mbasamwoga
Member
- Jul 6, 2011
- 70
- 12
Hakuna kisichowezekana bongo, huu ni usemi maarufu sana hapa mjini! Wanazuoni wengi wamekuwa wakiimba juu ya kuvurunda kwa serikali yetu na utumishi mbovu wa watendaji wetu. Chanzo kingine cha tatizo hili ni kukithiri kwa watumishi feki ambao hawana sifa na wanatumia vyeti vya kughushi. Hivyo hawamudu kazi husika na kusababisha hasara na umasikini kwa taifa. Tatizo hili ni kubwa hata kuliko lilivyo tatizo la rusha ambalo limeundiwa taasisi. Cha kushangaza kilakukicha zinaundwa tume hapa tanzania, lakini tume moja tu....... Tunaisubiri kwa hamu tume ya kuhakiki vyeti vya watumishi serikalini . ndugu wana jf amini nawaambia walioajiliwa hapa tzie wengi wana vyeti feki likipita fagio la tume kama hii ninayoipigia chapuo waliomtaani na vyeti vya ukweli watalamba dume.
Naomba sana tuwape habari za tume hii akina slaa, mbowe,zito, na akina shelukindo waipigie kelele mjengoni mpaka kieleweke. Kumbukeni hata baadhi ya wabunge walikuwa wamefoji vyeti wakagundulika labda ndio maana hawalioni hili maana hata wao ni waanga. Wengi wanajidai wamesoma nje kuuumbe ni uzushi mtupu......
Inaniuma sana kuona wasomi wa ukweli wako nje ya mfumo wa utendaji wakati wajinga wezi wakiendesha nchi kiendawazimu.
Naomba sana tuwape habari za tume hii akina slaa, mbowe,zito, na akina shelukindo waipigie kelele mjengoni mpaka kieleweke. Kumbukeni hata baadhi ya wabunge walikuwa wamefoji vyeti wakagundulika labda ndio maana hawalioni hili maana hata wao ni waanga. Wengi wanajidai wamesoma nje kuuumbe ni uzushi mtupu......
Inaniuma sana kuona wasomi wa ukweli wako nje ya mfumo wa utendaji wakati wajinga wezi wakiendesha nchi kiendawazimu.