Duplicate_90
JF-Expert Member
- Mar 29, 2020
- 272
- 308
Mwisho wenu waja acheni kutapatapa...
Ungetuambia ni kwa namna gani Tume sio independent ingependeza zaidi otherwise haya mapendekezo wanayotaka Tume ndio mambo ambayo muda wote wananchi na wadau wanazitaka.Tume ya sasa ni takataka kama takataka nyingine tu, tume inapaswa kuwa independent isiyoweza kuingiliwa na serikali.
Ni mapendekezo mazuri lakini tume ikiendelea kuteuliwa na mwenyekiti wa chama tawala ambaye pia ni mgombea mtarajiwa, Tume hiyo haitakuwa huru hata kama itakuwa na ofisi mpaka ngazi ya kata!Tume ya Taifa ya UCHAGUZI (NEC) inapendekeza yafuatayo:-
1. Sheria ya Uchaguzi irekebishwe ili kuongeza ufanisi.
2. Tume iwe na watumishi wake mpaka ngazi ya Wilaya.
3. Kuwe na sheria moja ya Uchaguzi.
4. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na Tume.
5. Wanaopita bila kupingwa Wabunge na Madiwani wapigiwe kura za NDIYO/ HAPANA.
6. Asasi zinazotoa elimu ya Uraia ziwezeshwe na Serikali.
=====
NEC YATOA MAPENDEKEZO 5 KUJIENDESHA KIUFANISI
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa mapendekezo matano kwa serikali kutaka itungwe Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi itakayoiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Mwenyekiti wa NEC , Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage alitoa mapendekezo hayo kwa Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwasilisha taarifa Taarifa ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2020 Ikulu Dar es Salaam jana.
Alisema tume kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, iliendesha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kwa pamoja walitoa mapendekezo hayo waliyoyawasilisha kwa Rais.
Aliyataja mapendekezo hayo kuwa ni pamoja na kutungwa kwa Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo itaiwezesha Tume kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Mapendekezo mengine ni kuwepo na watendaji wa Tume hadi ngazi ya halmashauri, mamlaka husika ziangalie uwezekano wa kuunganisha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa Sura ya 292 ili kurahisisha utekelezaji wa sheria hizo.
Pia Tume ilipendekeza kuwa sheria za uchaguzi zitafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili pamoja na serikali kuangalia uwezekano wa kuziwezesha kifedha asasi na taasisi zinazotoa elimu ya mpiga kura katika hatua mbalimbali za mchakato wa uchaguzi.
Akijibu kuhusu mapendekezo hayo, Rais Samia alisema yote ni ya msingi na jambo muhimu ni kwa wadau kuyajadili kwa kina na kupeleka mapendekezo yao serikalini ili ione namna itakavyoweza kuyafanyia kazi.
Hata hivyo, Samia alisema changamoto aliyoiona ni pale serikali ilipotakiwa kuwa na wasimamizi wa kudumu wa uchaguzi mpaka ngazi ya halmashauri jambo ambalo litasababisha kuwa na bajeti kubwa.
“Lakini lile pendekezo la kuzisaidia Taasisi za Kiraia nalo litabebesha mzigo mkubwa wa fedha serikalini. Lakini yote yanazungumzika na yanaweza yakafanyiwa kazi,”alisema Rais Samia.
Samia alisema kupitia uchaguzi, wananchi wanapata fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka na pia uchaguzi unawafanya viongozi waliochaguliwa kufanya kazi kwa kujiamini kwa kuwa wana ridhaa ya wananchi wanaowaongoza.
Alisema pamoja na ukweli huo, ili uchaguzi ukidhi malengo hayo, ni lazima usimamiwe vizuri na kinyume chake uchaguzi unaweza kuwa chanzo cha fujo na vurugu kama inavyotokea kwenye baadhi ya nchi.
Alipongeza NEC kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuendesha vizuri uchaguzi wa mwaka jana.
Baadhi ya wadau wa uchaguzi akiwamo aliyekuwa Mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia Makini, Cecilia Mmanga, alisema ripoti hiyo ya Tume ni nzuri na aliunga mkono kauli ya Rais Samia ya kuwataka wanawake kujitokeza kugombea nafasi za uongozi wa kisiasa.
“Wanawake tujitokeze kwa wingi uchaguzi ujao. Najua kuna tatizo la mfumo dume lakini pia tamaduni na mila zetu bado zinamwona mwanamke hawezi, baadhi ya vyama vya siasa bado vinakandamiza wanawake,”alisema Mmanga.
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo, aliunga mkono ushauri wa Rais Samia wa kutaka sheria ziangaliwe upya ili zisitumike kunyima watu haki ikiwemo kuenguliwa kwa kukosea kuandika jina pamoja na kuwa na watendaji wa NEC hadi ngazi ya halmashauri.
Viongozi mbalimbali walishuhudia makabidhiano ya ripoti hiyo kati ya Tume na Rais Samia. Miongoni mwao ni Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Hussein Katanga.
Chanzo: Habari leo
Tume ya uchaguzi (NEC)haitakiwi kuwa na wafanyakazi wa kudumu kwa ajili ya kusimamia uchaguzi. Uchaguzi ni mchakato...is a process. NEC itawajibika kuwaajiri kwa muda (on temporary basis) wasimamizi wa uchaguzi kwa muda mwafaka. Hivyo suala la budget haliwezi kuwa shida. Nchi nyingi zinafanya hivi...wakati wa uchaguzi ukiwadia watu wenye sifa za kuwa returning officers na wote watakaosimamia uchaguzi wataomba hizi kazi kwa NEC kwa kipindi maalumu na baada ya uchaguzi kumalizika mkataba unaishia hapo. Hii ni gharama ya kawaida kama nchi inataka kutenda HAKI, kuleta maendeleo na amani kwa raia wake.Tume ya Taifa ya UCHAGUZI (NEC) inapendekeza yafuatayo:-
1. Sheria ya Uchaguzi irekebishwe ili kuongeza ufanisi.
2. Tume iwe na watumishi wake mpaka ngazi ya Wilaya.
3. Kuwe na sheria moja ya Uchaguzi.
4. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na Tume.
5. Wanaopita bila kupingwa Wabunge na Madiwani wapigiwe kura za NDIYO/ HAPANA.
6. Asasi zinazotoa elimu ya Uraia ziwezeshwe na Serikali.
=====
NEC YATOA MAPENDEKEZO 5 KUJIENDESHA KIUFANISI
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa mapendekezo matano kwa serikali kutaka itungwe Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi itakayoiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Mwenyekiti wa NEC , Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage alitoa mapendekezo hayo kwa Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwasilisha taarifa Taarifa ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2020 Ikulu Dar es Salaam jana.
Alisema tume kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, iliendesha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kwa pamoja walitoa mapendekezo hayo waliyoyawasilisha kwa Rais.
Aliyataja mapendekezo hayo kuwa ni pamoja na kutungwa kwa Sheria ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo itaiwezesha Tume kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Mapendekezo mengine ni kuwepo na watendaji wa Tume hadi ngazi ya halmashauri, mamlaka husika ziangalie uwezekano wa kuunganisha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa Sura ya 292 ili kurahisisha utekelezaji wa sheria hizo.
Pia Tume ilipendekeza kuwa sheria za uchaguzi zitafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili pamoja na serikali kuangalia uwezekano wa kuziwezesha kifedha asasi na taasisi zinazotoa elimu ya mpiga kura katika hatua mbalimbali za mchakato wa uchaguzi.
Akijibu kuhusu mapendekezo hayo, Rais Samia alisema yote ni ya msingi na jambo muhimu ni kwa wadau kuyajadili kwa kina na kupeleka mapendekezo yao serikalini ili ione namna itakavyoweza kuyafanyia kazi.
Hata hivyo, Samia alisema changamoto aliyoiona ni pale serikali ilipotakiwa kuwa na wasimamizi wa kudumu wa uchaguzi mpaka ngazi ya halmashauri jambo ambalo litasababisha kuwa na bajeti kubwa.
“Lakini lile pendekezo la kuzisaidia Taasisi za Kiraia nalo litabebesha mzigo mkubwa wa fedha serikalini. Lakini yote yanazungumzika na yanaweza yakafanyiwa kazi,”alisema Rais Samia.
Samia alisema kupitia uchaguzi, wananchi wanapata fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka na pia uchaguzi unawafanya viongozi waliochaguliwa kufanya kazi kwa kujiamini kwa kuwa wana ridhaa ya wananchi wanaowaongoza.
Alisema pamoja na ukweli huo, ili uchaguzi ukidhi malengo hayo, ni lazima usimamiwe vizuri na kinyume chake uchaguzi unaweza kuwa chanzo cha fujo na vurugu kama inavyotokea kwenye baadhi ya nchi.
Alipongeza NEC kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuendesha vizuri uchaguzi wa mwaka jana.
Baadhi ya wadau wa uchaguzi akiwamo aliyekuwa Mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia Makini, Cecilia Mmanga, alisema ripoti hiyo ya Tume ni nzuri na aliunga mkono kauli ya Rais Samia ya kuwataka wanawake kujitokeza kugombea nafasi za uongozi wa kisiasa.
“Wanawake tujitokeze kwa wingi uchaguzi ujao. Najua kuna tatizo la mfumo dume lakini pia tamaduni na mila zetu bado zinamwona mwanamke hawezi, baadhi ya vyama vya siasa bado vinakandamiza wanawake,”alisema Mmanga.
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo, aliunga mkono ushauri wa Rais Samia wa kutaka sheria ziangaliwe upya ili zisitumike kunyima watu haki ikiwemo kuenguliwa kwa kukosea kuandika jina pamoja na kuwa na watendaji wa NEC hadi ngazi ya halmashauri.
Viongozi mbalimbali walishuhudia makabidhiano ya ripoti hiyo kati ya Tume na Rais Samia. Miongoni mwao ni Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Hussein Katanga.
Chanzo: Habari leo
Sick, hivi hata kwa uelewa mdogo unashindwa kufahamu ya kuwa tume ikiwa huru haitawezekana kuiwekea pressure or rather watumishi kuwekewa pressure na serikali(chama kilicho madarakani) na kutokuogopa kupoteza ajira kwa kutofuata matakwa ya serikali(chama kilicho madarakani).Ungetuambia ni kwa namna gani Tume sio independent ingependeza zaidi otherwise haya mapendekezo wanayotaka Tume ndio mambo ambayo muda wote wananchi na wadau wanazitaka.