Tumekwazana sana JF

Vaislay

JF-Expert Member
Jun 26, 2011
4,532
1,822
Habari za Jumapili wana MMU na wengine wooote toka majukwaa mbalimbali...

Nipo hapa leo kwajili ya Kutafuta amani kwa sie tunaotokea kukwazana kwa somecomments,
Inafikia hatua mtu kujenga chuki na mtu humu ndani,kiasi kwamba kila wakikutana sehemu yoyote JF lazima watoleane maneno ya karaha,

Japo wengine wanasema JF stress free lakini si kweli,kuna siku zinazotokea watu na watu kupishana mpaka kutukanana au kuitana majina tofauti.

Chuki haijengi ndugu zangu, Ni makosa tu ya kuelewa au kuchukuliana kama fulani hafikiri vizuri,Sisi ni wamoja TUPENDANE,TUSHIRIKIANE,TUSIKILIZANE

Leo tuchukue nafasi hii kutakiana amani,ili tuendeleze amaniiii na upendo daima wanaJF.

Wengine si wepesi kusema samahani ,lakina hata ukimtafuta hasimu wako na kumtakia hali na salamu inatosha sanaaa.

Love u JF members, lara1 mambo shostitooo mamaa first lady
 
Last edited by a moderator:
mi kuna mtu aliniambia nalipwa 7000 ya chama fulani kisa nimemwambia asimtukanie mtu mama yake kwenye michango yako!alinichefua sana hapa msamaha sitakuja kuupokea aiss hata iweje!!mimi na siasa wapi na wapi....nimetukana kimoyomoyo!!
 
Uvumilivu muhimu, watu hupishana kiwango cha uelewa; na baadhi ya wakati tukubaliane kutokukubaliana.
 
mi kuna mtu aliniambia nalipwa 7000 ya chama fulani kisa nimemwambia asimtukanie mtu mama yake kwenye michango yako!alinichefua sana hapa msamaha sitakuja kuupokea aiss hata iweje!!mimi na siasa wapi na wapi....nimetukana kimoyomoyo!!
Hapana,ukisema hivyo unakosea,kama binadamu,inabidi tujifunze kusamehe,halafu ukiangalia hapa hatufahamiani,unasamehe
Pia haimaanishi yule unayemfahamu akikukosa usimsamehe.Tuko watu wa kila aina hapa,na kila mtu na uelewa wake.
 
Unajua wengine humu wana Mabwana humu wanahisi wanaibiwaa inabid wawe wazii kuchukiana sio mpangoooo
Jaman tupendane tu chuki haifaii
 
Unajua wengine humu wana Mabwana humu wanahisi wanaibiwaa inabid wawe wazii kuchukiana sio mpangoooo
Jaman tupendane tu chuki haifaii

Umesema kweli mkuu kuchukiana hakufai kabisa humu .Tunatakiwa tupendane na kuishi kwa amani .Mkuu Nimefurahi Sana Kusikia habari hii.Ndio maana mimi watu wote niliowaweka kwenye ignore list yangu nimewatoa hasa yule madame wa lile jukwaa na hisi yeye ndo alikuwa mtu wa kwanza ambaye nilimweka kwenye igrore list hata hivyo nimesha mtoa .NAKUTAKIA JIONI NJEMA MKUU.
 
eti mtu unaanzisha uzi wa msaada, kabla ya kujibiwa unakosolewa sana then ndo unapata jibu.. au unamsaidia mtu kwenye uzi wake then anatokea mwengine anakudis na msaada wako..

hii binafsi inanikera sana..
 
mi kuna mtu aliniambia nalipwa 7000 ya chama fulani kisa nimemwambia asimtukanie mtu mama yake kwenye michango yako!alinichefua sana hapa msamaha sitakuja kuupokea aiss hata iweje!!mimi na siasa wapi na wapi....nimetukana kimoyomoyo!!

Hahaha...kurushiana kashfa za buku 7 ni kama salamu kwenye jukwaa la siasa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom