Wakuu natoka Iringa narudi Dar ila kwa sasa nipo hapa Mikumi mbugani tumepata pancha na basi la upendo lakini nje kuna simba wa 3 wamelala kwenye nyasi, cha ajabu konda na dereva wamegoma kushuka kwenda kubadili tairi wanaogopa wazee wa nyika simba.
Sasa abiria wote tumebaki tumejikunyata ndani ya basi tunasubiria labda tutapata msaada wa kuwatimua simba halafu wanaonekana wana njaa sana maana wanavyotuangalia.
Hawa wadudu wanatisha sana
Sasa abiria wote tumebaki tumejikunyata ndani ya basi tunasubiria labda tutapata msaada wa kuwatimua simba halafu wanaonekana wana njaa sana maana wanavyotuangalia.
Hawa wadudu wanatisha sana