Tumsaidieje mhindi huyu?

laurent Msembeyu

Senior Member
Oct 5, 2015
121
101
Anatoka India, Yuko Mtwara , alikuja mwaka 2009 akaomba kibali mali ya asili cha kukamata nyoka aina zote,akapewa kibali mali ya asili akamate manyoka idadi yoyote anayotaka maeneo ya kijiji cha Imekuwa na vijiji vya jilani muda kidogo tu alijaza mzigo akaondoka.

Kaja tena kakuta mambo yamebadilika maafisa mali ya asili wanamwogopa hata kuzungumza nae wanamwambia afuate taratibu zilizopo, taratibu hizo hazijui.

Anasema kwao India hakuna nyoka anayezubaa kila nyoka ni mwa mtu labda wale wa national park.

Wanawatumia nyoka hao kutengeneza dawa mbali mbali kwenye viwanda vya dawa.

Safari hii anatafuta zaidi Koboko, anasema koboko na ukali wake anamkamata kama vile anachuma mchicha, tatizo ni kibali tu.

Mytake.

Sasa ivi tukataza mtu asichukue manyoka tutayafanyia nini? Hao mali ya asili wanaomkwepe mhindi kawaomba kibali wao manyoka watayafanyia kazi gani?

Tumsaidieje mhindi huyu atupunguzie manyoka hasa makoboko ya sikonge Tabora?
 
Kibali cha kwanza aliombaje akapata mpaka sasa ishindikane kwa kisingizio cha kutojua taratibu?
Ni hivi nyakati zile shortcut zilikuwa nyingi na formalities nyingi hazikufuatwa watu walichepuka mno
Sasa kwa hali ilivyo hakidhi vigezo ajiondokee tu aende hata Congo kuna mijoka concord huko atayapata kwa matani
 
Wewe jamaa kichwa chako kinafikiri kwa njia gani??
Yaani aachiwe abebe tu hayo majoka kwasababu wewe hujui yanakazi gani??
Hivi wale tumbiri waliokamatwa airport unadhani wana kazi gani???
Wewe unadhani huyo Mhindi anawachukua kwasababu gani???
Yeye kaambiwa afuate taratibu zilizopo wewe unataka umsaidieje zaidi ya hapo??
 
Kibali cha kwanza aliombaje akapata mpaka sasa ishindikane kwa kisingizio cha kutojua taratibu?
Ni hivi nyakati zile shortcut zilikuwa nyingi na formalities nyingi hazikufuatwa watu walichepuka mno
Sasa kwa hali ilivyo hakidhi vigezo ajiondokee tu aende hata Congo kuna mijoka concord huko atayapata kwa matani
Umesema kweli yaani kuntu.
 
Nilishangaa Pia Wale Waliomkamata Sijui Mzungu Au Mwarabu, Alikuwa Kajibebea Ngedere Wake Kuwapeleka Nje. Hawa Ngedere Tunaofukuzana Nao Njiani
 
Duu umenikumbusha kile kiwanda nimekaa pale miezi miwili tukila ile nyama milo mitatu kwa siku
Halafu watu wanasema inaenda China yote wakati mabaki kama makongoro, vichwa na matumbo watu wanachemsha supu hapo hapo Dom na kuinywa vizuri tu na wateja kibao!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom