Tumeachana lakini mwenzangu ananitafuta ugomvi kilazima

Villky_J

JF-Expert Member
Mar 14, 2017
492
607
Habari wandugu wa jamii forum.

Yupo binti mmoja tuliyekuwa na mahusiano ya kimapenzi hapo..awali kutokana na sababu mbali mbali tukajikuta kila mtu anashika njia yake. Upande wangu, sikuwahi kumtukana wala kafanya chochote cha kumuuzi.

Cha ajabu mwenzangu ameanza kunitukana mitandaoni nikipost picha kwenye page yangu..anaandika comment za ajabu za kunishusha heshima yangu, nimejaribu kwenda nae kistaarabu naona mwenzangu namvimbisha kichwa. Sasa wadau hebu nishaurin maana wanasema hasira hasara, huyu mtu nimfanye nn kinacho mstahili.

Ili ajue mahusiano sio ndoa..maana anakoelekea anazid kunichafulia heshima yangu niliyoijenga kwa miaka mingi kwenye jamii, halafu yeye anakuja kuvuruga kirahisi rahisi.
 
mblock acha ujinga
giphy.gif
 
Nimesha m block waungwana ila cha kushangaza anaandika hadi sms za kawaida kibaya zaid anatumia namba tofauti..nashindwa kubadili namba sababu namba yangu natumia kwenye mambo yangu ya kibiashara
 
Ukiachana na mtu unatakiwa umfungie vioo vyote na kuweka tinted kali
 
Nimesha m block waungwana ila cha kushangaza anaandika hadi sms za kawaida kibaya zaid anatumia namba tofauti..nashindwa kubadili namba sababu namba yangu natumia kwenye mambo yangu ya kibiashara
Ni bora akikutumia kwenye No yako kuliko huko fb. Funga acct yako ya fb.
 
Mkuu, najua mtihani ulionao, mm iliwahi kunitokea kwa mchaga mmoja, uuuwi, yaani, nilikuwa nikiposti kitu anaandika we bwege tu, aliwahi kuja mpaka ofisini akaongea stit sana, akatishia kuniloga, akachunguza nilienae akaanza kumtumtukana. Aise, niliteseka sana mpaka nilipobadili namba
 
Habar wandugu wa jamii forum.
Yupo binti mmoja tuliyekuwa na mahusiano ya kimapenz hapo..awali kutokana na sababu mbali mbali tukajikuta kila mtu anashika njia yake. Upande wangu, sikuwahi kumtukana wala kafanya chochote cha kumuuzi.
Cha ajabu mwenzangu ameanza kunitukana mitandaoni nikipost picha kwenye page yangu..anaandika comment za ajabu za kunishusha heshima yangu, nimejaribu kwenda nae kistaarabu naona mwenzangu namvimbisha kichwa. Sasa wadau hebu nishaurin maana wanasema hasira hasara, huyu mtu nimfanye nn kinacho mstahili. Ili ajue mahusiano sio ndoa..maana anakoelekea anazid kunichafulia heshima yangu niliyoijenga kwa miaka mingi kwenye jamii, halafu yeye anakuja kuvuruga kirahisi rahisi.


!
!
Mpuuze au mblock, au labda sijaelewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom