#COVID19 Tumsikilize mchungaji Gwajima, tusimbeze. Chanjo zote zina bechi tofauti na kuna nchi hukataa baadhi ya bechi na nyingine ni zile zilizobakia

Kumbe na wewe hauna akili kama Gwajima? Umeandika utopolo mtupu! Kwanza hizo chanjo hazidhuru DNA kama wewe na Gwajiboy mnavyowadanganya watu.

Chanjo ya COVID-19 haibadili au kuingiliana na DNA yako kwa njia yoyote. Chanjo zote za mRNA na virusi vya virusi vya COVID-19 hutoa maagizo kwa seli zetu ili kuanza kujenga kinga dhidi ya virusi vinavyosababisha COVID-19. Lakini, nyenzo hizo haziingii kamwe kwenye kiini cha seli, ambayo ndio huhifadhiwa DNA yetu.

Pia Gwajima anasema hiyo COVID-19 itaisha yenyewe na hataki mwananchi yeyote apate chanjo. Hilo la kusema zipimwe “chemicals” zake, ni kama tu tayari keshaaminisha watu kuwa chanjo ni mbaya na kuzipima ni ili kusapoti hoja yake. Labda angesema zipimwe kwanza ndiyo maamuzi yafanyike, lakini yeye anaongea as if tayari keshafahamu kuwa chanjo ni mbaya. Angeacha kauli ambayo imeshatewa kuwa chanjo ni hiyari na siyo lazima. Lasivyo atakuwa responsible kwa watakaopoteza maisha yao kwasababu ya vitisho vyake.

Kuna wale wanaosema kuwa chanjo haizuii kupatwa tena na COVID-19. Ni kweli, lakini imetokea zaidi kwenye wimbi hili la “Delta variant”, hata hivyo, chanjo bado inasaidia wale waliochanjwa wasipate madhara makubwa yanayosababishwa na virusi hivyo ikiwemo kupelekwa hospitali na hata kupoteza maisha yao.

Muwe munajishughulisha kufanya viji “research” vidogo vidogo ili kuweza kuelewa jambo badala ya kukurupuka tu.

Haya kwa kuwa tunakupenda, angalia na huyu hapa. Kamab vipi, kwa kuwa mnaweza, waueni wote mkiwamaliza, mwende na mataifa mengine yanayopinga hiki kitu, nao muwaue, mbaki ninyi na billgates peke yenu.

 
Magufuli amewaharibu sana,hivi mwafrika utamkwepaje mzungu akidhamiria kukuua?
Unakataa chanjo ya corona,vipi kuhusu chanjo ya polio,ndui na surua?
Hivi ni nani aliyewaroga kiasi cha kushindwa kujua hata uji unaokula kila siku unaweza kukumaliza? Mnashinddwa nini kuelewa kuna watu wallipendana lakini baada ya muda wapenzi hao waka chomeana ndani ya nyumba na kuuana? Nikweli hujawahi kuona mtoto au mzazi akiua mtoto wake? Mbona mnakuwa kama hamko duniani? Matamshi ya Billy Gates na wenzake kuhusu mtumizi ya chanjo kupunguza idadi yawatu duniani hamjayasoma? Mbona yako kila kona? Hivi ninyi ni watu gani kama hamjui habari za new word order? Nini ni watu waina gain msiojua kuna agenda ya kudepopulate dunia ambayo iko dhahiri? Ni nini kifanyike ili muone? Kwa nini mnaishi kwa kukariri matukiio?

Kwa kuw mzugnu hashindwi kukuua , ndipo upeleke shingo yako Kibra?
Mbona mnatoa hoja za watu primitive sana? Hii ni ishara kwmba ujinga bado ni tatizo kubwa hapa tulipo?
 
Shida kubwa ya waTanzania walio wengi ni kutumia mahaba baada ya akili........

Yaani mtu kabla hajaangalia content ya habari kwanza anatazama hii habari imeletwa na nani kuanzia hapo ndio akili yake itaamua kwamba aipinge au aikubali habari........

Akili zetu tumewakabidhi wanasiasa, hakuna tena mwenye kufikiria nje ya maoni na utashi wa wanasiasa......

Siku waTanzania watapoanza kutumia akili zao baada ya kuabudu fikra za wanasiasa ndio safari ya mabadiliko ya kweli itakapoanza.........
 
Utangulizi- Nawaomba Mods msihamishe uzi huu.

Mchungaji Josephat Gwajima asimamia maeneo mawili katika hoja yake.

Kwanza, kilichomo kwenye chanjo na pili chanjo dhidi ya wanajeshi na walinda usalama wa nchi.

La kwanza kuhusu kilichomo kwenye chanjo au (content).

Mchungaji Gwajima anadai ni lazima madaktari wajiridhishe kuwa kilichomo katika chanjo nyingi zilizowasili Tanzania jana ni sawa na kilichomo katika chanjo walopewa raia wa nchi zilizoendelea.

