Tumelifanyia nini Taifa? Je tunatakiwa tufanye nini zaidi kwa taifa ?

Gembe

JF-Expert Member
Sep 25, 2007
2,483
159

Heshima Mbele,

Mchana huu nimetafakari sana maneno ambayo nimeulizwa na Ndugu Msimbe.Sanctus kaniuliza mpaka sasa nimelifanyia nini Taifa,Inawezekana likawa swali langu ila ni swali ambalo tunapaswa kujiuliza kila mmoja wetu(hata yeye kama yeye amelifanyia nini taifa?).

Ili swali si geni sababu hta wapinzani wamekuwa wakiulizwa wamelifanyia nini taifa na viongozi wa CCM na imekuwa ni swali la kawaida kuulizwa kwa mtu yeyote ambaye anaonekana ni mpinzani au anshabikia jambo flani lenye maslahi.

Ila hii si hoja ya leo ili ki-ukweli kila mtu amelisaidia taifa kwa njia moja ama nyingine na kwa wapinzania wanatakiwa wapewe nafasi(pindi wakiwa tayari )ili waoneshe wanweza kufanya nini

Wana Jamii wenzangu,
Tumekuwa wachangiaji wakubwa sana hapa, tumekuwa waandishi mahiri hapa, tumeweza kujenga hoja nzuri,nyingine zenye mbembwe na kejeli,zingine zenye mistari ilipangwa kwa sanaa ambayo inavutia ila sasa kila mmoja ajiulize amelifayia nini taifa,na tutanatikiwa tufanye nini kwa taifa hivi sasa.

Mie binafsi michango yangu humu imeweza kuleta mabadiliko makubwa sana katika taifa hili,na hii ni mifano michache tu

1.Nilikuwa mtu na kama risasi kali ambayo ilieleza umma kuhusu mikataba ya Buzwagi iliyosainiwa visivyo huko UK.

2.Nilisababisha Bunge likamng'oa Mamvi na kashfa yake ya RDC

3.Nilimwambia Mkulu kuhusu kuchukizwa kwangu na Masuala ya EPA,na nikamweleza atenganishe siasa na sheria.

MY TAKE
Mambo ambayo tuanatakiwa kujiuliza kwa sasa ni nini tufanye ili kulisadia taifa

1.Tufute yote na tuanze upya kabisa,tuwasamehe wale wote waliotufikisha hapa,ndiyo kesi za IPTL,RDC na za EPA na za kina Mramba zifutwe kuanzia mwaka huu
ili mwaka 2010 tuanze upya kabisa kujenga taifa jipya lenye misingi ya utu,lenye kujali wananchi wake,lenye viongozi wanaojua wananchi wanahitaji nini kwanza,lenye wansiasa wanaojali maendeleo ya majimbo yao.

2.Tufute ile kadhia kwamba mtu anaweza kutupa maisha Bora,hivyo tuangalie ni nani anaweza akatuongoza na siyo kutawala

Mie uwezo wangu ni kuandika,na michango yangu hapa JF imeweza kulisaidia Taifa kuondokana na wizi,ufisadi na utawala mbovu,nimeweza pia kujenga ujasiri kwa watu wengi hivyo taifa limefadika na mawazo yangu.


 
Last edited:
Ila sasa unakuwa na mawazo hasi kwa Wtz kujumuika pamoja ktk kufahamiana?

Hizi hoja zako nzuri..nakushauri pia kama mzalenzo mkakutana ktk hiyo ghafla ya Watz this week na kupanga haswa nini ktk picha pana zaidi tufanye baadae!

Big things start with small ideas!
 
Mkuu Gembe
Lazima nikupongeze kwa michango yako. Kama hakuna anayeoa umelifanyia nin taifa basi inawezekana anataka tuende hatua moja mbele zaidi. Na hilo sio dhambi kulifikiri kama matokeo yake ni mema.
Mimi naona sikubaliani na wewe kusema kuwa tuwasamehe wezi halafu tuende mbele na 2010. Hivyo tutakuwa hatulifanyii kitu taifa, sana sana tukiulizwa tutakuwa na jibu la kubwa tumelibomoa taifa. Na mafisadi wanaweza kuendelea kutuona wajinga kuliko wanavyotuona sasa. Naona ni vema kama tukiendlea na uzi ule ule mpaka utakapokatika.
 
Tuanze ktk kila familia!

kama binadam hebu anza kuwasomesha jirani zako hata wawili wasio na uwezo kwanza kama unavyofanya kwa familia yako!

Mimi nawasomesha jirani zangu watatu.. wazazi wao hawana uwezo na sasa mmoja yupo form IV, wapili form II na mdogo yupo STD IV!

Kuna mambo waweza kufanya individually mengine mnayafanya kama taifa..kama kupiga vita ufisadi!
 
Heshima Mbele,

Mchana huu nimetafakari sana maneno ambayo nimeulizwa na Ndugu Msimbe.Sanctus kaniuliza mpaka sasa nimelifanyia nini Taifa,Inawezekana likawa swali langu ila ni swali ambalo tunapaswa kujiuliza kila mmoja wetu(hata yeye kama yeye amelifanyia nini taifa?).

Ili swali si geni sababu hta wapinzani wamekuwa wakiulizwa wamelifanyia nini taifa na viongozi wa CCM na imekuwa ni swali la kawaida kuulizwa kwa mtu yeyote ambaye anaonekana ni mpinzani au anshabikia jambo flani lenye maslahi.

Ila hii si hoja ya leo ili ki-ukweli kila mtu amelisaidia taifa kwa njia moja ama nyingine na kwa wapinzania wanatakiwa wapewe nafasi(pindi wakiwa tayari )ili waoneshe wanweza kufanya nini

Wana Jamii wenzangu,
Tumekuwa wachangiaji wakubwa sana hapa, tumekuwa waandishi mahiri hapa, tumeweza kujenga hoja nzuri,nyingine zenye mbembwe na kejeli,zingine zenye mistari ilipangwa kwa sanaa ambayo inavutia ila sasa kila mmoja ajiulize amelifayia nini taifa,na tutanatikiwa tufanye nini kwa taifa hivi sasa.

Mie binafsi michango yangu humu imeweza kuleta mabadiliko makubwa sana katika taifa hili,na hii ni mifano michache tu

1.Nilikuwa mtu na kama risasi kali ambayo ilieleza umma kuhusu mikataba ya Buzwagi iliyosainiwa visivyo huko UK.

2.Nilisababisha Bunge likamng'oa Mamvi na kashfa yake ya RDC

3.Nilimwambia Mkulu kuhusu kuchukizwa kwangu na Masuala ya EPA,na nikamweleza atenganishe siasa na sheria.

MY TAKE
Mambo ambayo tuanatakiwa kujiuliza kwa sasa ni nini tufanye ili kulisadia taifa

1.Tufute yote na tuanze upya kabisa,tuwasamehe wale wote waliotufikisha hapa,ndiyo kesi za IPTL,RDC na za EPA na za kina Mramba zifutwe kuanzia mwaka huu
ili mwaka 2010 tuanze upya kabisa kujenga taifa jipya lenye misingi ya utu,lenye kujali wananchi wake,lenye viongozi wanaojua wananchi wanahitaji nini kwanza,lenye wansiasa wanaojali maendeleo ya majimbo yao.

2.Tufute ile kadhia kwamba mtu anaweza kutupa maisha Bora,hivyo tuangalie ni nani anaweza akatuongoza na siyo kutawala

Mie uwezo wangu ni kuandika,na michango yangu hapa JF imeweza kulisaidia Taifa kuondokana na wizi,ufisadi na utawala mbovu,nimeweza pia kujenga ujasiri kwa watu wengi hivyo taifa limefadika na mawazo yangu.

Hoja yako ni nzuri lakini rekebisha kidogo kwani unaponda michango ya hapa JF lakini mwishoni unajisifia wewe binafsi kwa michango yako hapa JF.

Kuwa makini usije ukabeba ile dhana ya ubinafsi ya ccm ambapo kile kinachofanywa na wao ndicho cha maana haijalishi hata kama wengine wanafanya the same thing,unapofananisha upinzani na ccm na wakati ccm inapinga mambo yote ambayo si ya chama una maana gani? Ni kivipi ulinganishe wale waliopata dhamana ya kusimamia mali za Taifa na wale wanapiga kelele kuhusu ubadhirifu?

Kwasababu ulishaponda michango ya JF kuwa hailisaidii Taifa,basi usinge refer michango yako ya JF kuwa ni ya tofauti na ya wengine na hivyo ni valuable. Unajenga classes bila kujuwa na kwa upande mwingine kwasababu wewe ni wazi una msimamo wa kiitikadi,basi ni kama politics tu.

Pili umetueleza uwezo wako wa kusikilizwa na mkuu wa nchi...Ukadai ulimwambia hivi na vile na wewe pia kudai ulisimamia issue za kashfa pale ulipopinga mikataba huko UK..Labda Gembe useme kuwa michango yako ya hapa JF na matendo yako ni tofauti?
 
This is a good question...naona wengi tuna piga sound tu bila kujiuliza nini cha maana tumelifanyia hili Taifa letu
 


1.Tufute yote na tuanze upya kabisa,tuwasamehe wale wote waliotufikisha hapa,ndiyo kesi za IPTL,RDC na za EPA na za kina Mramba zifutwe kuanzia mwaka huu
ili mwaka 2010 tuanze upya kabisa kujenga taifa jipya lenye misingi ya utu,lenye kujali wananchi wake,lenye viongozi wanaojua wananchi wanahitaji nini kwanza,lenye wansiasa wanaojali maendeleo ya majimbo yao.

Hatuwezi kuanza upya tukiwa na watu wale wale wa zamani na mawazo yale yale ya zamani. Kama kweli tunataka mabadiliko inabidi mfumo mzima ubadilike na tuanze upya kweli kweli na watu wapya na mawazo mapya.
Tuanze upya kufundishana uzalendo kwa nchi yetu na kuachana na u-MIMI. Tatizo la ufisadi ni kubwa kuliko tunavyofikiri, tujiulize ni nani kati yetu ambaye angekuwa katika nafasi ya hawa watuhumiwa angeaiachia nafasi ya kutajirika haraka?
 
Kwa maoni yangu wengi tuna nia ya kulifanyia mema Taifa letu lakini kutokana na viongozi wabovu na mafisadi walio madarakani tunashindwa kufanya hivyo. Viongozi hawa hawaambiliki na wanajiona wao ndiyo wanaojua kila kitu na kuponda ushauri wa Watanzania wengine ambao wanaitakia mema nchi yetu na wako tayari kufanya kila wawezalo ili Watanzania tupate maendeleo ya kweli.

Tuchukulie mfano wa ununuzi wa rada. Ununuzi ule ulipingwa na Watanzania walio wengi ndani na nje ya nchi yetu. Kama mtakumbuka Pesambili Mramba akatamka kwamba "hata majani Watanzania tutakula lakini rada lazima inunuliwe" matokeo yake tunayajua ya kashfa ya ufisadi wa bilioni 12. Kama ushauri wa Watanzania ungesikilizwa basi kusingekuwa na ufisadi wa rada.
Huu ni mfano mmoja tu lakini mifano kama hii ipo mingi sana na ndiyo inawakimbiza Wataalamu wetu mbali mbali kwenda nchi za nje siyo tu kufuata mishahara mizuri bali pia kuheshimiwa kama Wataalam, kupewa vitendea kazi na kuachwa wafanye kazi bila kuingiliwa na yeyote yule.
 
Wakuu, mchango kwa taifa hata kama wa mawazo kama wa hapa JF ni namna mojawapo ya kulisaidia taifa na uthibitisho wa hilo upo,, hakuna ubishi

ila sasa nimepata wasi wasi na hili wimbi la kama 'kusafishana' hapa JF...naona kuna watu wana mawazo kuwa sasa 'tuanze upya', tuachane na yaliyopita, tugange yajayo

Mimi binafsi sikubaliani na hilo vita lazima iendelee hadi kieleweke.

Tutaset a bad precedence kama tukiwaachia 'huru' watuhumiwa wetu wa ufisadi

SO mkuu wangu Gembe, mawazo yako ni mazuri sana, ila kuwaachia mimi sikubali 'hata kidogo' (tonation ya Mwalimu Nyerere)
 
Kesi dhidi ya mafisadi lazima ziendelee.
Zipo kashfa mpya zimetokea,TTCL,NA TUCTA, nadhani,na sehemu nyingine,jambo ambalo linaonyesha kwamba mafisadi hawajababaishwa na juhudi zinazoendelea.
 
Mkuu Gembe;

I think now we are talking the same language:

Mchana huu nimetafakari sana maneno ambayo nimeulizwa na Ndugu Msimbe.Sanctus kaniuliza mpaka sasa nimelifanyia nini Taifa,Inawezekana likawa swali langu ila ni swali ambalo tunapaswa kujiuliza kila mmoja wetu(hata yeye kama yeye amelifanyia nini taifa?).

Kama wote kwa nia ya dhati kabisa na uzalendo wa hali ya juu, tutajiuliza swali hili na kuchukua hatua, nina uhakika tutasonga mbele. Kuna mengi yanatokea na kuleta mabadiliko ambayo inawezekana yametokea hapa JF. Cha kujiuliza ni je, hii inatosha?

Ni nini tunafanya katika kuleta maendeleo kama watu binafsi? Katika familia, sehemu tunazoishi, kazini, katika jamii inayotuzunguka nk?

Kila mmoja kwa nafasi yake naamini kabisa kama akiamua anaweza kuleta mabadiliko katika sehemu husika. I know for sure it is possible.

So Swali hili linafaa kama tu linatafuta PRACTICAL ANSWERS na si majibu ya Kisiasa.
 
Wanabodi,
Kuna maswali ambayo huulizwa kutokana na hoja ya msingi lakini swali hili halikukaa sawa kabisa na nitasema kwa nini..
Siku zote ukisikia viongozi wanaosema umelifanyia nini Taifa huwa wana maana kuwa wao wamekwisha weka misingi bora ya Uongozi na Biashara hivyo uwezo wa ujenzi wa Taiafa sio kazi yao isipokuwa wewe mwananchi.. Ni sawa na shirika lolote hupata uzalishaji mzuri kutokana na wafanyakazi wake na ndipo swali linapolenga...huwezi kuuliza wafanyakazi umelifanyia nini shirika ikiwa shirika hilo mitambo ya kazi imesimama..
Kifupi kwa nchi yetu ni vigumu sana kuuliza swali hilo kwa sababu kwanza Kiutawala nchi yetu ni sawa na mzazi malaya ambaye anaendesha maisha yafamilia kwa kutumia Umalaya huo.. sasa unapoulizwa na mama au mtu yeyote kuhusiana na mchango wako ktk familia ni lazima iwe wazi kama ana maana kuhusiana na umalaya unaofanyika, au kupinga Umalaya huo au kitu kingeine nje ya kutegemea Umalaya wa mzazi..
Ikumbukwe tu kuwa mchango wa kila Mtanzania unategemea sera na malengo ya familia nzima sio pato linalotokana na umalaya kukabiri matatizo ya chakula ndani ya nyumba..na mchjango wa kila mwananchi utahesabika tu ikiwa yeye atapewa nguvu ya kuchangia mchango nje ya umalaya.. jambo ambalo haliwezekani Tanzania wala nyumba ya mzazi anayetegemea Umalaya..

Mchango mkubwa ni ushauri na kuomba Mungu, mzazi asijefikia kubuya Unga - kwani ndiko tunakoelekea!
 
Kama ingekuwa kunasikilizwa mtu angeweza kusema amelifanyia kitu Taifa lake,lakini utawala uliokuwepo ni mgumu hausikilizi wala haukosoleki,unategemea kufanya nini kwa hali hiyo.

Mtu huwezi kujisifu kwa kuwa tu ameondolewa Manvi na swaiba zake ,hilo halijawa kitu maana ,hao ambao umesababisha kuondolewa ,wapo na wanapeta ,hatujawaona kubeba adhabu yeyote au sheria kufuata mkondo wake juu ya yale ambayo yamewasababishia kuondoka madarakani,na inawezekana kabisa kuwa sasa hivi wapo katika hali nzuri kabisa katika kutumia kile ambacho wametuhumiwa nacho ,ni faida gani imepatikana tokea wajiuzulu ,hakuna bado Taifa limezama katika athari zilizosababishwa na watu hao ,na bado mbali ya kuwa wamejiuzulu sijui ni tija gani imepatikana ,labda mtueleze mnaosema kuwa mmesababisha fulani na fulani kuondoka madarakani ,maana kwanaza hawakuondolewa wameondoka ,na kila siku wanajisifu kuwa wameondoka wenyewe bila ya kusukumwa na mtu yeyote ,at list wanakula vinono ,kwa ufupi hawajaathirika kama ni wezi.

Jambo ambalo litaweza kufanikisha kila mtu ni kuungana na kuidai Katiba Mpya ,tume mpya ya Uchaguzi ,mahakama mpya zilizo huru ,bunge lililo huru ,vyombo vya dola vilivyo huru ,mambo yote hayo yanahitaji kuwa huru bila ya kuingiliwa na Chama Tawala.

Kinachohitajika ni kuunda umoja wa kudai mambo hayo yawe au yapewe kipau mbele kuliko jambo lingine lolote hapa Tanzania ,jambo au mambo hayo yakishawezekana tutakuwa tumepiga hatua moja kubwa sana kama ya Adam kumtafuta Eva.

Kupatikana kwa mambo hayo makuu kutawezesha kuzivua hatamu za Nchi hii kutoka kwenye Utawala wa Chama kimoja na kuzipeleka kwenye mfumo wa vyama vingi ,natumai madai haya yakivaliwa njuga ndani ya miezi mitatu serikali na utawala wa CCM lazima utasalimu amri na kuanza kuijenga Tanzania Mpya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom