GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,652
- 14,247
Miaka hiyo sisi tuliozaliwa mjini tulikuwa tunapata shida sana na watu wa mkoani. Wakifika Dar Kuna maeneo Matatu itabidi uwapeleke.
1. Uwapeleke soko la Kariakoo
2. Uwapeleke Ferry wakashangae meli
3. Usisahau kuwapeleka daraja la Manzese wakapige picha.
Ilikuwa ni usumbufu sana. Maana mgeni akija kama ni umri wako au kakuzidi kidogo wewe ndo unachaguliwa kumpa hizo tours.kwa sisi ambao tulikuwa hatupend kutembea tembea tulikuwa tunakwazika sana.
Ndo wajasiliamali wakagundua kuwa pale manzese mtu akitaka kupiga picha kwa camera yake basi analipia lile daraja na ama sivyo apige picha kwao maana wao ndo wameidhinishwa na serikal kupiga picha raia.
Aisee... Watu walikuwa wanalizwa sana kwa mtindo huu. Walikuwa wanalipa tsh 200-500 kwa kutumia daraja lile. Ilikuwa mida flan ukipita unakuta kumejaa sana watu kule juu wakiweka pozi mbalimbal wakipiga picha.
Nawashaur sasa ni wakati wa kuenda kudai hizo pesa kwa wahusika... Maana kuna siku nlimwona jamaa mmoja alitekuwa akipenda kuulamba na tai na kofia zile za ki cow boy umri umeenda bado yupo pale na camera yake. Waswas wangu na haya madaraja ya mwendokasi yanaweza tumika kijasiriamali.
Wakumbuke jamaw zako mbalimbali ambao sasa wanatamba mjini ila walipofika chuo miaka ile lazima waliomba ukawape tour maeneo hayo.wape hi tu kishkaj.
1. Uwapeleke soko la Kariakoo
2. Uwapeleke Ferry wakashangae meli
3. Usisahau kuwapeleka daraja la Manzese wakapige picha.
Ilikuwa ni usumbufu sana. Maana mgeni akija kama ni umri wako au kakuzidi kidogo wewe ndo unachaguliwa kumpa hizo tours.kwa sisi ambao tulikuwa hatupend kutembea tembea tulikuwa tunakwazika sana.
Ndo wajasiliamali wakagundua kuwa pale manzese mtu akitaka kupiga picha kwa camera yake basi analipia lile daraja na ama sivyo apige picha kwao maana wao ndo wameidhinishwa na serikal kupiga picha raia.
Aisee... Watu walikuwa wanalizwa sana kwa mtindo huu. Walikuwa wanalipa tsh 200-500 kwa kutumia daraja lile. Ilikuwa mida flan ukipita unakuta kumejaa sana watu kule juu wakiweka pozi mbalimbal wakipiga picha.
Nawashaur sasa ni wakati wa kuenda kudai hizo pesa kwa wahusika... Maana kuna siku nlimwona jamaa mmoja alitekuwa akipenda kuulamba na tai na kofia zile za ki cow boy umri umeenda bado yupo pale na camera yake. Waswas wangu na haya madaraja ya mwendokasi yanaweza tumika kijasiriamali.
Wakumbuke jamaw zako mbalimbali ambao sasa wanatamba mjini ila walipofika chuo miaka ile lazima waliomba ukawape tour maeneo hayo.wape hi tu kishkaj.