Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Uchaguzi wa Ghana umemalizika kwa wapinzani kuchukua madaraka ya kuiongoza dola ya Ghana. Uchaguzi ulikuwa huru na wa haki kutokana na maelezo ya wanasiasa na vyombo vingi vya habari.
Je wanaona umekuwa huru na wa haki kwa wapinzani kushinda au kuna mambo mengine. Wengi walitegemea pawepo na vurugu kama uchaguzi wa Kenya na Zambia. Au ina maana Ghana wameiva kisiasa zaidi ya Kenya na Zambia. Kihistoria Ghana ni moja ya nchi za kwanza kupata uhuru barani Afrika.
Ninachoweza kusema ni kwamba tuna kitu tumejifunza. Tusitegemee chama kimoja kiwepo madarakani maisha. Chama kitakachoshinda tukubali matokeo. Wachaguaji ni wapiga kura. Tutoe matokea ya haki na kwa wakati.
Je wanaona umekuwa huru na wa haki kwa wapinzani kushinda au kuna mambo mengine. Wengi walitegemea pawepo na vurugu kama uchaguzi wa Kenya na Zambia. Au ina maana Ghana wameiva kisiasa zaidi ya Kenya na Zambia. Kihistoria Ghana ni moja ya nchi za kwanza kupata uhuru barani Afrika.
Ninachoweza kusema ni kwamba tuna kitu tumejifunza. Tusitegemee chama kimoja kiwepo madarakani maisha. Chama kitakachoshinda tukubali matokeo. Wachaguaji ni wapiga kura. Tutoe matokea ya haki na kwa wakati.