Tume ya Katiba mbinu kuteka mjadala-Lissu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Tume ya Katiba mbinu kuteka mjadala-Lissu


Na Reuben Kagaruki

MBUNGE wa Singida Magharibi, Bw. Tindu Lissu, amesema Tume ya Maalumu ya Katiba itakayoundwa na Rais Jakaya Kikwete, ni mbinu ya miaka yote ya
kuteka mijadala hatari kwa CCM na serikali na kuielekeza palipo salama.

Katika maoni yake kwenye mtandao wa Wanabidii jana na baadaye kulithibitishia gazeti hili kuwa hayo ni maoni yake binafsi na si msimamo wa chama, Bw. Lissu amesema mara mjadala unapoanzia nje ya chama au dola ni hatari kwa watawala, hasa pale ukiachwa ujiendee wenyewe bila kuingiliwa.

"Hapa ndipo watawala wanaingia kwa 'gear' ya Tume ya Katiba. Tume hiyo inajengewa hoja yenye maneno matamu na rais, inakolezwa utamu kwa kuwekwa mtu mmoja au wawili (kwa mfano 'mwanasheria aliyebobea)," alisema Bw. Lissu na kuongeza;

"Kwa hiyo, maneno kama 'Tume yenye uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kiraia' ni chumvi tu inayopakwa kwenye mhogo mchungu ili ulike kirahisi."

Alisema wananchi wanaambiwa tuwe na subira hadi Tume ya Rais itakapomaliza kazi yake.

"Tunaaswa tuwe wavumilivu ili tule mbivu na katu tusiwe na jazba, munkari au kelele wakati mjadala unauawa pole pole kwa kupitia tume," alisema Bw. Lissu.

Alisema watu wachache wanaoendelea kupiga kelele kuwa mjadala umetekwa nyara, wanashambuliwa kuwa wanaonea wivu wale walioteuliwa kwenye Tume ya Rais, au wanaitwa walalamikaji tu wasiokuwa na lolote la kujenga au ni wakosoaji wa kila kitu kinachofanywa na mtukufu Rais hata kama kina maslahi kwa nchi.

Bw. Lissu alitoa mfano wa tume nyingi ambazo ziliwahi kuundwa, lakini ripoti zake hazijawahi kutekelezwa.
 
"Hapa ndipo watawala wanaingia kwa 'gear' ya Tume ya Katiba. Tume hiyo inajengewa hoja yenye maneno matamu na rais, inakolezwa utamu kwa kuwekwa mtu mmoja au wawili (kwa mfano 'mwanasheria aliyebobea)," alisema Bw. Lissu na kuongeza;

"Kwa hiyo, maneno kama 'Tume yenye uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kiraia' ni chumvi tu inayopakwa kwenye mhogo mchungu ili ulike kirahisi."

Alisema wananchi wanaambiwa tuwe na subira hadi Tume ya Rais itakapomaliza kazi yake.

"Tunaaswa tuwe wavumilivu ili tule mbivu na katu tusiwe na jazba, munkari au kelele wakati mjadala unauawa pole pole kwa kupitia tume," alisema Bw. Lissu.

Alisema watu wachache wanaoendelea kupiga kelele kuwa mjadala umetekwa nyara, wanashambuliwa kuwa wanaonea wivu wale walioteuliwa kwenye Tume ya Rais, au wanaitwa walalamikaji tu wasiokuwa na lolote la kujenga au ni wakosoaji wa kila kitu kinachofanywa na mtukufu Rais hata kama kina maslahi kwa nchi.

Bw. Lissu alitoa mfano wa tume nyingi ambazo ziliwahi kuundwa, lakini ripoti zake hazijawahi kutekelezwa.

Tume ya JK ya kukusanya maoni hiyo ni yake sisi tunasubiri Bunge lipitishe sheria ya kuanzisha mchakato huu rasmi na upewe meno ya kisheria............mchakato huu uwe na mkutano wakikatiba wenye wajumbe ambao wapigakura tutawachagua rasmi kutuwakilisha kwa ajili ya suala hili tu..................
 
Mie namshangaa huyu Lissu, hoja ya Katiba mpya nchi hii hakuianzisha yeye, watu wamefikia hata kutoa rasimu ya Katibu miaka 10 nyuma, jee na yeye alikuwa akiiteka hiyo kujitakia umaarufu kupitia katiba na kujaribu kuifanya ni hoja yake binafsi?

WaTanzania wachache wamesema inatakiwa katiba mpya miaka mingi iliopita, wengine ndio kwanza wameliona hilo na kuingia kwa gea ya kasi, wengine wanasema irekebishwe na wengine wamefikia kusema CCM ndio kikwazo cha katiba mpya Kikwete kayona hayo na kawasikiliza wote na kaamuwa iundwe tume ili imridhishe kila mwenye kiu kuhusu katiba, nalo hilo pia ni kosa? Ama kweli, watu wanashangaza sana.

Karata za siasa zipo nyingi sana, na ilikuwa ni vizuri huyu Lissu akaanza kwa ng'anda badala ya turufu, kwani turufu ikishachezwa ndio imekwenda hiyo, hairudi. Angoje karata zipigwe tena.

Ndio kwanza kafika jamvini, hata hajakaa sawa kupigiana na wenzake yeye anatupa jike? Kikarata unaolewa mapema. Pole Lissu, ngoja karata zipigwe upya. Na safari hii uwe makini kwa kuanza na ng'anda.
 
Mie namshangaa huyu Lissu, hoja ya Katiba mpya nchi hii hakuianzisha yeye, watu wamefikia hata kutoa rasimu ya Katibu miaka 10 nyuma, jee na yeye alikuwa akiiteka hiyo kujitakia umaarufu kupitia katiba na kujaribu kuifanya ni hoja yake binafsi?

WaTanzania wachache wamesema inatakiwa katiba mpya miaka mingi iliopita, wengine ndio kwanza wameliona hilo na kuingia kwa gea ya kasi, wengine wanasema irekebishwe na wengine wamefikia kusema CCM ndio kikwazo cha katiba mpya Kikwete kayona hayo na kawasikiliza wote na kaamuwa iundwe tume ili imridhishe kila mwenye kiu kuhusu katiba, nalo hilo pia ni kosa? Ama kweli, watu wanashangaza sana.

Karata za siasa zipo nyingi sana, na ilikuwa ni vizuri huyu Lissu akaanza kwa ng'anda badala ya turufu, kwani turufu ikishachezwa ndio imekwenda hiyo, hairudi. Angoje karata zipigwe tena.

Ndio kwanza kafika jamvini, hata hajakaa sawa kupigiana na wenzake yeye anatupa jike? Kikarata unaolewa mapema. Pole Lissu, ngoja karata zipigwe upya. Na safari hii uwe makini kwa kuanza na ng'anda.

Nadhani hujasoma alichokiandika Tundu Lisu, halafu kwa nini siku zote unakuwa mswahili swahili kwamba kila anaetoa hoja fulani against CCM/ JK basi ni wivu, kutafuta umaarufu au njaa???????. That is a trend ambayo umekuwa ukiionyesha kila siku. Man up bro!! Hizo rhetoric za kina Makamba, JK hazitatufikisha popote! If u are against hoja ya mwenzio basi toa yako na siku zote lete solution sio kutoa toa povu tu kila wakati kama mabishano ya kwenye kahawa.

Tundu Lisu

Ndugu wanabidii,

Heri ya Mwaka Mpya '11 popote mlipo. Nimefuatilia sana mjadala juu ya Katiba mpya ambao umeendelea humu ndani. Vile vile nimefuatilia kwa makini mjadala juu ya Wiki
leaks na mawasiliano ya kibalozi ya Marekani kuhusu Tanzania. Kwa vile inaelekea (niliko sijaweza kuiangalia hotuba yenyewe!) Serikali ya JK imekubali kutengenezwa kwa Katiba mpya nadhani ni muda muafaka kwangu kutoa maoni yangu juu ya msimamo huu mpya wa Serikali. Nitazungumzia expose za Wikileaks kuhusu watawala wa Tanzania na maana yake kwetu katika ujumbe nitakaoutuma baada ya huu.

