Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Uchaguzi, (NEC), Lawamani Kuwaengua Wagombea Kwa Hoja Nyepesi Nyepesi, Je ni Ukiukwaji wa Haki za Binaadamu? Jicho Letu

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,578
Wanabodi,
Naafuatilia kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kinachorushwa live na Star TV kila Jumamosi asubuhi, kwenye kipindi cha leo, kutoka Mwanza, kinaongozwa na mkongwe, Doto Bulendu, na wageni wake waandishi wakongwe, Moses Mathew na Odero, na Dar es Salaam yuko Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri, Neville Meena.

Mjadala unahusu Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Uchaguzi, (NEC), imeingizwa lawamani kwa kitendo chake cha kuwaengua wagombea mbalimbali kwa makosa madogo madogo ya ujazaji wa fomu, au kwa hoja nyepesi nyepesi, ambazo hazina mashiko ya kisheria kumfanya mgombea akose sifa na uhalali wa kugombea, mwanajopo mmoja akasema, kinachofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ni ukiukwaji wa haki za binaadamu!.

Mwana jopo huyo, amesema, kanuni za uchaguzi zimeeleza wazi kuwa kabla fumu haijapokelewa, huwa inahakikiwa. Lengo la uhakiki ni kurekebisha dosari ndogo ndogo za ujazaji fomu hiyo, na kutolea mfano, kuna mgombea ameenguliwa kwa dosari ndogo tuu ya kutumia initio ya jina lake.

Kugombea ni moja kati ya haki za msingi za binaadamu ziliziainishwa kwenye Katiba ya JMT, hivyo kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwaengua baadhi ya wagombea kwa dosari ndogo ndogo ni ukiukwaji wa haki za wagombea.

Mwendeshaji kipindi, Mkongwe Doto Bulendu, amelipongeza Jukwaa la Wahariri, kuwapatanisha TBC na Chadema, baada ya Chadema kuwafukuza TBC kwenye kampeni zao. Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri, Neville Meena, amezipokea shukrani hizo kwa shingo upande kwa kutumia msemo wa lugha ya Kilatini, kuwa "hupaswi kushukuriwa kwa kutimiza wajibu wako".

Meena amekiri waandishi wa habari na vyombo vya habari, havikutimiza wajibu wake kikamilifu kwa kunyamazia unfairness iliyofanywa na NEC kuwaengua wagombea na kukubali pingamizi zenye hoja nyepesi nyepesi. Kama media zingeliangazia suala hili kikamilifu, lingeisaidia NEC kutenda haki.

Pia NEC, imeingizwa lawamani, kwa kuelezwa kuwa uamuzi wa NEC kuengua wagombea ni uamuzi wa mwisho, final and conclusive, huu ni udikiteta. Katiba ya JMT, inaeleza wazi mahakama ndio mamlaka ya mwisho ya utoaji haki, sasa NEC isipotenda haki, kwa kumuengua mgombea kwa maonevu, mgombea kama huyu aende wapi?.

Jopo pia limeilaumu sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayafanya uwanja wa mapambano usiwe sawa, kwa mgombea mmoja kugombea huku akiwa ni rais wa JMT, anagombea na urais mkononi, halafu anashindana wagombea wengine with nothing!. Usawa uko wapi? Japo limenote kuna wakati mgombea mmoja anatoa ahadi za kampeni ambazo ni firm akiwa kama ni rais wa JMT na sio kama mgombea wa CCM.

My Take
Lawama hizi kwa NEC, zisiposhughulikiwa in time, zitatuharibia matokeo ya uchaguzi wetu kwa kusababisha bitterness ndani ya mioyo ya watu kuwa uchaguzi Mkuu ujao sio huru na haki. Dhulma hii itasababisha accumulation ya bad karma, ambayo itakuja kuponza watu mbele ya safari kwa wahusika na dhulma Hugo kukumbwa na majanga ya ajabu!. Na kitu kibaya kuhusu karma, huwa inawatandika wahusika na wasio husika, kwasababu wameona dhulma hiyo na walikuwa na uwezo wakuzuia but they did nothing.

Kwavile JPM na CCM watashinda kwa ushindi wa kishindo kikubwa anyway na anyhow, naiomba Tume ya Taifa Uchaguzi, iache milango wazi kwa wagombea wote wa vyama vyote hata wenye mapungufu, waruhusiwe tuu, wajaribu na washindwe wenyewe ili kuizuia bad karma ya kutumia kudhulumiwa. Watakaposhindwa kwenye sanduku la kura, hata wasipate sababu na visingizio, na hata wakiumia, hakuna karma.

Paskali
 
Wagombea wengi wa Upinzani walivunja kanuni za Uchaguzi makusudi ili waondolewe
Kwasababu hawana uhakika wa ushindi hata 1%
 
Bora hata ingekua ukiukwaji wa haki!! Wanachokifanya Tume ya Uchaguzi wakishilikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri (Makada wa CCM walioshindwa kwenye mchakato wa kura za maoni wa mwaka 2015) ni kitendo cha kitoto kinachofanywa na watu wazima.

Mbaya zaidi huu utoto ulianza rasmi mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 kupita. Ipo siku majibu ya hivi vitendo yatakuja kuonekana. Na kwa nini wanao enguliwa wawe ni wagombea wa vyama vya upinzani tu!!!

Yaani wagombea wa CCM tu ndiyo wenye sifa ya kujaza vizuri! Na iweje kama mtu amekosea kujaza asiitwe aje arekebishe kasoro zake?

Kwa nini mapingamizi yasiwe ni yale ya msingi tu? mfano kama mgombea ni mhamiaji haramu na ushahidi wa wazi upo, mgombea ana matatizo ya akili, nk. Hii kitu inakera sana! Na inakera zaidi pale unapoona inafanywa na watu "waliosoma" Eti Madokta wenye PhD!!
 
Ni kweli, NEC inanajisi katiba katika vipengele vifuatavyo

1. Katiba inasema mamlaka yote yatatoka kwa wananchi

2. Kila Mtanzania mwenye vigezo vinavyojulikana ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa.

Kitendo chochote cha kuweka vizingiti ili kuthibiti vipengele hivyo viwili ni kuonyesha kuwa NEC haijitambui in the first place. NEC ilianzishwa ili kimsingi kutetea principle hizo mbili.

NEC ilipaswa kuzilinda hizo principles kwa wivu mkubwa sana. Lakini bahati mbaya inaongozwa na watu shortsighted ambao akili zao zinawatuma kulipa fadhila kwa waliowateua badala ya katiba ya nchi
 
Msitake kuilaumu NEC pekee kwa lengo la kumnusuru Muhusika Mkuu wa mambo haya ambayo awamu zilizopita hatakuyashuhudia kwa kiwango hiki.

NEC kwa kushirikisha na Wasimamizi wa Uchaguzi , wanafanya haya kumfurahisha Bwana fulani aliejiapiza kuua upinzani by 2020.
Ushahidi ni kuwa Jiwe alishayatamka maneno yafuatayo "Ninakupa nyumba nzuri ya kuishi, gari ya kifahari ya kutembelea na mshahara mnono, halafu nisikie unamtangaza mpinzani ameshinda kwenye eneo lako, jihesabu kuwa umeshajifukuzisha kazi" mwisho wa kunukuu.

Kama alivyoeleza mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chadema, alipoongea na waandishi wa habari wa hapa nchini pamoja na wamiliki wao, kuwa nchi hii imejazwa HOFU, HOFU, HOFU, na watawala wa serikali hii ya kidhalimu ya awamu ya tano. Full Stop.
 
Naona Mosses Mathew amepanick sana hapo studio. Huo ni muendelezo wa wanaccm karibu wote kupanick pindi haki inapozungumziwa. Huyo Odero anakata issue kwa uhakika bila kupanick. Huu uhuni unaondelea kwenye chaguzi za nchi hii, unaagizwa na Magufuli kutokana na kiburi cha madaraka.
 
Wanabodi,
Naafuatilia kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kinachorushwa live na Star TV kila Jumamosi asubuhi, kwenye kipindi cha leo, kutoka Mwanza, kinaongozwa na mkongwe, Doto Bulendu, na wageni wake waandishi wakongwe, Moses Mathew na Odero, na Dar es Salaam yuko Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri, Neville Meena.

Mjadala unahusu Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Uchaguzi, (NEC), imeingizwa lawamani kwa kitendo chake cha kuwaengua wagombea mbalimbali kwa makosa madogo madogo ya ujazaji wa fomu, au kwa hoja nyepesi nyepesi, ambazo hazina mashiko ya kisheria kumfanya mgombea akose sifa na uhalali wa kugombea, mwanajopo mmoja akasema, kinachofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ni ukiukwaji wa haki za binaadamu!.

Mwana jopo huyo, amesema, kanuni za uchaguzi zimeeleza wazi kuwa kabla fumu haijapokelewa, huwa inahakikiwa. Lengo la uhakiki ni kurekebisha dosari ndogo ndogo za ujazaji fomu hiyo, na kutolea mfano, kuna mgombea ameenguliwa kwa dosari ndogo tuu ya kutumia initio ya jina lake.

Kugombea ni moja kati ya haki za msingi za binaadamu ziliziainishwa kwenye Katiba ya JMT, hivyo kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwaengua baadhi ya wagombea kwa dosari ndogo ndogo ni ukiukwaji wa haki za wagombea.

Mwendeshaji kipindi, Mkongwe Doto Bulendu, amelipongeza Jukwaa la Wahariri, kuwapatanisha TBC na Chadema, baada ya Chadema kuwafukuza TBC kwenye kampeni zao. Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri, Neville Meena, amezipokea shukrani hizo kwa shingo upande kwa kutumia msemo wa lugha ya Kilatini, kuwa "hupaswi kushukuriwa kwa kutimiza wajibu wako".

Meena amekiri waandishi wa habari na vyombo vya habari, havikutimiza wajibu wake kikamilifu kwa kunyamazia unfairness iliyofanywa na NEC kuwaengua wagombea na kukubali pingamizi zenye hoja nyepesi nyepesi. Kama media zingeliangazia suala hili kikamilifu, lingeisaidia NEC kutenda haki.

Pia NEC, imeingizwa lawamani, kwa kuelezwa kuwa uamuzi wa NEC kuengua wagombea ni uamuzi wa mwisho, final and conclusive, huu ni udikiteta. Katiba ya JMT, inaeleza wazi mahakama ndio mamlaka ya mwisho ya utoaji haki, sasa NEC isipotenda haki, kwa kumuengua mgombea kwa maonevu, mgombea kama huyu aende wapi?.

Jopo pia limeilaumu sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayafanya uwanja wa mapambano usiwe sawa, kwa mgombea mmoja kugombea huku akiwa ni rais wa JMT, anagombea na urais mkononi, halafu anashindana wagombea wengine with nothing!. Usawa uko wapi?. Japo limenote kuna wakati mgombea mmoja anatoa ahadi za kampeni ambazo ni firm akiwa kama ni rais wa JMT na sio kama mgombea wa CCM.

Paskali
Ni woga wa CCM, ni ishara ya kutojiamini na ni kipimo cha incapacity ya serikali hii.
 
Halafu NEC wanaona sawa na kufurahi kuona mgombea amepitishwa bila kupingwa!
Yaani NEC ina sahau kabisa kuwa, jukumu lake la msingi ni kuhakikisha watu wanagombea na wanachi wanachagua mgombea wanayemtaka katika uchaguzi. Na ikitokea jambo hilo halifanyiki ipasavyo, maana yake NEC imeshindwa kutimiza wajibu waje, hivyo viongozi wake wajiuzuru na chombo hicho kiundwe upya.
 
Soma maamuzi ya ZEC dhidi ya mapingamizi aliyowekewa Maalim Seif ndio utajua kuwa NEC ni tume isiyo huru, isiyo ma weledi na iliyojaa wahuni.

Kwakifupi, NEC wamevuliwa nguo na kuonekana ni wapumbavu, wazandiki na watu wasiolitakia mema taifa letu.
 
Yaani vyama vinawahamasisha wanachama wao wajitokeze kugombea, wanachama wakutosha wanajitokeza ndani ya vyama vyao kuomba kuteuliwa, wanashindana vyema, kisha vyama vinateua wagombea wanaoonekana kuwa bora. Ghafla tu tume ya uchaguzi inakuja kuwaengua kwa sababu za kiuwendawazimu tu.

Huu ni upumbavu.
 
Tume ya uchaguzi Tanzania Ni kituko sana! Eti inamuengua mtu kisa ajajaza fomu vzuri. Kwani kumuita aje arekebishe mnapungukiwa na nn
 
Back
Top Bottom