Ado Shaibu
Member
- Jul 3, 2010
- 99
- 108
Tunamshtaki Rais Magufuli Mahakamani kwa Malengo Maalum.
Tangu mwaka jana nilipokata shauri kufungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupitia kwa Mwanasheria wangu Wakili Fatma Karume kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Kilangi, kumekuwepo na mjadala kuhusu maeneo kadha wa kadha ya shauri hilo.
Sehemu yenye mjadala zaidi ni uamuzi wetu wa kumjumuisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kama sehemu ya Wajibu Maombi (Respondents). Imezoeleka, kiutamaduni kuwa "Rais hashtakiwi". Tumeaminishwa na tukaamini hivyo. Ndio maana hakuna mtu, kwa kumbukumbu zangu, tangu uhuru aliyemshtaki Rais Mahakamani hapa nchini.
Mjadala wenyewe umeongezwa na kitendo cha Rais Mwenyewe, siku ya sheria nchini kugusia suala la yeye kustakiwa. Rais aliweka bayana mshangao wake kwa watu tunaomshataki wakati ipo ibara ya 46 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayompa kinga.
Ni muhimu kufahamu kwa nini tunamshtaki Rais? Tunajifurahisha tuu ama tunayo malengo?
Mbali na sababu mbalimbali, tumelazimika kumfanya Rais kuwa Respondent kwa sababu yeye ndiye aliyemteua Mwanasheria Mkuu wa Serikali asiyekidhi sifa za kikatiba za kuwa na sifa za kuwa wakili na mtumishi wa umma kwa miaka 15. Kwa kumbukumbu zilizopo Dk. Kilangi amepata uwakili mwaka 2011 hivyo hakidhi sifa hizo zilizowekwa na Katiba.
Swali linakuja kwa nini tuendelee kumshtaki Rais wakati anayo kinga? Sisi tumesoma ibara ya 46 ya Katiba (nimeiambatanisha). Hatujaona popote kwenye ibara hiyo kuwa Rais ana kinga ya kutoguswa moja kwa moja. Tulichoona;
1. Kwenye masuala ya jinai kinga ya Rais ni absolute. Hagusiki kabisa Mahakamani
2. Kwenye masuala ya madai anayoyafanya kama Raia, kinga yake ina mipaka. Anaweza kushtakiwa lakini sharti apewe notisi kwanza.
3. Kwa makosa anayoyafanya kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama hili la kumteua Mwanasheria Mkuu asiye na sifa, hatujaona kikwazo cha kikatiba.
Hivyo basi, suala hili kuletwa mbele ya Mahakama, linaipa Mahakama nafasi ya kutoa tafsiri juu ya kinga ya Rais. Mahakama itatueleza kama kinga ya Rais ni ya kutoguswa moja kwa moja ama ina mipaka. Hii ni fursa kwa Mahakama kuimarisha jurisprudence ya eneo la kinga ya Rais specifically na uwajibishwaji wa Rais kwa ujumla.
Mahakama isingeweza kutoa ufafanuzi wake yenyewe bila kupelekewa suala hilo.
Sisi tumejitolea kulipeleka jambo hilo ili Mahakama itekeleze wajibu wake wa kutafsiri sheria.
Tunaliachia jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Kiongozi Feleshi, Masoud na Luvanda linaloendesha kesi hii lifanye kazi yake.
Ado Shaibu, Katibu Mwenezi, ACT Wazalendo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tangu mwaka jana nilipokata shauri kufungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupitia kwa Mwanasheria wangu Wakili Fatma Karume kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Kilangi, kumekuwepo na mjadala kuhusu maeneo kadha wa kadha ya shauri hilo.
Sehemu yenye mjadala zaidi ni uamuzi wetu wa kumjumuisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kama sehemu ya Wajibu Maombi (Respondents). Imezoeleka, kiutamaduni kuwa "Rais hashtakiwi". Tumeaminishwa na tukaamini hivyo. Ndio maana hakuna mtu, kwa kumbukumbu zangu, tangu uhuru aliyemshtaki Rais Mahakamani hapa nchini.
Mjadala wenyewe umeongezwa na kitendo cha Rais Mwenyewe, siku ya sheria nchini kugusia suala la yeye kustakiwa. Rais aliweka bayana mshangao wake kwa watu tunaomshataki wakati ipo ibara ya 46 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayompa kinga.
Ni muhimu kufahamu kwa nini tunamshtaki Rais? Tunajifurahisha tuu ama tunayo malengo?
Mbali na sababu mbalimbali, tumelazimika kumfanya Rais kuwa Respondent kwa sababu yeye ndiye aliyemteua Mwanasheria Mkuu wa Serikali asiyekidhi sifa za kikatiba za kuwa na sifa za kuwa wakili na mtumishi wa umma kwa miaka 15. Kwa kumbukumbu zilizopo Dk. Kilangi amepata uwakili mwaka 2011 hivyo hakidhi sifa hizo zilizowekwa na Katiba.
Swali linakuja kwa nini tuendelee kumshtaki Rais wakati anayo kinga? Sisi tumesoma ibara ya 46 ya Katiba (nimeiambatanisha). Hatujaona popote kwenye ibara hiyo kuwa Rais ana kinga ya kutoguswa moja kwa moja. Tulichoona;
1. Kwenye masuala ya jinai kinga ya Rais ni absolute. Hagusiki kabisa Mahakamani
2. Kwenye masuala ya madai anayoyafanya kama Raia, kinga yake ina mipaka. Anaweza kushtakiwa lakini sharti apewe notisi kwanza.
3. Kwa makosa anayoyafanya kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama hili la kumteua Mwanasheria Mkuu asiye na sifa, hatujaona kikwazo cha kikatiba.
Hivyo basi, suala hili kuletwa mbele ya Mahakama, linaipa Mahakama nafasi ya kutoa tafsiri juu ya kinga ya Rais. Mahakama itatueleza kama kinga ya Rais ni ya kutoguswa moja kwa moja ama ina mipaka. Hii ni fursa kwa Mahakama kuimarisha jurisprudence ya eneo la kinga ya Rais specifically na uwajibishwaji wa Rais kwa ujumla.
Mahakama isingeweza kutoa ufafanuzi wake yenyewe bila kupelekewa suala hilo.
Sisi tumejitolea kulipeleka jambo hilo ili Mahakama itekeleze wajibu wake wa kutafsiri sheria.
Tunaliachia jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Kiongozi Feleshi, Masoud na Luvanda linaloendesha kesi hii lifanye kazi yake.
Ado Shaibu, Katibu Mwenezi, ACT Wazalendo.
Sent using Jamii Forums mobile app