AUGUSTINO CHIWINGA
JF-Expert Member
- Apr 23, 2017
- 220
- 689
Uongozi ni karama kutoka kwa MUNGU.Bila ya karama yake hata hukitumia nguvu aina gani huwezi kuupata uongozi.Rais wa Tanzania anayo hii karama ya uongozi ukianzia kumtazama tangu siku alipoenda kuchukua fomu ya kuchukua Urais pale Makao Makuu ya CCM mpaka alipoapishwa. Ni wazi MUNGU mwenyewe alitaka awe na bila shaka alikua na sababu zake maalumu za kumchagua kuwa Rais wetu.
Ukitazama namna Rais Magufuli anavyojitoa katika kuwatumikia wananchi unaona wazi huyu ni kiongozi aliyeletwa kwa ajili ya kulikomboa Taifa hili.
Mambo makubwa anayoshughulika nayo Rais wetu katika kupambana na mafisadi, wezi, wauza madawa ya kulevya, majangili na vibaraka wasioitaka nchi yetu isiwe na Amani ni wazi kwamba Rais anahitaji sala na maombi yetu kila siku.
Sio wote wanaofurahi jinsi anavyobana mirija yao ya upigaji dili, hivyo ulinzi wa MUNGU ni muhimu kwa Rais wetu dhidi ya maadui wa Taifa waliopo ndani na nje.
Nilikuwepo katika viwanja vya Mkwakwani kwenye kampeni nilipomsikia Rais Magufuli akitamka kwamba anajitoa kafara kwa ajili ya Watanzania.Baada ya kuapishwa nimeamini na kuyasadiki yale maneno yake wala hayakua maneno ya kuombea kura tu bali anayafanyia kazi kwa vitendo halisi.
Ndugu zangu Watanzania nawahimiza wote wenye dini na wasio na dini katika imani zao mbalimbali katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka kumuombea Rais wetu ili akaikamilishe kazi yake kwa ya kitume kwa Taifa letu hili.
Ni imani yangu mpaka kufikia mwaka 2025 atakapokua anahitimisha miaka yake 10 ya Urais ataiacha Tanzania ikiwa katika uchumi imara na kuliziba lile pengo baina ya wenye nacho na wasio nacho, ataiacha Tanzania ikiwa imepiga hatua kubwa kimaendeleo.
Wasalaam,
Augustino Chiwinga
0659438889.
Ukitazama namna Rais Magufuli anavyojitoa katika kuwatumikia wananchi unaona wazi huyu ni kiongozi aliyeletwa kwa ajili ya kulikomboa Taifa hili.
Mambo makubwa anayoshughulika nayo Rais wetu katika kupambana na mafisadi, wezi, wauza madawa ya kulevya, majangili na vibaraka wasioitaka nchi yetu isiwe na Amani ni wazi kwamba Rais anahitaji sala na maombi yetu kila siku.
Sio wote wanaofurahi jinsi anavyobana mirija yao ya upigaji dili, hivyo ulinzi wa MUNGU ni muhimu kwa Rais wetu dhidi ya maadui wa Taifa waliopo ndani na nje.
Nilikuwepo katika viwanja vya Mkwakwani kwenye kampeni nilipomsikia Rais Magufuli akitamka kwamba anajitoa kafara kwa ajili ya Watanzania.Baada ya kuapishwa nimeamini na kuyasadiki yale maneno yake wala hayakua maneno ya kuombea kura tu bali anayafanyia kazi kwa vitendo halisi.
Ndugu zangu Watanzania nawahimiza wote wenye dini na wasio na dini katika imani zao mbalimbali katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka kumuombea Rais wetu ili akaikamilishe kazi yake kwa ya kitume kwa Taifa letu hili.
Ni imani yangu mpaka kufikia mwaka 2025 atakapokua anahitimisha miaka yake 10 ya Urais ataiacha Tanzania ikiwa katika uchumi imara na kuliziba lile pengo baina ya wenye nacho na wasio nacho, ataiacha Tanzania ikiwa imepiga hatua kubwa kimaendeleo.
Wasalaam,
Augustino Chiwinga
0659438889.