna hii kama mtu hujui Kingereza ni vizuri ukatafuta mtu wa kukusaidia ujibu tuhuma mtandaoni

Vijana wanaojua lugha wako wengi hata kazi hawana wako mitaani

Tafuta kijana mmoja Kaa nae Mahali muambie andika hapa hivi na hivi na hivi

Then ana submit biashara imeisha
Let the world know we're alive
Tusiwe kama inchi mfu (deadland)

Asante.
 
Bora tu wamekaa kimya. Hakuna haja ya kua defensively Corona sio jambo jipya what if huyo jamaa kaipata akiwa kwenye ndege au akiwa transit?
 
Umenikumbusha enzi za Jiwe anakwambia 'Kuna watu wameenda huko nje wamechoma chanjo wametuletea ma Corona ya ajabu ajabu nchini 😄😄😄'.
 
Dah Bwana wee nilipoiona na mm nilishangaa sana na vile vile wajue Duniani sasa kuna vita ya BIASHARA sio wakae tu wapweteke mapumbu yao tuko katika ulimwengu wa DOT COM kitu kidogo tu kinakuchafulia mpango mzima .
 
Ingekuwa vema ungeweka na screenshot ya huo upotoshaji unaofanywa na hao wahindi
 
aisee ulivyoandika, nikajua unaongelea kuhusu hawa COVID-19 wa bungeni kwamba wanachafua nchi yetu.
 
Yes na mm nilishangaa kuona wahusika wako kimya. Wahusika wawe proactive na kuwepo na information sharing kama mhusika hajaona , amshtue mwenye dhamana hiyo. Vita siyo risasi tu, hizo ni zana za mwisho, kinachoanza ni maneno. Ungekua kwa wenzetu masoko ya hisa na fedha ghafla vingeshuka thamani. Hata kwetu ni kwa Sababu mfumo wa kupima athari wa hizo habari haujakaa sawa ,lakin nina uhakika kuna image na attractiveness kwa wageni na wawekezaji vimekua affected.
 
Hii nchi Ina laana kama balaa bluu.

Tangu juzi India inalalamika kupokea watu wao wanaorudi kutoka Tanzania wakiwa na Omicron the latest COVID-19 na walipimwa huku wakawa Negative. Nashangaa hakuna mwenye dhamana anayejibu chochote. Watu wamekaa kimya na kisheria ukinyamaza Ina maana umekubali

Inawezekana Waziri wa afya hajui Kingereza Kwa hiyo hana ujasiri wa kujibu. Au inawezekana hata hata hajui nini kinaendelea huko Duniani

Nikuombe Mama Samia hebu hebu ongoza nchi kisasa. Ongoza nchi kimataifa. Kaa na teamwork inayojielewa. Hawa mbwa wanaobwekea ndani tu sio wawindaji watatuchelewesha. Dunia siku hizi ni kama Kijiji. Taarifa inatakiwa ijibiwe punde tu inapotoka otherwise kuna nia ovu inakuja.

Nishauri tu jambo Moja Kwa kiongozi unaeona linamfaa achukue hili

Kwenye utalii Kuna kitu kinaitwa REVIEWS
Kila ukipata mgeni unajitahidi kumhudumia vizuri Ili kwenye TripAdvisor akuandikie review nzuri
Huwa wageni wakitaka kusafiri na Company yako wanaangalia waliokwisha kusafiri na wewe kwanza wameandika nini mtandaoni (reviews) wanashauri nini wenzao Ili wachague kusafiri na wewe.
Kama mgeni akisema nilisafiri na wewe mfano BAKARI TOURS lakini sikufanikiwa kuona rhino
Basi saa hiyo hiyo inatakiwa BAKARI TOURS ijibi Ile review Sababu ya mgeni kutokuona rhino kulisababishwa na nini
BAKARI TOURS akinyamaza ana kuwa amekubali kuwa mgeni hakuna rhino na ni Kosa la kampuni na guide alikuwa sio professional Kwa hiyo adhabu inakuja hutapokea booking

So ushauri wangu Kwa Waziri wa afya na utalii waache kukaa tu wakijua mambo yanakuja kirahisi
Hii taarifa inaenda kulaza chini utalii uliokuwa umechangamka tayari zaidi ya nchi yeyote Africa mashariki kama sio Africa nzima
Mambo yalishaanza kuwa mazuri
Tanzania has became alread the best destination of Tourism kipindi hiki hali ilivyotulia na hata wakati wa covid iliyopita

Ombila langu viongozi msibweteke namna hii kama mtu hujui Kingereza ni vizuri ukatafuta mtu wa kukusaidia ujibu tuhuma mtandaoni
Vijana wanaojua lugha wako wengi hata kazi hawana wako mitaani
Tafuta kijana mmoja Kaa nae Mahali muambie andika hapa hivi na hivi na hivi
Then ana submit biashara imeisha
Let the world know we're alive
Tusiwe kama inchi mfu (deadland)

Asante.
Kwa kweli masikini tuna uzalendo japo sisi ndo tuna nyoonywa zaid na ma tozo, mtu kaandika kwa hisia kali, ila hana nyumba dar au gari au kazi ya sarikali, ila anapenda serikali yake
 
Hiyo Omnicron nimeona taarifa moja kuwa aliyetoka Tanzania kaenda nayo India. Wala sina sababu ya kuwabishia najua utendaji kazi wetu hapa nchini ni wa ovyo kila sekta. Nchi ambayo Professor alitengeneza chachandu akatia kwenye chupa ya tomato sauce akadai ni dawa ya uviko na mwingine Professor akaenda airport kunywa miti shamba iliyoletwa kwa ndege maalumu siwezi shangaa kama wenye diploma wakishindwa kupima na kutambua.

Unataka wizara itoe tamko gani kwamba huyo Mhindi hana corona ama aliipatia ukouko. Kwenye afya hakuna politics, North Korea ilifunga mpaka wa China, US ilizuia wasafiri kutoka UK. Hata sio hii variant pekee, tangu tunakataa hatuna corona India ilikuwa inawakuta wasafiri kadhaa kutoka Tanzania wakiwa nayo
 
Back
Top Bottom