Tume ya Jenerali Waitara kuzama kwa MV Nyerere anza na hili

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Sijui hadidu za rejea kwa Tume ya Jeneral mstahafu Waistara katika uchunguzi wa chanzo cha kuzama kwa MV Nyerere hadi kupelekea kupotea kwa maisha ya Watanzania 224.

Mimi kama raia napenda kumshauri Kiongozi wa Tume Jenerali Waistara aanze na kuchunguza Mapato ya Kivuko hichi kwa muda wote kilipokuwa kinafanya kazi kabla ya ajali. Tunajua uwezo wa MV. Nyerere ni abiria 101, Tani 25 za Mizigo na magari 3 tu. Kama kweli hawa Wafanyakazi wa MV.Nyerere walikuwa wanabeba idadi ya Abiria na Mizigo inayotakiwa basi Mapato yake yatakuwa constant kwa safari hizo 2 kwa siku, kwa wiki, mwezi na mwaka.

Kama walikuw awanzidisha abiria kila siku kwa ujazo wa karibu mara 2 au 3 na mizigo kadhalika tunategemea Mapato yalikuwa ni makubwa sana na Serikali ilikuwa inapata mapato mazuri lakini kwa kuvunja sheria. Hapa ndipo tunaweza kujua kama Serikali ilikuwa ikijinufaisha kwa mapato haya ya ujanja ujanja.

Iwapo Makusanyo siku zote yalikuwa wastani kwa kiwango cha abiria 101 na mizigo tani 25 kwa siku kutwa mara 2 kwa miaka yote(2004-2018) basi TEMESA,SUMATRA na WATUMISHI WOTE MAZI GA NYANZA. Na iwapo Serikali ilikuwa inakusanya mapato makubwa kupindukia kutokana na kuzidisha Mizigo na Abiria basi SERIKALI IWAJIBIKE kwa maana ya Waziri mwenye dhamana na Timu yake. Waziri wa Ujenzi Mhe. KAMWELWE aache kuwatisha watu wanaomtaka ajiuzulu kuwa atawaweka ndani!!!.

Kujiuzulu ni sehemu ya Uongozi kuonesha kuwa umewajibika kwa madudu yaliyotokea chini ya Wizara unayoisimamia ingawa wewe mwenyewe huhusiki moja kwa moja.
Kamwele anatakiwa akapate ushauri nasaha kutoka kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya 2 Mzee Alhaji Ali Hassani Mwinyi ambaye mwaka 1974 alijiuzulu kutokana na mauaji ya vikongwe yaliyofanywa na Jeshi la Polisi yeye akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani....Lakini huyuhuyu Mzee Mwinyi mwaka 1985 akaja kuwa Rais wa Awamu 2...Simple!
 
Law of Flotation states that when a body is partially or totally immersed it displaces the amount of fluid equals to its own weight ''Idadi ya abiria ilizidi sawa kwanini haikuzama iliko anza safari izame ilipofika ama karibia kutia Nanga Hata tukujenga nyingine abiria wapewe elimu hatua kwa hatua''
 
Kama hiyo tume itawaacha Ninja, Kamwel na binti wa ofisi ya Cacm salama basi hakuna haja ya kupoteza muda na fedha.
 
Ni kweli kabisa. Kwa kutupia kigezo cha mapato yaliyokuwa yanapatikana, basi tume itaweza kugundua ni nani walikuwa wanachochea kivuko kujaza kupita kiasi na hatua za kisheria zianze na hao! (kuna watu wameanza kusema kama wangeongeza trip nyingine ili kivuko kisijaze sana basi ingekuwa hasara. Hapa napata hisia kuwa safari zilipunguzwa ili watu wafaidie)
 
Bahati Mbaya Waitara ni wa kanda ya Ziwa. Hakuna kitu hapo. Jamaa wa hii kanda wanabebana sana!

Mhe. Joseph Mkundi(MB) Jimbo la Ukerewe-CHADEMA yupo kwenye Tume.
Naamini atasimama kidete kutetea hoja za Wana Ukerewe kwa kuzingatia maslahi mapana ya Wapiga Kura wake waliopoteza Maisha na walio Hai.
 
Hivi ile tume iliyoundwa baada ya kuzama kwa meli ya Mv Bukoba, haikutoa ripoti yake hadharani..? Haikusema sababu na jinsi gani tungeweza kuzuia maafa mengine ya kwenye maziwa..?

Swali la msingi sasa; Tume imeundwa kuchunguza kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere, ina maana tunavyoambiwa kivuko kilizama baada ya kuzidisha abiria na mizigo, na kisha abiria kuanza kusogea upande wa mbele na kusababisha boti kupinduka hazikuwa za kweli hizo..? Na mbona sasa kuna hatua zilishachukuliwa (japo waliochukuliwa hatua ni mbuzi wa kafara tuu), wametumia uchunguzi gani kuchukua hatua hiyo, iwapo tume waliyoiteua haijaleta majibu..?

Na jee, hao wajumbe wa hiyo tume, wanalipwa posho au wanafanya kazi kizalendo..?
 
Mhe. Joseph Mkundi(MB) Jimbo la Ukerewe-CHADEMA yupo kwenye Tume.
Naamini atasimama kidete kutetea hoja za Wana Ukerewe kwa kuzingatia maslahi mapana ya Wapiga Kura wake waliopoteza Maisha na walio Hai.
Huyo hana nguvu yoyote na inasemekana alikuwa kwenye mazungumzo na SISIEM ili kuunga mkono juhudi za asiyehudhuria misiba ya kitaifa kwa masharti ya mganga aliyetafutiwa na Bashite.
 
Hivi ile tume iliyoundwa baada ya kuzama kwa meli ya Mv Bukoba, haikutoa ripoti yake hadharani..? Haikusema sababu na jinsi gani tungeweza kuzuia maafa mengine ya kwenye maziwa..?

Swali la msingi sasa; Tume imeundwa kuchunguza kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere, ina maana tunavyoambiwa kivuko kilizama baada ya kuzidisha abiria na mizigo, na kisha abiria kuanza kusogea upande wa mbele na kusababisha boti kupinduka hazikuwa za kweli hizo..? Na mbona sasa kuna hatua zilishachukuliwa (japo waliochukuliwa hatua ni mbuzi wa kafara tuu), wametumia uchunguzi gani kuchukua hatua hiyo, iwapo tume waliyoiteua haijaleta majibu..?

Na jee, hao wajumbe wa hiyo tume, wanalipwa posho au wanafanya kazi kizalendo..?

sosoliso,

Hii nchi inaishi kwa matukio(events)...!!
Wazungu walishasema ''Intelligent/Great minds discuss ideas; average minds discuss events; small minds discuss people''. - Eleanor Roosevelt.
Tanzania tuko kwenye AVERAGE MINDS na kazi yetu ni kujadili tukio baada ya tukio. Kutokana na tatizo hili la kuwa na AKILI ZA WASTANI watawala walishageuza kuwa ni mtaji wa kisiasa kwa kuibua matukio ya kila siku ili kuhamisha akili za watu kila inapoonekana kuna issue/ideas ambazo zinaweza ku-trend na kuchafua hali ya hewa ya Utawala wao. Kwa watu wafuatiliaji wa matukio ya nchi hii kuna MATUKIO AMBAYO HUWA YANATENGENEZWA ILI KUHAMISHA AKILI NA MAWAZO YA WATU.....Hapo ndipo tulipo. Ooh, poor Tanzanians!!!
 
Law of Flotation states that when a body is partially or totally immersed it displaces the amount of fluid equals to its own weight ''Idadi ya abiria ilizidi sawa kwanini haikuzama iliko anza safari izame ilipofika ama karibia kutia Nanga Hata tukujenga nyingine abiria wapewe elimu hatua kwa hatua''

Benny Haraba,
Makes me to remember my O-Level Physics about Law of Floatation and Archimedes Principles.
Yawezekana hata haya majitu ya CCM yanayosimamia Meli, Boat na Feri zetu hawajawahi kusikia kitu kama KANUNI ZA KITU KUELEA. Nakumbuka swali moja lilikuwa linanifurahisha sana kwamba: ELEZA KWANINI SHILINGI INAZAMA MAJINI ILHALI MELI CHOMBO KIKUBWA KULIKO SHILINGI HAKIZAMI?
Nina hakika hili swali hata huyu Captain wa MV Nyerere na Mkurugenzi wa SUMATRA hawawezi kulijibu,,,,nina chelea hata huyu Waziri Kamwelwe anayetishia kuwaweka watu ndani wanaomwambia ajiuzulu......hawezi kujibu swali hili...!!

''.....TATIZO NI NCHI HII TUMERUHUSU AKILI NDOGO KUONGOZA AKILI KUBWA...'' Mhe. Peter Msigwa-MB Iringa Mjini(CHADEMA).
 
Tume ya uchunguzi kazi yake ni nini hasa ,kwamba kivuko kilikuwa na idadi sawa na inayohitajika zikatoka idadi ya uongo au ? Swali la kijana wangu kaniuliza jana
 
Tume ya uchunguzi kazi yake ni nini hasa ,kwamba kivuko kilikuwa na idadi sawa na inayohitajika zikatoka idadi ya uongo au ? Swali la kijana wangu kaniuliza jana

Ukweli ni kwamba hii Tume haina tija zaidi ya kuongeza gharama na ulaji wa Fedha za walipa Kodi.
Kama uwezo wa kivuko ni kubeba watu 101 na maiti zilizo opolewa kwenye maji ni 224 jumlisha 41 waliookolewa wakiwa hai jumla inakuwa 265....Huu ni ushahidi tosha kabisa kuwa MV Nyerere ilizidisha uwezo wake karibia mara 2 na nusu,,,,,bado kuna magy=unia mamia kadahaa ya mahindi, kuna lorry lilikuwa na nguzo za Tanesco na magari mengine madogo zaidi ya 3...sasa unapounda Tume ifanye nini hasa kama siyo Serikali kutaka kucheza na akili za Watanzania.....???
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Ukweli ni kwamba hii Tume haina tija zaidi ya kuongeza gharama na ulaji wa Fedha za walipa Kodi.
Kama uwezo wa kivuko ni kubeba watu 101 na maiti zilizo opolewa kwenye maji ni 224 jumlisha 41 waliookolewa wakiwa hai jumla inakuwa 265....Huu ni ushahidi tosha kabisa kuwa MV Nyerere ilizidisha uwezo wake karibia mara 2 na nusu,,,,,bado kuna magy=unia mamia kadahaa ya mahindi, kuna lorry lilikuwa na nguzo za Tanesco na magari mengine madogo zaidi ya 3...sasa unapounda Tume ifanye nini hasa kama siyo Serikali kutaka kucheza na akili za Watanzania.....???
wacha nimsikilize mr Ebo kwanza
 
Swali la msingi sasa; Na mbona sasa kuna hatua zilishachukuliwa (japo waliochukuliwa hatua ni mbuzi wa kafara tuu), wametumia uchunguzi gani kuchukua hatua hiyo, iwapo tume waliyoiteua haijaleta majibu.


ninavyohisi: wamechukuliwa hatua kwa kua wameshindwa kuchukua hatua, how come siku 3 zimepita toka kuzama kivuko watendaji wakuu wapo kimya yani wameshindwa ata kuchimba mkwara kwa port master WHY aliruhusu kivuko kiondoke kikiwa na abiria wengi??
 
Swali la msingi sasa; Na mbona sasa kuna hatua zilishachukuliwa (japo waliochukuliwa hatua ni mbuzi wa kafara tuu), wametumia uchunguzi gani kuchukua hatua hiyo, iwapo tume waliyoiteua haijaleta majibu.


ninavyohisi: wamechukuliwa hatua kwa kua wameshindwa kuchukua hatua, how come siku 3 zimepita toka kuzama kivuko watendaji wakuu wapo kimya yani wameshindwa ata kuchimba mkwara kwa port master WHY aliruhusu kivuko kiondoke kikiwa na abiria wengi??

huku ndio kufanya kazi kwa mazoea..jamani zama zimebadilika hizi hii ni awamu ya5 na rais ni Magufuli
 
ninavyohisi: wamechukuliwa hatua kwa kua wameshindwa kuchukua hatua, how come siku 3 zimepita toka kuzama kivuko watendaji wakuu wapo kimya yani wameshindwa ata kuchimba mkwara kwa port master WHY aliruhusu kivuko kiondoke kikiwa na abiria wengi??

huku ndio kufanya kazi kwa mazoea..jamani zama zimebadilika hizi hii ni awamu ya5 na rais ni Magufuli
Hivi muda gani umepita toka mbunge wa huko Ukerewe kulalamika kuhusu kivuko..? Alisikilizwa..? Hao waliochukuliwa hatua ndo wangeweza kununua kivuko kingine..? Walio na uwezo kimaamuzi mbona bado wapo makazini..? Hakuna tofauti naona, shida ni ile ile..
 
WAKATI ZOEZI LAQ KUWATAFUTA WAHUSIKA WALIOSABABISHA MAUWAJI YA HALAIKI MV NYERERE

SERKL IMEUNDA TUME KUCHUNGUZA CHANZO.. USHAURI TU WATU HAWA WANA MAJIBU YOOTE YA MAUWAJI HAYA

1))CAPT WA MELI
HUYU N MSHTAKIWA WA KWANZA
1A)) KURUHUSU MELI KUBEBA UZITO MKUBWA KUPITA UWEZO WAKE
1B)KURHUSU KUBEBA WATU WANAOZIDI UWEZO WA MELI HUKU AKIJUA IDADI KAMILI INAYOTAKIWA


1C))KUSABABISHIA HASARA SERIKALI KUANZIA MAPATO YA ABIRIA WALIOOLIPA IKUMBUKWE WALIKUWA ZAIDI YA 265

NA WANAOTAKIWA 110 MNS HAKA KAMCHEZO AKAKUANZA LEO.... 265-110($($@) ILIOBAKIA ZIDISHA NA NAULI MMOJA HIZO HELA ZILIKUWA ZINAINGIA MIFUKONI MWA WATU KILA SIKU NA HIO N KWENDA ZIDISHA NA KURUDI.. ZIDISHA MARA 30 KWAMWEZI

1D))KOSA LA UDANGANYIFU.. KILA MELI KABLA YA KUONDOKA KUNA DOCS WANAJAZA ZILE DOCS MNS KIASI CHA ABIRIA KILICJOPO TOFAUTI...UZITO ULIOSAINIWA N UONGO MTUPU

-2((ENGINEER)
HUYU AHOJIWE TU KWA KUONA IDADI KUBWA YA ABIRIA NA KUSHINNDWA KUMSHAURI CAPT ASIONDOE NDEGE MPAKA WAKAGUE UPYA IDADI YA ABIRIA


3))----MSIMAMIZI WA KUKATA TKT--

HUYUU ANAHUSIKA ZAIDI BAADA YA CAPT
1)KULISABABISHIA SERKL HASARA KUBWA
YA MAPATO

2))MAUWAJI YA HALAIKI
3))UDANGANYIFU MKUBWA


MANAGER WA KITUO

HUYU LAZIMA ATUELEZE MAHESABU KAMILI YA TKT ZOTEE ZILIIFZOKATWA

AELEZE NANI ALIESAINI MAPATO YALIOKUSANYWA SIKUHIOO JE N IDADI SAWA YA WALIOKUWEPO KWENYE MELI

HUYUU LAZIMA AKAE PEMBENI KUPISHAA UCHUNGUZI......

HUYUU WAKIMBANAAA ATAELEZA UPUUZ8 WOOTE WANAOFANYA KILA SIKU HAPO KWENYE KIVUKO

MWISHO SERKL IANGALIE INAFANYAJE KUONDIOA UBADHIRIFU WA TKT... IONEKANAVYO KUNA VITABU VY SERIKALI NA VYA DILI TUTAFTE SOLN YA HII KTK MELI INAYOKUJA

......ITAENDELEAA BAADA YA UCHUNGUZI
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom