Tumfundishe siasa Humphrey Polepole: Watumishi nchini, mpuuzeni huyu kijana na CCM yake

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Wiki jana nimeona kuna video ikimuonyesha mtu aliyejitambulisha kuwa ni Humphrey Polepole Katibu wa Itikadi na Ueneze CCM, Katika video hii anaonekana akiwatishia watumishi wa umma nchini kwamba lazima wote wawe wanaccm, anasisitiza watakao kaidi watashughulikia kwakupoteza ajira zao au hila nyingine nyingi watafanyiwa.

Naomba kwa ridhaa yenu wadau, nimfundishe siasa kidogo Ndugu yangu Polepole na Chama chake cha Mapinduzi ili waache ulaghai na vitisho kwa watumishi wa Umma nchini. Nafanya hivyo kwakutambua dhana ya vitisho hivyo ambavyo kimsingi vinatokana na ama kutojua siasa na mantiki zake zote.

Kwanza kabisa Polepole namfundisha jambo muhimu kwamba Tanzania ni nchi ya mfumo wa vyamba vingi, na kubwa zaidi afahamu mfumo wa serikali iliyotokana na mfumo wa vyama vingi ni tofauti sana kiutendaji na mfumo wa chama kimoja ambao huwa unataka watumishi wote katika nchi kuwa wanachama wa chama kilichoshika hatamu. Hapa tu ndio Polepole na ccm wanapolewa madaraka kwasababu katba ya ccm mpaka leo ina elements za Chama kimoja nchini na inawapumbaza wanaccm wengi ikiwemo Polepole kuhisi upinzani ni haramu nchini hali inayofikia wakalipuka kwa kauli za kitoto kama hizi kwamba watumishi wote wawe wanaccm, hata azimio la Zanzibar la 1992 lililozaa mfumo wa vyama vingi ccm hawalielewi au hawalitaki kabisa

Siasa ni itikadi inayofuatwa na kundi au jamii fulani ambayo ni msingi kuendesha uchumi, utamaduni na mwenendo mzima maisha ya jamii hiyo. Siasa maana yake ni njia azitumiazo mtu au kundi la watu kupata nguvu na madaraka, na ikitokea mtu akapata nguvu hizo huendelea na hatua ya pili ya njia hizo ili kuhahihisha anabaki na nguvu zake au na madaraka yake kwa lengo la kuendelea kufanya kile alichokikusudia. Kinachogomba hapo ni mamlaka/madaraka/nguvu azipatazo mwanasiasa anazitumia kwa maslahi ya nani. Hapa ndipo Polepole na CCM walipo, wao maslahi ni ya chama zaidi kuliko taifa.

Kifalsafa Mwanasiasa ni adui wa uzalendo, simuumini wa uzalendo, huamini katika itikadi ya siasa yake. Uzalendo na siasa hukinzana lakini uzalendo huo huhanikizwa katika siasa.
Chama cha kisiasa ni maungano ya watu wanaotafuta mamlaka katika dola na hasa serikali kwa kusudi la kutekeleza shabaha za kisiasa au za kifalsafa pamoja na faida kwa ajili ya vikundi fulani, faida zao za binafsi.

Vyama mara nyingi hutamka mwelekeo au itikadi fulani inayoandikwa katika ilani yao. Katika mfumo wa vyama vingi kila chama kinagombea nafasi za bunge au serikali dhidi ya vyama vingine. Wakati wa uchaguzi kila chama kinapaswa kujieleza, kutetea matendo yake ya nyuma na kuonyesha jinsi kinavyotaka kuboresha mambo tofauti na vyama vingine. Kwa njia hii kila chama huchangia harakati ya kujenga nia ya jamii inamofanya kazi kama inashinda au kushindwa kwenye uchaguzi.

Penye mfumo wa chama kimoja kazi ya chama itakuwa tofauti. Historia ina mifano ya kwamba chama pekee katika nchi, kinaelekea kwenye udikteta kwa viwango tofauti. Vyama hutofautiana sana kuhusu kiasi cha tofauti za maoni zinazoruhusiwa ndani yao, uhusiano kati ya viongozi na wanachama, kiasi cha uwezo wa wanachama kuathiri mwelekeo wa chama na umuhimu wa ilani.

Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa, ili kuleta maendeleo ya nchi upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani (hususani Tanzani wanaccm), kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia katika jamii huska. Chama kinaposhika madaraka kinaunda serikali, baada tu ya kuunda serikali, basi serikali ile KAMWE haitaongozwa kwa sheria, katiba, kanuni, mfumo wa chama wala kuingiliwa katika utendaji wake.

Nchini Tanzania serikali huanza kutenda kazi zake kwa mjibu wa Katiba, Kanuni na Sheria za nchi pale tu inaposhika madaka yake na sio Katiba ya CCM au sheria za CCM.
Wizara ya utumishi wa umma ndio inayoratibu watumishi wa umma wote, kila mtumishi atafanya kazi kwakuzingatia sheria ya utumishi wa umma na miiko ya utumishi wa umma tu, na sio miiko na miongozo ya ccm. Vilevile serikali itatekeleza sera za kiinchi kwakufuata sera zilizopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Hii ndio wizara inayohusika na Sera za kitaifa.

Kifungu cha 3 cha Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, na Kifungu cha 1(26) cha Kanuni za Kudumu za mwaka 2009 vinatoa tafsiri ya neno mtumishi wa umma, kuwa ni yule aliyeajiriwa,kuteuliwa au kuchaguliwa kufanya kazi katika mihimili yote mitatu ya Tanzania ambayo ni serikali ya Jamhuri ya Muungano, Bunge na Mahakama, na ni yule anayelipwa mshahara na serikali ya Jamhuri ya Muungano. Katika maelezo hayo ya tafsiri, ccm ya Polepole haijatajwa popote.

Mpaka hapo ukiangalia hata kwa mantiki ya kitoto tu, huoni ccm ikiingizwa katika utumishi wala sera kiutendaji, Unawza kujiuliza Polepole ametumia sheria ipi kutoa kauli ile ya kichama? Je anajua anachokizungumza au anazungumza kutishia tu watumishi nchini?

Kwakumsaidia tu Polepole namna chama chake kinavyoweza kuingia na kujua serikali yake inatekelezaje mapendekezo ya ilani ya ccm, ni pale tu ambapo vikao vya chama vinapokaa ndipo katiba ya ccm inasema wajumbe wa kata,wilaya, mkoa na taifa ambao wapo kwenye utumishi wa umma, (DC, RC na Rais) hawa wanatakiwa kupeleka mrejesho wa namna serikali ilivyotumia mapendekezo ya ilani yake.

Hapa kumbuka, Serikali iliyoundwa na chama tawala hailazimishwi kutumia 100% ya ilani na sera zilizonadiwa na chama hicho kwenye uchaguzi. HAKUNA sheria ya kuilazimisha kutumia ilani hiyo. Mfano mzuri ni Serikali ya Rais Magufuli ununuzi wa ndege, ujenzi wa uwanja Chato nk, mengi inayoyatenda hayapo kwenye Ilani ya ccm, wakati huo ccm hana uwezo wakuwajibisha serikali hii kwakuwa hakuna kifungu cha sheria za nchi kitakachotafsiri kuwa serikali imekivunja kwakutotumia ilani ya ccm.

Wajibu pekee wa kisiasa wa chama cha mapinduzi ni kuishauri serikali yake kutekeleza ilani na sera zake, Narudia ni kushauri tu na sio vinginevyo, yaani kushauri kuna mambo mawili, ama ushauri upokelewe, ama upigwe chini. Hakuna ushauri wa lazima. Ndio malengo na nadharia halisi ya mfumo wa vyama vingi.

Hivyo porojo za Hamfrey Polepole ni porojo za mzee Kimweri mjukuu wa Abunuwasi, Watumishi wa Umma mpuuzeni Polepole na CCM yake hawana uwezo wakuwafukuza kazi wala kuwagusa, ccm sio mamlaka yenu ya uajiri, ccm inaishia kwenye kuunda serikali tu, bada ya hapo ikafie Lumumba kule sio kuvuruga watumishi wala kuwatisha, Mamlaka ya watumishi ni wizara ya Utumishi na sio CCM ya Polepole.

Na Yericko Nyerere
 

Attachments

  • VID-20180115-WA0012.mp4
    3.8 MB · Views: 33
Mkuu;
Hii elimu ungeanza kwanza kumpa Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Pwani, Sumaye ambaye alituambia kuwa tukitaka mambo yetu yanyoke lazima kwanza tujiunge CCM.

Inawezekana Polepole amepata hoja zake kutoka kwa Sumaye!

Kwa kukuelisha zaidi nadhani unashindwa kuelewa kuwa chama tawala ndicho kimeiweka serikali madarakani kupitia kura za wananchi wengi.

Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Uwezekano wa kumfukuza Rais na serikali yake ni mkubwa ndani ya chama kuliko bunge pale anaposhindwa kutekeleza ilani ya chama kama ambavyo chama kilipewa ridhaa na watanzania wengi.

Mfanyakazi wa serikali lazima atekeleze sera za chama tawala hata kama hazipendi. Kutokutekeleza sera za chama tawala ni sababu tosha ya kufukuzwa kazi kwa sababu atakuwa amevunja mkataba wake.

Kwa mfano, Serikali ikija na sera ya matibabu bure katika hospitali za serikali halafu kukatokea daktari wa hospitali hizo na kuanza kutoza pesa, huyo daktari atakuwa anavunja sheria na anaweza kufukuzwa kazini.

Kumbuka sera hutungiwa sheria na kanuni ili zitumike kisheria.

Kumbuka wakuu wa wafanyakazi serikalini ni wateuliwa wa Rais,
 
Chama kinachoshika mamlaka ya dola katika Nchi kinapaswa kuichunga serikali yake na kuishauri, kuionya na kuikosoa serikali katika utekelezaji wa majukumu yake ya kuhudumia wananchi.

Inashangaza kuona chama kinashindwa kujitofautisha na serikali hivyo na chenyewe kuwa kama Serikali.

Kwa mfano kuna kauli kama [HASHTAG]#ccmmpya[/HASHTAG] na [HASHTAG]#tanzaniampya[/HASHTAG] katika muktadha MPANA nashindwa kujua nani Kati ya ccm na Tanzania nani awe mpya ili mwananchi wa nchi hii apate maendeleo ya moja kwa moja.

Kwa maoni yangu binafsi sioni haja ya upya wa ccm ili nchi ipate maendeleo isipokuwa serikali inatakiwa kuwekeza rasilimali zake kuhudumia matarajio ya wananchi. Ilhali hiyo ccm mpya ikifanya shughuli zake za ki-ccm huku ikiitazama serikali ili kutimiza malengo ya ilani ya uchaguzi.

Kwa kuhitimisha tushughulike zaidi na upya wa Tanzania kuliko upya wa CCM. Hata Rais Trump pamoja na Serikali yake anashughulika na ile anayoiita [HASHTAG]#MAGA[/HASHTAG] kwa manufaa ya Nchi yake na siyo [HASHTAG]#MAGA[/HASHTAG] kwa manufaaa ya GOP.
Mungu ibariki Afrika,
Mungu ibariki Tanzania
 
Hii elimu ungeanza kwanza kumpa Mwenyekiti wa CHADEMA kabda ta Pwani, Sumaye ambaye alituambia kuwa tukitaka mambo yetu yanyoke lazima kwanza tujiunge CCM.
Tayari keshaokoka na hata wana wa Nchi hii nadhani walishamsamehe mintarafu kauli Ile.
Isitoshe ile ilikuwa ni ulevi tu wa Madaraka, umeshamtoka. He is completely sober.
 
Wiki jana nimeona kuna video ikimuonyesha mtu aliyejitambulisha kuwa ni Humphrey Polepole Katibu wa Itikadi na Ueneze CCM, Katika video hii anaonekana akiwatishia watumishi wa umma nchini kwamba lazima wote wawe wanaccm, anasisitiza watakao kaidi watashughulikia kwakupoteza ajira zao au hila nyingine nyingi watafanyiwa.

