Tumekwisha....Mkuu wa kituo cha polisi mbaroni kwa ujambazi

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,963
10,457
Mkuu wa kituo cha polisi mbaroni kwa ujambazi

2007-10-26 09:29:16
Na Renatus Masuguliko, PST Chato


Polisi Mkoani Kagera inamshikilia Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Bwanga, Wilayani Chato kwa tuhuma za kushiriki katika tukio la ujambazi wa kutumia silaha lililotokea wilayani humo hivi karibuni.

Wakati hilo likiendelea, watu wanaoaminika kuwa majambazi yameteka nyara mabasi matatu na kufanikiwa kuondoka na mali chache huku basi moja likipinduka katika harakati za kuyakimbia majambazi hayo.

Katika tukio la mkuu wa kituo kukamatwa, imeelezwa kuwa kunafutia wanananchi wilayani hapa wakiwemo?baadhi ya abiria?kumtambua kwamba alikuwa miongoni mwa watu wanaodaiwa kuwa majambazi katika eneo la tukio.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kagera, Bw. Abdallah Msika alithibitisha kwa njia ya simu jana kushikiliwa kwa mkuu huyo wa kituo na kumtaja kwa jina la Koplo Rajabu.

Hata hivyo, hakutaja ni lini alikamatwa kwa mahojiano lakini alisema hatua hiyo ilichukuliwa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi.

`Kwa kuzingatia utaratibu wa jeshi baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakiwemo waliokumbwa na tukio la uvamizi wa kutumia silaha lililotokea katika kijiji cha Mkungo Kata ya Busaka, wakidai kumtambua kuwepo kwenye tukio tulimkamata na tunaendelea kumhoji toka wiki iliyopita,` alisema Kamanda Msika.

`Tunataka kujua ukweli, kwani katika moja ya matukio yanayodaiwa kuwa alishiriki, sisi tunajua kuwa hakuwepo katika eneo hilo bali alikuwa wilayani Ngara kwenye operesheni maalum, lakini bado tunajiuliza kwa vipi wananchi wamtaje?` aliongeza.

Alisema kinachofanyika sasa ni kuwashirikisha wananchhi waliotoa taarifa hizo na uongozi wa polisi wilayani Ngara alikokuwa kwenye shughuli maalum kufahamu kwa kina ilikuwaje akahusishwa na kuonekana eneo la tukio.

`Kwa sasa ni mapema mno kusema kwa kina kuhusiana na tukio la kukamatwa kwake lakini nitatoa taarifa kwa vyombo vya habari baada ya uchunguzi kukamilka... Nisingependa kumhusisha moja kwa moja kuwa amekamatwa kwa kushiriki ujambazi,` alisisitiza Kamanda Msika.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka wilayani humo, mkuu huyo wa kituo anatuhumiwa kuhusika kushirikiana na majambazi walioteka magari kadhaa katika kijiji cha Mkungo likiwemo gari la hospitali.

Habari hizo zilidai kuwa kiongozi? huyo na baadhi ya watu waliokuwa wakisafiri na moja ya gari lililotekwa na majambazi hao, yaliyokuwa na silaha, walimfahamu bayana mkuu huyo na walilazimika kuwajulisa baadhi ya viongozi katika maeneo jirani.

Ilidaiwa kuwa wananchi hao walikusanyika huku wakiwa wameshatoa taarifa katika kituo cha polisi cha Buselesele na Chato ambapo walifanikiwa kuweka mawe barabarani ili kuyazuia magari yasipite.

Wakati wakiwa katika harakati hizo, gari lililokuwa likitumiwa na majambazi hao akiwemo mkuu huyo wa polisi, lilifika na mkuu huyo kuteremka haraka na kuwaambia wananchi hao kuwa lile gari lilikuwa la walinda amani hivyo waliruhusu lipite.

Wananchi hao waliliruhusu baada ya amri hiyo, lakini baada ya muda mfupi kupita? gari la polisi lilifika katika eneo hilo likilifukuza gari hilo la majambazi na walipoambiwa kuwa limekwishapita, polisi walilazimika kuwafuatilia bila mafanikio.

Wananchi hao walidai kuwa? walilaghaiwa na ofisa huyo wa polisi baada ya kudanganya kuwa gari hilo llilikuwa na watu wema na kuliruhusu kupita hatua iliyosababisha watoe taarifa kwa mara ya pili kwa mamlaka husika na hatua kuanza kuchukuliwa.
Chanzo: www.ippmedia.com
Sasa kama mpaka Mkuu wa kituo anashiriki ujambazi, sie wananchi tusiojua hata moja kuhusu matumizi ya silaha tutajilindaje?
 
