waneemayote
Member
- Oct 20, 2019
- 56
- 153
Baada ya Laizer kupiga hela ya TANZANITE mengi yamezungumzwa, Mimi nimelitazama Jambo hili katika Kona nyingine. Nimeaangalia matajiri wetu wakubwa Tanzania kuanzia wa kwanza Hadi wa 12 list yao Ni Kama ifuatavyo:-
1.Mohammed Dewji.
2.Rostam Azizi.
3.Said Salim Bakhresa.
4.Reginald Mengi.
5.Ally Awadh.
6.Shekhar Kanabar.
7.Shubash Patel.
8.Fida Hussein Rashid.
9.Yusuph Manji
10.Salim Turkey
11. Ghalib said Mohamed
12.Yogesh Manek
Kuna Mambo ya kujifunza hapa.
✓ Tuwekeze zaidi kwenye Elimu ya ujasiriamali kwani kwenye list ya watu Hawa 12 wote ni wafanyabiashara. Kwa Sasa Tanzania vijana kwa wazee wanawekeza Sana kwenye Siasa kitu ambacho kinaleta reflection ya kizazi Cha baadaye kukosa matajiri kwani kila mtu anafikiria Siasa. Rwanda wao SoMo la ujasiriamali lipo kwenye mtaala Kama SoMo la lazima kwa wanafunzi wote wa advance. Yaani ni sawa na hapa kwetu SoMo la GS.
✓ Katika list hiyo amejitokeza Mengi tu Kama mtu mwenye Asili ya kibantu na Mswahili mwenzetu. Hapa hata watoto wanaokuwa wanajengeka mentality kuwa ili uwe tajiri kazima uwe na Asili Fulani. Katika hili wanakosa Mambo makubwa mawili Moja motivation kuwa watafanikiwa wakiwekeza, lakini la Pili role Model wa kumfuata. Kwa bahati mbaya mzee wetu Mengi ameshatangulia mbele ya haki hivyo tumebakia patupu kwa Sasa. Kuna watu wanaweza kudhani Ni ubaguzi Ila Kuna Jambo la muhimu Sana hapa hasa la kutengeneza matajiri wenye vinasaba na sisi.
✓ Matajiri wengi ni wale wale, yaani hakuna matajiri wapya wanaoibuka na kuleta ushindani. Hii inatokana na watu kutokuzifahamu fursa au fursa zinapojitokeza wale wale wenye mitaji wanazichukua. Serikali Ina wajibu mkubwa Sana wa kukuza, kutoa Elimu, na kusaidiwa kitaalamu kwa wanaotaka kujaribu Jambo fulan.
✓ Matajiri wanalisaidia Taifa katika Mambo makuu mawili, moja husaidia kutoa ajira kwa raia wake. Hivyo kila tunapopata Tajiri mpya Kama Laizer tumefungua ajira mpya mahali lakini la Pili wana kazi ya kulisiaidia Taifa pale linapokumbwa na majanga kwa kuchangia. Hili la Pili ni la kizalendo zaidi, mzee wetu Mengi alifanya na ziada kwa kuwatafuta Walemavu na kukaa nao meza Moja.
✓ Maeneo mawili ambayo kwa Sasa ukiwekeza unatajirika ni kwenye ujasiriamali na kwenye uvumbuzi (hasa Technology). Matajiri wengi wanatokea kwenye Sector hizi mbili. TUWEKEZE zaidi kwenye maeneo haya. Tuwekeze zaidi kwa vijana wetu wa veta na wabunifu wetu.
✓Katika Maelezo yake Laizer anataka kujenga shule na kufungua Mall kuna maswali mawili matatu najiuliza hiyo shule anajenga maeneo gani yasiokuwa na shule? (Do we have demand of schools in Arusha?) kwa kanda ya Kaskazini hatuna tatizo la majengo ya shule, ila tuna tatizo la walimu bora na mitaala mizuri.
Ukanda wa Kaskazini una shule lukuki zenye majina makubwa mno na ufaulu Bora kabisa. Hata shule za Serikali ukanda huu zinafanya vizuri Sana na wazazi wameshaelewa wengi hawapeleki private wanakimbizia shule za kawaida hili sio eneo sahihi la kupeleka mtaji kwa Sasa.
Kuhusu mall watanzania hatuna utamaduni wa kununua vitu malls, walikuja uchumi super markets kutoka kenya walifunga walikuja shoprites walifunga NAKUMAT walifunga, Moshi kulikuwa na mr. Price alifunga. Tanzania Tuna utamaduni wa kununua magengeni na kuamini malls ni za matajiri na ni expensive.
✓Laizer ajifunze kwa jamaa aliyeitwa Askofu yupo wapi kwa Sasa huyu jamaa alipataga pesa akazimwaga tokea Gorofani watu wakapigania chini ya Gorofa, kabla ya kutumia hizo fedha atulie Kama Mwezi mmoja au hata miwili then atafute washauri wa kibiashara wamshauri. Mtaji kwa Sasa anao lakini anahitaji mshauri Bora, Kuna kitu anapaswa kukifanya na kingemlipa haswa asiende haraka atulie na atafute washauri Bora.... Wala hana haja ya kuiga biashara za watu wengine. Narudia Kuna Jambo ambalo anapaswa kulifanya lingemlipa vibaya sana.....
Kila la Kheri Laizer tunatarajia baada ya miaka 10 uingie kwenye top ten hapa.
1.Mohammed Dewji.
2.Rostam Azizi.
3.Said Salim Bakhresa.
4.Reginald Mengi.
5.Ally Awadh.
6.Shekhar Kanabar.
7.Shubash Patel.
8.Fida Hussein Rashid.
9.Yusuph Manji
10.Salim Turkey
11. Ghalib said Mohamed
12.Yogesh Manek
Kuna Mambo ya kujifunza hapa.
✓ Tuwekeze zaidi kwenye Elimu ya ujasiriamali kwani kwenye list ya watu Hawa 12 wote ni wafanyabiashara. Kwa Sasa Tanzania vijana kwa wazee wanawekeza Sana kwenye Siasa kitu ambacho kinaleta reflection ya kizazi Cha baadaye kukosa matajiri kwani kila mtu anafikiria Siasa. Rwanda wao SoMo la ujasiriamali lipo kwenye mtaala Kama SoMo la lazima kwa wanafunzi wote wa advance. Yaani ni sawa na hapa kwetu SoMo la GS.
✓ Katika list hiyo amejitokeza Mengi tu Kama mtu mwenye Asili ya kibantu na Mswahili mwenzetu. Hapa hata watoto wanaokuwa wanajengeka mentality kuwa ili uwe tajiri kazima uwe na Asili Fulani. Katika hili wanakosa Mambo makubwa mawili Moja motivation kuwa watafanikiwa wakiwekeza, lakini la Pili role Model wa kumfuata. Kwa bahati mbaya mzee wetu Mengi ameshatangulia mbele ya haki hivyo tumebakia patupu kwa Sasa. Kuna watu wanaweza kudhani Ni ubaguzi Ila Kuna Jambo la muhimu Sana hapa hasa la kutengeneza matajiri wenye vinasaba na sisi.
✓ Matajiri wengi ni wale wale, yaani hakuna matajiri wapya wanaoibuka na kuleta ushindani. Hii inatokana na watu kutokuzifahamu fursa au fursa zinapojitokeza wale wale wenye mitaji wanazichukua. Serikali Ina wajibu mkubwa Sana wa kukuza, kutoa Elimu, na kusaidiwa kitaalamu kwa wanaotaka kujaribu Jambo fulan.
✓ Matajiri wanalisaidia Taifa katika Mambo makuu mawili, moja husaidia kutoa ajira kwa raia wake. Hivyo kila tunapopata Tajiri mpya Kama Laizer tumefungua ajira mpya mahali lakini la Pili wana kazi ya kulisiaidia Taifa pale linapokumbwa na majanga kwa kuchangia. Hili la Pili ni la kizalendo zaidi, mzee wetu Mengi alifanya na ziada kwa kuwatafuta Walemavu na kukaa nao meza Moja.
✓ Maeneo mawili ambayo kwa Sasa ukiwekeza unatajirika ni kwenye ujasiriamali na kwenye uvumbuzi (hasa Technology). Matajiri wengi wanatokea kwenye Sector hizi mbili. TUWEKEZE zaidi kwenye maeneo haya. Tuwekeze zaidi kwa vijana wetu wa veta na wabunifu wetu.
✓Katika Maelezo yake Laizer anataka kujenga shule na kufungua Mall kuna maswali mawili matatu najiuliza hiyo shule anajenga maeneo gani yasiokuwa na shule? (Do we have demand of schools in Arusha?) kwa kanda ya Kaskazini hatuna tatizo la majengo ya shule, ila tuna tatizo la walimu bora na mitaala mizuri.
Ukanda wa Kaskazini una shule lukuki zenye majina makubwa mno na ufaulu Bora kabisa. Hata shule za Serikali ukanda huu zinafanya vizuri Sana na wazazi wameshaelewa wengi hawapeleki private wanakimbizia shule za kawaida hili sio eneo sahihi la kupeleka mtaji kwa Sasa.
Kuhusu mall watanzania hatuna utamaduni wa kununua vitu malls, walikuja uchumi super markets kutoka kenya walifunga walikuja shoprites walifunga NAKUMAT walifunga, Moshi kulikuwa na mr. Price alifunga. Tanzania Tuna utamaduni wa kununua magengeni na kuamini malls ni za matajiri na ni expensive.
✓Laizer ajifunze kwa jamaa aliyeitwa Askofu yupo wapi kwa Sasa huyu jamaa alipataga pesa akazimwaga tokea Gorofani watu wakapigania chini ya Gorofa, kabla ya kutumia hizo fedha atulie Kama Mwezi mmoja au hata miwili then atafute washauri wa kibiashara wamshauri. Mtaji kwa Sasa anao lakini anahitaji mshauri Bora, Kuna kitu anapaswa kukifanya na kingemlipa haswa asiende haraka atulie na atafute washauri Bora.... Wala hana haja ya kuiga biashara za watu wengine. Narudia Kuna Jambo ambalo anapaswa kulifanya lingemlipa vibaya sana.....
Kila la Kheri Laizer tunatarajia baada ya miaka 10 uingie kwenye top ten hapa.