Tumuenzi Kikwete Historia isije Ikamsahau

unajua uongozi huwa unaleta bubble hivi....
una loose touch na reality....

kama kuna mtu leo alimsikiliza kikwete akihojiwa kuhusu
birthday yake na east africa radio...kipindi cha saa nane....ilikuwa aibu tupu....

yaani hilo bubble alilomo ni la aina yake....so sad...

Sikuamini yale niliyosikia toka kwa huyo mjomba!! Hapa chini ni baadhi ya majamboz aliyoyasema...
'nikisafiri uwa narudi na CDs nyingi sana, hata mwanangu Ritz1 anafahamu'
'ninapokuwepo mjini lazima niende taifa kama Taifa Stars wanacheza'
'ninapendekeza muwe na kipindi cha nyimbo mpya; kiitwe mpya za mwezi huu'

Duh! Hayo ni maneno ya mheshimiwa mtukufu mpendwa daktari alhaji rais!!
 
Saint Kikwete Kigamboni brdge

Kikwete space station - vision 2050
Kikwete center for diseases control and prevention

na kwa kuheshimu mchango wake hasa kwenye michezo tuwaite taifsa stars = kikwete wanderers
Na kuhusu ule mradi wake wa viburudisho, aenziwe kwa kupublish journal yenye jina, 'Dr JM Kikwete the polygamist of the century'
 
Kwa kutambua mchango wake katika tamasha la fiesta,nilikuwa nashauri tamasha la fiesta lilite “JK Carnival“ na may be Joseph Kusaga anaweza ku~add middle name “Jakaya“ ikawa Josph Jakaya Kusaga.
 
Hivi wewe jamaa utaacha lini kuandika pumba? Unashindwa hata na Kubenea kwa kujenga hoja ingawa mpaka sasa hajui aliyemmwagia tindikali. Jitahidi kupunguza porojo mkuu!

Nyani haoni kundule.....
 
. lolo.jpg
Kwasababu ya kupenda mabinti.........shindano la Miss Tanzania liitwe Jakaya Kikwete Miss Tanzania competition....
 
hizi zinaitwa sifa za kijinga ambazo huwa zinatolewa na mjinga, Mmbeya, mpuuzi, mpumbavu au mnafiki!! itakuwa vyema sana sifa hizi akipewa Dr. W.P.S.; KWA MFANO LILE GARI MOSHI LITAKALOTUMIA SAA 3 KUTOKA DAR MPAKA MWANZA LITAKAPO NUNULIWA LIITWE "DR. W.P.S. CENTRAL RAILWAY LINE"


"inchi hii ya tanzania ina wenyewe!! na wenyewe hao si wengine bali ni ccm"
 
Nimecheka sana, sina comment mkuu. Sometimes I wonder you. Serious or joking.
 
Hivi wewe jamaa utaacha lini kuandika pumba? Unashindwa hata na Kubenea kwa kujenga hoja ingawa mpaka sasa hajui aliyemmwagia tindikali. Jitahidi kupunguza porojo mkuu!
Mkuu soma taratibu then support or oppose. Huu si upupu soma mawazo ya mtu sio tu kilichoondikwa. Hii ni habari nyuma ya pazia soma tafakari utapata jibu.
 
