Elections 2010 Tume ya uchaguzi ijumuishe pia wapinzani

Mantissa

JF-Expert Member
Jul 24, 2010
876
166
Nachelea kusema kuwa mamlaka aliyopewa Rais kuunda tume ya uchaguzi anyang'anywe mara moja kwani hapo hakuna democrasia hata kidogo. Nafikiri ijumuishe pia wapinzani ili kuondoa huu upuuzi unaofanyika. Si rahisi mtu aliyeteuliwa na rais kutangaza matokeo ambayo yanamuangusha mtu aliyemweka hapo. Mfano sahihi mnajionea wenyewe pale ambapo matokeo yanachakachuliwa live na CCM. Tufike mahali tuseme hapana kwani hakuna haki inayotendeka.

Jamaa mmoja kada wa CCM nilipoongea nae, alidai hapa duniani hakuna haki hata kidogo, ukisubiria haki utakufa maskini. Hili ni jibu tosha kuonesha kuwa tutaendelea kutawaliwa kibabe kama hivi ilivyo sasa.

Inaniuma sana
 
Tume HURU ni ile ambayo haiuhusishi members wa chama chochote na haichaguliwi na Rais/serikali a(i)liyeko madarakani....
 
Back
Top Bottom