Tumeshindwa mtihani rahisi saaaana, tutaiweza migumu?

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Kwa wale waliofuatilia habari za Babu wa Loliondo, watakumbuka jinsi ambavyo baadhi yetu tulipaza sauti za kuonya kuwa dawa ya mzee huyo ilikuwa kanyaboya! Hata hivyo tulipuuzwa na kuonekana watu wa ajabu sana kwenye jamii. Kuna baadhi ya marafiki na ndugu zangu walinizuia kabisa kupinga hadharani habari ya uponyaji wa Babu wa Loliondo.

Sasa imethibitika kuwa hakuna kitu kama uponyaji katika hiyo dawa ya Babu. Binafsi niina ushahidi wa ndugu 3 wa karibu sana, ambao wametumia dawa hiyo na hawana nafuu ya aina yoyote.

Lawama sasa zinaelekezwa kwa viongozi wetu ambao walijifanya mbao za matangazo kuitangaza dawa ya Babu kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kana kwamba ilikuwa ni mwarobaini wa matatizo yetu ya afya na akili. Babu mwenyewe tayari keshawakana walioshindwa kupona kwa kueleza kuwa ni kutokana na imani yao ndogo.

Suala la Babu na tiba yake ni zito sana na viongozi wetu wanayo maswali mengi ya kujibu ingawa na sisi pia tuna mzigo mkubwa wa lawama ambao tunastahili kuubeba katika ujumla wetu. Hili ni anguko kubwa la Watanzania kama taifa na linaonesha kuwa hatuko tayari kukabiliana na mambo magumu!
 
Umenikumbusha mbali mkuu, kuna mtu nilimueleza kuusu hili swala kabla, akaniambia bwana usilete usomi wako kwenye mambo ya imani.
Akaniambia "Kuna mambo mengi ambayo mwanadamu hayajui, kwa hiyo usinishawishi kabisa kutokuamini dawa ya babu".
Baada ya mwezi, nilumuuliza vipi tiba, jamaa alibaki kulalamika tu kama kawaida ya watz.
 
Umenikumbusha mbali mkuu, kuna mtu nilimueleza kuusu hili swala kabla, akaniambia bwana usilete usomi wako kwenye mambo ya imani.
Akaniambia "Kuna mambo mengi ambayo mwanadamu hayajui, kwa hiyo usinishawishi kabisa kutokuamini dawa ya babu".
Baada ya mwezi, nilumuuliza vipi tiba, jamaa alibaki kulalamika tu kama kawaida ya watz.

Hii tabia tunayozidi kuhalalisha ya kutoa majibu mepesi mepezi kwa maswali mazito ndiyo inayotugharimu sana. Nafurahi sana kwamba pamoja na kunyamazishwa kwa nguvu, ukweli sasa uko hadharani. Ngoja tuwasubiri wadau watupe ushahidi wa imani kama wamepona au la!
 
Tiba ya Loliondo ilishikiwa bango na baadhi ya Maaskofu kisha likabebwa na baadhi ya viongozi wa nchi kisha "vyombo vyetu vya habari" vikapata pa kuuzia magazeti.
Kazi ndio hiyo. Wewe umia na ulie, mwenzako manufaa na kicheko eeenhhhh??????
 
Tiba ya Loliondo ilishikiwa bango na baadhi ya Maaskofu kisha likabebwa na baadhi ya viongozi wa nchi kisha "vyombo vyetu vya habari" vikapata pa kuuzia magazeti.
Kazi ndio hiyo. Wewe umia na ulie, mwenzako manufaa na kicheko eeenhhhh??????

Kweli mkuu? Unaongea katika nafsi ya mtu mmoja mmoja au katika mtazamo wa nchi isiyojua lipi la kufanya na lipi la kuacha??
 
Polea yako....

kwa taarifa nilizopata mimi
watu wa kisukari pamoja na pumu
wana afadhali sana baada ya kuchukua kikombe
cha babu ..
 
Polea yako....

kwa taarifa nilizopata mimi
watu wa kisukari pamoja na pumu
wana afadhali sana baada ya kuchukua kikombe
cha babu ..

Hata mimi mwanzoni nilisikia hivyo. Ila kadri ziku zinavyoenda naona kama hiyo tiba ina-expire na exp dates inaonekana tayari zimepita!

Ngoja tusubiri wenye ma-ushuhuda.

Mzima lakini wewe?
 
Hata mimi mwanzoni nilisikia hivyo. Ila kadri ziku zinavyoenda naona kama hiyo tiba ina-expire na exp dates inaonekana tayari zimepita!

Ngoja tusubiri wenye ma-ushuhuda.

Mzima lakini wewe?

mmmmmhhh
haya tuzidi kusubiri ..

Nway mi mzima kabisa Mzee DC
umeukataa ubabu jumla naona.....

Vipi we mzima kabisa dear ??
 
mmmmmhhh
haya tuzidi kusubiri ..

Nway mi mzima kabisa Mzee DC
umeukataa ubabu jumla naona.....

Vipi we mzima kabisa dear ??

Safi sana Mjukuu..

Babu ni mzima na alisharudia jina lake tamu baada ya huyo mtu aliyemkera kuonekana tapeli....

Kila kitu shwari kabisa...Karibu supu ya pweza pale Chuda!
 
Ilikuwa ni kipindi cha sakata la dowans kulipwa bilioni 94! Babu wa loliondo akashika kasi!
Huku na huku mara tunasikia dowans imekuwa symbion!
Napenda sana huu muziki wa habari (single ya babu iliuza sana!)
sasa turudi kwa dowans, hivi iliishia wapi vile?! Wadau tukumbushane!

kwa wale waliofuatilia habari za babu wa loliondo, watakumbuka jinsi ambavyo baadhi yetu tulipaza sauti za kuonya kuwa dawa ya mzee huyo ilikuwa kanyaboya! Hata hivyo tulipuuzwa na kuonekana watu wa ajabu sana kwenye jamii. Kuna baadhi ya marafiki na ndugu zangu walinizuia kabisa kupinga hadharani habari ya uponyaji wa babu wa loliondo.

Sasa imethibitika kuwa hakuna kitu kama uponyaji katika hiyo dawa ya babu. Binafsi niina ushahidi wa ndugu 3 wa karibu sana, ambao wametumia dawa hiyo na hawana nafuu ya aina yoyote.

Lawama sasa zinaelekezwa kwa viongozi wetu ambao walijifanya mbao za matangazo kuitangaza dawa ya babu kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kana kwamba ilikuwa ni mwarobaini wa matatizo yetu ya afya na akili. Babu mwenyewe tayari keshawakana walioshindwa kupona kwa kueleza kuwa ni kutokana na imani yao ndogo.

Suala la babu na tiba yake ni zito sana na viongozi wetu wanayo maswali mengi ya kujibu ingawa na sisi pia tuna mzigo mkubwa wa lawama ambao tunastahili kuubeba katika ujumla wetu. Hili ni anguko kubwa la watanzania kama taifa na linaonesha kuwa hatuko tayari kukabiliana na mambo magumu!
 
kama hukuwa na iman au imani yako ilikuwa haba huezi pona,ingawa kuna habari kuwa 78% ya walokunywa dawa walipona!
 
Polea yako....

kwa taarifa nilizopata mimi
watu wa kisukari pamoja na pumu
wana afadhali sana baada ya kuchukua kikombe
cha babu ..

AD,
Nina binamu yangu alienda kupata kikombe cha babu kwa ajili ya kisukari, lakini tumemzika kama wiki 3 zilizopita! Binafsi sijapata nafasi ya kumwona aliyepona aliyepata kikombe.............mhhhh!!!!
 
Safi sana Mjukuu..

Babu ni mzima na alisharudia jina lake tamu baada ya huyo mtu aliyemkera kuonekana tapeli....

Kila kitu shwari kabisa...Karibu supu ya pweza pale Chuda!


asante sana Babu
ilikuwa rahisi sana kukuita
Babu kuliko Mzee..

na kuja kuinywa hiyo supu ili unipe
story za "hapo zamani za kale"
sante babu...
 
AD,
Nina binamu yangu alienda kupata kikombe cha babu kwa ajili ya kisukari, lakini tumemzika kama wiki 3 zilizopita! Binafsi sijapata nafasi ya kumwona aliyepona aliyepata kikombe.............mhhhh!!!!

Duhhhh
Pole sana mami..

Wachache nilio bahatika kuongea nao
wanamatumani na wanajisikia vema tu...
 
Ilikuwa ni kipindi cha sakata la dowans kulipwa bilioni 94! Babu wa loliondo akashika kasi!
Huku na huku mara tunasikia dowans imekuwa symbion!
Napenda sana huu muziki wa habari (single ya babu iliuza sana!)
sasa turudi kwa dowans, hivi iliishia wapi vile?! Wadau tukumbushane!
Na Babu bado hajaweka wazi hesabu za mshiko mpaka sasa. Jiandaeni kumpokea Texas, Florida au Nevada maana watu wakishatupiga changa la macho na kuzoa mabilioni wanakimbilia U. S. of A. kivulini. Na hilo ni swali zuri Katikazi, hivi Dowans tuliishalipa deni au litaingizwa kwenye gharama za umeme wa Symbion? Tutakoma. Wapiga vita ufisadi Bungeni wako wapi mbona hili limepotea kinyemera?
 
Duhhhh
Pole sana mami..

Wachache nilio bahatika kuongea nao
wanamatumani na wanajisikia vema tu...
Tuna-compile ushahidi. Tupatie contacts za hao waliopona ilil tuweze kuwajumuisha katika ushuhuda. So far hatujampata anayesema bila "lakini" kuwa amepona kabisa. Wengine hata kwa macho wanaonekana afya zao bado ni mgogoro.
 
Back
Top Bottom