View attachment 38509 Baada ya kutafakari sana na kutumia muda mwingi kuwaza jinsi gani kama ningepewa nafasi ya kumuenzi Rais Kikwete ningefanya nini nimejikuta na mapendekezo mengi sana yaliyonijia kwa ghafla kichwani kama maporomoko ya maji kwenye magema ya Udzungwa. Kama ukungu ukiinuka na kuachana na manyasi kwenye kona za Mlima Kilimanjaro alfajiri na mapema ndivyo fikra zangu zilivyofunguka na kutambua kuwa Rais Kikwete hajaenziwa vya kutosha kutoka na mchango wake mkubwa katika maisha, historia, hali, na hatma ya watu wetu. Hivyo mapendekezo yangu nimeyatoa kwa moyo wa furaha uliojaa tabasamu, kicheko na matumaini kuwa yatakubaliwa na wale wote wenye kuitakia mema nchi yetu ambao hawapendi kuendeleza chuki binafsi, udini, ukabila na ubaguzi wa aina yoyote. Ni mapendekezo ya kiungwana ya kumuenzi Rais wetu wa nne. Pale Ikulu pabadilishwe na kuitwa Kikwete House Barabara ya Morogoro iitwe Jakaya Highway Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam ambapo alisomea kibadilishwe kwa heshima yake na mchango wake katika uchumi na kuitwa Jakaya Kikwete Dar-es-Salaam University (tunaweza kuongeza "national" kwenye hiyo title) Jengo jipya la sanaa lililojengwa na Wachina liitwe Jakaya Kikwete Center for Performing Arts Chuo Kipya cha Kijeshi kule Kigamboni kiitwe Lt. Col. J. M. Kikwete War College Jeshi la Wananchi ambalo alilitumikia kwa umakini na umahiri limpandishe cheo ili we Gen. Jakaya Kikwete ili kuonesha mchango wake wa jinsi alivyoliendeleza jeshi hilo hadi kukamata maharamia nane. Kwa vile nimekuwa nikipigia sana kampeni ya kujengwa kwa hospitali ya taifa ya watoto naamini kama atalifanyia kazi wazo hili hospitali hiyo iitwe Dr. Jakaya Kikwete National Children's Hospital kwa masharti kwamba kama itatokea ikajengwa wakati hayupo basi tunaweza kuongeza neno "Memorial" humo katikati. Kutokana na kuendelesha mahusiano yake ya karibu na viongozi mbalimbali wa dini napendekeza viongozi wa Kiislamu waangalie ni Msikiti gani maarufu nchini upewe hadhi ya Kikwete Mosque; Viongozi wa Makanisa wanaweza nao - kutokana na mambo mbalimbali ambayo amewasaidia - kutafuta mahali ambapo pangeweza kupewa jina la Jakaya Kikwete National Chapel. Kama ni kubwa sana tunaweza kuliita Cathedral! Kama ni Wakatoliki na jengo hilo lina hadhi ya Kipapa tunaweza kuita "Kikwete Basilica of Our Lady of Fatima" Daraja linalotarajiwa kujengwa la Kigamboni kwa ushirikiano mkubwa wa serikali na NSSF laweza kupewa jina la Kikwete International Bridge (sasa hii 'international' ni kwa sababu tu watu watakuwa wanavuka kwenda ng'ambo kupitia daraja hilo). Nimekumbuka kuwa ile Maktaba ya Taifa kwa kweli haina hadhi ya kitaifa kwani haina jina la kiongozi wa kitaifa. Hivyo naipendekeza - sidhani kama kuna watu watanipinga - iitwe Dr. Kikwete National Library. Hii ni kutokana na mchango wake wa kuendeleza usomaji nchini na huduma ya library na hasa kutokana na mipango ya miaka kumi iliyopita ya ujenzi wa maktaba mpya jijini Dar kukidhi mahitaji ya watoto wetu ambayo inatarajiwa kuanza kutekelezwa mwishoni mwa utawala wa Rais Kikwete Ukiondoa maeneo hayo nadhani wapo watu wengine wanaoweza kufikiria maeneo, vitu na hata majengo mbalimbali ambayo yatalibeba jina la Rais Kikwete. Na licha ya hivyo wakati umefika wa kuanza kuweka picha zake sehemu mbalimbali nchini. Picha kubwa zinaweza kuanza kupambwa kuanzia uwanja wa ndege na maeneo yote ya kuingilia mijini. Kwa vile ofisi zote tayari zinapambwa na picha ya rais ndani nafikiri hii si heshima nzuri kwa maana si watu wote wanaingia maofisini humo. Napendekeza picha kubwa za rangi (zinaweza kuwa zile za kutabasamu au akimpa mtoto peremende) ziwekwe maeneo ya wazi ya nje ili ionekane. Sasa tukiwa tunafanya hivyo napendekeza kuwa kumtaja kwa jina la Dr. Kikwete kwa kweli hakuendani hasa na hisia za Watanzania wengi. Binafsi kuanzia leo hii nitamtambulisha kama Kiongozi Mpendwa Dr. Sasa hili ni muhimu sana kusema hivi kwa sababu isije ikaonekana anachukiwa. Kwa kiingereza tunaweza kumuiwa "Dear Leader" au "Beloved Leader" ili kuonesha mapenzi yetu kwa uongozi wake mahiri na jinsi gani amegusa mioyo ya watu wetu na kuwafanya wainuke kujiletea maendeleo. Kama unakubaliana na mapendekezo yangu nawe unaweza kupendekeza ni maeneo au vitu gani muhimu vibebe jina la Rais Mpendwa Kikwete? Sasa ni lazima viwe ni vitu vya heshima visiwe vitu vya kejeli ili tusionekane kabisa tunamdharau. Sasa kwa vile haya ni maamuzi ya wananchi wenyewe hayahitaji kibali kwani kama jina la mahali likishazoeleka sana ndivyo linavyokuwa na baadaye kutambulika hivyo.
your point here is ...unamvalisha kiremba cha ukoka huyo jamaa anayeitwa.. sijui dr. kikwete!!! but your thread sound pointless due to the fact that, you have marked no boundary btn jokes and facts(seriousness). nchi hii ina matatizo mengi kama rushwa, ufisadi, injustices etc. lakini cha kushangaza unakuja na thread za kipuuzi!! try to be fair on yourself and to the public. watu tunalia na janga hili linalotukabiri la serikali ya kishetani na wewe unatuletea mizaha? so what? aaghh. umezalilisha utu wako, heshima yako na elimu yako pia kwani ni zambi kubwa kusema usichokiamini(lies)
 
your point here is ...unamvalisha kiremba cha ukoka huyo jamaa anayeitwa.. sijui dr. kikwete!!! but your thread sound pointless due to the fact that, you have marked no boundary btn jokes and facts(seriousness). nchi hii ina matatizo mengi kama rushwa, ufisadi, injustices etc. lakini cha kushangaza unakuja na thread za kipuuzi!! try to be fair on yourself and to the public. watu tunalia na janga hili linalotukabiri la serikali ya kishetani na wewe unatuletea mizaha? so what? aaghh. umezalilisha utu wako, heshima yako na elimu yako pia kwani ni zambi kubwa kusema usichokiamini(lies)
Fahamu kuwa kuna namna nyingi ya kuyaona na kuyasema mambo, hivyo basi hutendi haki kumshambulia mtoa mada kwa vile ameyaona na kuyasema mambo tofauti na mtazamo wako. Utaishi kwa raha sana kama utakubali kutokubaliana na ukavumilia kutokubaliana.
 
Napendekeza bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu "High Edecation Student Loan Board" iitwe Dr Kikwete High Education Student Loan Board" maana katika kipindi cha uongozi wake imeweka "means testing" inayofanya kazi kwa ufanisi na kuweza kuwatambua watoto wa matajiri wanaojilipia huku watoto wa masikini wakikopeshwa 100%. Pia reli ya kati iitwe Dr. Kikwete Central Railway maana katika uongozi wake amefanya jitihada za kuhakikisha inapata mwekezaji mpya ikiwa ni pamoja na kuleta injini mpya kutoka India.
 
Ili kuenzi mchango wake katika elimu naona wizara ya elimu kupitia NECTA waweke utaratibu wa kuhakikisha kila cheti cha mwanafunzi aliyesoma shule ya kata kinakuwa na nembo iliyoandikwa "Dr Kikwete Product" maana alama zilizo katika kile cheti (na/au ufanisi/uwezo wa kitaaluma wa mwenye cheti) vitalitangaza jina la mheshimiwa kwa kila atakayekiona hicho cheti.
 
Katika maraisi watakao kupotea haraka sana katika masikio ya Watanzania ni huyu maana hakuna kitu alichofanya zaidi ya haya madudu mengi ya Richmond na mdogo wake Dowans
 
your point here is ...unamvalisha kiremba cha ukoka huyo jamaa anayeitwa.. sijui dr. kikwete!!! but your thread sound pointless due to the fact that, you have marked no boundary btn jokes and facts(seriousness). nchi hii ina matatizo mengi kama rushwa, ufisadi, injustices etc. lakini cha kushangaza unakuja na thread za kipuuzi!! try to be fair on yourself and to the public. watu tunalia na janga hili linalotukabiri la serikali ya kishetani na wewe unatuletea mizaha? so what? aaghh. umezalilisha utu wako, heshima yako na elimu yako pia kwani ni zambi kubwa kusema usichokiamini(lies)
Uliwa serious sana huwezi pata ufumbuzi wa matatizo ya nchi hii, jaribu leo kuwa serious wakati walioko juu yako wanacheka cheka tu....kama hujarusha ngumi........tunahitaji mizaha, lakini iwe imeandaliwa kwa umakini baada ya tafakuri ya kina...
 
Back
Top Bottom