Tume ya kuhakiki vyeti vya watumishi serikalini lini/ tcu mko wapi

mbasamwoga

Member
Jul 6, 2011
70
12
Hakuna kisichowezekana bongo, huu ni usemi maarufu sana hapa mjini! Wanazuoni wengi wamekuwa wakiimba juu ya kuvurunda kwa serikali yetu na utumishi mbovu wa watendaji wetu. Chanzo kingine cha tatizo hili ni kukithiri kwa watumishi feki ambao hawana sifa na wanatumia vyeti vya kughushi. Hivyo hawamudu kazi husika na kusababisha hasara na umasikini kwa taifa. Tatizo hili ni kubwa hata kuliko lilivyo tatizo la rusha ambalo limeundiwa taasisi. Cha kushangaza kilakukicha zinaundwa tume hapa tanzania, lakini tume moja tu....... Tunaisubiri kwa hamu tume ya kuhakiki vyeti vya watumishi serikalini . ndugu wana jf amini nawaambia walioajiliwa hapa tzie wengi wana vyeti feki likipita fagio la tume kama hii ninayoipigia chapuo waliomtaani na vyeti vya ukweli watalamba dume.
Naomba sana tuwape habari za tume hii akina slaa, mbowe,zito, na akina shelukindo waipigie kelele mjengoni mpaka kieleweke. Kumbukeni hata baadhi ya wabunge walikuwa wamefoji vyeti wakagundulika labda ndio maana hawalioni hili maana hata wao ni waanga. Wengi wanajidai wamesoma nje kuuumbe ni uzushi mtupu......


Inaniuma sana kuona wasomi wa ukweli wako nje ya mfumo wa utendaji wakati wajinga wezi wakiendesha nchi kiendawazimu.


 
Mbona ilishaundwa siku nyingi na ikafanya kazi nadhani kati ya mwaka 2006 na 2009 na bado tuka survive. Hakuna haja ya kuchunguza watumishi wote, vyeti feki vipo polisi na ualimu
 
Kweli wewe polisi maana unaandika kikamavu bila kificho, kwahiyo unaona raha ziro kuongezeka kwa watoto wetu na askari vibaka kujipenyeza kwa vyeti feki we unaonasawa tu....... Hujasurvive kimbunga kinakuja kitaanza kusikika igunga hicho ulichokiona hapo juu.......
 
Kweli wewe polisi maana unaandika kikamavu bila kificho, kwahiyo unaona raha ziro kuongezeka kwa watoto wetu na askari vibaka kujipenyeza kwa vyeti feki we unaonasawa tu....... Hujasurvive kimbunga kinakuja kitaanza kusikika igunga hicho ulichokiona hapo juu.......

Mawazo yako wewe unataka kuelekeza tume ichunguze WATU kitu ambacho ni UPUUZI. Kama ni tume ichunguze MFUMO (SYSTEM) ili kuhakikisha hakuna LOOPHOLE ya wenye ZERO kujipenyeza. YOU UNDERSTAND WHAT AM SAYING?
 
nimependa majibu yako ingawa mi si miongoni wa hao wanaotafutwa...
Mbona ilishaundwa siku nyingi na ikafanya kazi nadhani kati ya mwaka 2006 na 2009 na bado tuka survive. Hakuna haja ya kuchunguza watumishi wote, vyeti feki vipo polisi na ualimu
 
Back
Top Bottom