Hawa maafande mbona tulishawazoea. Huyo wameamua kumtoa kafala, au alikuwa hajawasiliana na wakuu wake.
 
hee heee nimeipenda hiyo..yanii alikua hajwasilianan na wakuu wake hivyo hata wakuu nao wanaweza kuwa huwa wanahusika na mambo ya ujambazi na wizi...halafu na sie wa tanzania tumeweka imani kuwa twalindwa nao..tena tukio likitokea twawapigia na simu....
 
''Kwa sasa ni mapema mno kusema kwa kina kuhusiana na tukio la kukamatwa kwake lakini nitatoa taarifa kwa vyombo vya habari baada ya uchunguzi kukamilka... Nisingependa kumhusisha moja kwa moja kuwa amekamatwa kwa kushiriki ujambazi,'' alisisitiza Kamanda Msika.
ILIPOTOKEA WANANCHI KUVAMIA VITUO VYA POLISI WENGI WALISEMA SERIKALI IJIULIZE KWANINI WANANCHI WANAVAMIA VITUO VYA POLISI?
LEO NAMIMI NASEMA HIVI KWANINI POLISI WETU WAJIHUSISHE NA UJAMBAZI????NI WAKATI UMEFIKA KWA SERIKALI YETU WAKIWEMO VIONGOZI WA JUU HUKO POLISI(AMBAO WENGI WAO MISHAHARA YAO NI MIKUBWA TOFAUTI NA WAPIGANAJI WENGINE)KUJIULIZA NA KUTUPATIA MAJIBU KWANINI POLISI WANAJIHUSISHA NA UJAMBAZI?KUWAFUKUZA SIYO KUTATUA ILA CHANZO NININI?MASLAHI DUNI?WAKUU WAO KUJILIMBIKIZIA MALI?KUDANGANYWA KILA LEO KWA SERA ZA KIANA MWAPACHUe.g(mfuko wa afya kwa polisi)MAKAZI DUNI KAMA YA MBWA?KWA MUJIBU WA NINAVYOONA MIMI TATIZO KUBWA NI UGUMU WA MAISHA WALIONAO ASKARI WA VYEO VYA CHINI.HEBU JIFIKIRIE ASKARI ANAPEWA TSH 105,000(LAKI MOJA NA ELFU TANO)NDO MSHAHARA WA ASKARI POLISI TUNAYEMTARAJIA AKAKOSWEKOSWE NA RISASI WAKATI ANAPIGANIA MALI ZA RAIA(WAKIWEMO MAFISADI)UNAFIRI MWISHO WA SIKU ATAFIKIRIA NINI?KAMA WAKUBWA WENGI SERIKALINI WANAJIPATIA FEDHA ZA KUTOSHA KWA NJIA ZISIZO HALALI ITAKUWAJE KWA HUYU POLISI?JE ATEGEMEE MSHAHARA WAKE WA LAKI MOJA AFE KWA NJAA AU AUNGANE NA MAJAMBAZI?UNATEGEMEA WATOTO WAKE WATASOMA VIPI?KUMBUKENI MAPOLISI WA CHEO CHA CHINI NDIO WANAOKAA FRONT KTK MATUKIO YA UJAMBAZI HUKU WAKUBWA WAO WAKIWA NA REDIO CALL OFISINI.ASKARI WADOGO TUNAPOWAPA KIJIMSHAHARA KAMA HICHO MATOKEO NDO KAMA HAYO!!
KWANZA TUSHUKURU MUNGU BADO WANA NIDHAMU KWANI KTK NCHI AMBAYO HAITHAMINI ASKARI WAKE WA CHINI TANZANIA NI MOJAWAPO.SASA HUYO ASKARI ANATHAMINI VIPI NCHI AMBAYO HAIMTHAMINI?AKIENDA VITANI ATAPIGANIA VIPI NCHI AMBAYO HAIMTHAMINI?MBUNGE,WAZIRI,MKURUGENZI.MAKATIBU WAKUU NA WENYE MIVYEO MINGI TANZANIA NDIO WAKAE FRONT KWENYE VITA KWANI WAO NDIO NCHI INAONA UMUHIMU WAO NAWAO WATAONA UMUHIMU WA KUIPIGANIA NCHI YAO.SIWALAUMU SANA MAPOLISI HASA WA VYEO VYA CHINI KUWA WALA RUSHWA VINGINEVYO WAISHI VIPI?

"HII NDIYO HIVYO NDIVYO YANGU"
 
hee heee nimeipenda hiyo..yanii alikua hajwasilianan na wakuu wake hivyo hata wakuu nao wanaweza kuwa huwa wanahusika na mambo ya ujambazi na wizi...halafu na sie wa tanzania tumeweka imani kuwa twalindwa nao..tena tukio likitokea twawapigia na simu....


Huenda suala hili lipo, si unaona kesi inayomkabili afande Zombe? Si inasemekana aliwaua raia na kuwasakizia ujambazi?
 
Wanajeshi washiriki ujambazi Z’bar




na Mwandishi Wetu



JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja limesema kuna mtandao wa ujambazi Zanzibar unaohusisha baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Shutuma hizo zimetolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Amin Mahimba, siku moja baada ya kukamatwa watu watatu na kuhusishwa na matukio ya ujambazi. Kati ya watu hao, yupo askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Nyugu Salum Nyugu (35).

Kamanda Mahimba alisema kwamba askari huyo baada ya kukamatwa na kufanyiwa uchunguzi alikutwa na risasi 30 na silaha aina ya SMG, risasi 16 za bastola pamoja na magazine moja.

Aidha, kamanda huyo alisema askari huyo alikutwa na laini za simu, zikiwemo 11 za Tigo, tisa za Zantel, mbili za Vodacom na mbili za Celtel.

Alisema kwamba askari huyo na mtu mwingine ambaye ni mmiliki wa gari lililotumika katika ujambazi, walikamatwa baada ya kukamatwa dereva wa gari aina ya Suzuki ESCUDO, lililokuwa likitumika katika tukio la ujambazi.

Alisema kwamba dereva huyo alikuwa akiendesha gari lililotumika wiki iliyopita katika tukio la ujambazi kwenye duka la mfanyabiashara, Ali Mohammed Salum, katika eneo la Kidimni, Wilaya ya Kati Unguja, ambapo mfanyabiashara huyo alijeruhiwa pamoja na mali kadhaa kuibwa.

Dereva huyo alikamatwa mara baada ya tukio hilo kwa msaada mkubwa wa wananchi, huku wenzake watatu wakifanikiwa kutoroka.

Dereva huyo, Ahmed Salim Saleh (40), mkazi wa Mtaa wa Kokoni, Mji Mkongwe Zanzibar, alikamatwa baada ya askari mmoja wa JWTZ kufanikiwa kumpiga kabari alipokuwa ameegesha gari hilo majira ya saa mbili usiku huku wenzake wakifanya uhalifu.

Kamanda huyo alisema kwamba mbali na kukamatwa kwa vitu hivyo, hivi karibuni, askari huyo alinunua pikipiki aina ya Honda yenye thamani ya sh milioni mbili, yenye namba za usajili ZNZ 11919, kwa fedha zinazosadikiwa zilipatikana katika tukio la ujambazi wiki iliyopita huko Mtaa wa Fuoni.

Alisema kwamba gari hilo aina ya Suzuki ESCUDO linasadikiwa ndilo lililotumika katika matukio kadhaa ya ujambazi, ikiwemo la kuvamiwa dalali maarufu Zanzibar na kuporwa sh milioni 3.6, tukio la ujambazi Bububu na tukio la ujambazi Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Habari zilizopatikana zinasema kuwa baada ya askari huyo kukamatwa aliwataja askari wenzake watatu kutoka kambi ya KJ 12, Migombani, Mkoa wa Mjini Magharibi na KJ 11 Ubago, iliyopo Mkoa wa Kusini Unguja.

Aidha, imeelezwa kuwa baada ya dereva huyo kutoboa siri, viongozi wa jeshi waliitisha gwaride la utambulisho, ambapo askari walitakiwa kujipanga na dereva huyo kupitishwa mbele yao, lakini hakuweza kuwatambua.

Baadaye, askari hao ambao walijipanga wakiwa wamevalia sare za jeshi, waliamriwa kubadili nguo na kuvaa za kiraia, lakini dereva huyo alishindwa kuwatambua washirika wake.

Kwa mujibu wa askari mmoja aliyehusika katika gwarde hilo lililofanyika kambi ya Migombani, baadaye askari waliotajwa na dereva huyo walikamatwa na kufikishwa katika Kituo cha Polisi Mwera.

Gari aina ya Suzuki lililokamatwa lilikutwa likiwa limewekwa namba mbili tofauti, moja ikisomeka ZNZ 37360 na nyingine ZNZ 37880. Gari hilo ni mali ya Halfan Ali Sharif, mkazi wa Jang’ombe.

Mfanyabiashara aliyejeruhiwa katika tukio la ujambazi bado amelazwa katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja akiuguza majeraha aliyoyapata katika sehemu za kichwa. Hadi hivi sasa kiasi cha fedha kilichoporwa katika tukio hilo hakijafahamika.
Chanzo: Tanzania Daima, 21/01/2007



Nashindwa kuelewa shida ilipo haswaa!
Sasa kama mpaka walinzi wetu wa amani wanashiriki kutunyang'anya kile tulichowakabidhi kutulindia tukimbilie wapi?
Shida iko wapi haswa kwa hawa walinzi wetu?
1. Ni tamaa zinawatuma kupata utajiri wa haraka haraka?
2. Ni mishahara haiwatoshi?
3. Kuna mtu kawatuma?
4. Walikwenda kulipiza kisasi?

Nini chanzo cha kadhai hii?
 
Habari za wakuu hawa kushiriki kwenye ujamabazi tumekuwa tukizisikia mara kwa mara, lakini indirectly, ila hii ya mkuu kuingia front mwenyewe ni kali!!!!!! - Sidhani kwamba udogo wa mshahara unaweza kujustify vitendo kama hivi!!!!!!!!
 
Mh, kwani mlikuwa hamjui kuwa ili uwe OCS au OCD kagera lazima uwe mzee wa kazi!
 
HUUU NI MCHANGA WA MACHO WANA JF....
HATA HUYU BASI NAKUPONGEZA MKUU MMOJA ALISEMA AKUSHIRIKIANA NA MKUU WAKE,,VINGINEVYO ASINGETOLEWA KAFARA..WAPI

1)) YULE MKUU WA POLISI PALE KILIMANJARO SASA YUKO MAKAO MAKUU
AMEORODHESHA MAGARI YA KUTUPA ,NA HIVI SASA TUNAMWACHIA MUNGU,,

2))WAPI YULE MKUU WA POLICI SHINYANGA TUKADANGANYWA NA CHANGES NK,,,MPKA LEO HII
4))WAPI YULE BIBI YAKE OMAR MAHITA ALIEKUWA AMEMPA URAHISI WA MILELE KULE TANGA ALIPOKUJA WEMA AKAAMBIWA MENGI TU JUU YAKE KAISHIA KUMBADILISHA..

Mwisho ninachoona hapa ni kwamba huyu bwana atapelekwa tu KIRARACHA na kuendelea cheo chake.....

....KUMBUKENI MKUU WA POLISI (MWEMA))ALIKUJA NA MBWEMBWE NYINGI KUBADILISHA MAPOLISI NA MENGINEYO...HAKUNACHA ZIADA KILICHOFANYIKA

NAMTAKIA HERI HUYU BWANA ASITUPWE KWELI KIRARACHA MAANA HAKUNA DILI KABISA .......
 
HUUU NI MCHANGA WA MACHO WANA JF....
HATA HUYU BASI NAKUPONGEZA MKUU MMOJA ALISEMA AKUSHIRIKIANA NA MKUU WAKE,,VINGINEVYO ASINGETOLEWA KAFARA..WAPI

1)) YULE MKUU WA POLISI PALE KILIMANJARO SASA YUKO MAKAO MAKUU
AMEORODHESHA MAGARI YA KUTUPA ,NA HIVI SASA TUNAMWACHIA MUNGU,,

2))WAPI YULE MKUU WA POLICI SHINYANGA TUKADANGANYWA NA CHANGES NK,,,MPKA LEO HII
4))WAPI YULE BIBI YAKE OMAR MAHITA ALIEKUWA AMEMPA URAHISI WA MILELE KULE TANGA ALIPOKUJA WEMA AKAAMBIWA MENGI TU JUU YAKE KAISHIA KUMBADILISHA..

Mwisho ninachoona hapa ni kwamba huyu bwana atapelekwa tu KIRARACHA na kuendelea cheo chake.....

....KUMBUKENI MKUU WA POLISI (MWEMA))ALIKUJA NA MBWEMBWE NYINGI KUBADILISHA MAPOLISI NA MENGINEYO...HAKUNACHA ZIADA KILICHOFANYIKA

NAMTAKIA HERI HUYU BWANA ASITUPWE KWELI KIRARACHA MAANA HAKUNA DILI KABISA .......

Kama huku ndiko tulikofikia, basi balaa hili ni kubwa kuliko ninavyodhani!
 
Hili sio jambo la kushangaza hata kidogo hapa Bongo.Zipo habari mitaani kuwa hata baadhi Ma RPC wana vijana wao wa kazi ambao huwa wanatakiwa kuleta commission ya mapato yao monthly ili waendelee kulindwa.Huyo wa Chato ni mchezo wa kuigiza tu.
 
Back
Top Bottom