#COVID19 Tumsikilize mchungaji Gwajima, tusimbeze. Chanjo zote zina bechi tofauti na kuna nchi hukataa baadhi ya bechi na nyingine ni zile zilizobakia

Dunia ya leo ukiwa na opinion tofauti na wakubwa wewe ni uahini.
Ndiyo mana dawa za asili kipindi kile zilifanya kazi lakini hupati kumbukumbu kwamba zilifaa.

Turudi Tanzania, tena juzi tu, 2020! Juhudi za uongozi wa serikali kipindi hicho zilipelekea watu kutumia matunda na dawa za asili(kufukiza, tangawizi, etc) mbinu za kuondoa woga na tukaishinda korona! Lakini cha ajabu tusivyo na akili tumesahau kabisa kwamba ni jana tu tulivushwa kwenye janga hili hili!

Nchi jirani walifuata WHO protocals lakini korona iliwapelekesha sana tofauti na Tz tuliofuata Magufuli protocals .

Siyo bure akili zetu zilishachezewa uhenda kupitia chanjo kama ndui au vyakula vya GM nk
Hakuna mtu aliekataza kutumia dawa asili wala kula matumda na limau na vyote mnavyotaka.
Kuhusu kuwa magufuri aliiweza corona kwa dawa asili,haya ni madai yasio na ushahid,sababu huwezi kusema dawa asili zilisaidia wakati hakukua na uthibitisho uo,watu walikuwa hawapimwi na taarifa za corona hazikuruhusiwa kuandikwa,sasa utajuaje kama dawa zilisaidia bila kupima.
Chukua tahadhari corona inaua.
 
Back
Top Bottom