Warumi wa zamani walikuwa na msemo ufuatao juu ya Wagiriki waliowatawala zama za kale: 'Nawaogopa Wagiriki hasa hasa wanapotuletea zawadi'! Wagiriki za zama hizo walikuwa hatari sana hasa hasa walipotaka waonekane kama watu wema kwa kuwapelekea wakoloni wao zawadi. Kama umesoma tamthilia ya Homer iitwayo Iliad kuhusiana na Farasi wa Troy (Trojan Horse) utafahamu ninachokisema. Napendekeza kwamba tunahitaji kuufikiria msemo huo wa Warumi wa kale katika mazingira ya nchi yetu ili kuona kama matamshi ya JK kuhusu Katiba mpya ni ya kusherehekewa au ya kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa. Mimi napendekeza tahadhari kubwa!

Mwaka '92 wakati Tume ya Nyalali juu ya mfumo wa siasa ilipowasilisha Ripoti yake kwa Rais Mwinyi wakati huo, kulikuwa na mjadala mkubwa sana juu ya umuhimu wa Katiba mpya kama sehemu ya mabadiliko ya kisiasa ili kuingia katika mfumo wa vyama vingi. Tume ya Nyalali yenyewe ilishauri hivyo, pamoja na mambo mengine mengi. CCM, na sehemu kubwa ya Watanzania waliohojiwa na Tume ya Nyalali, walikataa sio tu umuhimu wa Katiba mpya bali pia walikataa mfumo wa vyama vingi. Hata hivyo, Mwalimu Nyerere, aliyekuwa amesoma vizuri alama za nyakati hizo, aliishauri CCM kwamba ikubali tuingie katika mfumo wa vyama vingi LAKINI BILA KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA YA KIMFUMO WA UTAWALA!

Katika hilo, Mwalimu Nyerere alipendekeza Katiba ya '77 ifanyiwe marekebisho kwenye vipengele vilivyokuwa vinataja chama kimoja moja kwa moja na vile ambavyo visingekubalika katika mazingira ya vyama vingi kama vile utaratibu wa mfumo wa uchaguzi, n.k. Nguzo nyingine zote muhimu za kimfumo zilizojengwa chini ya dola ya kiimla ya chama kimoja kama vile urais wa kifalme, udhibiti wa kiimla wa wananchi na taasisi huru za wananchi, udhoofishaji wa vyombo vingine vya dola kama Bunge na Mahakama na mfumo wa serikali isiyowajibika kwa wananchi wala kwa vyombo vya uwakilishi vya dola na/au mahakama ziliachwa kama zilivyokuwa chini ya chama kimoja.

Kwa maana nyingine, mwaka '92 tulipata mfumo wa vyama vingi bila mabadiliko ya kimfumo ambayo yangefanya mfumo wa vyama vingi kuwa na maana ya kupanuka kwa demokrasia. Kwa wanaofahamu vema historia yetu ya kikatiba, mwaka '92 tulijikuta na mfumo uliofanana kimsingi na mfumo wa kikatiba tuliokabidhiwa na Waingereza mwaka '61. Yaani, tulijikuta na Katiba ya kiliberali ya vyama vingi lakini iliyoangikwa katika mfumo wa kisheria na kiutawala wa dola la kiimla la chama kimoja au wa bila vyama kama ilivyokuwa wakati wa ukoloni. Tulijikuta na Katiba bila ukatiba, kile ambacho watalaalamu wa katiba wamekiita kwa Kiingereza 'constitutions without constitutionalism'! Kama ilivyokuwa kwa Wagiriki wa kale na zawadi zao, CCM na Nyerere walituletea zawadi ya Katiba ya vyama vingi bila ukatiba wa vyama vingi.

Mabadiliko mengine yote ya kikatiba yaliyofuata baada ya mwaka '92 yamedhihirisha kwamba CCM haijawa tayari kuondokana na 'usia' huu wa Baba wa Taifa. Ndio maana, licha ya mabadiliko hayo, dhana ya kikatiba ya urais wa kifalme, udhibiti wa kiimla wa wananchi na/au taasisi zao huru na udhoofu wa vyombo vya udhibiti na/au vya uwakilishi vya dola kama Bunge na Mahakama vimendeelea chini ya mfumo wa vyama vingi kama ilivyokuwa wakati wa chama kimoja. Sijui ni wangapi wetu humu ndani wanaofahamu kwamba Rais wetu sio tu ni mkuu wa nchi na serikali (kwa maana ya 'head of state and executive') bali pia ana mkono mrefu sana katika vyombo vingine vya udhibiti na/au uwakilishi kama Bunge na Mahakama. Na hapa sina maana tu kwamba Rais ni sehemu ya Bunge kwa maana ya mfumo wetu wa utungaji wa sheria ambao hauna tofauti za kimsingi na mfumo wa Kimarekani au wa nchi nyingine za kiliberali. La hasha!

Rais wetu ana mamlaka kikatiba ya kuteua wabunge pia (hata kama ni kumi tu!) Kwa maana hiyo, ukichanganya na Wabunge wa Viti Maalumu ambao ni theluthi nzima ya Wabunge wote na wao hawachaguliwi moja kwa moja na wananchi, na ukichanganya na Wabunge wa kuteuliwa wanaowakilisha Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, dhana ya Bunge kama chombo cha uwakilishi wa wananchi na cha kuisimamia serikali imekuwa diluted kama ilivyokuwa zama za chama kimoja! (Kwa analysis zamivu zaidi juu ya dhana hii unaweza kusoma makala ya Harrison Mwakyembe na Palamagamba Kabudi - kabla hawajaanza kumtumikia kafiri ili wapate miradi yao, that's - iitwayo 'The Party and the Electoral Process' katika Kitabu kilichohaririwa na Profesa I.G. Shivji 'The State and the Working People in Tanzania' cha mwaka 1987.)

Aidha, Rais ana mamlaka kikatiba na kisheria ya kuteua Mtendaji Mkuu wa Bunge (Katibu wa Bunge, sio Spika!) na hata kuamua kiwango cha mishahara na marupurupu ya Wabunge. Wale wanaofikiria Wabunge wanajipangia mishahara na marupurupu yao hawajui wasemalo na Mungu awasaidie! Rais pia anateua majaji wote wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ya Tanzania na kwa hiyo ana mkono mrefu sana katika composition na, kwa hiyo, mwelekeo wa Mahakama kama chombo cha udhibiti wa serikali na/au kile kinachoaminiwa kuwa ni cha utoaji haki. Na kwa wasiofahamu, majaji wa mahakama zetu za juu ni watunga sheria vile vile hata kama wao wenyewe wanapenda kusema kwamba kazi yao ni ya kutafsiri sheria tu!

Nafahamu wengi watasema hata Rais wa nchi za kiliberali kama Marekani anateua majaji na kwa hiyo sisi hatuna tofauti sana na 'wenzetu' hao! Ni kweli lakini mfumo wa uteuzi wa majaji wa Marekani na nchi nyingine za kiliberali una udhibiti mkubwa sana wa Bunge na vyombo vingine huru vya wananchi kwa kutumia utaratibu wa uthibitishaji wa uteuzi huo kabla haujaanza rasmi. Kwa hiyo Jaji wa Marekani au wa Ghana au wa Nigeria na/au wa Kenya chini ya Katiba yao mpya ni lazima athibitishwe kwanza na Bunge baada ya confirmation hearings. Vivyo hivyo watendaji wakuu wote wa serikali na idara zake wakiwemo mawaziri n.k. lazima wathibitishwe na Bunge kabla ya uteuzi wao kuwa na nguvu za kisheria. Bunge lisipothibitisha basi na uteuzi unakoma pale pale. Ukiachia uteuzi wa Waziri Mkuu - ambaye mfumo wa kumthibitisha Bungeni umegeuzwa na Bunge la CCM kuwa wa kugonga mhuri na kumpitisha - Rais wetu anateua watendaji wote muhimu wa kila idara au taasisi ya serikali bila
vyombo vya uwakilishi na usimamizi kama Bunge kuwathibitisha na kwa hiyo kuhakiki busara za Rais.

