Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Yawezekana Watanzania tuna "Mind Crisis Syndrome Disease(MCSD)" na hii hutupelekea kushangilia kila jambo, kuunga mkono kila jambo na kutofanya tathmini ya kile tunachokiunga mkono na kushangilia!
-----------------------------------
Hii inajidhihirisha pia hata kwenye matamko yetu ya kuhama vyama nayo yana Crisis na lack of authority! Mwakilishi wa wananchi anasema anahama chama kwa sababu "fulani" anatekeleza ahadi zilizokuwa ndio agenda yake, nonsense! Ulitegemea atekeleze nini? Huo si ndiyo wajibu wake na wako?
Kutekekeleza ahadi ni wajibu wa msingi wa kimkataba kati ya Kiongozi(Serikali) na Mlipa kodi(Umma- Wananchi). Ni ujinga kabisa tena wa kiwango duni kabisa kuwahi kutokea kudhani kwamba kuna mtu mmoja anatekeleza ahadi kama hisani na kama vile financing ya utekelezaji wa ahadi hizo unatoka kwenye mfuko wake! Huu ni uzwazwa wa hali ya juu sana!.
Governance ni coordinated and integrated duty. Na kwa msingi huo huwezi kuona matokeo chanya ya uwajibikaji huo kama mtu mmoja anafilisi akili za watu wengine!
Ninachokiona kwa karibu ni kwamba, hama hama na jitihada kubwa za kuwarubuni wapinzani wasio na fikra pevu ni kutaka kutengeneza justification ya kukubalika hasa pale uchaguzi wa marudio utafanyika na kama ilivyo ada uporaji wa matokeo nje ya [HASHTAG]#ballotpapers[/HASHTAG] ndiyo umekuwa mtindo mpya wa demokrasia katika taifa letu!
Kimsingi tuseme ukweli kwamba utawala huu unalazimisha kukubalika pasipo kuonesha dhati ya utendaji na uwajibikaji unaoweza kuleta ustawi wa maisha ya watanzania.
Kuwarubuni wanasiasa kuhamia chama chako tena kwa gharama kubwa hakuondoi ugumu wa maisha ya mtanzania, sana sana kunazidi kumuongezea adha na taabu kubwa!
Kwanza, ni muhimu nikaeleweka kwamba mtu kuhamia chama kingine ni HAKI yake ya MSINGI kabisa na hahitaji mjadala. Hoja TATA ni namna gani huyo mtu kahama toka sehemu moja kwenda nyingine! Ameshawishiwa? Amerubuniwa? Au amehama kwa hiari yake mwenyewe kwa kuchoshwa na aina fulani ya ghiriba za watawala wasioishi kwa kile wanachokihubiri?
Pili, ijulikane kuwa kwa mwakilishi wa jimbo ambaye kimsingi anahama chama kwa sababu za kijinga kabisa na hasa kwa kununuliwa au kwa njia yoyote ya hovyo huyo mtu ni [HASHTAG]#LAANA[/HASHTAG] na [HASHTAG]#MKOSI[/HASHTAG] kwa jamii ya watanzania wote ikiwemo waliomchagua kuwawakilisha kwa kipindi cha miaka mitano.
Kwa nini nasema hivyo? Ni ukweli usiotia shaka kwamba mzigo wa fedha za kugharamia uchaguzi mpya wa marudio utatokana na fedha za mlipa kodi mtanzania! Huu ni mzigo unaobebeshwa watanzania bila sababu yoyote! Alaaniwe anayewarubuni wawakilishi hawa na alaaniwe pia mwakilishi huyu mwenye akili ya Kikunguni!
Kwa mfano; unahamaje kwa kuhongwa na/au ahadi ya kulipiwa madeni yako unayodaiwa? Ni jambo lisilokuwa na fikra pevu hata kidogo!
Watanzania tudai KATIBA mpya! Tuamke tudai Katiba na Tume huru ya Uchaguzi!
[HASHTAG]#AmkeniTuaamke[/HASHTAG]!
