Elections 2010 Tumpe pole Mheshimiwa JK, tumwombe aachie urais hana cha kupoteza

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Binadamu wenye ubinadamu tunasikitika sana na kumpa pole JK kwa kuanguka jukwaani akiwa kwenye kazi za chama. Tunamtakia afya njema rais. Hali hii imemtokea JK mara nyingi akiwa kwenye kazi za siasa. Tunaona uhusiano wa kazi anazofanya sasa za kisiasa na kuanguka kwake. Tunaona ni jambo la busara kwa JK kuacha siasa za jukwaani kabisa kwa vile afya na uzima ni muhimu zaidi kuliko madaraka au mali. Tunaomba JK aache siasa ili atunze afya yake. Akifanya hilo hana cha kupoteza bali ataitunza afya yake kwa manufaa yake, familia yake n.k. Hana cha kupoteza kwa vile atatunza heshima kwa kukubaliana na hali ya afya yake. Hana cha kupoteza kwa sababu atawaacha watanzania katika mikono salama ya urais wa Dr. Slaa. Na atakuwa ameacha historia ya pekee kwa kuacha demokrasia ichukue mkondo wake kwa kukubali chama mbadala cha Chadema kuongoza Tanzania.
 
Hivi inawezekana kumpinga mahakamani kwamba asigombee Urais kutokana na hali yake ya afya? Mtikila yuko wapi Jamani? Kama kuna mwenye contact za Mtikila aniPM. Nafikiri kuna haja ya kwenda mahakamani kupinga JK kugombea Urais kwa kuwa kuna ushahidi tosha kwamba afya yake ni mgogoro. Asije siku nyingine akaanguka kwenye mkutano wa UN ikawa ni changamoto kwa Taifa.
 
Hivi inawezekana kumpinga mahakamani kwamba asigombee Urais kutokana na hali yake ya afya? Mtikila yuko wapi Jamani? Kama kuna mwenye contact za Mtikila aniPM. Nafikiri kuna haja ya kwenda mahakamani kupinga JK kugombea Urais kwa kuwa kuna ushahidi tosha kwamba afya yake ni mgogoro. Asije siku nyingine akaanguka kwenye mkutano wa UN ikawa ni changamoto kwa Taifa.

Siyo lazima kufanya hivyo. Ni kumuomba apime uzito wa kutunza afya yake. Hali inaonyesha kuwa kazi za siasa zinamharibia afya yake. Yeye ni mtu mzima, tukimwomba watanzania ataacha urais kwa hiari yake.
 
Hivi inawezekana kumpinga mahakamani kwamba asigombee Urais kutokana na hali yake ya afya? Mtikila yuko wapi Jamani? Kama kuna mwenye contact za Mtikila aniPM. Nafikiri kuna haja ya kwenda mahakamani kupinga JK kugombea Urais kwa kuwa kuna ushahidi tosha kwamba afya yake ni mgogoro. Asije siku nyingine akaanguka kwenye mkutano wa UN ikawa ni changamoto kwa Taifa.

Lukolo Ndeti???
Huna habari kuwa kuna kesi tayari mahakamani ya kumzuia kugombea urais iliyofunguliwa na mtanzania mmoja mwalimu nani sijui, kwa hiyo kwa kesi kama hii sio mtikila mtafute huyo mwalimu ambaye ameshamfungulia kesi ya kumzuia kwa sababu za kutumia vibaya pesa za umma akiwa rais kipindi cha kwanza.
 
Hivi inawezekana kumpinga mahakamani kwamba asigombee Urais kutokana na hali yake ya afya? Mtikila yuko wapi Jamani? Kama kuna mwenye contact za Mtikila aniPM. Nafikiri kuna haja ya kwenda mahakamani kupinga JK kugombea Urais kwa kuwa kuna ushahidi tosha kwamba afya yake ni mgogoro. Asije siku nyingine akaanguka kwenye mkutano wa UN ikawa ni changamoto kwa Taifa.

======
Mimi nadhani kuna kifungu cha katiba kinachomtaka Rais awe na afya nzuri kiakili (Mental health). Huku kuzimika zimika ni aina fulani ya magonjwa ya akili, yaani kunagusa mental part of him ndiyo maana kuna wanaosema ana shida ya nerve fulani katika nerves za fahamu.
Kwa maana hiyo, capacity yake ya kufanya kazi iko limited (no offense intended please). Ama kwa njia ya mahakama au heskima, zinahitajika juhudi za kufanya kitu fulani kuokoa afya yake na ya taifa. Anaweza kesho na keshokutwa akapitisha maamuzi fulani yakakataliwa kwa kutumia ushahidi huu wa kuzimia zimia.
 
Lukolo Ndeti???
Huna habari kuwa kuna kesi tayari mahakamani ya kumzuia kugombea urais iliyofunguliwa na mtanzania mmoja mwalimu nani sijui, kwa hiyo kwa kesi kama hii sio mtikila mtafute huyo mwalimu ambaye ameshamfungulia kesi ya kumzuia kwa sababu za kutumia vibaya pesa za umma akiwa rais kipindi cha kwanza.
Be mdimi Mbogela, hiyo kesi ya huyo Mwalimu ni tofauti na hii. Kwa hiyo kama watu kadhaa watafungua kesi ya kumpinga kwa sababu tofauti tofauti, naamini hata mahakama itazipa uzito hizo kesi. Kwanza yule Mwalimu mbona nasikia kesi aliyofungua imefutwa kwa kukosa ushahidi? sasa hii tuna ushahidi kabisa kwamba ameanguka mara tatu tena mbele ya hadhira. Hatujua ameanguka mara ngapi akiwa Ikulu au safarini huko nje ya nchi anakokwenda kila siku. Kwa hiyo hii kesi itakuwa na nguvu ukilinganisha na ile ya Mwalimu.
Kwanza ashauriwe aachie ngazi, na iwapo hatataka kufanya hivyo basi aweke pingamizi mahakamani.
 
Kama kweli watanzania na wana - CCM wanampenda sana basi ni busara kumpumzisha kwa kutomchagua - la sivyo yale ya Nigeria yatatukuta hapa TZ in the near future!
 
Unaota mchana....Dr Slaa na CHADEMA wataingia Ikulu kwa nguvu na jitihada zao sio kutegemea kuachiwa, that is not true democracy..afterall Kikwete is not the only person that can lead CCM
 
Lukolo Ndeti???
Huna habari kuwa kuna kesi tayari mahakamani ya kumzuia kugombea urais iliyofunguliwa na mtanzania mmoja mwalimu nani sijui, kwa hiyo kwa kesi kama hii sio mtikila mtafute huyo mwalimu ambaye ameshamfungulia kesi ya kumzuia kwa sababu za kutumia vibaya pesa za umma akiwa rais kipindi cha kwanza.

Hiyo ya mwalimu imeshakataliwa na mwendesha mashitaka
 
Slaa nae kudondoka kama kawa.
Binadamu wenye ubinadamu tunasikitika sana na kumpa pole JK kwa kuanguka jukwaani akiwa kwenye kazi za chama. Tunamtakia afya njema rais. Hali hii imemtokea JK mara nyingi akiwa kwenye kazi za siasa. Tunaona uhusiano wa kazi anazofanya sasa za kisiasa na kuanguka kwake. Tunaona ni jambo la busara kwa JK kuacha siasa za jukwaani kabisa kwa vile afya na uzima ni muhimu zaidi kuliko madaraka au mali. Tunaomba JK aache siasa ili atunze afya yake. Akifanya hilo hana cha kupoteza bali ataitunza afya yake kwa manufaa yake, familia yake n.k. Hana cha kupoteza kwa vile atatunza heshima kwa kukubaliana na hali ya afya yake. Hana cha kupoteza kwa sababu atawaacha watanzania katika mikono salama ya urais wa Dr. Slaa. Na atakuwa ameacha historia ya pekee kwa kuacha demokrasia ichukue mkondo wake kwa kukubali chama mbadala cha Chadema kuongoza Tanzania.
 
Slaa nae kudondoka kama kawa.

Tunajua watu wanafaidika na urais wa JK. Lakini ni vizuri wawe na ubinadamu, wasimtumie bila huruma kwa tamaa za mali hadi iwe kama Michel Jackson ambaye alitumika na watu bila kujali afya yake hadi akapoteza uhai wake.
 
Back
Top Bottom