Tumia watu wakutengenezee pesa

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,270
40,085
Tuanze na mtaji mdogo tu, labda una shilingi laki 5 na hujui ufanyie shughuli gani; fanya yafuatayo:-
  • Nenda sokoni, na utafute wamama watu wazima watano wenye vibanda; ambao ni wapambanaji
  • Tathmini utokaji wa biashara zao, kama unaridhisha nenda hatua inayofuata
  • Hakikisha hawa wamama hawajuani, ikiwezekana kuwepo na umbali fulani kati ya kibanda cha mama mmoja mpaka mwingine.
  • Ingia nao makubaliano, ya wewe kuwekeza kiasi cha laki moja kwa kila mmoja; na ikiwezekana kila jioni uwe unapita kwa ajili ya kupata mgao, baada ya mauzo.
  • Ukiona biashara inaenda vizuri na uaminifu uko vizuri; ongeza mtaji.
  • Kama inazidi kulipa zaidi, ongeza wamama wengine tena na tena.
  • Nenda kwenye masoko mengine tena na tena, wilaya kwa wilaya, mkoa kwa mkoa
  • Baada ya mafanikio kuwa mazuri sajili biashara yako kama micro-finance
  • Jipigie makofi kwa kuwa CEO aliyejiajiri
 
Ni wazo zuri ila kama tu utawapata watu waaminifu vinginevyo unaweza kubaki unalia.
Ni kuwa makini katika kuchagua timu yako (pa kuwekeza), ndio maana mabenki hutaka vielelezo vingi kujihakikishia usalama wa fedha wanazokukopesha
 
Ulishawahi kuwa afisa mikopo (mikopo ya vikundi vya akina mama) ? Wao mfumo unao wafaa Ni vikundi zaidi kuliko mmoja mmoja...tafuta watano WANAOJUANA VIZURI waanzishe kikundi wabanane wao kwa wao pesa ya marejesho irudi.itakuwa rahisi kwako otherwise kichwa Chako kitavurugika maana unavyomkopesha mmoja mmoja kwa mfano kila mmoja laki moja usitegemee pesa yako kuipa yote ndani ya Mwezi hao vipato vyao ni vidogo ,so wanatakiwa kulipa kila wiki kwa miezi mitatu Hadi sita..pia elewa ni wazoefu wa mikopo ukiwawekea riba kubwa au upate pesa nyingi kwa haraka huwezi pata mtu.
 
Ulishawahi kuwa afisa mikopo (mikopo ya vikundi vya akina mama) ? Wao mfumo unao wafaa Ni vikundi zaidi kuliko mmoja mmoja...tafuta watano WANAOJUANA VIZURI waanzishe kikundi wabanane wao kwa wao pesa ya marejesho irudi.itakuwa rahisi kwako otherwise kichwa Chako kitavurugika maana unavyomkopesha mmoja mmoja kwa mfano kila mmoja laki moja usitegemee pesa yako kuipa yote ndani ya Mwezi hao vipato vyao ni vidogo ,so wanatakiwa kulipa kila wiki kwa miezi mitatu Hadi sita..pia elewa ni wazoefu wa mikopo ukiwawekea riba kubwa au upate pesa nyingi kwa haraka huwezi pata mtu.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app

 
Ulishawahi kuwa afisa mikopo (mikopo ya vikundi vya akina mama) ? Wao mfumo unao wafaa Ni vikundi zaidi kuliko mmoja mmoja...tafuta watano WANAOJUANA VIZURI waanzishe kikundi wabanane wao kwa wao pesa ya marejesho irudi.itakuwa rahisi kwako otherwise kichwa Chako kitavurugika maana unavyomkopesha mmoja mmoja kwa mfano kila mmoja laki moja usitegemee pesa yako kuipa yote ndani ya Mwezi hao vipato vyao ni vidogo ,so wanatakiwa kulipa kila wiki kwa miezi mitatu Hadi sita..pia elewa ni wazoefu wa mikopo ukiwawekea riba kubwa au upate pesa nyingi kwa haraka huwezi pata mtu.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Nakubaliana na wewe
Ukianza kutumia vikundi, unaiweka kuwa 'formal' na watakusumbua
Mtazamo wangu:-
  • Tumia muda mwingi kumtathimini muhusika kabla ya kuwekeza- Itakusaidia kumpata mtu sahihi
  • Mtafute wewe, sio yeye akutafute
  • Tengeneza ushirika-partnership (win/win)
  • Tengeneza makubaliano,wewe na yeye (MOU)
  • Weka 'terms' baada ya siku ngapi, marejesho uchukue -usiweke siku nyingi sana
  • Usiwekeze pesa nyingi kwa mtu mmoja
  • Pesa yako iwekeze kwenye vitu 'specific'
 
Back
Top Bottom