Naomba kwa ridhaa yenu wadau, nimfundishe siasa kidogo Ndugu yangu Polepole na Chama chake cha Mapinduzi ili waache ulaghai na vitisho kwa watumishi wa Umma nchini. Nafanya hivyo kwakutambua dhana ya vitisho hivyo ambavyo kimsingi vinatokana na ama kutojua siasa na mantiki zake zote.

Kwanza kabisa Polepole namfundisha jambo muhimu kwamba Tanzania ni nchi ya mfumo wa vyamba vingi, na kubwa zaidi afahamu mfumo wa serikali iliyotokana na mfumo wa vyama vingi ni tofauti sana kiutendaji na mfumo wa chama kimoja ambao huwa unataka watumishi wote katika nchi kuwa wanachama wa chama kilichoshika hatamu. Hapa tu ndio Polepole na ccm wanapolewa madaraka kwasababu katba ya ccm mpaka leo ina elements za Chama kimoja nchini na inawapumbaza wanaccm wengi ikiwemo Polepole kuhisi upinzani ni haramu nchini hali inayofikia wakalipuka kwa kauli za kitoto kama hizi kwamba watumishi wote wawe wanaccm, hata azimio la Zanzibar la 1992 lililozaa mfumo wa vyama vingi ccm hawalielewi au hawalitaki kabisa

Siasa ni itikadi inayofuatwa na kundi au jamii fulani ambayo ni msingi kuendesha uchumi, utamaduni na mwenendo mzima maisha ya jamii hiyo. Siasa maana yake ni njia azitumiazo mtu au kundi la watu kupata nguvu na madaraka, na ikitokea mtu akapata nguvu hizo huendelea na hatua ya pili ya njia hizo ili kuhahihisha anabaki na nguvu zake au na madaraka yake kwa lengo la kuendelea kufanya kile alichokikusudia. Kinachogomba hapo ni mamlaka/madaraka/nguvu azipatazo mwanasiasa anazitumia kwa maslahi ya nani. Hapa ndipo Polepole na CCM walipo, wao maslahi ni ya chama zaidi kuliko taifa.

Kifalsafa Mwanasiasa ni adui wa uzalendo, simuumini wa uzalendo, huamini katika itikadi ya siasa yake. Uzalendo na siasa hukinzana lakini uzalendo huo huhanikizwa katika siasa.
Chama cha kisiasa ni maungano ya watu wanaotafuta mamlaka katika dola na hasa serikali kwa kusudi la kutekeleza shabaha za kisiasa au za kifalsafa pamoja na faida kwa ajili ya vikundi fulani, faida zao za binafsi.

Vyama mara nyingi hutamka mwelekeo au itikadi fulani inayoandikwa katika ilani yao. Katika mfumo wa vyama vingi kila chama kinagombea nafasi za bunge au serikali dhidi ya vyama vingine. Wakati wa uchaguzi kila chama kinapaswa kujieleza, kutetea matendo yake ya nyuma na kuonyesha jinsi kinavyotaka kuboresha mambo tofauti na vyama vingine. Kwa njia hii kila chama huchangia harakati ya kujenga nia ya jamii inamofanya kazi kama inashinda au kushindwa kwenye uchaguzi.

Penye mfumo wa chama kimoja kazi ya chama itakuwa tofauti. Historia ina mifano ya kwamba chama pekee katika nchi, kinaelekea kwenye udikteta kwa viwango tofauti. Vyama hutofautiana sana kuhusu kiasi cha tofauti za maoni zinazoruhusiwa ndani yao, uhusiano kati ya viongozi na wanachama, kiasi cha uwezo wa wanachama kuathiri mwelekeo wa chama na umuhimu wa ilani.

Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa, ili kuleta maendeleo ya nchi upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani (hususani Tanzani wanaccm), kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia katika jamii huska. Chama kinaposhika madaraka kinaunda serikali, baada tu ya kuunda serikali, basi serikali ile KAMWE haitaongozwa kwa sheria, katiba, kanuni, mfumo wa chama wala kuingiliwa katika utendaji wake.

Nchini Tanzania serikali huanza kutenda kazi zake kwa mjibu wa Katiba, Kanuni na Sheria za nchi pale tu inaposhika madaka yake na sio Katiba ya CCM au sheria za CCM.
Wizara ya utumishi wa umma ndio inayoratibu watumishi wa umma wote, kila mtumishi atafanya kazi kwakuzingatia sheria ya utumishi wa umma na miiko ya utumishi wa umma tu, na sio miiko na miongozo ya ccm. Vilevile serikali itatekeleza sera za kiinchi kwakufuata sera zilizopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Hii ndio wizara inayohusika na Sera za kitaifa.

Kifungu cha 3 cha Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, na Kifungu cha 1(26) cha Kanuni za Kudumu za mwaka 2009 vinatoa tafsiri ya neno mtumishi wa umma, kuwa ni yule aliyeajiriwa,kuteuliwa au kuchaguliwa kufanya kazi katika mihimili yote mitatu ya Tanzania ambayo ni serikali ya Jamhuri ya Muungano, Bunge na Mahakama, na ni yule anayelipwa mshahara na serikali ya Jamhuri ya Muungano. Katika maelezo hayo ya tafsiri, ccm ya Polepole haijatajwa popote.

Mpaka hapo ukiangalia hata kwa mantiki ya kitoto tu, huoni ccm ikiingizwa katika utumishi wala sera kiutendaji, Unawza kujiuliza Polepole ametumia sheria ipi kutoa kauli ile ya kichama? Je anajua anachokizungumza au anazungumza kutishia tu watumishi nchini?

Kwakumsaidia tu Polepole namna chama chake kinavyoweza kuingia na kujua serikali yake inatekelezaje mapendekezo ya ilani ya ccm, ni pale tu ambapo vikao vya chama vinapokaa ndipo katiba ya ccm inasema wajumbe wa kata,wilaya, mkoa na taifa ambao wapo kwenye utumishi wa umma, (DC, RC na Rais) hawa wanatakiwa kupeleka mrejesho wa namna serikali ilivyotumia mapendekezo ya ilani yake.

Hapa kumbuka, Serikali iliyoundwa na chama tawala hailazimishwi kutumia 100% ya ilani na sera zilizonadiwa na chama hicho kwenye uchaguzi. HAKUNA sheria ya kuilazimisha kutumia ilani hiyo. Mfano mzuri ni Serikali ya Rais Magufuli ununuzi wa ndege, ujenzi wa uwanja Chato nk, mengi inayoyatenda hayapo kwenye Ilani ya ccm, wakati huo ccm hana uwezo wakuwajibisha serikali hii kwakuwa hakuna kifungu cha sheria za nchi kitakachotafsiri kuwa serikali imekivunja kwakutotumia ilani ya ccm.

Wajibu pekee wa kisiasa wa chama cha mapinduzi ni kuishauri serikali yake kutekeleza ilani na sera zake, Narudia ni kushauri tu na sio vinginevyo, yaani kushauri kuna mambo mawili, ama ushauri upokelewe, ama upigwe chini. Hakuna ushauri wa lazima. Ndio malengo na nadharia halisi ya mfumo wa vyama vingi.

Hivyo porojo za Hamfrey Polepole ni porojo za mzee Kimweri mjukuu wa Abunuwasi, Watumishi wa Umma mpuuzeni Polepole na CCM yake hawana uwezo wakuwafukuza kazi wala kuwagusa, ccm sio mamlaka yenu ya uajiri, ccm inaishia kwenye kuunda serikali tu, bada ya hapo ikafie Lumumba kule sio kuvuruga watumishi wala kuwatisha, Mamlaka ya watumishi ni wizara ya Utumishi na sio CCM ya Polepole.

Na Yericko Nyerere
 

Attachments

  • Polepole+ccm+ijiandae+kukabidhi.mp4
    235.8 KB · Views: 18
Aina ya siasa wanayofanya ccm haipo duniani isipokuwa bongo tu. Mimi ni mhanga wa vitisho hivyo, lakini huwa ni mikwala tu ccm ni kama mbwa asiye na meno wanatisha sana ukikomaa nao wanasepa. Ni ujinga kuwatisha watumishi wa uma ili hali kuna wanaccm wanashiriki siasa wakiwa watumishi. Nasema ni ujinga.
 
