Tumpongeze rais Magufuli

JINOME

JF-Expert Member
May 29, 2017
958
1,424
Sheria ya Madini ilimpa mandatory Waziri husika na Mwanasheria Mkuu ku sign mikataba ya kuchimba bila kupitishwa na Bunge wala kumshirikisha Rais.

NAMPONGEZA JPM KWA KUFANYA YAFUATAYO:-
1.Kuanzia sasa mikataba yote ya madini ikafanyiwe review Bungeni.
2.Mawaziri na Wanasheria wote walio husika na mikataba hii wachunguzwe na kupelekwa Mahakamani kwa hatua stahiki.
3.Kuzuia Makanikia mpaka itakapo jengwa melting point Tanzania na kusimamia Madini yote machimboni ili kujua kiasi cha Madini kinacho ondoka,pia kulipwa kwa kodi na tozo zote stahiki.
4.Kuhakikisha transactions zote zinafanyika Tz ili kuinua uchumi na kukuza dhamani ya Tsh.
5.Kuhakikisha uchakachuaji wa Makanikia unafanyika Nchini.
6.Wawekezaji kusomesha watz ili migodi yote kwa 100% iajiri watz.
Kuhakikisha Kampuni zote zinaingia kwenye soko la hisa la Dar es salaam.

Pamoja na mengine meeeengi,kwa nini wewe Mtanzania hata Mwanachama wa Chama cha upinzani unasita kutoa sifa kwa Mh Rais?
Tukumbuke JPM anayafanya haya yote sio kwa ajili ya wana CCM,nikwaajili ya Watanzania wote,Hospitali zetu ziwe na Madawa ya kutosha,Watoto wetu wasome vizuri na kuongeza mzunguko wa fedha Nchini.

#SEMA_NENO_MOJA_KUMPONGEZA_JPM.

#TANZANIA_KWANZA_VYAMA_BAADAE

Maxi.J.Luhanga.
 
Back
Top Bottom