Tumeshinda kwenye Operation “Vaa Barakoa” sasa tuhamie kwenye Chanjo

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Hapo Mwanzo msimamo wa Rais na serikali nzima ulikuwa Tanzania HAKUNA KORONA kwa hiyo hakuna haja ya kuvaa barakoa. Baada ya wananchi, wanaharakati na baadhi ya viongozi wa dini kuonyesha msimamo wao wa kuvaa barakoa, serikali ikaanza kubadilika, tukaanza kusikia Tanzania ina korona chache sana mara hakuna aliyezuia kuvaa barakoa, mwisho wakakubali eti ukitaka kuvaa vaa za Tanzania, kwa wananchi huo ni ushindi.

Hatua inayofuata ni kuishinikiza serikali ikubali kuleta chanjo ya virusi vya korona.

Dalili ni nzuri, kwanza wameanza kusema chanjo ni ghari kitu ambacho hakina msingi wowote kwenye afya ya mtu, halafu wanasema eti hazijajaribiwa kwenye nchi za joto kama yetu sijui hizo taarifa wamezitoa wapi.

Najua mwanzo wataona aibu kukiri kama ilivyokuwa vigumu kukiri uwepo wa Covid 19, watakuja na maneno mengi wakijidai kuchagua aina ya chanjo inayofaa lkn mwisho watakuja kukubali kuileta kwa aibu kubwa.

Aluta continua.
 
Upo sahihi. Tuzidi kuwasihi viongozi wa dini, wazidi kuihimiza Serikali kuutimiza wajibu wake.

Kwa kuwa hoja ya msingi ya Serikali ni ughali wa chanjo (ule utopolo wa Mwigulu kuwa eti Dar kuna joto Ni upuuzi), tupiganie hospitali binafsi na taasisi binafsi zinazojihusisha na masuala ya afya kupewa uhuru wa kuagiza na kutoa chanjo.

Kauli ya viongozi wa dini imeonekana kuwa na nguvu kwa serikali kuweza kubaeili fikra zile zisizo sahihi dhidi ya corona, basi hawa hawa watuongoze katika kulipigania hili la chanjo. Lakini chanjo iambatane na upimaji.
 
Hapo Mwanzo msimamo wa Rais na serikali nzima ulikuwa Tanzania HAKUNA KORONA kwa hiyo hakuna haja ya kuvaa barakoa. Baada ya wananchi, wanaharakati na baadhi ya viongozi wa dini kuonyesha msimamo wao wa kuvaa barakoa, serikali ikaanza kubadilika, tukaanza kusikia Tanzania ina korona chache sana mara hakuna aliyezuia kuvaa barakoa, mwisho wakakubali eti ukitaka kuvaa vaa za Tanzania, kwa wananchi huo ni ushindi.
 
Mjifunze basi kuomba kistaarabu,,kwani mkiomba kwa unyenyekevu kitaharibika kitu?,,sio lazima kutunishiana msuli,,nna hakika mkiomba kwa staha,hizo chanjo zitakuja tu...
 
Be Careful what you wish for.

Hapo Chanjo usijepata ya Mrusi au kesho ukasikia Mkuu wa Wilaya fulani fulani amekuja na Chanjo.

Wakati chanjo zenye positive results tunasema kwamba sio za marifiki zetu.

We live in very Dangerous Times.
 
Back
Top Bottom