Tumepigwa ganzi ya ufisadi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Licha ya kashfa nyingi ambazo zimeiandama serikali ya CCM inaonekana kana kwamba Watanzania siyo tu tumekuwa wavumilivu bali pia tumekuwa hatusikii tena maumivu kwani tumekuwa kama tuliopigwa ganzi ya ufisadi. Kiwango cha hasira bado hakijafikia mahali ambapo wananchi wanaweza kusema "imetosha" na badala yake tumekuwa kama tuliokubali kushindwa na tunainamisha vichwa vyetu kwa aibu.

Je, tukate tamaa na kusalimu amri na kukubali hali halisi kuwa "mambo ndivyo yalivyo?" Je tukubali kuwa utawala wa CCM ndivyo ulivyo na hivyo jitihada zetu za kuamsha fikra za watu wetu ni za bure? Kuna faida gani ya kupigia kelele ufisadi na uhalifu wa kila aina hasa kama wananchi bado wako pale pale na wanakubali yale yale?

Ni jinsi gani tunaweza kuizibua na kuizimua hii ganzi ya ufisadi ili watu waelewe kuwa mambo mengi mabovu yanayoendelea nchini yanatokana na utawala mbovu wa CCM? Ni jinsi gani tunaweza kushiriki katika ujenzi wa mawazo ya mapya ya kifikra na kuweza kuliamsha Taifa katika ujenzi mpya wa Taifa.

Sikiliza matangazo yangu ya leo nikijaribu kutafuta majibu ya maswali haya.
 
Wengine wanajikomba kwa mafisadi, wengine wanapiga mahesabu ya jinsi gani kufika kwenye ufisadi, wengine wamekata tamaa wanakwenda na Falsafa za Marijani Rajabu za "Kula Ugali wako ukalale" katika "Sikia Mambo", wengine wanatafuta uraia nchi nyingine, wengine wanapiga mayowe ya kisiasa huku wakisikilizia tumbo, wachaaache wana nia ya kweli ya kuleta mabadiliko.
 
Pundit, tufanye nini sasa tuwazirie nchi mafisadi na tukubali yaishe au wale wachache ambao wanashikilia hoja zao kama mwanga wa koroboi kwenye giza totoro waendelee kujitahidi kumulika wakiamini kuwa moto wao utawasha na mishumaa na chemli zilizozima?
 
Mtazamo wangu,
UJUE HATA CCM haikuanza tu maramoja kuwa fisadi, hii tabia ya ubinafsi na ufisadi ilianza taratibu hasa pale baada ya kuua miiko ya uongozi!, kwa vile wabongo hii hali imetuingia taratibu, itatuchukua muda kwa walio wengi kuzinduka na kungamua kinacho endelea,

lakini kwa hali ilivo sasa, ganzi hiyo imeanza kuondoka kwa kasi ya ajabu, watu wametoka usingizini, tumeshuhudia zomea zomea.. nadhani huu ni mwanzo mzuri, kinacho takiwa ni kuendelea kukaza uzi.. tuelekeopo ni kuzuri zaidi.

CCM siraha inayo itumia ni kuhakikisha wananchi wote ni masikini, then inatumia umasikini wao kuwanunua kwa chumvi na tshirt, kinacho takiwa sasa ni kununua akili yao masikini, kuwaamsha waelewe kwanini wako hivo, mpambano ndo unasonga, nina hakika tutafaulu, hakuna kukata tamaa. alutacontinua..
 
Tatizo sio ngazi
wananchi wengi wanaelewa ila tatizo ni fikra za mawazo za kidikiteta walizo nazo viongozi.

yani hawaendi pale kuleta changes ila kufuja mali na hawako tayari kuachia madaraka.
Na only best soln kwa nchi nyingi za afrika hasa Tz mabadiriko ni mpaka mtutu yani kuwatoa kwa nguvu na kuua watu kibao.
Hilo ndio mtihani unapokuja je wananchi washike mtutu?????

Kusema wananchi ni kuwaonea Zanzibar tangu 1995 hawachagui mafisadi lakini kwa ufisadi wao hako tayari kuachia madaraka labda kwa maana nyingine tuambiwe kushika mtutu? maana kwa ballot hakieleweki kitu.
 
M.Mwanakijiji

Hata mwili au akili ikipata gazi huwa inaisha na mwisho wa ganzi hiyo ni maumivu makali yasiyo na kifani. Hata Kenya yalikua hivi hivi ilipopatikana sababu(ignition point) matokeo tunayaona sasa.
Pia ikumbukwe kwa sasa watu wanatumia muda mwingi kutafuta kitu cha kula kuliko siasa ndio maana kuna ganzi fulani

Maombi yangu ni kwamba ganzi walio nayo wadanganyika ningependa iishe 2010 September ili waweze kifanya maamuzi huku wakisikia maumivu makali.