[HASHTAG]#Tusinyamaze[/HASHTAG] [HASHTAG]#Tusiogope[/HASHTAG]!
-----------------------------------
Hii inajidhihirisha pia hata kwenye matamko yetu ya kuhama vyama nayo yana Crisis na lack of authority! Mwakilishi wa wananchi anasema anahama chama kwa sababu "fulani" anatekeleza ahadi zilizokuwa ndio agenda yake, nonsense! Ulitegemea atekeleze nini? Huo si ndiyo wajibu wake na wako?
Kutekekeleza ahadi ni wajibu wa msingi wa kimkataba kati ya Kiongozi(Serikali) na Mlipa kodi(Umma- Wananchi). Ni ujinga kabisa tena wa kiwango duni kabisa kuwahi kutokea kudhani kwamba kuna mtu mmoja anatekeleza ahadi kama hisani na kama vile financing ya utekelezaji wa ahadi hizo unatoka kwenye mfuko wake! Huu ni uzwazwa wa hali ya juu sana!.
Governance ni coordinated and integrated duty. Na kwa msingi huo huwezi kuona matokeo chanya ya uwajibikaji huo kama mtu mmoja anafilisi akili za watu wengine!
Ninachokiona kwa karibu ni kwamba, hama hama na jitihada kubwa za kuwarubuni wapinzani wasio na fikra pevu ni kutaka kutengeneza justification ya kukubalika hasa pale uchaguzi wa marudio utafanyika na kama ilivyo ada uporaji wa matokeo nje ya [HASHTAG]#ballotpapers[/HASHTAG] ndiyo umekuwa mtindo mpya wa demokrasia katika taifa letu!
Kimsingi tuseme ukweli kwamba utawala huu unalazimisha kukubalika pasipo kuonesha dhati ya utendaji na uwajibikaji unaoweza kuleta ustawi wa maisha ya watanzania.
Kuwarubuni wanasiasa kuhamia chama chako tena kwa gharama kubwa hakuondoi ugumu wa maisha ya mtanzania, sana sana kunazidi kumuongezea adha na taabu kubwa!
Kwanza, ni muhimu nikaeleweka kwamba mtu kuhamia chama kingine ni HAKI yake ya MSINGI kabisa na hahitaji mjadala. Hoja TATA ni namna gani huyo mtu kahama toka sehemu moja kwenda nyingine! Ameshawishiwa? Amerubuniwa? Au amehama kwa hiari yake mwenyewe kwa kuchoshwa na aina fulani ya ghiriba za watawala wasioishi kwa kile wanachokihubiri?
Pili, ijulikane kuwa kwa mwakilishi wa jimbo ambaye kimsingi anahama chama kwa sababu za kijinga kabisa na hasa kwa kununuliwa au kwa njia yoyote ya hovyo huyo mtu ni [HASHTAG]#LAANA[/HASHTAG] na [HASHTAG]#MKOSI[/HASHTAG] kwa jamii ya watanzania wote ikiwemo waliomchagua kuwawakilisha kwa kipindi cha miaka mitano.
Kwa nini nasema hivyo? Ni ukweli usiotia shaka kwamba mzigo wa fedha za kugharamia uchaguzi mpya wa marudio utatokana na fedha za mlipa kodi mtanzania! Huu ni mzigo unaobebeshwa watanzania bila sababu yoyote! Alaaniwe anayewarubuni wawakilishi hawa na alaaniwe pia mwakilishi huyu mwenye akili ya Kikunguni!
Kwa mfano; unahamaje kwa kuhongwa na/au ahadi ya kulipiwa madeni yako unayodaiwa? Ni jambo lisilokuwa na fikra pevu hata kidogo!
Watanzania tudai KATIBA mpya! Tuamke tudai Katiba na Tume huru ya Uchaguzi!
[HASHTAG]#AmkeniTuaamke[/HASHTAG]!
[HASHTAG]#Tusinyamaze[/HASHTAG] [HASHTAG]#Tusiogope[/HASHTAG]!