Itakumbukwa kuwa mapema mwaka huu nchi nyingi zilizoendelea zilipokea idadi kubwa ya chanjo za Covid-19 na kufikia mwezi Juni mwaka huu Marekani pamoja na Uingereza zikaanza kusema kuwa zitapeleka dawa zilizobakia katika nchi maskini.

Ahadi hiyo ilitolewa na Raisi Biden na Boris Johnson wa Uingereza katika mkutano wa nchi tajiri 7 au G7 ulofanyikia katika mji wa Cornwall nchini Uingereza.

Covid vaccine: UK and US to give leftover doses to poorer countries kupitia BBC Covid vaccine: UK and US to give leftover doses to poorer countries - CBBC Newsround

Lakini siku moja kabla ya mkutano huo raisi Biden aliahidi kutoa msaada wa dawa za chanjo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 500-

US to donate 500 million Pfizer COVID-19 vaccine doses globally: Report- US to donate 500 million Pfizer COVID-19 vaccine doses globally: Report

Sasa tukirudi katika hoja ya mchungaji Gwajima kwamba lazima tuangazie kilichomo (Content) katika chanjo hizo zote ni ya kuzingatiwa.

Wenzetu wazungu wao walikwishajipanga vilivyo katika suala zima la kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO -19 na kwa muktadha huo waliweza kutengeneza vipeperushi na vielelezo vingine ambavyo zinalenga kumuelimisha mchanjwaji mtarajiwa kuwa ni aina ipi ya chanjo anaweza kupata, imetengenezwa vipi kwa kutumia nini, na inabeba vitu gani na kisha madhara yake baada ya kudungwa au "side effects"

Hivyo taarifa zoote kuhusu UVIKO-19 zimo katika tovuti za serikali za nchi zote zilizoendelea na mtu aweza kusoma na kuelewa bila shida.

Serikali ya Tanzania ingeweza kabisa kufanya hili ilipokuwa ikijiandaa kupokea chanjo na kuondoa uwezekano wa mijadala ambayo yaonekana wazi kuwa haiwezi kuzuia utekelezaji wa kudunga watanzania chanjo hizo.

Sasa hizo chanjo zina namba maalum au bechi au kwa kiingereza batch number hivyo pfizer yaweza kuitwa BNT163C1 au 161C2 na kadhalika.

Hizi namba zinatofautina na ukiwa umedungwa BNT163C1 basi ni lazima uje udungwe dozi ya pili ambayo ni kutoka katika bechi hiyohiyo yaani yaweza kuwa BNT163C3 lakini haiwezi kuwa BNT200b1 ambayo yaweza kuwa ndo inoleta madhara kama kuganda kwa damu.

Ni hivyohivyo kwa chanjo za Moderna, Johnson &Johnson na Moderna ambazo pia zinatumia bechi tofauti.

Moderna inayoyumika kwa mtu A yenye bechi namba 3001729 ndo hiyohiyo itayotumika kwa mtu huyohuyo A lakini itafuatia kidogo na kuwa 3001830.

Mtu anechanjwa Pfiser BioNTech ni lazima achanjwe dozi hiyohiyo ya chanjo hiyohiyo.

Nchi kadhaa za Ulaya na Marekani wakiangalia namba ya bechi ambayo msafiri amechomwa kuna ambao wanakataliwa kuingia katika nchi hizo kwa kuwa amechomwa chanjo ambayo ni ya kutoka kwenye bechi ambayo ina matatizo ya kuleta kuganda kwa damu na homa kali isokwisha.

Katika chanjo zote chanjo ya Oxford Astra Zeneca ndo chanjo ambao haihitaji baridi kali kuitunza hivyo kuifanya iwe rahisi kuihifadhi katika jokovu la kawaida kama yale ya majumbani.

Chanjo zingine zote huitaji majokovu maalum ambayo pia ni lazima yawe katika mazingira ya kutoweza kuvurugwa na waswahili au kuwa "compromised".

Hivyo hapa nina imani pia kuwa Serikali imewekeza vilivyo katika idara ya uhifadhi na ugavi wa chanjo hizi na hakutakuwa na dalili za kuzivuruga chanjo hizo.

Sasa basi, mchungaji Gwajima anadai ni lazima tujiridhishe kuwa dawa hizi za chanjo zina kiwango kilichomo (content) sawa na chanjo walochomwa wazungu huko Ulaya na Marekani.

Kwenye hili ana hoja kwani hatufahamu dawa hizi za chanjo zimepitia wapi, zimehifadhiwa vipi, zitabadilika vipi kiubora (yaani quality) na je zitaleta madhara yepi mwilini?

Lakini kwa kuwa dawa za chanjo zimekwishatua nchini na pamoja na maoni kadhaa yakiwemo niliyowahi kuyatoa huko nyuma kuwa tuwe waangalifu na chanjo hizi cha msingi ni kuanza na wale wananchi ambao wako hoi mahospitalini na wengine ambao wameathirika zaidi.

Kisha kama nilivyowahi kupendekeza huko nyuma ni kwamba serikali itengeneze makundi ya wataochanjwa na kuweka utaratibu kulingana na mahitaji yaani wazee, wale wenye hali tata kiafya na kisha wale wanotaka kusafiri kwenda nchi zingine ambako wanataka msafiri awe amechanjwa dozi mbili.

