rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
Tumeamua kwenda Arumeru ili kusaidia kwenye ulinzi wa kura za Chadema,nia yetu ni kuchangia katika mabadiliko ya taifa letu,viongozi wachache wa Chadema wakiachiwa peke yao mabadiliko yatachukuwa muda mrefu na inawezekana kizazi chetu tusiyaone au kushuhudia matunda ya mabadiliko kama wenzetu Zambia wanavyo shuhudia,wapenda mabadiliko mlio karibu na maeneo haya naomba mjitokeze kwa wingi kuhakikisha jimbo linachukuliwa na Chadema!!natoa mwito kwa wapenda mabadiliko nchi nzima kushiriki katika mapambano ya ukombozi kwa sababu kazi hii ni ngumu kuachiwa watu wachache,Mungu ibariki Tanzani!!