Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Kwa wale waliofuatilia habari za Babu wa Loliondo, watakumbuka jinsi ambavyo baadhi yetu tulipaza sauti za kuonya kuwa dawa ya mzee huyo ilikuwa kanyaboya! Hata hivyo tulipuuzwa na kuonekana watu wa ajabu sana kwenye jamii. Kuna baadhi ya marafiki na ndugu zangu walinizuia kabisa kupinga hadharani habari ya uponyaji wa Babu wa Loliondo.
Sasa imethibitika kuwa hakuna kitu kama uponyaji katika hiyo dawa ya Babu. Binafsi niina ushahidi wa ndugu 3 wa karibu sana, ambao wametumia dawa hiyo na hawana nafuu ya aina yoyote.
Lawama sasa zinaelekezwa kwa viongozi wetu ambao walijifanya mbao za matangazo kuitangaza dawa ya Babu kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kana kwamba ilikuwa ni mwarobaini wa matatizo yetu ya afya na akili. Babu mwenyewe tayari keshawakana walioshindwa kupona kwa kueleza kuwa ni kutokana na imani yao ndogo.
Suala la Babu na tiba yake ni zito sana na viongozi wetu wanayo maswali mengi ya kujibu ingawa na sisi pia tuna mzigo mkubwa wa lawama ambao tunastahili kuubeba katika ujumla wetu. Hili ni anguko kubwa la Watanzania kama taifa na linaonesha kuwa hatuko tayari kukabiliana na mambo magumu!
Sasa imethibitika kuwa hakuna kitu kama uponyaji katika hiyo dawa ya Babu. Binafsi niina ushahidi wa ndugu 3 wa karibu sana, ambao wametumia dawa hiyo na hawana nafuu ya aina yoyote.
Lawama sasa zinaelekezwa kwa viongozi wetu ambao walijifanya mbao za matangazo kuitangaza dawa ya Babu kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kana kwamba ilikuwa ni mwarobaini wa matatizo yetu ya afya na akili. Babu mwenyewe tayari keshawakana walioshindwa kupona kwa kueleza kuwa ni kutokana na imani yao ndogo.
Suala la Babu na tiba yake ni zito sana na viongozi wetu wanayo maswali mengi ya kujibu ingawa na sisi pia tuna mzigo mkubwa wa lawama ambao tunastahili kuubeba katika ujumla wetu. Hili ni anguko kubwa la Watanzania kama taifa na linaonesha kuwa hatuko tayari kukabiliana na mambo magumu!