Hii elimu ungeanza kwanza kumpa Mwenyekiti wa CHADEMA kabda ta Pwani, Sumaye ambaye alituambia kuwa tukitaka mambo yetu yanyoke lazima kwanza tujiunge CCM.
Kunyooka kwa mambo kunalingana na kuwalazimisha watumishi Wa umma wajiunge na chama?
Mkuu mbona ushabiki unazidi kukushusha viwango? Halafu hiyo haramu aliyoisema Sumaye (ambayo haikuwa agizo bali ushauri) alishaigundua ndio maana kaitema!
 
Wiki jana nimeona kuna video ikimuonyesha mtu aliyejitambulisha kuwa ni Humphrey Polepole Katibu wa Itikadi na Ueneze CCM, Katika video hii anaonekana akiwatishia watumishi wa umma nchini kwamba lazima wote wawe wanaccm, anasisitiza watakao kaidi watashughulikia kwakupoteza ajira zao au hila nyingine nyingi watafanyiwa.

Naomba kwa ridhaa yenu wadau, nimfundishe siasa kidogo Ndugu yangu Polepole na Chama chake cha Mapinduzi ili waache ulaghai na vitisho kwa watumishi wa Umma nchini. Nafanya hivyo kwakutambua dhana ya vitisho hivyo ambavyo kimsingi vinatokana na ama kutojua siasa na mantiki zake zote.

Kwanza kabisa Polepole namfundisha jambo muhimu kwamba Tanzania ni nchi ya mfumo wa vyamba vingi, na kubwa zaidi afahamu mfumo wa serikali iliyotokana na mfumo wa vyama vingi ni tofauti sana kiutendaji na mfumo wa chama kimoja ambao huwa unataka watumishi wote katika nchi kuwa wanachama wa chama kilichoshika hatamu. Hapa tu ndio Polepole na ccm wanapolewa madaraka kwasababu katba ya ccm mpaka leo ina elements za Chama kimoja nchini na inawapumbaza wanaccm wengi ikiwemo Polepole kuhisi upinzani ni haramu nchini hali inayofikia wakalipuka kwa kauli za kitoto kama hizi kwamba watumishi wote wawe wanaccm, hata azimio la Zanzibar la 1992 lililozaa mfumo wa vyama vingi ccm hawalielewi au hawalitaki kabisa

Siasa ni itikadi inayofuatwa na kundi au jamii fulani ambayo ni msingi kuendesha uchumi, utamaduni na mwenendo mzima maisha ya jamii hiyo. Siasa maana yake ni njia azitumiazo mtu au kundi la watu kupata nguvu na madaraka, na ikitokea mtu akapata nguvu hizo huendelea na hatua ya pili ya njia hizo ili kuhahihisha anabaki na nguvu zake au na madaraka yake kwa lengo la kuendelea kufanya kile alichokikusudia. Kinachogomba hapo ni mamlaka/madaraka/nguvu azipatazo mwanasiasa anazitumia kwa maslahi ya nani. Hapa ndipo Polepole na CCM walipo, wao maslahi ni ya chama zaidi kuliko taifa.

Kifalsafa Mwanasiasa ni adui wa uzalendo, simuumini wa uzalendo, huamini katika itikadi ya siasa yake. Uzalendo na siasa hukinzana lakini uzalendo huo huhanikizwa katika siasa.
Chama cha kisiasa ni maungano ya watu wanaotafuta mamlaka katika dola na hasa serikali kwa kusudi la kutekeleza shabaha za kisiasa au za kifalsafa pamoja na faida kwa ajili ya vikundi fulani, faida zao za binafsi.

Vyama mara nyingi hutamka mwelekeo au itikadi fulani inayoandikwa katika ilani yao. Katika mfumo wa vyama vingi kila chama kinagombea nafasi za bunge au serikali dhidi ya vyama vingine. Wakati wa uchaguzi kila chama kinapaswa kujieleza, kutetea matendo yake ya nyuma na kuonyesha jinsi kinavyotaka kuboresha mambo tofauti na vyama vingine. Kwa njia hii kila chama huchangia harakati ya kujenga nia ya jamii inamofanya kazi kama inashinda au kushindwa kwenye uchaguzi.

Penye mfumo wa chama kimoja kazi ya chama itakuwa tofauti. Historia ina mifano ya kwamba chama pekee katika nchi, kinaelekea kwenye udikteta kwa viwango tofauti. Vyama hutofautiana sana kuhusu kiasi cha tofauti za maoni zinazoruhusiwa ndani yao, uhusiano kati ya viongozi na wanachama, kiasi cha uwezo wa wanachama kuathiri mwelekeo wa chama na umuhimu wa ilani.

Madhumuni ya kuwa na vyama vingi vya siasa ni kuleta ushindani wa kisiasa, ili kuleta maendeleo ya nchi upinzani wa kisiasa sio uadui kama watu wengi kwenye nchi zinazoendelea wanavyodhani (hususani Tanzani wanaccm), kuwa na vyama vingi ni kuongeza wigo wa demokrasia katika jamii huska. Chama kinaposhika madaraka kinaunda serikali, baada tu ya kuunda serikali, basi serikali ile KAMWE haitaongozwa kwa sheria, katiba, kanuni, mfumo wa chama wala kuingiliwa katika utendaji wake.

Nchini Tanzania serikali huanza kutenda kazi zake kwa mjibu wa Katiba, Kanuni na Sheria za nchi pale tu inaposhika madaka yake na sio Katiba ya CCM au sheria za CCM.
Wizara ya utumishi wa umma ndio inayoratibu watumishi wa umma wote, kila mtumishi atafanya kazi kwakuzingatia sheria ya utumishi wa umma na miiko ya utumishi wa umma tu, na sio miiko na miongozo ya ccm. Vilevile serikali itatekeleza sera za kiinchi kwakufuata sera zilizopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Hii ndio wizara inayohusika na Sera za kitaifa.

Kifungu cha 3 cha Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, na Kifungu cha 1(26) cha Kanuni za Kudumu za mwaka 2009 vinatoa tafsiri ya neno mtumishi wa umma, kuwa ni yule aliyeajiriwa,kuteuliwa au kuchaguliwa kufanya kazi katika mihimili yote mitatu ya Tanzania ambayo ni serikali ya Jamhuri ya Muungano, Bunge na Mahakama, na ni yule anayelipwa mshahara na serikali ya Jamhuri ya Muungano. Katika maelezo hayo ya tafsiri, ccm ya Polepole haijatajwa popote.

Mpaka hapo ukiangalia hata kwa mantiki ya kitoto tu, huoni ccm ikiingizwa katika utumishi wala sera kiutendaji, Unawza kujiuliza Polepole ametumia sheria ipi kutoa kauli ile ya kichama? Je anajua anachokizungumza au anazungumza kutishia tu watumishi nchini?

Kwakumsaidia tu Polepole namna chama chake kinavyoweza kuingia na kujua serikali yake inatekelezaje mapendekezo ya ilani ya ccm, ni pale tu ambapo vikao vya chama vinapokaa ndipo katiba ya ccm inasema wajumbe wa kata,wilaya, mkoa na taifa ambao wapo kwenye utumishi wa umma, (DC, RC na Rais) hawa wanatakiwa kupeleka mrejesho wa namna serikali ilivyotumia mapendekezo ya ilani yake.

Hapa kumbuka, Serikali iliyoundwa na chama tawala hailazimishwi kutumia 100% ya ilani na sera zilizonadiwa na chama hicho kwenye uchaguzi. HAKUNA sheria ya kuilazimisha kutumia ilani hiyo. Mfano mzuri ni Serikali ya Rais Magufuli ununuzi wa ndege, ujenzi wa uwanja Chato nk, mengi inayoyatenda hayapo kwenye Ilani ya ccm, wakati huo ccm hana uwezo wakuwajibisha serikali hii kwakuwa hakuna kifungu cha sheria za nchi kitakachotafsiri kuwa serikali imekivunja kwakutotumia ilani ya ccm.

Wajibu pekee wa kisiasa wa chama cha mapinduzi ni kuishauri serikali yake kutekeleza ilani na sera zake, Narudia ni kushauri tu na sio vinginevyo, yaani kushauri kuna mambo mawili, ama ushauri upokelewe, ama upigwe chini. Hakuna ushauri wa lazima. Ndio malengo na nadharia halisi ya mfumo wa vyama vingi.

