Tumeingiliwa! na nadhani nchi imeshauzwa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Mwalimu Nyerere na Wamarekani tangu lini!? :confused:

Wamarekani wafunza askari wa JWTZ
Mwandishi Wetu
Daily News; Thursday,February 14, 2008 @00:05

MAREKANI imeanza kutoa mafunzo kwa askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambao watatumika katika shughuli za kulinda amani, imefahamika.

Ubalozi wa Marekani umeeleza katika taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari kwamba mafunzo hayo yalianza Januari 21 katika sehemu ambayo haikutajwa, ikiwa ni mchango wa nchi hiyo katika kutekeleza kwa vitendo ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika kudumisha amani.

"Mwalimu Nyerere alikuwa na ndoto ya kuwa na Afrika ambayo ina amani, yenye utulivu na yenye haki. Alitaka Tanzania iwe mstari wa mbele katika kuhakikisha ndoto hiyo inatimizwa.

"Katika kufuata mfano wake, Rais Jakaya Kikwete anajiandaa kupeleka askari wa kulinda amani katika maeneo kama Darfur na Somalia. Marekani inajivunia katika kumsaidia Rais Kikwete na JWTZ katika kutekeleza nia hiyo," taarifa hiyo ya ubalozi imesema.

Msaada wa Marekani unatolewa kupitia programu inayofahamika kama Acota na unahusisha mafunzo na vifaa kwa batalioni tatu. Batalioni ya kwanza iliyoanza mafunzo Januari inatarajiwa kumaliza mafunzo hayo ya wiki 10 mwishoni mwa mwezi ujao na itakayofuata itaanza Aprili.

Vifaa vinavyotolewa na Marekani katika mafunzo hayo ni vya mawasiliano, jenereta, vifaa vya tiba, vya kuchujia maji na kufahamu eneo (GPS). Kabla ya mafunzo yanayosaidia na Marekani, Tanzania ilikuwa tayari imepeleka Polisi-Wanajeshi 77 huko Lebanon kama sehemu ya Jeshi la Kulinda amani la Umoja wa Mataifa. Nafasi zao zitachukuliwa na askari wengine 85 ambao walifunzwa na Marekani chini ya mpango wa Acota.

Tangu kuanzishwa kwa programu ya Acota zaidi ya wanajeshi 92,000 kutoka Afrika wamefunzwa kuhusu masuala ya ulinzi wa amani na lengo ni kufikisha askari 228,000 ifikapo 2010.

Nchi nyingine ambazo zimenufaika chini ya Acota ni Benin, Botswana, Burkina Faso, Cameroon, Ethiopia, Gabon, Ghana, Kenya, Malawi, Mali, Msumbiji, Niger, Nigeria, Rwanda, Senegal, Afrika Kusini, Uganda na Zambia.
 
Mkuu wa Majeshi anakujwa tembelea kituo na kukifungua rasmi "AFRICOM"!

Kishoka, is it confirmed that Tanzania will be a base for AFRICOM? i would really like to know this. It is very interesting to know where our government stand on this!
 
Una maanisha Joji Bushi!?

NDio maana yake...JK hatimaye amekubali; zile safari nyingi za Marekani tuliambiwa ni kuleta wawekezaji sasa ndio hawa wanakuja na bunduki zao.

Mimi naona hii pengine ni nafasi nzuri kwa dada na kaka zetu kupata watoto wengi tu wenye damu za kizungu...!!
 
Jiandaeni dada zenu kubakwa na wanajeshi wakimaekani kama wanavyofanya huko japan... na jinsi wanawake wakibongo walivyo na tamaa. Mbaya zaidi huyu muungwana anawa sevu majamaa uhuru wetu kama waiter wa rose garden. Siunajua inabidi ngozi nyeusi ndio zikafe Somalia na kwengineko in their secret war.TUMEKWISHA.. welcome to the AMERICAN EMPIRE...
 
Hapa kweli tumeingilia na tusipokuwa makini tutakaliwa kabisa...marekani hana urafiki usio na faida asilani..sasa ni kweli tunashuhudia zile trip za vasco da gama ndani USA..sijui tuite matatizo ya baadae au matunda ya sasa?!Kuna habari kuwa pale AIRPORT wamefunga system zao mpya za usalama na kuondoa za kwetu kisa haziaminiki! Huyu George kichaka kweli mbabe Sidhani Vasco da gama hata akienda Comoro kama wawezakubadilisha System ya usalama...Kichaka anakuja kukamilisha Ndoa yetu na wao
 
Haya, siri za ujio wa bushi zinaanza kufichuka. Tunawapeleka vijana wetu wakauliwe huko. Bush anamajeshi kede kede na yanavifaa kede kede vya kisasa kabisa, kwa nini asipeleke jeshi lake?

