MKEHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 714
- 1,137
Siku hizi nimeanza kupata wasiwasi sana juu ya utambulisho wetu wa makabila. Sijui nini kinatokea kwenye jamii zetu.
Juzi nilikiwa na kijana mmoja kutoka mkoani Mara katika kujitambulisha mpaka nilishtuka sana, kwani kwenye utambulisho wake sikusikia majina niliyo yazoea kutoka mkoa huo kama Marwa, Mwita, Nyambaza, Marogo na kadhalika.
Unakuwaje Mkurya halafu unaajina yote ya kizungu? Eti Mkurya anaitwa James Michael Charles.
Kuna sehemu tunakwama sana kama taifa.
Si kwa Wakurya pekee, hata Wahaya majina kama Rwechungura, Rweikaza, Mjwahuzi, Rwegoshora yanaishia taratibu.
Waha nao majina kama Ndalichako, Bhilikundi, Bhilikunzira, Chubwa, Kalankwiye hayapo tena, kule Mbeya nako majina kama akina Mwandosya, Mwampiki, Mwakatika yanapungua sana.
Kule Tanga Lushoto akina Shebughe, Shelutete yako mwishoni sana kuishia.
Zamani kwa Wachaga ilikuwa ni kawaida sana kusikia majina kama Kileo, Munisi, Shayo nao siku hizi umkuta Mchaga anaitwa Albert Robert Bryson. Hii ni hatari sana.
Kuna haja ya kupitisha sheria kila Mtanzania kumlazimisha jina lake la tatu angalau liwe la ukoo ambalo ni UNIQUE na liwe la kibantu kabisa vinginevyo tutapoteza utambulisho wetu kama taifa na majina hayo kupotea.
Zamani mtu akijitambulisha umajua kabisa katokea upande gani wa Tanzania kwa kutaja jina kale tu.
Kwa nchi kama Rwanda na Burundi bado wanatumia sana majina yao ya asili kama ilivyo pia kwa Nigeria na Ghana kuna majina ukiyasikia moja kwa moja unajua yanatokea nchi hizo
Juzi nilikiwa na kijana mmoja kutoka mkoani Mara katika kujitambulisha mpaka nilishtuka sana, kwani kwenye utambulisho wake sikusikia majina niliyo yazoea kutoka mkoa huo kama Marwa, Mwita, Nyambaza, Marogo na kadhalika.
Unakuwaje Mkurya halafu unaajina yote ya kizungu? Eti Mkurya anaitwa James Michael Charles.
Kuna sehemu tunakwama sana kama taifa.
Si kwa Wakurya pekee, hata Wahaya majina kama Rwechungura, Rweikaza, Mjwahuzi, Rwegoshora yanaishia taratibu.
Waha nao majina kama Ndalichako, Bhilikundi, Bhilikunzira, Chubwa, Kalankwiye hayapo tena, kule Mbeya nako majina kama akina Mwandosya, Mwampiki, Mwakatika yanapungua sana.
Kule Tanga Lushoto akina Shebughe, Shelutete yako mwishoni sana kuishia.
Zamani kwa Wachaga ilikuwa ni kawaida sana kusikia majina kama Kileo, Munisi, Shayo nao siku hizi umkuta Mchaga anaitwa Albert Robert Bryson. Hii ni hatari sana.
Kuna haja ya kupitisha sheria kila Mtanzania kumlazimisha jina lake la tatu angalau liwe la ukoo ambalo ni UNIQUE na liwe la kibantu kabisa vinginevyo tutapoteza utambulisho wetu kama taifa na majina hayo kupotea.
Zamani mtu akijitambulisha umajua kabisa katokea upande gani wa Tanzania kwa kutaja jina kale tu.
Kwa nchi kama Rwanda na Burundi bado wanatumia sana majina yao ya asili kama ilivyo pia kwa Nigeria na Ghana kuna majina ukiyasikia moja kwa moja unajua yanatokea nchi hizo