Nikija kwenye suala la pili kuhusu wanajeshi, watu wa usalama na wengine wenye majukumu mazito ya kuilinda nchi hii, hapa pia Mchungaji Gwajima ana hoja.

Tusishabikie tu kuwa kwa kuwa wanajeshi watachanjwa basi ni sawa, inatubidi kama taifa tuangalie maslahi ya taifa hili, usalama wake na mstakabali wake kwa miaka 5 na kuendelea.

Tujiulize ni kwanini Russia, Iran, Israeli, China na nchi zingine makini kwanini wao wametengeneza chanjo zao?

Vita ya sasa duniani imehamia kwa muda katika madawa, biolojia (bilogical warfare) kutoka kwenye vita ya kukimbilia silaha zingine.

Tukumbuke hakuna silaha mbaya sana kama silaha ya kibaolojia ambayo hukaa mwilini kwa muda mrefu usojulikana.

Hivyo viwanda vya madawa navyo vimeamua kujikita katika sekta hivyo ya vita kwa kushindana kutengeneza dawa za chanjo.

Si kwamba dawa hizi za chanjo hazikuwepo, bali kilichotokea ni kwa wenye viwanda hivi kufanikiwa katika kuomba fedha za ufadhili katika kufanya tafiti zao na suala la UVIKO-29 lilipoingia wote wakahamia huko.

Chanjo zote hizi zinatumia teknolojia maalum ili kuweza kutumwa kwenda mwilini na kukutana na chembechembe za damu, baada ya hapo ni utaratibu wa kubadili chembechembe hizi pamoja na Vinasaba au DNA na kutengeneza kitu kingine.

Hivyo je, baada ya miaka 5 hado 10 ijayo endapo rasilimali watu ya vyombo hivi vya ulinzi na usalama itaathirika Serikali itakuwa imejiandaa vipi maana hakutakuwa na jeshi imara, lenye uwezo wa kuilinda nchi ipasanyo dhidi ya uvamizi wowote wenye nguvu kubwa.

Hivyo haya Mchungaji Gwajima ana hoja asikilizwe na asibezwe kwani yeye anatumia jicho la tatu katika kuangalia na kusoma alama za nyakati.

Sie wengine wote tunapaswa kutafakari maoni kama hayo na kuyatumia katika kutafuta ukweli zaidi

Nimalizie kwa kusema mimi nilipokuwa nasoma sekondari enzi hizo, somo la jiografia lilikuwa ni moja ya masomo niloyapenda sana.

Kuna siku mwalimu alituuliza darasani nini vyanzo vya mmomonyoko wa ardhi na maporoko yake yaani "Landslide".

Lakini usiku wa jana yake palinyesha mvua kubwa sana na tukasikia kuna mifugo kadhaa imebebwa na na kusombwa na maji na kupotea ziwani.

Pia kulikuwepo na katetemeko kadogo ka ardhi yaani (Earth tremor) ambako kalisababisha nyumba kuyumba kidogo kwa muda wa dakika kadhaa.

Asubuhi katika kipindi mwalimu akasimulia juu ya ile "landslide" na vifo vya mifugo, kisha akauliza nini kinasababisha mmomonyiko wa ardhi khasa lile lilotokea usiku?

Mimi kwa kukumbuka ile hali ya usiku nikajibu kuwa moja ni tetemeko, na pili ni mvua kubwa pamoja na shughuli kama ukataji miti na ujenzi.

Mwanafunzi mwingine kajibu kuwa ni kuyeyuka kwa mapande ya barafu au Glaciers.

Mwalimu akatabasamu na kuinua kichwa kuashiria amekubaliana na majibu yote, lakini akamgeukia mwanafunzi mwenzetu na akamwambia" umesema Glaciers lakini hapa hatupo Greenland au Patagonia Pampas"

Akaendelea, "tujaribu sana kutafuta majibu katika mazingira tuliyopo kabla ya kwenda mbali na ng'ambo huko". akamaliza.

Hii sentensi yake sijaweza kuisahamu hadi leo na imenisaidia sana katika kutafuta masuluhisho ndani ya mazingira niliyopo.

Hivyo pamoja na misaada tuipatayo kutoka nje zikiwemo chanjo cha magonjwa kama UVIKO-19 bado tuna budi kama taifa kujiwekea utaratibu kuwa tunajenga maabara za kisasa na vituo vya kufanya utafiti na kuhakikisha tunamwaga fedha humo kutafuta chanjo ya UVIKO- 19 ya Kitanzania.

Kwa njia hiyo tutakuwa tumejitatulia matatizo yetu wenyewe kwa kutumia wataalam wetu wenyewe na rasilimali zetu wenyewe, huko nje tukazane kuomba misaada ya teknolojia.
Wanajua lugha ya kibeberu tusaidieni hii forum inasema?

8B0A3C82-F854-4183-B7DD-E55C7A2FB768.jpeg
 
Hivi ni nani aliyewaroga kiasi cha kushindwa kujua hata uji unaokula kila siku unaweza kukumaliza? Mnashinddwa nini kuelewa kuna watu wallipendana lakini baada ya muda wapenzi hao waka chomeana ndani ya nyumba na kuuana? Nikweli hujawahi kuona mtoto au mzazi akiua mtoto wake? Mbona mnakuwa kama hamko duniani? Matamshi ya Billy Gates na wenzake kuhusu mtumizi ya chanjo kupunguza idadi yawatu duniani hamjayasoma? Mbona yako kila kona? Hivi ninyi ni watu gani kama hamjui habari za new word order? Nini ni watu waina gain msiojua kuna agenda ya kudepopulate dunia ambayo iko dhahiri? Ni nini kifanyike ili muone? Kwa nini mnaishi kwa kukariri matukiio?

Kwa kuw mzugnu hashindwi kukuua , ndipo upeleke shingo yako Kibra?
Mbona mnatoa hoja za watu primitive sana? Hii ni ishara kwmba ujinga bado ni tatizo kubwa hapa tulipo?


Mkuu ili uwe na fikra kama hizi jambo la kwanza unatakiwa huru kifikra.......jambo ambalo waTanzania wengi hawana.....

Yaani hapo mpaka aje kuelewa ni mpaka kiongozi wake wa kisiasa abadili fikra zake ndio na yeye anaji update.......

Kwa lugha nyepesi wanasiasa wametengeneza kizazi cha mazezeta wa fikra.....ndio maana haishangazi kumuona mtu hata tukio la kudai haki yake anangoja kauli ya mwanasiasa.......

Haya mambo yako mbali na fikra za waTanzania kwa kuwa hayajawahi kusemwa na wanasiasa...............
 
Kwanini serikali ikatae kuwajibika kwa usalama wa chanjo wanayodai ni salama kwa asilimia 99.99.....???

Kutatokea nini endapo nitachanjwa ambacho serikali haitawajibika.......??

Na kwanini serikali isiwajibike hali ya kuwa ndio iliyoleta chanjo.....??
20210729_074718.jpg
 
Mnamtukuza tu huyo gwajima.toka alivyomtukana pengo sijawahi muona wa maana na u team tu unaendekezwa TZ.
 
Utangulizi- Nawaomba Mods msihamishe uzi huu.

Mchungaji Josephat Gwajima asimamia maeneo mawili katika hoja yake.

Kwanza, kilichomo kwenye chanjo na pili chanjo dhidi ya wanajeshi na walinda usalama wa nchi.
Mkuu Richard , kwanza asante sana kwa bandiko elimishi, mabandiko kama haya they add value kwa jf and to the society, thanks for this.

Pili hongera kwako binafsi, kutumia muda wako, uwezo wako na elimu yako kuwaelimisha wengine. Ni kupitia bandiko lako hili, mimi ndio nimejua na kuelimika kuhusu batch no. Hivyo maana yake kama Tanzania tumepatiwa hizo chanjo milioni 1, za JJ, ina maana hizo chanjo zitachanja watu 500,000 ili kuepuka kuisha na wengine kulazimika kutumia a different batch.

Suluhisho ni kuepuka chanjo za double jabs ni kutumia chanjo za single jab kama hii ya JJ huku bara, na ile Sputnik ya Urusi inayotumiwa Zanzibar, zote ni single jab, ukichanjwa, umechanja, you are done.

Nikirudi kwa Mchungaji Gwajima, kwa vile yeye ni kiongozi wa umma, ni mbunge kupitia CCM na pia kiongozi wa kiroho kwa waumini wa kanisa lake, hivyo ni mtu mwenye big influence, chochote atakachosema kina big impact, badala ya kupinga chanjo, nafuu akae kimya.

Kitendo cha Mwenyekiti wake, rais Samia kuhamasisha chanjo, halafu yeye kutoa maoni tofauti na kuhamasisha watu wasichanje,ni usaliti
P
 
Mkuu Richard , kwanza asante sana kwa bandiko elimishi, mabandiko kama haya they add value kwa jf and to the society, thanks for this.

Pili hongera kwako binafsi, kutumia muda wako, uwezo wako na elimu yako kuwaelimisha wengine. Ni kupitia bandiko lako hili, mimi ndio nimejua na kuelimika kuhusu batch no. Hivyo maana yake kama Tanzania tumepatiwa hizo chanjo milioni 1, za JJ, ina maana hizo chanjo zitachanja watu 500,000 ili kuepuka kuisha na wengine kulazimika kutumia a different batch.

Suluhisho la double jabs ni kutumia chanjo ya Urusi ya Sputnik ambayo ni single dose, inatumika Zanzibar.

Nikirudi kwa Mchungaji Gwajima, kwa vile yeye ni kiongozi wa umma, ni mbunge kupitia CCM na pia kiongozi wa kiroho kwa waumini wa kanisa lake.

Kitendo cha Mwenyekiti wake, rais Samia kuhamasisha chanjo, halafu yeye kutoa maoni tofauti na kuhamasisha watu wasichanje,ni usaliti
P
Kwahiyo avue ubongo kama nguo, auweke chini ili asiwe msaliti?
 
