Uchaguzi 2020 Tume ya taifa ya uchaguzi bado inashughulikia pingamizi & rufaa dhidi ya wagombea, Watanzania waombwa kuwa na subira

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,199
4,670
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema inaendelea kushughulikia rufani na pingamizi ziliyowekewa na wagombea wa vyama mbalimbali vya siasa.

Mkurugenzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera, alisema wanaendelea kufanya uchambuzi wa rufani na pingamizi hizo na kuwataka wananchi kuwa na subira.

“Masuala ya pingamizi na rufani yamewekwa kotekote na ndiyo tunaendelea kuyashughulikia ,haya ni mambo ya kisheria, muwe na subira,” alisema Dk. Mahera.

Hivi karibuni, baadhi ya vyama hususani vya upinzani vimewalalamikia wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo 57 na kata 600 kuwaengua wagombea wao.

Juzi NEC ilitangaza majina ya wagombea 18 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliopita bila kupingwa na wanasubiri kukabidhiwa cheti cha ushindi wa ubunge mara baada ya uchaguzi kukamilika.

b9bd1b41dade18ceaf17fbc8528c5f1e.jpg
 
Wakiweza kutujibu haya maswali kwanini wapinzani ndio wamekatwa na sio ccm ndio tutamwelelewa vinginevyo usanii juu ya nyumba ya sanaaa
 
Hivi hiyo document umeiamini? Yaani hata kama ndio kukosea, kweli mtu anaweza kujaza tarehe ya kuzaliwa ambayo hata hatujaifikia??!!
Mkuu, hata mimi nashangaa! Hivi kweli mtu anafikia mpaka hatua ya kuitaka nafasi hiyo, hajui alichoulizwa hapo? Kuna haja, waombaji wawe wanabaki na kopi.
 
Mkuu, hata mimi nashangaa! Hivi kweli mtu anafukia mpaka hatua ya kuitaka nafasi hiyo, hajui alichoulizwa hapo? Kuna haja, waombaji wawe wanabaki na kopi.
Ccm na tume wametudharau sana watanzania ndio maana wanaweza hata kubadili fomu za wagombea au kuongeza taarifa kwenye fomu, ila hata pono na usingizi wake huwa anaamka!!
 
Rufaa zinacheleweshwa na wataachiwa zimebaki siku 3 kabla ya uchaguzi.


CCM Mungu anawaona
 
Anaweza kujaza kimakosa akiwa na dhamira ya kujaza: 'tarehe ya kujaza fomu'.
Inategemeana na jinsi mtu alivyoamka siku hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza kufikiri hivyo lakini ukitazama kwenye hiyo fomu tarehe iliyojazwa hapo ni 10/09/2020, tarehe ambayo kimsingi hatujaifikia.

Sasa unajiuliza hata kama ndio kukosea mtu ukosee kwa kiwango hicho?
Tazama hapa
tapatalk_1598867031940.jpeg
 
Ccm na tume wametudharau sana watanzania ndio maana wanaweza hata kubadili fomu za wagombea au kuongeza taarifa kwenye fomu, ila hata pono na usingizi wake huwa anaamka!!
Una uhakika fomu zimebadilishwa au unabwabwaja tuuu!!?
 
Hivi hiyo document umeiamini? Yaani hata kama ndio kukosea, kweli mtu anaweza kujaza tarehe ya kuzaliwa ambayo hata hatujaifikia??!!
Huoni amejaza. Na mbona juzi juzi kuna wizara ya fedha Uganda ilipima wafanyakazi korona tarehe 28.08.2020 majibu yakarudi tare 14.08.2020 kuwa wana korona
 
Wagombea wa vyama vya Upinzani wanatakiwa wawatumie wanasheria katika kujaza fomu za wagombea. Halafu wazipige fotokopi na kubaki na nakala ili wanapoharibiwa fomu zao kuzitia makosa wapeleke kopi ya fomu halisi.

Haya mambo yasipo heshimiwa yatariharibia mustakabari wa Taifa letu.

Tunajua kila kinachoendelea.

Natuma Salamu.
 
Back
Top Bottom