Masulupwete
JF-Expert Member
- Feb 15, 2012
- 2,366
- 2,397
Serikali ilionekana kuridhia kirahisi sana mapendekzo ya waheshimiwa kuongezewa posho pale mjengoni. Bila shaka waheshimiwa walifanya hivyo wakiamini hakuna atayeleta 'zengwe' pengine wakiamini kwa kuwa wao ndo kila kitu. Madaktari wamewaprove wrong! Kwani waheshimiwa si binadamu nao? na wao si wanahudhuria hospitali kama binadamu wengine?
Ombi la madaktari limeleta shubiri kwa serikali na kwa wananchi kwa ujumla. Nakumbuka kuna wadau walitoa hadhari juu ya hatua ya serikali kukubali maombi ya waheshimiwa kuwa ingechochea makundi mengine kudai maslahi yao pia. Serikali haikuwa tayari kusikiliza ndoto hizi.
Na sasa hali ndo hiyo, jamaa wanakusudia kurejea kwenye mgomo kwa mara nyingine tena...hivi kwa hali hii ni nani wa kulaumiwa....Serikali, Madaktari au Waheshimiwa?
Ombi la madaktari limeleta shubiri kwa serikali na kwa wananchi kwa ujumla. Nakumbuka kuna wadau walitoa hadhari juu ya hatua ya serikali kukubali maombi ya waheshimiwa kuwa ingechochea makundi mengine kudai maslahi yao pia. Serikali haikuwa tayari kusikiliza ndoto hizi.
Na sasa hali ndo hiyo, jamaa wanakusudia kurejea kwenye mgomo kwa mara nyingine tena...hivi kwa hali hii ni nani wa kulaumiwa....Serikali, Madaktari au Waheshimiwa?