Rais wetu vile vile ana mkono mrefu sana katika mfumo mzima wa uchaguzi ambao yeye mwenyewe anakuwa an interested party. Chini ya mfumo wetu wa kikatiba na kisheria, Rais anateua makamishna wote wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wake na afisa mtendaji mkuu wa Tume hiyo, yaani Mkurugenzi wa Uchaguzi. Hawa, kwa upande wao, ndio wanaomtangaza aliyewateua kuwa ameshinda uchaguzi wa Rais. Na kama inavyofahamika, wakishamtangaza aliyewateua kuwa ndiye mshindi, hakuna mtu au chombo chochote chenye mamlaka kikatiba na kisheria ya kuhoji busara za wateuliwa hawa wa Rais!

Na wala mkono wa Rais hauishii kwenye 'Tume' hii ya Uchaguzi tu. Kisheria, chaguzi za Tanzania zinasimamiwa na Wakurugenzi Watendaji wa Serikali za Mitaa na watendaji wa chini yao. Wote hawa ni wateuliwa wa Tume ya Utumishi wa Serikali za Mitaa ambayo inateuliwa na Rais na Waziri husika na kwa hiyo ultimately wanawajibika kwa mamlaka hizo za uteuzi wao. Tume ya Taifa ya Uchaguzi haina uwezo kisheria kuteua wasimamizi wa uchaguzi nje ya watumishi hawa wa TUMITAA na/au TAMISEMI. Na mara nyingi katika uchaguzi, watendaji hawa hawasikilizi maagizo ya Tume kama wanavyosikiliza maagizo ya akina Makamba na/au ya akina Pinda ambao ndio wanapaka mikate yao siagi! Na ndio maana, kwetu sisi wenye uzoefu halisi wa kiuchaguzi kama wapinzani wa CCM, adui yetu nambari moja mara nyingi ni Mkurugenzi wa Halmashauri na watendaji wa chini yake badala ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyoko Dar es Salaam!

Nirudi kwenye mada yangu. Mara nyingi ambapo CCM na watawala 'wamekubali' kilio cha wananchi katika masuala ya kisiasa, wamefanya hivyo sio kwa malengo ya kutoa haki zaidi na/au kubadili nguzo muhimu za mfumo wa utawala wao. 'Wamekubali' kelele za wananchi na/au magazeti ili kuuteka nyara mjadala na kuupeleka katika maeneo ambayo sio ya hatari kwao. Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Tume ya Nyalali mwaka '92 na ndivyo ambavyo imekuwa katika mabadiliko yaliyofuata ya Katiba tangu wakati huo.

Na ndivyo alivyofanya JK mwaka '05 na '07 kuhusiana na vugu vugu la sera za madini. Baada ya kuwatumikia 'makafiri' wa nchi za nje kwa kuwapa leseni za madini akiwa Waziri wa Madini na Nishati katika miaka ya mwanzo ya tisini na baadaye kushiriki kuwatungia sheria za madini zilizowatajirisha makafiri hao, JK aliingia madarakani mwaka '05 kwa ahadi ya kuzifanyia marekebisho sera na sheria hizo ili kuwezesha nchi yetu kupata stahili yake kutokana na utajiri wetu wa madini. Mara akaunda Tume ya Masha ('06) na baadaye Kamati ya Bomani ('07) kwa ajili hiyo. Tuliohoji na/au kupinga utaratibu huo tulizomewa na kuambiwa hatulitakii taifa letu mema na JK akasherehekewa kama anavyoanza kusherehekewa humu ndani mara baada ya hotuba yake ya leo! Lakini kama ilivyokuwa kwa Tume ya Nyalali mwaka '92, mapendekezo yote ya kimsingi Tume ya Masha na Kamati ya Bomani juu mfumo mpya wa sekta ya madini yalipuuzwa na badala yake tukaongezewa mrahaba wa madini kutoka asilimia
3 ya zamani hadi asilimia nne ya sasa!