Hivi ni nani aliyewaroga kiasi cha kushindwa kujua hata uji unaokula kila siku unaweza kukumaliza? Mnashinddwa nini kuelewa kuna watu wallipendana lakini baada ya muda wapenzi hao waka chomeana ndani ya nyumba na kuuana? Nikweli hujawahi kuona mtoto au mzazi akiua mtoto wake? Mbona mnakuwa kama hamko duniani? Matamshi ya Billy Gates na wenzake kuhusu mtumizi ya chanjo kupunguza idadi yawatu duniani hamjayasoma? Mbona yako kila kona? Hivi ninyi ni watu gani kama hamjui habari za new word order? Nini ni watu waina gain msiojua kuna agenda ya kudepopulate dunia ambayo iko dhahiri? Ni nini kifanyike ili muone? Kwa nini mnaishi kwa kukariri matukiio?

Kwa kuw mzugnu hashindwi kukuua , ndipo upeleke shingo yako Kibra?
Mbona mnatoa hoja za watu primitive sana? Hii ni ishara kwmba ujinga bado ni tatizo kubwa hapa tulipo?
Wasabato masalia mnatabu sana,endeleeni kusubiri pasi zakusafiria kwa maombi muende ulaya.
Sasa mwendazake kilichomuua ni chanjo ama korona?
 
Siku Gwaji boy atakapo hitaj kwenda ktk makanisa ya nje ya nchi ndionatajua chanjo inadhuru DNA au lagasha
 
Utangulizi- Nawaomba Mods msihamishe uzi huu.

Mchungaji Josephat Gwajima asimamia maeneo mawili katika hoja yake.

Kwanza, kilichomo kwenye chanjo na pili chanjo dhidi ya wanajeshi na walinda usalama wa nchi.

La kwanza kuhusu kilichomo kwenye chanjo au (content).

Mchungaji Gwajima anadai ni lazima madaktari wajiridhishe kuwa kilichomo katika chanjo nyingi zilizowasili Tanzania jana ni sawa na kilichomo katika chanjo walopewa raia wa nchi zilizoendelea.

Itakumbukwa kuwa mapema mwaka huu nchi nyingi zilizoendelea zilipokea idadi kubwa ya chanjo za Covid-19 na kufikia mwezi Juni mwaka huu Marekani pamoja na Uingereza zikaanza kusema kuwa zitapeleka dawa zilizobakia katika nchi maskini.

Ahadi hiyo ilitolewa na Raisi Biden na Boris Johnson wa Uingereza katika mkutano wa nchi tajiri 7 au G7 ulofanyikia katika mji wa Cornwall nchini Uingereza.

Covid vaccine: UK and US to give leftover doses to poorer countries kupitia BBC Covid vaccine: UK and US to give leftover doses to poorer countries - CBBC Newsround

Lakini siku moja kabla ya mkutano huo raisi Biden aliahidi kutoa msaada wa dawa za chanjo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 500-

US to donate 500 million Pfizer COVID-19 vaccine doses globally: Report- US to donate 500 million Pfizer COVID-19 vaccine doses globally: Report

Sasa tukirudi katika hoja ya mchungaji Gwajima kwamba lazima tuangazie kilichomo (Content) katika chanjo hizo zote ni ya kuzingatiwa.

Wenzetu wazungu wao walikwishajipanga vilivyo katika suala zima la kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO -19 na kwa muktadha huo waliweza kutengeneza vipeperushi na vielelezo vingine ambavyo zinalenga kumuelimisha mchanjwaji mtarajiwa kuwa ni aina ipi ya chanjo anaweza kupata, imetengenezwa vipi kwa kutumia nini, na inabeba vitu gani na kisha madhara yake baada ya kudungwa au "side effects"

Hivyo taarifa zoote kuhusu UVIKO-19 zimo katika tovuti za serikali za nchi zote zilizoendelea na mtu aweza kusoma na kuelewa bila shida.

Serikali ya Tanzania ingeweza kabisa kufanya hili ilipokuwa ikijiandaa kupokea chanjo na kuondoa uwezekano wa mijadala ambayo yaonekana wazi kuwa haiwezi kuzuia utekelezaji wa kudunga watanzania chanjo hizo.

Sasa hizo chanjo zina namba maalum au bechi au kwa kiingereza batch number hivyo pfizer yaweza kuitwa BNT163C1 au 161C2 na kadhalika.

Hizi namba zinatofautina na ukiwa umedungwa BNT163C1 basi ni lazima uje udungwe dozi ya pili ambayo ni kutoka katika bechi hiyohiyo yaani yaweza kuwa BNT163C3 lakini haiwezi kuwa BNT200b1 ambayo yaweza kuwa ndo inoleta madhara kama kuganda kwa damu.

Ni hivyohivyo kwa chanjo za Moderna, Johnson &Johnson na Moderna ambazo pia zinatumia bechi tofauti.

Moderna inayoyumika kwa mtu A yenye bechi namba 3001729 ndo hiyohiyo itayotumika kwa mtu huyohuyo A lakini itafuatia kidogo na kuwa 3001830.

