Tume ya Maadili ya Viongozi - The Joke and the Joker!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Tanzania tuna counterfeits nyingi sana; Yaani vitu ambavyo vinaonekana kama vitu original kumbe ni counterfeits. Tatizo ni kuwa kwa mtu wa pembeni akiviangalia vitu hivyo si rahisi kwake kugundua kuwa ni feki kwani vimefanana sana na vitu halisi.

Hali hii ya kununua na kutumia vitu feki imefika mahali hadi tumeanza kuanzisha taasisi za kubiri. Zinaonekana na sura nzuri na zina majina ambayo yanafanya ziaminike kuwa si za kugeza lakini kwa yeyote mwenye kuziangalia anaweza kuona ubiri wake.

Miongoni mwa taasisi hizo ni Tume ya Maadili ya Viongozi ambayo ina Sekretariati ya kudumu ambayo jukumu lake ni kusimamia utekelezaji (compliance) ya sheria ya Maadili ya 1995 as ammended.

Tatizo kubwa la Tume/Sekretariati hii ni kuwa wao hawawezi kuanzisha uchunguzi wa uvunjaji wa maadili kwa viongozi hadi pale mtu au chombo kingine kilete malalamiko rasmi dhidi ya kiongozi huyo. Bila malalamiko hakuna uchunguzi. Yaani, kisheria hakuna "trigger mechanism" kuwa jambo fulani likitokea basi Tume inafanya hivi au vile.

So, where is the joke and who is the joker?
 
Mzee Mwanakijiji

mkuu naona siku hizi umechafuka KUMEZIDI NINI TENA. Manake hatujakaa sawa mara issue ya RO, haijaisha sijui nini. Anyway keeps its up bana.
 
Last edited by a moderator:
tuko matatani.. Taifa letu liko matatani... na tusipoangalia waliposema Taifa limetekwa walikuwa hawatanii... tumetekwa na hatuna budi kufanya juhudi zote kujinasua.. vinginevyo na watoto na wajukuu wetu watazaliwa katika Taifa la mateka...

Tutakuwa kama wana wa Israeli Misri ambako kutokana na njaa walijikuta utumwani kwa miaka 400! Wakazoea vitunguu saumu, matikiti maji na masufuria ya nyama!
 
mimi ndio nimechoka kabisa,ndio maana hata nashindwa kuzungumza sana,hivi hizi fomu za hawa wabunge na watumishi wengine wanaojaza kila mwaka ni nani mwenye uwezo wa kuziona au ni utaratibu gani watu wanaweza kuziona na kujua kilichomo.
 
So, where is the joke and who is the joker?
Kaka, these people could be jokers!
Lakini kama ni issue ya Chenge na mifweza yake naomba kuuliza kitu maana kuuliza ndo kujifunza; Je, viongozi wanapotaja mali wanazomiliki hutaja pia na cash waliyonayo? Sheria zinasemaje?

Tusijekuwa tunawalaumu bure!
 
Nataka kuamini kuwa Vyombo kama Tume ya Maadili ya Viongozi vilikuwa na maana wakati wa Mwl (awamu ya kwanza) na sio kipindi hiki. Tusinge sikia utajiri usio rasmi wa viongozi wetu wanaanikwa na taasisi za kimataifa kama issue ya Chenge, wabunge/vyombo vya habari kama ilivyokuwa issue ya EL kama chombo hiki kingekuwa active! Sana sana kinaweza kutumiwa na wakubwa kuwafanyizia wanasiasa wenzao kama ambavyo wakati mwingine wanavyotumia TRA, POLISI, TAKUKURU, nk.

mkuu naona siku hizi umechafuka KUMEZIDI NINI TENA.
manake hatujakaa sawa mara issue ya RO,haijaisha sijui nini.

Sina uhakika kama nimekuelewa hapa, Engineer Mohamed. MKJJ unafanyakazi nzuri, Pongezi!
 
Kaka, these people could be jokers!
Lakini kama ni issue ya Chenge na mifweza yake naomba kuuliza kitu maana kuuliza ndo kujifunza; Je, viongozi wanapotaja mali wanazomiliki hutaja pia na cash waliyonayo? Sheria zinasemaje?

