Uchaguzi 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yamtangaza Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu ya pili

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imemtangaza Dkt. John Magufuli, aliyekuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kuwa mshindi wa Uchaguzi uliofanyika Oktoba 28. Pia imemtangaza Mama Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu wa Rais Mteule.

Dkt. Magufuli ameshinda kwa kupata kura 12,516,252 (sawa na 84.4% ya kura halali) akifuatiwa na aliyekuwa mgombea wa Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu ambaye amepata kura 1,933,271 (sawa na 13.04% ya kura halali)

Dkt. Magufuli ambaye pia ni Rais wa Tanzania amepata ridhaa ya kuongoza kwa muhula wa pili kama Marais waliotangulia.

Tume imesema walikuwa na jumla ya watu 29,754,699 waliojiandikisha kupiga kura, na waliopiga kura walikuwa 15,091,950. Kura halali zilikuwa 14,830,195 huku kura 261,755 zikiwa zimeharibika.

Magu.jpg
 
Si wangemtangaza tu kabla hata ya kampeni, kuliko kuekti sinema ya matrillioni kwa kodi zetu, tungeokoa hayo matrillioni yakasaidia kutubambikizia kesi zisizo na dhamana wananchi na kununua virungu vilivyo vunjika baada ya kutupiga navyo.

Natamani Mw. Nyerere afufuke kwa siku moja, aje ajionee.

#LINK# Askari polisi wakamata shehena za mabegi yenye kura zilizopigwa nje ya kituo, zilikua zinaingizwa kwa njia ya panya ndani ya vituo vya kupigia kura. Washangaa na kukiri kuna defender la polisi limejaa shehena ya mabegi ya kura zilizokamatwa kama vielelezo.



Zitto Tundu Lissu
 
Back
Top Bottom