Mtu anechanjwa Pfiser BioNTech ni lazima achanjwe dozi hiyohiyo ya chanjo hiyohiyo.

Nchi kadhaa za Ulaya na Marekani wakiangalia namba ya bechi ambayo msafiri amechomwa kuna ambao wanakataliwa kuingia katika nchi hizo kwa kuwa amechomwa chanjo ambayo ni ya kutoka kwenye bechi ambayo ina matatizo ya kuleta kuganda kwa damu na homa kali isokwisha.

Katika chanjo zote chanjo ya Oxford Astra Zeneca ndo chanjo ambao haihitaji baridi kali kuitunza hivyo kuifanya iwe rahisi kuihifadhi katika jokovu la kawaida kama yale ya majumbani.

Chanjo zingine zote huitaji majokovu maalum ambayo pia ni lazima yawe katika mazingira ya kutoweza kuvurugwa na waswahili au kuwa "compromised".

Hivyo hapa nina imani pia kuwa Serikali imewekeza vilivyo katika idara ya uhifadhi na ugavi wa chanjo hizi na hakutakuwa na dalili za kuzivuruga chanjo hizo.

Sasa basi, mchungaji Gwajima anadai ni lazima tujiridhishe kuwa dawa hizi za chanjo zina kiwango kilichomo (content) sawa na chanjo walochomwa wazungu huko Ulaya na Marekani.

Kwenye hili ana hoja kwani hatufahamu dawa hizi za chanjo zimepitia wapi, zimehifadhiwa vipi, zitabadilika vipi kiubora (yaani quality) na je zitaleta madhara yepi mwilini?

Lakini kwa kuwa dawa za chanjo zimekwishatua nchini na pamoja na maoni kadhaa yakiwemo niliyowahi kuyatoa huko nyuma kuwa tuwe waangalifu na chanjo hizi cha msingi ni kuanza na wale wananchi ambao wako hoi mahospitalini na wengine ambao wameathirika zaidi.

Kisha kama nilivyowahi kupendekeza huko nyuma ni kwamba serikali itengeneze makundi ya wataochanjwa na kuweka utaratibu kulingana na mahitaji yaani wazee, wale wenye hali tata kiafya na kisha wale wanotaka kusafiri kwenda nchi zingine ambako wanataka msafiri awe amechanjwa dozi mbili.

Nikija kwenye suala la pili kuhusu wanajeshi, watu wa usalama na wengine wenye majukumu mazito ya kuilinda nchi hii, hapa pia Mchungaji Gwajima ana hoja.

Tusishabikie tu kuwa kwa kuwa wanajeshi watachanjwa basi ni sawa, inatubidi kama taifa tuangalie maslahi ya taifa hili, usalama wake na mstakabali wake kwa miaka 5 na kuendelea.

Tujiulize ni kwanini Russia, Iran, Israeli, China na nchi zingine makini kwanini wao wametengeneza chanjo zao?

Vita ya sasa duniani imehamia kwa muda katika madawa, biolojia (bilogical warfare) kutoka kwenye vita ya kukimbilia silaha zingine.

Tukumbuke hakuna silaha mbaya sana kama silaha ya kibaolojia ambayo hukaa mwilini kwa muda mrefu usojulikana.

Hivyo viwanda vya madawa navyo vimeamua kujikita katika sekta hivyo ya vita kwa kushindana kutengeneza dawa za chanjo.

Si kwamba dawa hizi za chanjo hazikuwepo, bali kilichotokea ni kwa wenye viwanda hivi kufanikiwa katika kuomba fedha za ufadhili katika kufanya tafiti zao na suala la UVIKO-29 lilipoingia wote wakahamia huko.

Chanjo zote hizi zinatumia teknolojia maalum ili kuweza kutumwa kwenda mwilini na kukutana na chembechembe za damu, baada ya hapo ni utaratibu wa kubadili chembechembe hizi pamoja na Vinasaba au DNA na kutengeneza kitu kingine.

Hivyo je, baada ya miaka 5 hado 10 ijayo endapo rasilimali watu ya vyombo hivi vya ulinzi na usalama itaathirika Serikali itakuwa imejiandaa vipi maana hakutakuwa na jeshi imara, lenye uwezo wa kuilinda nchi ipasanyo dhidi ya uvamizi wowote wenye nguvu kubwa.

Hivyo haya Mchungaji Gwajima ana hoja asikilizwe na asibezwe kwani yeye anatumia jicho la tatu katika kuangalia na kusoma alama za nyakati.

Sie wengine wote tunapaswa kutafakari maoni kama hayo na kuyatumia katika kutafuta ukweli zaidi

Nimalizie kwa kusema mimi nilipokuwa nasoma sekondari enzi hizo, somo la jiografia lilikuwa ni moja ya masomo niloyapenda sana.

Kuna siku mwalimu alituuliza darasani nini vyanzo vya mmomonyoko wa ardhi na maporoko yake yaani "Landslide".

Lakini usiku wa jana yake palinyesha mvua kubwa sana na tukasikia kuna mifugo kadhaa imebebwa na na kusombwa na maji na kupotea ziwani.

