The Humble Dreamer
JF-Expert Member
- Oct 12, 2015
- 7,440
- 10,232
Wakuu Salaam:
Siku za karibuni kumekuwa na usambaaji wa video chafu kwenye mitandao ya kijamii na jambo hili linaendelea kukua miongoni mwa wanafunzi wa Elimu ya juu.
Na waliohusika katika video wapo pamoja na kwamba kumekuwa na matamko toka uongozi wa vyuo lakini bado hakuna fundisho.
Hawa wanafunzi wa vyuo vikuu watakapohitimu ndiyo wanaotegemewa kuwa viongozi na wazalishaji katika sekta mbalimbali ili kuinua maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.
TCU wanatakiwa kuwafuta usajili wote waliohusika kwenye hizo video na wasipewe nafasi ya kusoma chuo chochote kabisa.
Kila mtu ni kama kashazoea habari kama hizi kusikika, hakuna maadili tena. Unakaa siku 2,3 unapata habari mpya.
Wanafunzi wa elimu ya juu tatizo liko wapi hadi kufikia hatua hii?
TCU chukueni hatua.
Siku za karibuni kumekuwa na usambaaji wa video chafu kwenye mitandao ya kijamii na jambo hili linaendelea kukua miongoni mwa wanafunzi wa Elimu ya juu.
Na waliohusika katika video wapo pamoja na kwamba kumekuwa na matamko toka uongozi wa vyuo lakini bado hakuna fundisho.
Hawa wanafunzi wa vyuo vikuu watakapohitimu ndiyo wanaotegemewa kuwa viongozi na wazalishaji katika sekta mbalimbali ili kuinua maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.
TCU wanatakiwa kuwafuta usajili wote waliohusika kwenye hizo video na wasipewe nafasi ya kusoma chuo chochote kabisa.
Kila mtu ni kama kashazoea habari kama hizi kusikika, hakuna maadili tena. Unakaa siku 2,3 unapata habari mpya.
Wanafunzi wa elimu ya juu tatizo liko wapi hadi kufikia hatua hii?
TCU chukueni hatua.