Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Wakati Rais Kikwete amepokea maandamano ya kupinga mauaji ya Albino kwa kupiga mkwara wa kunyonga watu... habari ndiyo hii..
Mtoto mmoja Albino auawa kikatili mkoani Shinyanga
2008-10-20 18:21:20
Na Radio One Habari
Wimbi la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi -Albino limeingia mkoani Shinyanga kufuatia mauji ya mtoto mmoja Albino katika kijiji cha Shilela, Kata ya Segese wilayani humo.
Mtoto huyo wa kike aitwaye Esther Charles, mwanafunzi wa Darasa la Tatu katika shule ya msingi kijiji hapo ameuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana.
Diwani wa Kata ya Segese Bwana Joseph Mayala amesema watu wasiojulikana wakiwa na mapanga usiku wa manane walivamia nyumba ya Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bwana Mzolewa Mashili ambaye ni baba wa mtoto huyo kwa kuvunja mlago wa nyumba yake kwa kutumia jiwe kubwa.
Amesema watu hao waliwaweka chini ya ulinzi wazazi wa mtoto huyo na kuanza kumchuna sehemu za usoni, kichwa hadi ngozi ya kisogoni na kumkata miguu yake kuanzia sehemu za nyonga na kuondoka nayo.
Diwani huyo amewataka wananchi wakiwemo walinzi wa jadi Sungusungu Wilayani Kahama kuhakikisha watu wanaojihusisha na mauaji hayo wanafichuliwa.
My Take:
Tuombe msaada kwa wazungu kutusaidia kukomesha mauaji haya? Lakini zaidi siyo tu kwenye suala la mauaji haya bali usimamizi mzima wa sheria zetu kuna aina fulani ya kigugumizi au kusita kuchukua hatua za dhati.
Leo nimeona picha ya jinsi gani mgambo wa jiji wakiwasweka kwenye makarandinga (mafuso) wamachinga maeneo ya Posta (Dar) katika kile ambacho bila ya shaka wanaamini ni kulisafisha jiji. Lakini hadi sasa hatujaona jinsi gani waliochafua nchi kwa ufisadi wao hawajasweka kwenye makarandinga zaidi ya kusubiri maelezo ya kuwa "very soon, watachukuliwa hatua".
Ni wazi tumeshindwea kusimamia sheria zetu wenyewe hasa zinapokuja kwenye masuala yanayohusu mambo makubwa zaidi; tumeshindwa kufanya mambo mengi ambayo jamii yoyote inapaswa kufanya yenyewe. Vile vilivyo msingi tumeviweka pembeni na tumeng'angania vya sekondari.
Je kuna ubaya gani tukiomba timu ya waendesha mashtaka toka Commonwealth, kuna ubaya gani tukiomba timu ya wahandishi kutoka Japani au Ujerumani kusimmamia infrastructure development? Kuna ubaya gani tukakubaliana na vyuo vikuu mahiri duniani vikatuendeshea UDSM au Mzumbe n.k na kugeuza vyuo vyetu kuwa World Class Higher Education institution?
Kama hatuwezi kufanya kitu na tunajua hatuwezi (licha ya kujibaraguza) kwanini tusiombe msaada kwa wale wanaoweza? Hata Nyerere wakati wa maasi ya 1964 aligundua kuwa pamoja na uzalendo wake wote asingeweza kuzima uasi bila msaada wa Waingereza. Je tuwaombe tena wazime uasi unaochochewa na ufisadi?
Mtoto mmoja Albino auawa kikatili mkoani Shinyanga
2008-10-20 18:21:20
Na Radio One Habari
Wimbi la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi -Albino limeingia mkoani Shinyanga kufuatia mauji ya mtoto mmoja Albino katika kijiji cha Shilela, Kata ya Segese wilayani humo.
Mtoto huyo wa kike aitwaye Esther Charles, mwanafunzi wa Darasa la Tatu katika shule ya msingi kijiji hapo ameuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana.
Diwani wa Kata ya Segese Bwana Joseph Mayala amesema watu wasiojulikana wakiwa na mapanga usiku wa manane walivamia nyumba ya Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bwana Mzolewa Mashili ambaye ni baba wa mtoto huyo kwa kuvunja mlago wa nyumba yake kwa kutumia jiwe kubwa.
Amesema watu hao waliwaweka chini ya ulinzi wazazi wa mtoto huyo na kuanza kumchuna sehemu za usoni, kichwa hadi ngozi ya kisogoni na kumkata miguu yake kuanzia sehemu za nyonga na kuondoka nayo.
Diwani huyo amewataka wananchi wakiwemo walinzi wa jadi Sungusungu Wilayani Kahama kuhakikisha watu wanaojihusisha na mauaji hayo wanafichuliwa.
My Take:
Tuombe msaada kwa wazungu kutusaidia kukomesha mauaji haya? Lakini zaidi siyo tu kwenye suala la mauaji haya bali usimamizi mzima wa sheria zetu kuna aina fulani ya kigugumizi au kusita kuchukua hatua za dhati.
Leo nimeona picha ya jinsi gani mgambo wa jiji wakiwasweka kwenye makarandinga (mafuso) wamachinga maeneo ya Posta (Dar) katika kile ambacho bila ya shaka wanaamini ni kulisafisha jiji. Lakini hadi sasa hatujaona jinsi gani waliochafua nchi kwa ufisadi wao hawajasweka kwenye makarandinga zaidi ya kusubiri maelezo ya kuwa "very soon, watachukuliwa hatua".
Ni wazi tumeshindwea kusimamia sheria zetu wenyewe hasa zinapokuja kwenye masuala yanayohusu mambo makubwa zaidi; tumeshindwa kufanya mambo mengi ambayo jamii yoyote inapaswa kufanya yenyewe. Vile vilivyo msingi tumeviweka pembeni na tumeng'angania vya sekondari.
Je kuna ubaya gani tukiomba timu ya waendesha mashtaka toka Commonwealth, kuna ubaya gani tukiomba timu ya wahandishi kutoka Japani au Ujerumani kusimmamia infrastructure development? Kuna ubaya gani tukakubaliana na vyuo vikuu mahiri duniani vikatuendeshea UDSM au Mzumbe n.k na kugeuza vyuo vyetu kuwa World Class Higher Education institution?
Kama hatuwezi kufanya kitu na tunajua hatuwezi (licha ya kujibaraguza) kwanini tusiombe msaada kwa wale wanaoweza? Hata Nyerere wakati wa maasi ya 1964 aligundua kuwa pamoja na uzalendo wake wote asingeweza kuzima uasi bila msaada wa Waingereza. Je tuwaombe tena wazime uasi unaochochewa na ufisadi?