Hivyo porojo za Hamfrey Polepole ni porojo za mzee Kimweri mjukuu wa Abunuwasi, Watumishi wa Umma mpuuzeni Polepole na CCM yake hawana uwezo wakuwafukuza kazi wala kuwagusa, ccm sio mamlaka yenu ya uajiri, ccm inaishia kwenye kuunda serikali tu, bada ya hapo ikafie Lumumba kule sio kuvuruga watumishi wala kuwatisha, Mamlaka ya watumishi ni wizara ya Utumishi na sio CCM ya Polepole.

Na Yericko Nyerere
TANGAZO:
INGEPENDEZA SANA ANDIKO HILI KILA MTU ALI PRINT NA KWENDA KUBANDIKA KWENYE NOTICE BOARD ZA OFISI ZA UMMA ILI KILA MTU ASOME NA KUELEWA
 
Ccm imevaa koti la serekali. Halafu kwa bahati mbaya mwenyekiti wake ambaye ni amiri jeshi hajui na wala haheshimu mipaka ya kiutendaji kati ya chama na serekali. Kibaya zaidi taasisi zote za nchi hii hazina nguvu dhidi ya rais. Rais wa nchi hii anaweza kufanya lolote na taasisi zote za kimamlaka zikasita au kushindwa kumuwajibisha. Katika mazingira haya ya rais kuwa mwenyekiti wa ccm tena anayechanganya hizi kofia mbili bila kujali mipaka, walevi wengine wa madaraka ndani ya chama wanatumia udhaifu huo kufanya yao.
 
Thubutu, wote wameufyata. Mbwembwe zote za kutuletea mrejesho zimeyeyuka, utafikiri hawakukaa kikao kama walivyotutangazia. Hawa jamaa kwisha habari yao.
Mawazo na akili zako kichwani na upumbavu ulionao una reflect akili za wazazi wako, Hivyo hatukulaumu wewe a big mistake from your parents
Huna la kujifunza wala la kufikiria kwenye kichwa chako zaidi ya kuandika maandishi na kuchangia kama muimba taarabu, Punguza Povu la uchama mdomoni jibu hoja za maelezo ya watumishi wa uma na sheria
Shame on you
 
Huyu pole pole ni mgonjwa wa Akili hayuko sawa Hii anatufunulia yaliofichwa katika utawala huu kua mambo yote tunayofanyiwa watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na kutoongezewa mishahara ni chuki ya ccm
 
Elimu Elimu Elimu Elimu. Ndio maana wanaendelea kuharibu mfumo wa elimu ili kuzalisha mambumbumbu na majitu majoga yasiyoweza kupambanua mambo ili wayatishie na kuyaswaga watakavyo. Akina magonjwa mtambuka na msemaji uongo ndio product/batch ya mwanzo ya mambumbumbu. Ndio cream. Yanayofuata yatakuwa zaidi yao ndio polepole aliowalenga. Mtu mzima huwezi kusimama na kuzungumza vile wakati huijui hadhira yako.

Bahati mbaya maprofesa ndo viongozi wa mambumbumbu kila mwaka wanahamisha magoli ili kuzalisha mabwege. Kuna haja gani ya kuwafanyisha watoto mitihani kama huwezi kuwapima kwa mitihani hiyo?

Na bado sana, mtatishiwa mno. Na kazi mtafukuzwa sana kwasababu hamjui hata haki zenu na nguvu zenu za kiutumishi ziko wapi.
 
hahahaha... hadi mugab na ubabe wake kaufyata kwa lowas.
Jifarijini tu hapo wakati ndugu zenu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Wewe Bayyo huwahurumii ndugu zako wairaqw hawajitambui, wanatoka kamasi tu na umaskini wa kutosha kwa kukosa elimu. Mmejichimbia mbulumbulu huko mkienda mjini mnashindia huko mnashangaa na kubugia ugoro tu.
 
Yerico Nyerere,weka hiyo video na sie tumuone
Mlalamikaji wewe,polisi wewe.na unahukumu kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom