Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,444
- 7,792
Mkurugenzi wa Uchaguzi: Tume ya uchaguzi baada ya kupokea pingamizi dhidi ya wagombea hao, imewataarifu wawekewa pingamizi mapema iwezekanavyo na wahusika wamewasilisha utetezi wao.
Pingamizi dhidi ya mgombea wa CUF kwamba hakurudisha fomu kwa mujibu wa masharti yaliwekwa na sheria, tume baada ya kupitia sababu za pingamizi pamoja na utetezi uliotolewa imejiridhisha, Professa Ibrahim Haruna Lipumba amerejesha fomu zake kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya tume ya taifa ya uchaguzi hivyo tume ya taifa ya uchaguzi imejiridhisha pingamizi halina msingi na imelitupilia mbali. Professa Ibrahim Lipumba anaendelea kuwa mgombea halali wa kiti cha Rais kupitia chama cha CUF.
Pingamizi dhidi ya mgombea wa CCM
- Mleta pingamizi anadai kwamba, mgombea Urais kwa tiketi ya CCM hakuambatanisha picha kwenye fomu ya uteuzi.
- Hakurudisha fomu ya uteuzi kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na sheria
Kwa mujibu wa kanuni ya 39 kanuni ndogo sita ya kanuni za uchaguzi wa Rais na wabunge za mwaka 2020, sababu za uamuzi huu wa tume watapewa kwa maandishi, aliyeweka na aliyewekewa pingamizi, kwa msingi wa uamuzi huu, vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mkuu wa kiti cha Rais na makamu wa Rais vinabaki kuwa 15.
Imetolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi
Pia soma; Tundu Lissu awawekea pingamizi wagombea wawili wa nafasi ya Urais wa Tanzania. John Magufuli (CCM) na Prof. Ibrahim Lipumba(CUF)