Tumepindisha misingi ya Public Health na tumeanza kuathirika vibaya na covid-19

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,302
24,142

Public health​

From Wikipedia, the free encyclopedia
Public health has been defined as "the science and art of preventing disease”, prolonging life and improving quality of life through organized efforts and informed choices of society, organizations (public and private), communities and individuals.[1] Analyzing the determinants of health of a population and the threats it faces is the basis for public health.


=======

Afya ina misingi yake, Public Health(Afya ya Jamii) ndio mlinzi wa kwanza wa afya ya binadamu.

Tukizembea misingi ya Afya ya Jamii, kinachofuata ni kutafuta tiba baada ya maambukizi.

Tukianzan kutafuta tiba, ugonjwa ukishampata mtu, basi ujue elimu na mazingira ya kinga yameshindikana.

Sasa hivi suala la Covid-19 linachukuliwa kimzaha mzaha, na ni katika ngazi zote.

Watu na viongozi wanakanzania na masuala ya dawa za kienyeji badala ya kuweka misingi imara ya Public Health.

Tunashangazwa Waziri wa Afya ambaye ni Daktari badala ya kukazania namna bora ya kinga, anaishia kujionyesha namna ya kujifukiza, step ambayo ni ya pili katika kupambanaa gonjwa hili.

Namna Covid inavyo enea tunajua sana kwa sasa hivi lakini kuna hatua kwa kweli zinakera, maana ndugu zetu wengi tumewapoteza hasa hizi wiki nane zilizopita.

Kiongozi anadiriki kuema HAKUNA KUVAA BARAKOA

Sijui tumweleweje?

Kuna kiongozi nafikiri huko Moshi, aliamuru waliokuwa kikao wavue barakoa.

Sijui kama ana akili timamu!

Lakini hatuwezi kumlaumu sana, ni kwa sababau wanasiasa wameamua kuliingilia hili suala la public Health bila hata wao kujua misingi yake.

Wizara ya Afya ianze kampeni mahsusi ya kuendelea kufundisha jamii jinsi ya kujikinga na gonjwa hili.
 
Nakumbuka nikiwa darasa la nne miaka ya 1972 ktk kipindi cha English, mwalimu alitukaririsha ka sentensi kanasema "Prevention is better than cure". Sijui alikuwa mwingo? Ni mpaka leo naishi kwa principle hiyo!
 
Mpaka sasa hivi, Corona ni Sawa na msemo wa wamakonde

Ukichimama, nchale, Ukikaa nchale!!

Kwa hiyo, Unapolaumu uwe na uhakika kwamba, Kwa namna zote na hatua zote za kujikinga na matamko yote ya Who yamefeli yote!!

Mungu tu, ndiye hajafeli!!
 
Mpaka sasa hivi, Corona ni Sawa na msemo wa wamakonde

Ukichimama, nchale, Ukikaa nchale!!

Kwa hiyo, Unapolaumu uwe na uhakika kwamba, Kwa namna zote na hatua zote za kujikinga na matamko yote ya Who yamefeli yote!!

Mungu tu, ndiye hajafeli!!
Mbaya zaidi ni ilekushadadia hata misingi ya afya ya jamii inapokiukwa iwe ni kwa kufahamu ama kwa makusudi,hii inazidi kuliweka taifa katika hatari ambayo yawezakuwa ya kujitafutia,mazingira ya asili tunaweza kuwa hatuna udhibiti wake,kwani mwenye uwezo huo no Mungu pekee,ila wenye mamlaka walione na wafanye uliokuwa wajibu wao.
 
Bila shasha "second wave" imekuja kwa makusudi tuweze kujua kati ya Dkt. Gwajima na Ummy nani waziri wa afya "wa kweli". Twende kazi...!!
 
Back
Top Bottom