majebsmafuru
JF-Expert Member
- May 1, 2017
- 453
- 628
Toka umetutoka hayati rais wa JMT. JPM mambo yamekuwa siyo mambo. Sijuwi tuanze wapi tumalizie wapi.
Umeme ni kukatika hovyo na kila baada ya masaa fulani. Ila wanakusingizia eti ulikuwa hutaki matengenezo wala maboresho.
Pia wanadai suluhisho siyo kufukuza watu kwa uzembe au kutokuwajibika bali kubembelezana (January Makamba)! Ndio mzee usishangae karudi kwa kishindo tena anapokezana na mama kwa safari
Swala la safari kwa viongozi ni kama wamefungulia bomba la maji. Wanaponda maisha kama wanakufa kesho
Swala la huduma ya maji ndio usiseme mzee. Wanaishi kifalme. Ungekuwepo wangejiongeza kuchimba visima ila haupo wao wamerudia tena kufanya kazi kwa mazoea
Rasimali na maliasili zinavyoibiwa ndio usiseme. Pale Mererani pamoja na ukuta wao wanapitisha Tanzanite getini
Mzee yaani nchi inavyoendeshwa ni kama bora liende. Mama ni trips every other day. Hivi hajawahi panda ndege au kwenda mamtoni nini? Maana kila raia kapigwa na butaa anavyopenda safari aise!
Juzi juzi twiga walionekana wamebebwa kwenye fuso! Wanaenda wapi hatujuwi.
Mzee yale ya kutishiana wanijuwa mie ni nani au nitakupoteza yamerudi mzee.
Yaani tuliowachaguwa na kutumwa watutumikie imekuwa nongwa. Wamekuwa miungu mitu.
Hivi mzee tukimuomba mwenyewe muumba kweli hawezi kukurudisha hata kwa miaka michache urekebishe jahazi?!
Umeme ni kukatika hovyo na kila baada ya masaa fulani. Ila wanakusingizia eti ulikuwa hutaki matengenezo wala maboresho.
Pia wanadai suluhisho siyo kufukuza watu kwa uzembe au kutokuwajibika bali kubembelezana (January Makamba)! Ndio mzee usishangae karudi kwa kishindo tena anapokezana na mama kwa safari
Swala la safari kwa viongozi ni kama wamefungulia bomba la maji. Wanaponda maisha kama wanakufa kesho
Swala la huduma ya maji ndio usiseme mzee. Wanaishi kifalme. Ungekuwepo wangejiongeza kuchimba visima ila haupo wao wamerudia tena kufanya kazi kwa mazoea
Rasimali na maliasili zinavyoibiwa ndio usiseme. Pale Mererani pamoja na ukuta wao wanapitisha Tanzanite getini
Mzee yaani nchi inavyoendeshwa ni kama bora liende. Mama ni trips every other day. Hivi hajawahi panda ndege au kwenda mamtoni nini? Maana kila raia kapigwa na butaa anavyopenda safari aise!
Juzi juzi twiga walionekana wamebebwa kwenye fuso! Wanaenda wapi hatujuwi.
Mzee yale ya kutishiana wanijuwa mie ni nani au nitakupoteza yamerudi mzee.
Yaani tuliowachaguwa na kutumwa watutumikie imekuwa nongwa. Wamekuwa miungu mitu.
Hivi mzee tukimuomba mwenyewe muumba kweli hawezi kukurudisha hata kwa miaka michache urekebishe jahazi?!