Pia ieleweke hali ya maisha kila kukicha inazidi kuwa mbaya bei ya vyakula na vitu muhimu inazidi kupanda so inaongeza chumvi kwenye kidonda.
 
Wote tunasukuma gari kuipandisha mlima lakini wapo wanaosukuma mbele badala ya nyuma. Tukisema wasukumaji wote waachie gari, gari litarudi nyuma na kupinduka. Tukiwaache wasukumaji wakae walivyo gari haliendi popote.

Tatizo liko kwenye kuondoa wale wanaosukuma kurudisha nyumba, hawa wako tayari watumie nguvu za ziada gari liporomoke ikiwa wataondolewa.

This is a catch 22 situation...
 
Na mbaya zaidi ni kwamba hao ambao CCM inajisifia kwamba ni support yake (The grassroots)ni watu wetu. Yaani I mean wajomba, mama zetu wadogo, babu, bibi walioko vijijini. Kwani wakipata matatizo huwa hawaendi CCM bali ni kutusumbua kila kukicha na vi-invoice visivyoisha.

Nadhani inabidi tuanze kuwa wawazi kwa hawa ndugu zetu extended family na hata wale wa familia moja kwamba wakiendelea kuchagua CCM na sisi tutafunga vimirija vyetu vidogodogo tulivyonavyo.

1. Haingii aiklini mtoto wa baba yako mdogo anataka umlipie asilimia 40 ya kuchangia elimu ya juu wakati baba yake ni kada wa bure CCM na haishi kuisifia lakini mabosi zake wanakula uchumi bila aibu.

2. Babu yako ambae pia ni kada wa bure wa CCM akiugua na kuja kupata matinbabu ya ziada mjini haendi pale Lumumba kwa kina makamba bali ankuja kwako, uchaguzi ukifika kura CCM. Wakati ndio hiyo iliyounda serikali iliyoshindwa kusimamia sekta ya afya.

3. Shangazi yako akibomolewa nyumba na mvua haendi CCM, lakini ndio mashabiki wakuu wa hicho chama

Kwa hiyo mzee mwanakijiji hii ganzi ya ufisadi nadhani ina loop ndefu na imejikita ndani ya uoga ile "FEAR OF THE UNKNOWNS"

Pia hata hii jamii ya vijana say middle class ya TZ ni kwamba mtu akisoma, akapata kijiajira akakopeshwa kagari (Brand new second hand RAV4)basi huwa wanaona mambo mswano tu. Hawaishi kulalamikia ugumu wa maisha lakini ni waoga na they are not ready for demand of change.

CONCLUSION

Tuwaelimishe ndugu zetu hasa wale wa vijini in a hard way. Point blank ukichagua CCM don't come to me for ur problems, uende CCM.
 
Ufisadi ni tatizo Tz, tena ni tatizo sugu. Leo tunaongelea moja, wajuaji wanaendelea na jingine, tukilishtukia hilo jingine, wao wako kwenye jingine. Hapa tunacheza mchezo wa kujificha.
Imagine tangu serikali ya Jk imeiongia madarakani ni fisadi skendo ngapi zimeongelewa, na bado zipo nyingine hatuzijui.
Leo Bot kumekucha; lakini tuna uhakika kuwa uzibuaji wa uozo huu umefanywa kwa nia njema? sio baada ya pressure? na je, wakati sisi tuko busy kujadili BoT wao wako busy wakijadili nini?
Nadhani imefika mahali watu wamechoka kuongea maana haisaidii; mchana tunapiga kelele usiku tunalala; wao usiku wanasafirisha matunda ya ufisadi. Hilo bunge limeanza tusikilize wataongea nini; si ajabu wakaanza hoja ya kuongeza marupurupu ya wabunge. Inakatisha tamaa.

Hata hivyo kuna njia mbili tu za kumaliza tatizo; tunaweza tu kuchukua moja; ama SHARI au HERI. Hilo la HERI ndio hivyo tena linakuwa hadithi za babu; na la SHARI mi naogopa kufa kwa panga... sasa nifanyeje?
 
Na mbaya zaidi ni kwamba hao ambao CCM inajisifia kwamba ni support yake (The grassroots)ni watu wetu. Yaani I mean wajomba, mama zetu wadogo, babu, bibi walioko vijijini. Kwani wakipata matatizo huwa hawaendi CCM bali ni kutusumbua kila kukicha na vi-invoice visivyoisha.