Na tusipokuwa waangalifu katika suala hili la Katiba mpya ndivyo itakavyokuwa kwenye mjadala huu! Sasa tufanyeje? Jibu langu fupi ni kwamba tutumie uzoefu wa historia yetu ...




 
Mh. Dar Es Salaam, Sijapenda gea uliyoingia nayo. Huko ni kujisifu kusiko na sababu ya msingi. Kama wewe ulitangulia mbona mambo hayakwenda. Sasa ina maana unataka uwazibe mdomo watu wenye mawazo yao? Hata kama una hoja hapa sio mahali pa kujisifia kwa vile tunajua umri wa mtu au kuwepo kwa mtu kwenye jambo fulani sio kigezo cha umaarufu wala busara. Wape watu nafasi ya kutoa maoni yao wala huna haki ya kuwasemea wengine na kuwakebehi kwa umri wao au upya wao kwenye jambo fulani.
 
Mnyika go ahead na ile hoja Binafsi.

Ofcourse kuna kila haja na after all si tunaambiwa kwamba bunge ni muhimili mwingime wa dola? Kwa hiyo Mnyika kuendelea na hiyo hoja binafsi ni okay kabisaaaa!!!!!
 
Jamani sina hakika km katiba ya sasa wengi wetu mmebahatika kuiona,achilia mbali kuipitia kabisa...nadhani tuipitie kwanza kisha tutoe comments za kitu tunachokifaham...kuna swala la haki za binadamu na uhuru binafsi wa mtu..ambapo ni kipengele tu ktk ibara mojawapo ya katiba..kuna maswali najiuliza hapa:-
1.Je katiba hii tunayotaka ishughulikie vipi ndoa za jinsia moja?
2.Je ifike mahali mtoto ampandishe mzazi kizimbani kwa kukatazwa kufanya jambo lisilo adilifu(ambalo ni uhuru wake binafsi)?
3.Katiba ya sasa inataja eneo la Tanzania kua pamoja na visiwa vya Zanzibar,choko choko nyingi za kutaka kuwepo katiba tatu tumezisikia muda mrefu,je hii iwe kisu cha mwisho kutugawa mafungu mafungu?
4.Ukomo wa madaraka ya Rais!......

Haya na mengine mengi tu ni muhimu tukayaangalia kwanza....ndiyo maana nashauri tusome Katiba ya sasa iliyotungwa 1977 hadi April 30 2000 na marekebisho ya vifungu vyake yaliyofanyika tokea hapo hadi sasa...
 
mie namshangaa huyu lissu, hoja ya katiba mpya nchi hii hakuianzisha yeye, watu wamefikia hata kutoa rasimu ya katibu miaka 10 nyuma, jee na yeye alikuwa akiiteka hiyo kujitakia umaarufu kupitia katiba na kujaribu kuifanya ni hoja yake binafsi?

Watanzania wachache wamesema inatakiwa katiba mpya miaka mingi iliopita, wengine ndio kwanza wameliona hilo na kuingia kwa gea ya kasi, wengine wanasema irekebishwe na wengine wamefikia kusema ccm ndio kikwazo cha katiba mpya kikwete kayona hayo na kawasikiliza wote na kaamuwa iundwe tume ili imridhishe kila mwenye kiu kuhusu katiba, nalo hilo pia ni kosa? Ama kweli, watu wanashangaza sana.

Karata za siasa zipo nyingi sana, na ilikuwa ni vizuri huyu lissu akaanza kwa ng'anda badala ya turufu, kwani turufu ikishachezwa ndio imekwenda hiyo, hairudi. Angoje karata zipigwe tena.

Ndio kwanza kafika jamvini, hata hajakaa sawa kupigiana na wenzake yeye anatupa jike? Kikarata unaolewa mapema. Pole lissu, ngoja karata zipigwe upya. Na safari hii uwe makini kwa kuanza na ng'anda.


trush
 
Back
Top Bottom