Pia kulikuwepo na katetemeko kadogo ka ardhi yaani (Earth tremor) ambako kalisababisha nyumba kuyumba kidogo kwa muda wa dakika kadhaa.

Asubuhi katika kipindi mwalimu akasimulia juu ya ile "landslide" na vifo vya mifugo, kisha akauliza nini kinasababisha mmomonyiko wa ardhi khasa lile lilotokea usiku?

Mimi kwa kukumbuka ile hali ya usiku nikajibu kuwa moja ni tetemeko, na pili ni mvua kubwa pamoja na shughuli kama ukataji miti na ujenzi.

Mwanafunzi mwingine kajibu kuwa ni kuyeyuka kwa mapande ya barafu au Glaciers.

Mwalimu akatabasamu na kuinua kichwa kuashiria amekubaliana na majibu yote, lakini akamgeukia mwanafunzi mwenzetu na akamwambia" umesema Glaciers lakini hapa hatupo Greenland au Patagonia Pampas"

Akaendelea, "tujaribu sana kutafuta majibu katika mazingira tuliyopo kabla ya kwenda mbali na ng'ambo huko". akamaliza.

Hii sentensi yake sijaweza kuisahamu hadi leo na imenisaidia sana katika kutafuta masuluhisho ndani ya mazingira niliyopo.

Hivyo pamoja na misaada tuipatayo kutoka nje zikiwemo chanjo cha magonjwa kama UVIKO-19 bado tuna budi kama taifa kujiwekea utaratibu kuwa tunajenga maabara za kisasa na vituo vya kufanya utafiti na kuhakikisha tunamwaga fedha humo kutafuta chanjo ya UVIKO- 19 ya Kitanzania.

Kwa njia hiyo tutakuwa tumejitatulia matatizo yetu wenyewe kwa kutumia wataalam wetu wenyewe na rasilimali zetu wenyewe, huko nje tukazane kuomba misaada ya teknolojia.
Gwajima ni wa kupuuza, hajui chochote kuhusu sayansi, muongo na elimu yake ya kuunga unga , tena ya dini yake.
Swali la msingi je Corona virus vaccine inabidili DNA ya mtu?
Jibu HAPANA.
Chanjo ya corona haina muingiliano wowote katika utendaji wake kazi na DNA. Ikutoshe tu wewe msomaji kujuwa kuwa, vinasaba vya chanjo (viral vector COVID-19) na mesenja RNA za mwili ( mRNA) hutuma maelekezo (genetic material) kwa seli za mwili zianze kutengeneza mfumo wa kujilinda dhidi ya virusi vinavosababisha COVID-19.
SASA HAPA PIGIA MSTARI.
HATA HIVYO MADAWA NA KEMIKALI HIZO KAMWE HAZIINGII NDANI YA NUKILIA YA SELI, SEHEMU AMBAYO NDIO DNA HUPATIKANA.
Biology ya O level hapa inahusika sasa kujua seli ya mwanadamu na sehem zake, wapi inapatikana mRNA, tRNA, Ribosome, mitochondria na Nucleus.
Huhitaji shahada ya virology kujua kuwa vinasaba chanjo( viral vector COVID-19) havina muingiliano wala kamwe haviwezi athiri DNA ambayo inapatikana ndani ya nukilia ya seli. Hazipenyi kwenye nukilia kuta mbili za ukuta wa nukilia.
Source kwa hisani ya taasisi ya kudhibiti na kuzuia maradhi ya Marekani.
(COVID-19 Vaccine Facts)
 
Utangulizi- Nawaomba Mods msihamishe uzi huu.
Mchungaji Josephat Gwajima asimamia maeneo mawili katika hoja yake.
Gwajima yupi anaongelewa hapa? Kama ni huyu hapa chini sina la kuongeza...



Hapa ndipo unapojua Watanzania ni viumbe wa pekee duniani. Richard, huu utafiti wako wote umeupata kwa kuungaunga vyanzo vya huko huko Marekani na kwingineko ambako wapo watu aina yako tena si wachache, ni wengi.

Laiti ungejua kuwa original vaccine deniers ndio wale wale waliokuwa original covid-19 deniers. Je unajua kitu gani kinawatokea hivi sasa? Wanapigana vikumbo kuwahi chanjo kwa sababu Covid-19 ikiwapigia hodi hakuna tena cha mswalie mtume.

Yeye Gwajima, askofu na mbunge, tapeli wa kidini na kisiasa, shetani katika umbo la binadam, kibwetere wa nyakati hizi ataondoka na wengi tu. Ajabu mwendakuzimu aliposalimu amri kwa corona, baunsa alijifungia asije akapewa tenda ya kumfufua!
 
Kwa maana hiyo ni sawa tu kopokea chochote tunachopewa, siyo?
Mtapokea tu hakuna namna!
Hio simu inayokutia kiburi wamekutengenezea wazungu unaosema wanataka kukuua!
Ngozi nyeusi tatizo sana,yani teknolojia pekee unayoitegemea kupambana na korona ni nyungu then unaleta kibesi.
 