Nadhani inabidi tuanze kuwa wawazi kwa hawa ndugu zetu extended family na hata wale wa familia moja kwamba wakiendelea kuchagua CCM na sisi tutafunga vimirija vyetu vidogodogo tulivyonavyo.

1. Haingii aiklini mtoto wa baba yako mdogo anataka umlipie asilimia 40 ya kuchangia elimu ya juu wakati baba yake ni kada wa bure CCM na haishi kuisifia lakini mabosi zake wanakula uchumi bila aibu.

2. Babu yako ambae pia ni kada wa bure wa CCM akiugua na kuja kupata matinbabu ya ziada mjini haendi pale Lumumba kwa kina makamba bali ankuja kwako, uchaguzi ukifika kura CCM. Wakati ndio hiyo iliyounda serikali iliyoshindwa kusimamia sekta ya afya.

3. Shangazi yako akibomolewa nyumba na mvua haendi CCM, lakini ndio mashabiki wakuu wa hicho chama

Kwa hiyo mzee mwanakijiji hii ganzi ya ufisadi nadhani ina loop ndefu na imejikita ndani ya uoga ile "FEAR OF THE UNKNOWNS"

Pia hata hii jamii ya vijana say middle class ya TZ ni kwamba mtu akisoma, akapata kijiajira akakopeshwa kagari (Brand new second hand RAV4)basi huwa wanaona mambo mswano tu. Hawaishi kulalamikia ugumu wa maisha lakini ni waoga na they are not ready for demand of change.

CONCLUSION

Tuwaelimishe ndugu zetu hasa wale wa vijini in a hard way. Point blank ukichagua CCM don't come to me for ur problems, uende CCM.

Kwikwikwiii..
Nyambala umenifurahisha kweli kweli, undugu na siasa? lakini unacho sema kina ukweli mwingi tu!
 
Na mbaya zaidi ni kwamba hao ambao CCM inajisifia kwamba ni support yake (The grassroots)ni watu wetu. Yaani I mean wajomba, mama zetu wadogo, babu, bibi walioko vijijini. Kwani wakipata matatizo huwa hawaendi CCM bali ni kutusumbua kila kukicha na vi-invoice visivyoisha.

Nadhani inabidi tuanze kuwa wawazi kwa hawa ndugu zetu extended family na hata wale wa familia moja kwamba wakiendelea kuchagua CCM na sisi tutafunga vimirija vyetu vidogodogo tulivyonavyo.

1. Haingii aiklini mtoto wa baba yako mdogo anataka umlipie asilimia 40 ya kuchangia elimu ya juu wakati baba yake ni kada wa bure CCM na haishi kuisifia lakini mabosi zake wanakula uchumi bila aibu.

2. Babu yako ambae pia ni kada wa bure wa CCM akiugua na kuja kupata matinbabu ya ziada mjini haendi pale Lumumba kwa kina makamba bali ankuja kwako, uchaguzi ukifika kura CCM. Wakati ndio hiyo iliyounda serikali iliyoshindwa kusimamia sekta ya afya.

3. Shangazi yako akibomolewa nyumba na mvua haendi CCM, lakini ndio mashabiki wakuu wa hicho chama

Kwa hiyo mzee mwanakijiji hii ganzi ya ufisadi nadhani ina loop ndefu na imejikita ndani ya uoga ile "FEAR OF THE UNKNOWNS"

Pia hata hii jamii ya vijana say middle class ya TZ ni kwamba mtu akisoma, akapata kijiajira akakopeshwa kagari (Brand new second hand RAV4)basi huwa wanaona mambo mswano tu. Hawaishi kulalamikia ugumu wa maisha lakini ni waoga na they are not ready for demand of change.

CONCLUSION

Tuwaelimishe ndugu zetu hasa wale wa vijini in a hard way. Point blank ukichagua CCM don't come to me for ur problems, uende CCM.

Nyambala Heshima mbele Mkuu

Huo ujumbe ni mzito especially kwa wapiga kura wa leo
 
Mimi naogopa kwa sababu, huku tunakokwenda itabidi aidha tusalimu amri na kutua manyanga kwenye njia panda ya uadilifu na ufisadi na kuchagu njia pana ielekeao Ufisadini!
 
Mimi naogopa kwa sababu, huku tunakokwenda itabidi aidha tusalimu amri na kutua manyanga kwenye njia panda ya uadilifu na ufisadi na kuchagu njia pana ielekeao Ufisadini!

Huo ndio mwanzo wa kufanya maamuzi mazito. Ikiwa ni pamoja na kukataa fedha za mafisadi hata kama tutalala njaa leo kesho tuwe na maisha bora zaidi, kuliko kuchukua za mafisadi leo kesho tukalala njaa na kulalama bila mtu wa kutupa mkono wa msaada.
 
Nyambala,

Ni complicated kidogo kuliko unavyofikiri

......Mkuu mbona mkali namna hiyo, nafikiri njia bora ni kuwaelimisha tu hawa ndg zetu..........lets say CUF ndio wamechukua Ikulu na wana idadi kubwa ya wabunge.........baada ya hapo................na wao wakaangukia ktk mitego ya mafisadi..........sasa utawaambia tena ndg zako ukiwapigia CUF kura...........!!!,

Cha msingi tutumie juhudi zetu za dhati (kama anvyotushauri Azimio Jipya) kuelimisha watu wajue kinachoendelea.......

ngoja nikupe mfano.......kuna watu kama akina Rtr PM Msuya.....hata ungemuita fisadi namna gani kule Mwanga angechukua tu Ubunge.....kwani hata kama lets say alijitajirisha yeye na pia alihakikisha vitu muhimu vinafika kwao....watu wa huko huwaambii kitu, leo hii DCM akiku-endorse ujue umeula ubunge

Pia chukua mfano kama Prof Mwandosya na endorsement yake kwa Prof Mwakyusa.......check pia Nimrod Mkono ktk Jimbo lake......hivi wanjimbo wake watakuelewa kweli??.........no tusikate tamaa, tuendelee na juhudi zetu individually.........zitazaa matunda one day

i mean when it come to uchaguzi ndio utajua politics sio tu ni dirty game but also complicated game.........unajiuliza mwishoni hivi TUMEPIGWA GANZI??

tuendelee kujenga vyama bora vya upinzani na tuendelee kuwaelimisha wananchi juu ya UBAYA wa UFISADI na wahusika wake, tukianza na ndugu zetu na marafiki zetu wa karibu......tuwape data za uhakika ili hata mhusika akiulizwa swali wakti wa kampeni inakuwa a BIG HIT
 
We are addicted to corruption. Leo nimesoma mahali eti mahabusu huwatuma polisi kwenda kununua Chipsi na Kuku maana chakula cha selo ni kibovu! Sasa what is next? will the same police be able to serve, provide justice or investigate if he now receive orders from suspects?
 
i mean when it come to uchaguzi ndio utajua politics sio tu ni dirty game but also complicated game.........unajiuliza mwishoni hivi TUMEPIGWA GANZI??

tuendelee kujenga vyama bora vya upinzani na tuendelee kuwaelimisha wananchi juu ya UBAYA wa UFISADI na wahusika wake, tukianza na ndugu zetu na marafiki zetu wa karibu......tuwape data za uhakika ili hata mhusika akiulizwa swali wakti wa kampeni inakuwa a BIG HIT



Has this been discussed here at JF?! I will be surprised if not.



.
 
Kwa kweli Tanzania inapoelekea ni pabaya lakini mimi nina swali ninaomba mnisaidie--- ufisadi ni nini hasa? maana hili neno linekuwa wimbo mtu akiiba anaitwa fisadi, ubadhirifu wa pesa fisadi, rushwa fisadi am confused kwa kweli.

na kwa jinsi linavyotumika hapa ndio kabisa nashindwa kujua maana yake halisi.

1. Matumizi mabaya ya fedha za walipakodi ni ufisadi (mheshimiwa Chenga za mpira na mwenzake Mlo unaowasha)
2. Kutotimiza ahadi walizozityoa wakati wa kuomba kura nako ni Ufisadi?
3. Kusaini mikataba feki nako kunaitwa ufisadi
yaani sielewi kabisa nielimisheni then niwezechangia mada.
Nawasilisha
 
Mm,mzee mwanakijiji,hata mimi nashangaa sana.Nimekuwa nikiwaangalia watanzania kwa mshangao sana.Kama kweli ni wema kiasi cha hata kunyang'anywa tonge mkononi na wao wakanyamaza kimya Mungu awasaidie sana.Mengi ya kushangaza, mabovu mno, yanaendelea machoni petu,wala sio ufisadi tu.Viongozi wa mitaa,viongozi wa vijiji,madiwani,wabunge,viongozi wengi wa ngazi za chini na juu za serikali wanafanya vituko lakini, tunawaangalia tuu.Labda nashauri utafiti wa kina ufanywe katika miili yetu.Inawezekana kabisa hizi chanjo za kila wakati zimetufanya tuwe na utindio wa ubongo.Watu tusio diagnostic nakadhalika.
 
Back
Top Bottom