RAKI BIG
JF-Expert Member
- Apr 26, 2020
- 394
- 456
Taarifa ya Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ndg. Ado Shaibu, leo tarehe 02 Juni 2020.
Chama cha ACT Wazalendo kinasikitishwa na kupinga vikali mwenendo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuendesha mchakato wa mabadiliko ya Kanuni mbalimbali za Uchaguzi bila kuwashirikisha vya kutosha wadau wa uchaguzi hasa vyama vya siasa. Hadi sasa, Tume imekwisharekebisha Maadili ya Uchaguzi na sasa kwa maelezo ya Mwenyekiti wa Tume Jaji Semistocles Kaijage, ipo mbioni kukamilisha marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi za Madiwani, Wabunge na Urais.
A. Maadili ya Uchaguzi
Tarehe 27 Mei 2020, NEC iliitisha kikao cha wadau kwa ajili ya mjadala wa Maadili ya Uchaguzi. Cha kushangaza, NEC ilipanga ratiba ya kujadiliana, kufanya marekebisho na vyama kusaini maadili yaliyopitishwa ndani ya masaa machache (saa mbili hadi saa nane mchana). Licha ya maboresho machache kufanyika, NEC ilivilazimisha vyama kusaini siku hiyohiyo bila kuwasilisha kwanza toleo la mwisho la Maadili ya Uchaguzi lililojumuisha marekebisho husika.
Chama cha ACT Wazalendo ambacho mimi nilikiwakilisha kiligomea kusaini na kuomba haki ya kusaini baada ya kuona toleo la mwisho la Maadili ya Uchaguzi lenye maboresho yaliyotokana na maoni ya wadau. Jawabu la NEC kuwa Chama ambacho hakitasaini Maadili ya Uchaguzi siku hiyo hakitashiriki kampeni, lilitulazimisha kusaini sambamba na vyama vingine vilivyosaini siku hiyo.
B. Kanuni za Uchaguzi
Kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa mjadala wa Maadili ya Uchaguzi, Mwenyekiti wa NEC Ndugu Jaji Kaijage aligusia kuwa mchakato wa kukusanya maoni kwa ajili ya marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi (Madiwani, Wabunge na Urais) umefanyika na NEC ipo mbioni kuzikamilisha. NEC inakusudia kufanya hivi bila kuwepo kwa kikao cha wadau kujadili rasimu ya mwisho ya Kanuni husika. Swali la kujiuliza ni kwa nini NEC inakwepa majadiliano na wadau? Ina jambo gani inalolificha? Ina njama gani kwenye kanuni za mwaka huu?
Rasimu za Kanuni ambazo zimewasilishwa kwetu zina mapungufu mengi. Licha ya kwamba tumeiandikia NEC kutoa maoni yetu, ni dhahiri NEC inataka kuyapuuza ndio maana inakwepa kikao cha wadau. Baadhi ya mapungufu kwenye rasimu hizo yanahatarisha amani na yanaweza kuitia nchi kwenye machafuko iwapo yataachwa kama yalivyo.
Baadhi ya mapungufu hayo ni;
i). Mawakala kunyimwa hati za viapo
Rasimu ya Kanuni zote mbili, ya Uchaguzi wa Madiwani na ya Uchaguzi wa Wabunge na Rais hazina sharti kwa wasimamizi wa uchaguzi kuwapa hati za viapo mawakala wa vyama vya siasa. Kanuni zote zimeweka utaratibu wa Wasimamizi wa Uchaguzi kutuma orodha na utambulisho wa mawakala kwa wasimamizi wa vituo. Kwa uzoefu, utaratibu huu utatumika kuwahujumu mawakala wengi wa vyama vya upinzani. Wasimamizi wa Uchaguzi wasio waadilifu watatumika kutowasilisha majina ya mawakala wa vyama vya upinzani.
ii). Mawakala kutopewa nakala za matokeo
Rasimu za Kanuni za Uchaguzi hazijaweka sharti kwa mawakala wa vyama vya siasa kupewa nakala za matokeo. Kanuni hizo zinasema nakala za matokeo zitatolewa iwapo kutakuwa na nakala za kutosha! (Kanuni ya 56(2) ya Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani na kifungu cha 63(2) cha Kanuni za Uchaguzi wa Wabunge na Rais). Swali la kujiuliza ni kuwa NEC haikujiandaa kwa uchaguzi? Haina hata fedha za kuzalisha nakala za kutosha na kuepusha mizozo isiyo ya lazima?
iii). Waangalizi wa Uchaguzi Kuzibwa Mdomo
Rasimu za Kanuni za Uchaguzi zinatumia lugha ya hiyari kwa NEC kuwaalika waangalizi wa kimataifa. Kanuni hizo pia zinakataza waangalizi wa kimataifa na wa ndani kuripoti kwa vyombo vya habari mapungufu ya uchaguzi watakayoyaona wakati uchaguzi ukiendelea (Kifungu cha 20(2)(j) cha Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani) na Kanuni za Wabunge na Rais.
Kuwawekea masharti waangalizi wa uchaguzi kuripoti baada ya uchaguzi kukamilika ni sawa na kuwaziba mdomo.
iv). Mfumo mbovu wa kuwajibisha Wasimamizi wa Uchaguzi
Rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani (Kanuni ya 66(1) na kifungu cha 74(1) cha Kanuni za Uchaguzi wa Wabunge na Rais) zinatamka kuwa iwapo Msimamizi wa Uchaguzi atakwenda kinyume na Kanuni za Uchaguzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi atamtaka Waziri mwenye dhamana kuchukua hatua za kinidhamu. Suala la kuwawajibisha wasimamizi wa uchaguzi linapaswa kuachwa mikononi mwa NEC pekee. Waziri ambaye ni kada wa CCM hawezi kuchukua hatua stahiki dhidi ya wasimamizi wa uchaguzi.
C: Wito Wetu
Kutokana na tuliyoyaeleza, wito wetu kwa NEC ni kama ifuatavyo;
i). NEC ishirikishe wadau vya kutosha kabla ya kufanya marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi. Ni muhimu kwa NEC kufanya kikao cha wadau na kujadiliana juu ya mabadiliko ya Kanuni kabla ya kufanya mabadiliko hayo. Haitoshi kuendelea kufanya mabadiliko ya Kanuni kwa kuegemea maoni ya vyama yaliyowasilishwa kimaandishi. Ni lazima vyama vione rasimu ya mwisho na kutoa maoni yao kwa kikao rasmi kabla haijawa Kanuni.
ii). NEC iiepushe nchi na machafuko yasiyo ya lazima kwa kuhakikisha inaondosha vifungu ambavyo vitahatarisha amani ya nchi. Eneo nyeti ni la mawakala kupewa nakala za viapo na nakala za matokeo. Kinyume na hapo, NEC ijue kwamba inawasha moto kwenye petroli na italipa gharama za matokeo yatakayotokea.
Ado Shaibu,
Katibu Mkuu
ACT Wazalendo.
Chama cha ACT Wazalendo kinasikitishwa na kupinga vikali mwenendo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuendesha mchakato wa mabadiliko ya Kanuni mbalimbali za Uchaguzi bila kuwashirikisha vya kutosha wadau wa uchaguzi hasa vyama vya siasa. Hadi sasa, Tume imekwisharekebisha Maadili ya Uchaguzi na sasa kwa maelezo ya Mwenyekiti wa Tume Jaji Semistocles Kaijage, ipo mbioni kukamilisha marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi za Madiwani, Wabunge na Urais.
A. Maadili ya Uchaguzi
Tarehe 27 Mei 2020, NEC iliitisha kikao cha wadau kwa ajili ya mjadala wa Maadili ya Uchaguzi. Cha kushangaza, NEC ilipanga ratiba ya kujadiliana, kufanya marekebisho na vyama kusaini maadili yaliyopitishwa ndani ya masaa machache (saa mbili hadi saa nane mchana). Licha ya maboresho machache kufanyika, NEC ilivilazimisha vyama kusaini siku hiyohiyo bila kuwasilisha kwanza toleo la mwisho la Maadili ya Uchaguzi lililojumuisha marekebisho husika.
Chama cha ACT Wazalendo ambacho mimi nilikiwakilisha kiligomea kusaini na kuomba haki ya kusaini baada ya kuona toleo la mwisho la Maadili ya Uchaguzi lenye maboresho yaliyotokana na maoni ya wadau. Jawabu la NEC kuwa Chama ambacho hakitasaini Maadili ya Uchaguzi siku hiyo hakitashiriki kampeni, lilitulazimisha kusaini sambamba na vyama vingine vilivyosaini siku hiyo.
B. Kanuni za Uchaguzi
Kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa mjadala wa Maadili ya Uchaguzi, Mwenyekiti wa NEC Ndugu Jaji Kaijage aligusia kuwa mchakato wa kukusanya maoni kwa ajili ya marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi (Madiwani, Wabunge na Urais) umefanyika na NEC ipo mbioni kuzikamilisha. NEC inakusudia kufanya hivi bila kuwepo kwa kikao cha wadau kujadili rasimu ya mwisho ya Kanuni husika. Swali la kujiuliza ni kwa nini NEC inakwepa majadiliano na wadau? Ina jambo gani inalolificha? Ina njama gani kwenye kanuni za mwaka huu?
Rasimu za Kanuni ambazo zimewasilishwa kwetu zina mapungufu mengi. Licha ya kwamba tumeiandikia NEC kutoa maoni yetu, ni dhahiri NEC inataka kuyapuuza ndio maana inakwepa kikao cha wadau. Baadhi ya mapungufu kwenye rasimu hizo yanahatarisha amani na yanaweza kuitia nchi kwenye machafuko iwapo yataachwa kama yalivyo.
Baadhi ya mapungufu hayo ni;
i). Mawakala kunyimwa hati za viapo
Rasimu ya Kanuni zote mbili, ya Uchaguzi wa Madiwani na ya Uchaguzi wa Wabunge na Rais hazina sharti kwa wasimamizi wa uchaguzi kuwapa hati za viapo mawakala wa vyama vya siasa. Kanuni zote zimeweka utaratibu wa Wasimamizi wa Uchaguzi kutuma orodha na utambulisho wa mawakala kwa wasimamizi wa vituo. Kwa uzoefu, utaratibu huu utatumika kuwahujumu mawakala wengi wa vyama vya upinzani. Wasimamizi wa Uchaguzi wasio waadilifu watatumika kutowasilisha majina ya mawakala wa vyama vya upinzani.
ii). Mawakala kutopewa nakala za matokeo
Rasimu za Kanuni za Uchaguzi hazijaweka sharti kwa mawakala wa vyama vya siasa kupewa nakala za matokeo. Kanuni hizo zinasema nakala za matokeo zitatolewa iwapo kutakuwa na nakala za kutosha! (Kanuni ya 56(2) ya Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani na kifungu cha 63(2) cha Kanuni za Uchaguzi wa Wabunge na Rais). Swali la kujiuliza ni kuwa NEC haikujiandaa kwa uchaguzi? Haina hata fedha za kuzalisha nakala za kutosha na kuepusha mizozo isiyo ya lazima?
iii). Waangalizi wa Uchaguzi Kuzibwa Mdomo
Rasimu za Kanuni za Uchaguzi zinatumia lugha ya hiyari kwa NEC kuwaalika waangalizi wa kimataifa. Kanuni hizo pia zinakataza waangalizi wa kimataifa na wa ndani kuripoti kwa vyombo vya habari mapungufu ya uchaguzi watakayoyaona wakati uchaguzi ukiendelea (Kifungu cha 20(2)(j) cha Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani) na Kanuni za Wabunge na Rais.
Kuwawekea masharti waangalizi wa uchaguzi kuripoti baada ya uchaguzi kukamilika ni sawa na kuwaziba mdomo.
iv). Mfumo mbovu wa kuwajibisha Wasimamizi wa Uchaguzi
Rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa Madiwani (Kanuni ya 66(1) na kifungu cha 74(1) cha Kanuni za Uchaguzi wa Wabunge na Rais) zinatamka kuwa iwapo Msimamizi wa Uchaguzi atakwenda kinyume na Kanuni za Uchaguzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi atamtaka Waziri mwenye dhamana kuchukua hatua za kinidhamu. Suala la kuwawajibisha wasimamizi wa uchaguzi linapaswa kuachwa mikononi mwa NEC pekee. Waziri ambaye ni kada wa CCM hawezi kuchukua hatua stahiki dhidi ya wasimamizi wa uchaguzi.
C: Wito Wetu
Kutokana na tuliyoyaeleza, wito wetu kwa NEC ni kama ifuatavyo;
i). NEC ishirikishe wadau vya kutosha kabla ya kufanya marekebisho ya Kanuni za Uchaguzi. Ni muhimu kwa NEC kufanya kikao cha wadau na kujadiliana juu ya mabadiliko ya Kanuni kabla ya kufanya mabadiliko hayo. Haitoshi kuendelea kufanya mabadiliko ya Kanuni kwa kuegemea maoni ya vyama yaliyowasilishwa kimaandishi. Ni lazima vyama vione rasimu ya mwisho na kutoa maoni yao kwa kikao rasmi kabla haijawa Kanuni.
ii). NEC iiepushe nchi na machafuko yasiyo ya lazima kwa kuhakikisha inaondosha vifungu ambavyo vitahatarisha amani ya nchi. Eneo nyeti ni la mawakala kupewa nakala za viapo na nakala za matokeo. Kinyume na hapo, NEC ijue kwamba inawasha moto kwenye petroli na italipa gharama za matokeo yatakayotokea.
Ado Shaibu,
Katibu Mkuu
ACT Wazalendo.