Kikwete, kama unataka ku-play role ya kulinda amani Darfur, naomba ufanye kama ulivyofanya kwa Somalia, hao wanaotaka kulinda amani waje hapa wafunzwe na usipeleke kabisa vijana wetu huko. Mama yangu weee, tunatumbukizwa pabaya sana na hawa wa Merekani. Eeeh Mwenyeezi Mungu wetu, inusuru Tanzania, wanusuru wa Tanzania na baa hili linalo tunyemelea.
 
Hapa naona mna wasiwasi usio na msingi. Kuna ubaya gani kupewa mafunzo ya kijeshi na Marekani? Jeshi letu lazima lifundishwe namna ya kutumia technolojia mpya za kivita. Kama sio Marekani basi nani afanye hiyo kazi?

Mnanikumbusha wakomunisti wa zamani ambao walidhani kila kinachohusu Marekani ni kibaya. They have been consigned to the dustbin of History, and the US thrives.

Ingekuwa vema sana kama Marekani ingeweka makao makuu ya Africa Command yao Tanzania. Ingetusaidia kwa namna nyingi mno. Ingekuza utalii na mawasiliano ya aina mbali mbali, na hata kungeweza kuweko direct flights kati ya New York na Dar.
Hamjasema kwa nini mnaogopa Marekani. Si maadui wetu. Wanaweza kuwa mapatna wazuri sana.
 
Hapa naona mna wasiwasi usio na msingi. Kuna ubaya gani kupewa mafunzo ya kijeshi na Marekani? Jeshi letu lazima lifundishwe namna ya kutumia technolojia mpya za kivita. Kama sio Marekani basi nani afanye hiyo kazi?

Mnanikumbusha wakomunisti wa zamani ambao walidhani kila kinachohusu Marekani ni kibaya. They have been consigned to the dustbin of History, and the US thrives.

Ingekuwa vema sana kama Marekani ingeweka makao makuu ya Africa Command yao Tanzania. Ingetusaidia kwa namna nyingi mno. Ingekuza utalii na mawasiliano ya aina mbali mbali, na hata kungeweza kuweko direct flights kati ya New York na Dar.
Hamjasema kwa nini mnaogopa Marekani. Si maadui wetu. Wanaweza kuwa mapatna wazuri sana.

Why now!? Walikuwa wapi miaka yote 46 tangu tupate uhuru? Hawakuijua Tanzania miaka hiyo iliyopita sasa ndio wamesikia kwamba kuna kanchi kanaitwa Tanzania na ghafla tu wakajenga interest kubwa na nchi yetu!? Tuwaogope kabisa hawa urafiki wao ni wa undumila kuwili na historia juu ya urafiki wao ipo ya kutosha kabisa. Wanafukuzwa na wajapan kila kukicha lakini hawana mpango wa kuondoka. Wakiingia kwetu basi itakuwa ni balaa tupu maana tutakuwa hatuna uhuru wa kuamua lolote bila wao kulikubali au watajenga uadui na sisi.

Sasa hivi hakuna nchi hata moja ya kiafrika iliyowakubalia kujenga kituo chao cha kijeshi katika Afrika, sasa inaelekea wameitarget Tanzania ili wajenge kituo hicho. Pia kupatikana kwa uranium nchini kwetu na uwezekano wa kupatikana mafuta kumewafanya hawa jamaa wenye tamaa kubwa ya rasilimali hizo kufanya kila njia kuhakikisha rasilimali hizo ndani ya nchi yetu zinakuwa chini ya control yao. Kumbuka hawa Wairaq walikuwa ni rafiki zao wakubwa sana, mara tu walipokataa kuwasikiliza basi wakawa maadui.

Jeshi letu limefundishwa na Watanzania wenyewe na limeweza kupambana na nduli na kumtwanga vizuri sana pia linasaidia kulinda amani katika nchi mbali mbali duniani hivyo tuna jeshi zuri tu ambalo halihitaji mafunzo toka kwa hawa mandumila kuwili

Fungua macho uone history ya urafiki wa Marekani siku zote si urafiki wa kweli ndio maana negative attributes zao ni kubwa mno kuliko positive attributes hata katika nchi wanazoziita ni marafiki kama UK, France, Germany etc. Kama umesikia Hillary katika kampeni zake anasema kwamba kama akishinda basi Clinton atakuwu ambassador wa kujenga upya reputation ya marekani iliyobomoka all over the World. Open your eyes bro.

 
Labda unaweza usimpende Bush, lakini kwa nini usiwapende Wamarekani? Ni watu tu kama Waingereza, Wajerumani n.k., ambao tuna uhusiano mzuri nao. Au umekuwa kama Wairani ambao wanasema Waamerika ni mashetani?

Watanzania wanaipenda Marekani, ndio maana wengi wangetaka kwenda kuishi huko, na baadhi wamefanya hivyo. Hata hivyo, lazima tuangalie maslahi ya taifa letu, kama vile Wamarekani wanavyoangalia maslahi ya taifa lao daima. Iwapo tutawekeana mkataba wa ushirikiano, lazima tuwe macho tusiuze taifa kwa mkataba mbaya.

Tuna swala hapa la cost / benefit analysis. Kwa kipengele hicho, mimi naona faida ya kuwa na kituo cha jeshi la marekani Tanzania inazidi sana hasara zake. Kenya ina kituo cha jeshi la Marekani. Sidhani hilo limeingilia uhuru wa Kenya.

Sidhani kama Marekani ingetaka kuwa na kituo cha jeshi Tanzania. Kama ingetaka, basi kwa maoni yangu faida yake ingezidi sana hasara zake.

Wako mafundamentalist wengi wasiotaka kusikia chochote kinachohusu Marekani. Tusiwaige bila kufikiria wenyewe maslahi ya taifa letu. Kila shetani na mguu wake.
 
Labda unaweza usimpende Bush, lakini kwa nini usiwapende Wamarekani? Ni watu tu kama Waingereza, Wajerumani n.k., ambao tuna uhusiano mzuri nao. Au umekuwa kama Wairani ambao wanasema Waamerika ni mashetani?

Watanzania wanaipenda Marekani, ndio maana wengi wangetaka kwenda kuishi huko, na baadhi wamefanya hivyo. Hata hivyo, lazima tuangalie maslahi ya taifa letu, kama vile Wamarekani wanavyoangalia maslahi ya taifa lao daima. Iwapo tutawekeana mkataba wa ushirikiano, lazima tuwe macho tusiuze taifa kwa mkataba mbaya.

Tuna swala hapa la cost / benefit analysis. Kwa kipengele hicho, mimi naona faida ya kuwa na kituo cha jeshi la marekani Tanzania inazidi sana hasara zake. Kenya ina kituo cha jeshi la Marekani. Sidhani hilo limeingilia uhuru wa Kenya.

Sidhani kama Marekani ingetaka kuwa na kituo cha jeshi Tanzania. Kama ingetaka, basi kwa maoni yangu faida yake ingezidi sana hasara zake.

Wako mafundamentalist wengi wasiotaka kusikia chochote kinachohusu Marekani. Tusiwaige bila kufikiria wenyewe maslahi ya taifa letu. Kila shetani na mguu wake.
ClemensStareMcNamee2.jpg
 
Labda unaweza usimpende Bush, lakini kwa nini usiwapende Wamarekani? Ni watu tu kama Waingereza, Wajerumani n.k., ambao tuna uhusiano mzuri nao. Au umekuwa kama Wairani ambao wanasema Waamerika ni mashetani?

Watanzania wanaipenda Marekani, ndio maana wengi wangetaka kwenda kuishi huko, na baadhi wamefanya hivyo. Hata hivyo, lazima tuangalie maslahi ya taifa letu, kama vile Wamarekani wanavyoangalia maslahi ya taifa lao daima. Iwapo tutawekeana mkataba wa ushirikiano, lazima tuwe macho tusiuze taifa kwa mkataba mbaya.

Tuna swala hapa la cost / benefit analysis. Kwa kipengele hicho, mimi naona faida ya kuwa na kituo cha jeshi la marekani Tanzania inazidi sana hasara zake. Kenya ina kituo cha jeshi la Marekani. Sidhani hilo limeingilia uhuru wa Kenya.

Sidhani kama Marekani ingetaka kuwa na kituo cha jeshi Tanzania. Kama ingetaka, basi kwa maoni yangu faida yake ingezidi sana hasara zake.

Wako mafundamentalist wengi wasiotaka kusikia chochote kinachohusu Marekani. Tusiwaige bila kufikiria wenyewe maslahi ya taifa letu. Kila shetani na mguu wake.

Kwanza sikubaliani nawe kwamba tunahitaji kuwa na kambi ya kijeshi ya Marekani ili tuendeleze uchumi wetu, i.e, utalii na hayo madege ya moja kwa moja. Tunaweza kuvipata vyote hivyo bila ya kujiuza kwa njia hiyo.

Pili, ninakubaliana na wewe kwamba si lazima Mmarekani atutongoze kiasi hiki kwa sababu ya kutafuta sehemu ya kuweka hiyo kambi, kwani hapo Kenya wanaililia kila siku (labda pawe na sababu maalum inayomzuia kuiweka hapo). Ni lazima pana sababu nyingine ya mhimu sana tusiyoijua inayosababisha hawa watu wawe na nia nasi kiasi hiki sasa hivi. Kwa vyovyote ni sababu ya msingi kwa manufaa yao.

Hilo la sisi kuwa waangalifu na mikataba itakayowekwa ili isitugandamize, sina shaka hapo hata wewe nadhani unatania.

Ninachojua ni kwamba kama watawala wetu wameamua kutuingiza, basi tuwe tayari kuyakubali matokeo yake mengi, mengine yasiyokuwa mazuri sana kwetu.
 
Haya, siri za ujio wa bushi zinaanza kufichuka. Tunawapeleka vijana wetu wakauliwe huko. Bush anamajeshi kede kede na yanavifaa kede kede vya kisasa kabisa, kwa nini asipeleke jeshi lake?

Kikwete, kama unataka ku-play role ya kulinda amani Darfur, naomba ufanye kama ulivyofanya kwa Somalia, hao wanaotaka kulinda amani waje hapa wafunzwe na usipeleke kabisa vijana wetu huko. Mama yangu weee, tunatumbukizwa pabaya sana na hawa wa Merekani. Eeeh Mwenyeezi Mungu wetu, inusuru Tanzania, wanusuru wa Tanzania na baa hili linalo tunyemelea.


It is difficult to believe I am on the same side with zomba today; hata kama ni kwa sababu tofauti.
 
Tumekwisha ingiliwa kwa kupitia mlango wa KIA( Chai Maharage)
Kilicho baki ni kukaza uzi tuimarishe elimu ili Technolojia ikue.

Wazee hao wa kazi wakiingiaga huwa hawatokkagi hata siku moja.

Nyerere alikuwa na uhusiano wa Karibu kabisa na JFK, kwa hiyo si jambo geni wamarekani kuingia na kuweka kambi Tanzania, it was abaout time.

Baada ya kennedy kuuawa Nyerere aligeukia kwa akina Mao.

Kwa muda mrefu tumejifanya eti hatufungamani na upande wowote wakati kuna watu tunawaunga mkono na wengine tunawakandia. Huko ndo kuto fungamana na upande wowote?
 
Tumekwisha ingiliwa kwa kupitia mlango wa KIA( Chai Maharage)
Kilicho baki ni kukaza uzi tuimarishe elimu ili Technolojia ikue.

Wazee hao wa kazi wakiingiaga huwa hawatokkagi hata siku moja.

Nyerere alikuwa na uhusiano wa Karibu kabisa na JFK, kwa hiyo si jambo geni wamarekani kuingia na kuweka kambi Tanzania, it was abaout time.

Baada ya kennedy kuuawa Nyerere aligeukia kwa akina Mao.

Kwa muda mrefu tumejifanya eti hatufungamani na upande wowote wakati kuna watu tunawaunga mkono na wengine tunawakandia. Huko ndo kuto fungamana na upande wowote?

TEKNOLOJIA YA NINI WAKATI WATU WANANJAA

KWANZA TUSHIBE NA TUWE NA CHAJKULA CHA KUTOSHA KISHA MAMBO MENGINE BAADAE
 
NDio maana yake...JK hatimaye amekubali; zile safari nyingi za Marekani tuliambiwa ni kuleta wawekezaji sasa ndio hawa wanakuja na bunduki zao.

Mimi naona hii pengine ni nafasi nzuri kwa dada na kaka zetu kupata watoto wengi tu wenye damu za kizungu...!!


There is no such a thing called "free lunch"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom