OMBI MAALUM:
Nimeamua kuliweka hapa hili ombi kwa sababu kuu mbili; Yakwanza ikiwa hapa ndipo wana-JF wengi zaidi wanafika ukifananisha na majukwaa mengi na sababu ya pili ikiwa ombi langu linawahusu viongozi wa kisiasa hivyo kama mod ataona halistahili basi anaweza kulipeleka anakoona yeye kunafaa.
Ninawaomba wana-JF wote tuwaombee kwa Mungu viongozi wetu wakuu wa nchi hii, hapa ninamaanisha Rais aliyepo madarakani sasa hivi Mheshimiwa Jakaya Kikwete, Rais mstaafu wa awamu ya pili Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi na zaidi sana tumuombee Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa.
Unaweza ukajiuliza tuwaombee juu ya nini, tumuombe Mungu awalinde hawa viongozi wetu. Sisi kama wanadamu tunajitahidi kuwapa ulinzi wa kibinadamu lakini ulinzi wa kweli unatoka kwa
Mungu. Hivyo basi tumuombe sana Mungu awalinde. Ulinzi huu tunaomuomba Mungu uwe zaidi kwenye hii mishafara yao ya barabarani. Uwe ulinzi juu ya ajali za barabarani.
Hawa ni viongozi wetu wa kitaifa ndio wakuu wa mamlaka ya taifa hili kwa vipindi tofauti hivyo kama ni mpango wa Mungu basi tumuombe mapenzi yake yatimizwe lakini kama ni mpango wa adui shetani basi ushindwe katika Jina la Yesu.
Najua kila mtu anaushabiki na ufuasi wa vyama tofauti lakini kwa hili naomba wote tujinyenyekeze kwa Mungu juu ya hawa viongozi wetu wa kitaifa. Na kwa wale wanaoweza kuwafikishia taarifa hii basi nao wafanye hivyo ili na wao binafsi waweze kumuomba Mungu awalinde. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU UTULINDE WATANZANIA!
Nimeamua kuliweka hapa hili ombi kwa sababu kuu mbili; Yakwanza ikiwa hapa ndipo wana-JF wengi zaidi wanafika ukifananisha na majukwaa mengi na sababu ya pili ikiwa ombi langu linawahusu viongozi wa kisiasa hivyo kama mod ataona halistahili basi anaweza kulipeleka anakoona yeye kunafaa.
Ninawaomba wana-JF wote tuwaombee kwa Mungu viongozi wetu wakuu wa nchi hii, hapa ninamaanisha Rais aliyepo madarakani sasa hivi Mheshimiwa Jakaya Kikwete, Rais mstaafu wa awamu ya pili Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi na zaidi sana tumuombee Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa.
Unaweza ukajiuliza tuwaombee juu ya nini, tumuombe Mungu awalinde hawa viongozi wetu. Sisi kama wanadamu tunajitahidi kuwapa ulinzi wa kibinadamu lakini ulinzi wa kweli unatoka kwa
Mungu. Hivyo basi tumuombe sana Mungu awalinde. Ulinzi huu tunaomuomba Mungu uwe zaidi kwenye hii mishafara yao ya barabarani. Uwe ulinzi juu ya ajali za barabarani.
Hawa ni viongozi wetu wa kitaifa ndio wakuu wa mamlaka ya taifa hili kwa vipindi tofauti hivyo kama ni mpango wa Mungu basi tumuombe mapenzi yake yatimizwe lakini kama ni mpango wa adui shetani basi ushindwe katika Jina la Yesu.
Najua kila mtu anaushabiki na ufuasi wa vyama tofauti lakini kwa hili naomba wote tujinyenyekeze kwa Mungu juu ya hawa viongozi wetu wa kitaifa. Na kwa wale wanaoweza kuwafikishia taarifa hii basi nao wafanye hivyo ili na wao binafsi waweze kumuomba Mungu awalinde. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU UTULINDE WATANZANIA!