Tusijekuwa tunawalaumu bure!

ndio wanapotakiwa kutaja mali (assets) inajumuisha na fedha taslimu za kwao, na za wale walio karibu nao! Huwezi kuona orodha ya mali hiyo hadi uandike barua kuomba na ueleze kwanini unataka kuona.
 
that u mean to tell me wanataja current asset na fixed asset? teh teh teh labda mkuu wa vijisenti alikuwa anataka kutokea hapo, lakini yeye si mwanasheria no offense but sifa moja ya mwanasheria lazima ujue ulaghai.
 
tuko matatani.. Taifa letu liko matatani... na tusipoangalia waliposema Taifa limetekwa walikuwa hawatanii... tumetekwa na hatuna budi kufanya juhudi zote kujinasua.. vinginevyo na watoto na wajukuu wetu watazaliwa katika Taifa la mateka...

Tutakuwa kama wana wa Israeli Misri ambako kutokana na njaa walijikuta utumwani kwa miaka 400! Wakazoea vitunguu saumu, matikiti maji na masufuria ya nyama!


nakubaliana na wewe mkuu maneno yako.
mie mtazamo wangu nahisi kama MUUNGWANA hayupo kimya,ila tu anaacha MWIZI SIKU ZAKE 40 zitimie,so tumeshaona ya CHENGE 40 yake imetimia,kwa maana hiyo JK anamuchia tu upepo uchukue nafasi yake mwenyewe aachie ngazi.
niliwahi sikia nyeti moja kuwa ile alivyoingia JK na kuwapa nafasi za uwaziri wapambe wake inasemakana aliwambia "haya jamani nakupeni nafasi za uwaziri/n.waziri etc mtu akifanya madudu na maozaoza basi wananchi watamhukumu wenyewe"tumeona akina EL na wenzake jinsi w'nchi walivyowahukumu na kupata AJALI ZA KISIASA.

i may be wrong,lalkini naamini JK term yake ya pili anaweza kufanya wonders kubwa sana,kwa nini nasema hivyo??? naamini kwa dhati ameshawasoma watendaji wake wote,anajua nani mbabaishaji nani mchapa kazi n.k

mkuu unajua unapoingia ktk madaraka kuna mambo mengi sana unakumbana nayo,system ilokuweka n.k huwezi tu kuingia na kuanza safisha safisha n.k,ingawa wengi wanaulaumu USALAMA WA TAIFA(RO na timu yake),mie bado naamini kuwa jamaa wanafanya kazi nzuri sana ila tu unajua usimhukumu mtu mchunguze kwa kina na mapana ili ujue ile chains nzima ya walaji ili ukija kuondoa unaondoa yote na sio kipande cha nyama tu.

mkuu nyimbo mbaya habembelezewi mtoto,kwa maana hiyo sio dua zuri kuliombea taifa letu.

kumbuka maneno ya INVISIBLE "TANZANIA NI YETU SOTE"

HUO NI MTAZAMO WANGU TU.i may be wrong.
 
Kwa hiyo Mohd unasema tumuache tu amalizie ngwe hii na tutarajie utendaji kazi wa kweli katika awamu ya pili. Now that is an idea!
 
nakubaliana na wewe mkuu maneno yako.
mie mtazamo wangu nahisi kama MUUNGWANA hayupo kimya,ila tu anaacha MWIZI SIKU ZAKE 40 zitimie,so tumeshaona ya CHENGE 40 yake imetimia,kwa maana hiyo JK anamuchia tu upepo uchukue nafasi yake mwenyewe aachie ngazi.
niliwahi sikia nyeti moja kuwa ile alivyoingia JK na kuwapa nafasi za uwaziri wapambe wake inasemakana aliwambia "haya jamani nakupeni nafasi za uwaziri/n.waziri etc mtu akifanya madudu na maozaoza basi wananchi watamhukumu wenyewe"tumeona akina EL na wenzake jinsi w'nchi walivyowahukumu na kupata AJALI ZA KISIASA.

i may be wrong,lalkini naamini JK term yake ya pili anaweza kufanya wonders kubwa sana,kwa nini nasema hivyo??? naamini kwa dhati ameshawasoma watendaji wake wote,anajua nani mbabaishaji nani mchapa kazi n.k

mkuu unajua unapoingia ktk madaraka kuna mambo mengi sana unakumbana nayo,system ilokuweka n.k huwezi tu kuingia na kuanza safisha safisha n.k,ingawa wengi wanaulaumu USALAMA WA TAIFA(RO na timu yake),mie bado naamini kuwa jamaa wanafanya kazi nzuri sana ila tu unajua usimhukumu mtu mchunguze kwa kina na mapana ili ujue ile chains nzima ya walaji ili ukija kuondoa unaondoa yote na sio kipande cha nyama tu.

mkuu nyimbo mbaya habembelezewi mtoto,kwa maana hiyo sio dua zuri kuliombea taifa letu.

kumbuka maneno ya INVISIBLE "TANZANIA NI YETU SOTE"

HUO NI MTAZAMO WANGU TU.i may be wrong.

Engineer,

Kawaida marais huchakalika term ya kwanza ili kujenga jina na kuweza kuchagulika term ya pili, halafu kama kufanya madudud wanakuja kufanya term ya pili.Case in point Mkapa.

Sasa huyu mwenzetu hata term ya kwanza hajamaliza kashajionesha hamnazo, amekuwa kama deer aliye katikati ya barabara anayemulikwa na mataa ya gari linalokuja kumgonga, hajui aendelee kuvuka kwenda upande wa pili au arudi alikotoka.Matokeo yake ajali mbaya.

Frankly speaking the presidency is on autopilot sasa hivi, na vile hata yule mwizi Lowassa aliyekuwa anamsaidia kuigiza kama vile tuna uongozi ndiyo kaachia ngazi basi salama yake ni safari za nje tu.

Zip zero, at this point muungwana anajionyesha angefaa zaidi kuwa mtu wa kuhamasisha chama mkoani huko, na hata uwaziri walimpendelea sana.
 
Tatizo kubwa la Tume/Sekretariati hii ni kuwa wao hawawezi kuanzisha uchunguzi wa uvunjaji wa maadili kwa viongozi hadi pale mtu au chombo kingine kilete malalamiko rasmi dhidi ya kiongozi huyo. Bila malalamiko hakuna uchunguzi. Yaani, kisheria hakuna "trigger mechanism" kuwa jambo fulani likitokea basi Tume inafanya hivi au vile.

This is very good observation!

Naturaly speaking... Kuna kiwango cha kufanya upuuzi kwenye misha ya kila siku! What always seem as "majanga ya kiasili" ni mambo yanayoepukika kabisa.

Nature ya Mtu ni Utu!

Utu ni pamoja na maadili yake.Na hasa maadili ya Uogozi. Hakuna mtu hakuzaliwa na utu..lakakini kwenye process ya kuishi maisha ya kila siku..wengine Utu unajengeka na kuimarika..na wengine UTU unafifia na kuporomoka hata kuuvaa unyama wazi hadharani.

Hili ndilo linalotokea kwa serakali yetu! Kuna ubishai..ajotokeze Mtu huyo kuoyesha kiwago cha UTU kilichopo madarakani sasa hivi!

Kwa sababu hakuna bingwa wa kupinga nature yake na akabaki salama...Hii tume ya maadili waamke na waone mchezo wanaoucheza hapa...kwa kufanya mzaha na mambo ya msingi ya wananchi waliowachagua Viongozi wetu ni hatari kubwa.

Ni tume ya Kuwaamsha warudi kwenye ASILI yao, maadili ya utu, utu katika uongozi! Ni tume ya kuwakumbusha kila mara viongozi wapi wameukana utu ndani ya uogozi wao!Na hilo linatakiwa kufanyika wakati wote!!

Kama hilo hawalifanyi...Wanategemea nini? Kama sio janga la kitaifa?

Janga la Viogozi wote kuukana utu na kuuvaa unyama ambao unajulika kama UFISADI au jina lolote la kuwakilisha Usaliti wa utu!

Naturaly mechanisim ya ku_recover asili ya mtu itatokea na kushika hatamu...Lakini nani anaweza kuitabiri itakuja kwa sura gani?

Kwa taarifa...Mara nyingi kwa nyakati kama hizo recovery process inakuja kama JANGA ...tunaadika hapa kuonya na kuonyesha kuwa janga kama hili linaweza kuepukika...!! Ni juu yenu nyie mlio na wajibu huu Kusikiliza na kutekeleza!! vinginevyo you will have to do this in hard way!! Is that what you want?
 
tuko matatani.. Taifa letu liko matatani... na tusipoangalia waliposema Taifa limetekwa walikuwa hawatanii... tumetekwa na hatuna budi kufanya juhudi zote kujinasua.. vinginevyo na watoto na wajukuu wetu watazaliwa katika Taifa la mateka...!
Kaka you have said it all, inasumbua akili namna ambavyo Watanzania tumeingia kwenye haya mateka na jinsi tutavyojinasua!! Hawa jamaa wana pesa sijapata kuona, kwa kifupi wana uwezo wa kununua watu wengi sana kutokana na ufukara ambao wameusababisha miongoni mwetu.

Chenge anaongea kwa kiburi na dharau akijua ana backup ya nguvu kama jeshi la NATO. Tusome ishara za nyaka toka uanzishwaji wa Tangold, pesa iliyomegwa Deep Green mpaka Mazingaombwe ya IMMMA! Hao watoto wanakula kilichowekezwa. Si Masha wala Mujuni wanaoweza kuongea, maana nao wameshalishwa fadhila zao!

Tunacheza na mzuka ambao kila kukicha tunausifia ujirudi ilhali unaweka mazingira ya kinga ya kutoshtakiwa (akina Suharto wanashtakiwa sembuse BM?)!!
 
Zip zero, at this point muungwana anajionyesha angefaa zaidi kuwa mtu wa kuhamasisha chama mkoani huko, na hata uwaziri walimpendelea sana.
...mmmh, yule Mzee (Mwl.) tutamkumbuka sana. Alikuwa na maovu yake lakini pia aliweza kuchambua mambo!

Tusiwalaumu Tume... hawa watu wamepigwa umasikini, akisikia "Presidential appointee" hawezi kubali kuumwaga ilhali Watanzania tu ndumilakuwili! Jiulize, kwanini 'institution' nyingi zinasubiri mpaka zisikie maoni ya Rais ndio zinatekeleza wajibu wao
(tena wa kikatiba)? RO (agaist ufisadi), Mwema (against washukiwa), Sita (US-trip against Mwakyembe), Naiko, Brela, kwa uchache! Wote hawa wanasubiri uelekeo wa mkuu ndio wanaanza kutekeleza wajibu wao. Ni vema tutafute kiini, sidhani kama Tume ina matatizo makubwa kuliko mfumo uliopo!!
 
Kuna thread moja alinzisha Mkjj, unayohusu uteuzi wa majaji na viongozi wengine hasa sehemu za sheria, nilitaka kuibua jana lakini nikakumbuka kuwa watu walisema JK alikuwa anatimiza wajibu wake kwenye uteuzi wa watu hawa lakini i have some observation kwenye uteuzi huu.
Hivi tunafikiri kuna taasisi yeyote ambayo inaweza kuanzisha uchunguzi wa aina yeyote kwa RA, Hivi mnafikiri Chenge akishitakiwa mahakamani tunaweza kupata hukumu ya haki, Hivi unafikiri kuna mtu anaweza akasimama mahakamani kutoa ushaidi dhidi ya EL.
Hizi Taasisi ni jokes kubwa sana maana zinashughulikia watu kulingana na status yao na sio kwa haki ndo maana watu wanatoa conclusion kuwa sheria zipo kwa ajiri ya kulinda masirahi ya wakubwa.
Sijawahi kusikia PCCB wamepeleka wala rushwa wakubwa mahakamani zaidi ya wanaopokea sh. 50,000 hivi hawa wala rushwa wakubwa wana immune gani kwenye hii taasisi, zaidi zaidi wamemtoa bangusilo Mzee mahalu ili waweze kutangaza kuwa wanafanya kazi kama walivyofanya kwa mzee kiula.
Hizi taasisi ni jokes siwezi kuamini kuwa TISS hawakuwa na taharifa kuwa meremeta ilikuwa ni offshore company ambayo haikusitahili kuoperate Tanzania, siwezi kuamini kuwa TISS hawakuwa na taharifa kuwa Mzee wa Vijisenti ana vijisenti vingi offshore accounts, siwezi kuamini kuwa TISS hawajui Balali alipo, siwezi kuamini kuwa TISS hawakujua kuwa BOT inaibiwa.
Tunaweza kusema mengi ni bora kukaa kimya maana hizi taasisi zote zipo kwa ajiri yao tu na sio wananchi.
 
Je yawezekana kuwa sisi ndio Joke kwao.. wanatucheka tunavyopiga makelele... ?

Ni kweli kabisa they are laughing us tunapopiga kelele, sioni sababu ya kuwaeleza watanzania kuwa hatuwezi kuwashitaki wezi wa EPA, sio wezi tu bali pia waliforge documents kwa kuogopa pesa yao.
nikiingia akilini mwao naona wanasema "Waache waseme mwisho watatulia, mangapi yamesemwa lakini hawafutilii tena na tukigombe tunashinda kwa kishindi"
Lakini siku za mwizi ni arobaini na za mwenyewe ni moja, one day yes tutawaonyesha kuwa we are people's power
 
Back
Top Bottom