Gwajima yupi anaongelewa hapa? Kama ni huyu hapa chini sina la kuongeza...

View attachment 1873155

Hapa ndipo unapojua Watanzania ni viumbe wa pekee duniani. Richard, huu utafiti wako wote umeupata kwa kuungaunga vyanzo vya huko huko Marekani na kwingineko ambako wapo watu aina yako tena si wachache, ni wengi.

Laiti ungejua kuwa original vaccine deniers ndio wale wale waliokuwa original covid-19 deniers. Je unajua kitu gani kinawatokea hivi sasa? Wanapigana vikumbo kuwahi chanjo kwa sababu Covid-19 ikiwapigia hodi hakuna tena cha mswalie mtume.

Yeye Gwajima, askofu na mbunge, tapeli wa kidini na kisiasa, shetani katika umbo la binadam, kibwetere wa nyakati hizi ataondoka na wengi tu. Ajabu mwendakuzimu aliposalimu amri kwa corona, baunsa alijifungia asije akapewa tenda ya kumfufua!
Don't insult my intelligence.

When you insult someone intelligence is when you tell them how to think and say things.

Waweza kuona nimeweka mifano hai ndani ya mada yangu wapi shida?

Hata ufanyapo utafiti si waweka references?

Na hiki ndicho kinachoendelea kwa waafrika kwa ujumla hawana "independent mind" kufikiria nje ya boksi, I repeat we are vulnerable na tunatumiwa kwa udhaifu huo, period.

Tuna wasomi wengi tu nchini lakini wawapi leo hii tupo katika shida ya ugonjwa? Weye wagonjea dawa ya chanjo kutoka nje, kisha wajisifu umesoma?

Sifahamu kiwango cha elimu yako na weye hiyo twaweza kuwa level moja au nimekuzidi au umenizidi who knows.

Mchungaji Gwajima na haki ya kutoa maoni/ fikra na mtazamo wake.

Mind you, mimi si mfuasi wa Mheshimiwa Gwajima, wala si mfuasi wa chama chochote, niliondoka kuwa mfuasi wa vyama na nikahamia kuwa mfuasi wa serikali itayojaribu kuwa na nguvu lakini fair katika maamuzi yake na utendaji wake wa kazi.

Wasema nimeungaunga jaribu kukubali kuwa nimefanya utafiti na kuna ambao wamenikubali maoni yangu, sidhani kama mtizamo wako ni upi.

Serikali ni lazima iwe na "Scientific advisory board" ambayo inampa brief mheshimiwa raisi ya kila kinachoendelea nchini.

Hivi nikuulize kamati iloundwa kumshauri raisi juu ya UVIKO-19 hadi leo imetoa taarifa yoyote baada ya ile ya kushauri watu wachanjwe?

Sisi tumsikilize tu kama tuwezavyo kuwasikiliza wengine.

Naamini tumechelewa kama taifa na ni jukumu la serikali kuhakikisha yajiandaa kutengeneza dawa ya chanjo ya kitanzania.

Dunia sasa imebadilika kila mtu ana uwezo wa kufikiri kwa makini na kwenda ndani zaidi.

Hizi si zama za kufuata upepo tu.

Huu ndio ushauri wangu.
 
Ana haki ya kutoa maoni/ fikra na mtazamao wake.

Sisi tumsikilize tu kama tuwezavyo kuwasikiliza wengine.

Dunia sasa imebadilika kila mtu ana uwezo wa kufikiri kwa makini na kwenda ndani zaidi.

Hizi si zama za kufuata upepo tu.

Huu ndio ushauri wangu.
Kwa hiyo nawe unaamini baunsa anafufua watu waliokufa au siyo. Kama ni hivyo basi usiwe na wasi wasi, Covid-19 ikikupigia hodi tapeli Gwajima yupo, atakufufua ila sijui alishindwaje kumfufua yule dhalimu mwendakuzimu. Na mimi huo ndio ushauri wangu.

Swali kwako: Je Mbowe na wenzake nao wana hiyo haki ya kutoa maoni/fikra na mtizamo wao?
 
Kwa hiyo nawe unaamini baunsa anafufua watu waliokufa au siyo. Kama ni hivyo basi usiwe na wasi wasi, Covid-19 ikikupigia hodi tapeli Gwajima yupo, atakufufua ila sijui alishindwaje kumfufua yule dhalimu mwendakuzimu. Na mimi huo ndio ushauri wangu.

Swali kwako: Je Mbowe na wenzake nao wana hiyo haki ya kutoa maoni/fikra na mtizamo wao?
Nimeshauri mara nyingi humu kuwa Mbowe abadili strategy na haijawa hivyo miaka nenda rudi.

Kisha awe na strategists kumsaidia.

Siasa ni sayansi na yahitaji pia kusoma alama za nyakati kama kweli kuna nia thabiti ya kukiondoa chama kilichoshika dola kwa miongo kadhaa.

Vinginevyo kila anachofanya hata kama kina nia thabiti kinaonekana si sawa na anakumbana na madhila ya vyombo vya dola.
 
Back
Top Bottom