Tumuenzi Kikwete Historia isije Ikamsahau

we kweli kichwa empy,ni miaka 6,anaenziwa mana mda wowote hata kesho anaweza akaachia ofice
 
Umepoteza muda wako mwingi wa maisha yako kusomea uandishi lakini taaluma imekutupa umebakia kuwa mercenary!! Ningekuita MALAYA kwani utamtumikia yeyote atakayelipa dau lako.!!
siyo kwamba ungekuwa malaya,...ndo kazi yako na unajua dau kwahiyo usingejua kuzitafsiri fasihi
 
Unaanzaje kumuenzi mtu ambaye bado ana miaka 4 madarakani?

mbona wengine wameshaanza kumuenzi kwa mengi ambayo ameyafanya? miaka mitano iliyopita amefanya mengi kuliko marais wengine watatu waliomtangulia ni rahisi hivyo kuweza kuona miaka minne ya neema itakuwaje. Pia tukianza sasa tutammotivate zaidi kufanya makubwa zaidi.
 
unataka aenziwe akishakufa? hebu acha wivu wa kike..
mkjj, how dare u forget airport mpya ya bagamoyo, nyumbani kwao! na kwa vile mtm amesuggest olympic team iitwe ridhiwan kikwete, basi walau mama salma aenziwe kwenye hii ya bagamoyo kwa uthubutu na umahiri wake wa kum-support baba mdogo wa taifa hili changa.
kwa sababu dr jk aliahidi na kutimiza ahadi yake ya bajaj kwa ajili ya wamama wajawazito, pengine zinaweza kuitwa saint kikwete ambulance (mbona kuna st john's?)
Unaanzaje kumuenzi mtu ambaye bado ana miaka 4 madarakani?
 
lazima ulalamike coz ameguswa mumeo. sidhani kama pumba zako zinamzidi mtu humu Mr. ingilishi a.k.a mwamiaji haramu

Umejibu sahihi sana, pumba zangu hazimzidi mtu humu meaning sina pumba kama za watu wengine. Ndiyo maana nimemwomba jamaa apungunze pumba kwasababu zinaharibu jamvi.
 
View attachment 38509
Baada ya kutafakari sana na kutumia muda mwingi kuwaza jinsi gani kama ningepewa nafasi ya kumuenzi Rais Kikwete ningefanya nini nimejikuta na mapendekezo mengi sana yaliyonijia kwa ghafla kichwani kama maporomoko ya maji kwenye magema ya Udzungwa. Kama ukungu ukiinuka na kuachana na manyasi kwenye kona za Mlima Kilimanjaro alfajiri na mapema ndivyo fikra zangu zilivyofunguka na kutambua kuwa Rais Kikwete hajaenziwa vya kutosha kutoka na mchango wake mkubwa katika maisha, historia, hali, na hatma ya watu wetu. Hivyo mapendekezo yangu nimeyatoa kwa moyo wa furaha uliojaa tabasamu, kicheko na matumaini kuwa yatakubaliwa na wale wote wenye kuitakia mema nchi yetu ambao hawapendi kuendeleza chuki binafsi, udini, ukabila na ubaguzi wa aina yoyote.

Ni mapendekezo ya kiungwana ya kumuenzi Rais wetu wa nne.

Pale Ikulu pabadilishwe na kuitwa Kikwete House
Barabara ya Morogoro iitwe Jakaya Highway
Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam ambapo alisomea kibadilishwe kwa heshima yake na mchango wake katika uchumi na kuitwa Jakaya Kikwete Dar-es-Salaam University (tunaweza kuongeza "national" kwenye hiyo title)
Jengo jipya la sanaa lililojengwa na Wachina liitwe Jakaya Kikwete Center for Performing Arts
Chuo Kipya cha Kijeshi kule Kigamboni kiitwe Lt. Col. J. M. Kikwete War College
Jeshi la Wananchi ambalo alilitumikia kwa umakini na umahiri limpandishe cheo ili we Gen. Jakaya Kikwete ili kuonesha mchango wake wa jinsi alivyoliendeleza jeshi hilo hadi kukamata maharamia nane.
Kwa vile nimekuwa nikipigia sana kampeni ya kujengwa kwa hospitali ya taifa ya watoto naamini kama atalifanyia kazi wazo hili hospitali hiyo iitwe Dr. Jakaya Kikwete National Children's Hospital kwa masharti kwamba kama itatokea ikajengwa wakati hayupo basi tunaweza kuongeza neno "Memorial" humo katikati.
Kutokana na kuendelesha mahusiano yake ya karibu na viongozi mbalimbali wa dini napendekeza viongozi wa Kiislamu waangalie ni Msikiti gani maarufu nchini upewe hadhi ya Kikwete Mosque; Viongozi wa Makanisa wanaweza nao - kutokana na mambo mbalimbali ambayo amewasaidia - kutafuta mahali ambapo pangeweza kupewa jina la Jakaya Kikwete National Chapel. Kama ni kubwa sana tunaweza kuliita Cathedral! Kama ni Wakatoliki na jengo hilo lina hadhi ya Kipapa tunaweza kuita "Kikwete Basilica of Our Lady of Fatima"
Daraja linalotarajiwa kujengwa la Kigamboni kwa ushirikiano mkubwa wa serikali na NSSF laweza kupewa jina la Kikwete International Bridge (sasa hii 'international' ni kwa sababu tu watu watakuwa wanavuka kwenda ng'ambo kupitia daraja hilo).
Nimekumbuka kuwa ile Maktaba ya Taifa kwa kweli haina hadhi ya kitaifa kwani haina jina la kiongozi wa kitaifa. Hivyo naipendekeza - sidhani kama kuna watu watanipinga - iitwe Dr. Kikwete National Library. Hii ni kutokana na mchango wake wa kuendeleza usomaji nchini na huduma ya library na hasa kutokana na mipango ya miaka kumi iliyopita ya ujenzi wa maktaba mpya jijini Dar kukidhi mahitaji ya watoto wetu ambayo inatarajiwa kuanza kutekelezwa mwishoni mwa utawala wa Rais Kikwete

Ukiondoa maeneo hayo nadhani wapo watu wengine wanaoweza kufikiria maeneo, vitu na hata majengo mbalimbali ambayo yatalibeba jina la Rais Kikwete. Na licha ya hivyo wakati umefika wa kuanza kuweka picha zake sehemu mbalimbali nchini. Picha kubwa zinaweza kuanza kupambwa kuanzia uwanja wa ndege na maeneo yote ya kuingilia mijini. Kwa vile ofisi zote tayari zinapambwa na picha ya rais ndani nafikiri hii si heshima nzuri kwa maana si watu wote wanaingia maofisini humo. Napendekeza picha kubwa za rangi (zinaweza kuwa zile za kutabasamu au akimpa mtoto peremende) ziwekwe maeneo ya wazi ya nje ili ionekane.

Sasa tukiwa tunafanya hivyo napendekeza kuwa kumtaja kwa jina la Dr. Kikwete kwa kweli hakuendani hasa na hisia za Watanzania wengi. Binafsi kuanzia leo hii nitamtambulisha kama Kiongozi Mpendwa Dr. Sasa hili ni muhimu sana kusema hivi kwa sababu isije ikaonekana anachukiwa. Kwa kiingereza tunaweza kumuiwa "Dear Leader" au "Beloved Leader" ili kuonesha mapenzi yetu kwa uongozi wake mahiri na jinsi gani amegusa mioyo ya watu wetu na kuwafanya wainuke kujiletea maendeleo.

Kama unakubaliana na mapendekezo yangu nawe unaweza kupendekeza ni maeneo au vitu gani muhimu vibebe jina la Rais Mpendwa Kikwete? Sasa ni lazima viwe ni vitu vya heshima visiwe vitu vya kejeli ili tusionekane kabisa tunamdharau. Sasa kwa vile haya ni maamuzi ya wananchi wenyewe hayahitaji kibali kwani kama jina la mahali likishazoeleka sana ndivyo linavyokuwa na baadaye kutambulika hivyo.
Kitufe cha Thanks naona kimerudi,haya,tumuenzi.
 
Umepoteza muda wako mwingi wa maisha yako kusomea uandishi lakini taaluma imekutupa umebakia kuwa mercenary!! Ningekuita MALAYA kwani utamtumikia yeyote atakayelipa dau lako.!!

Kama ungesoma kwa makini na kuelewa maana ya Mwanakijiji ungeweza kujua kuwa maana yake ni sawa na yako. Labda ya kwake imekwenda mbali zaidi. Mko ukurasa mmoja, lakini alichofanya Mwanakijiji ni kujaribu kumvika mfalme vazi ambalo ni watu wenye busara tu wanaweza kuliona.
 
Na yale majengo ya biashara yabadilishwe yaitwe Hon. Lt. Col. Chief. Alhajj. Dr of three PhD's J.K. Nadhani ina kautamu fulani hivi na heshima sana maana hajapata na hatapatatokea kiongozi kama yeye anaependa Wamachinga kiasi hiki! Vipi upande wa kilimo kwanza aitweje?
 
Sikujua kwamba Mzee Mwanakijiji ni MNAFIKI kiasi hiki. Acha utoto mzee, you are too matured to write pumbaz like these
 
wengi hawajakulewa mwanakijiji.......mfano kija nape hapa anaweka akausujudia kabisa.......

Sema wewe hujamuelewa, usiseme wengi Mpwa unakosea! Mie nimemwelewa na hata walio comment earlier wamemwelewa hata MWITA25 nae amemwelewa ndio maana comment zake ziko vile!
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom