Tume ya Haki za binadamu waichunguza Hospitali Mwananyamala

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Tume ya Haki za binadamu waichunguza Hospitali Mwananyamala

Na Jackson Odoyo

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, imenza kuchunguza tukio la mama mjamzito alyefariki dunia katika Hospitali ya Mwananyamala Juni Mosi, mwaka huu kwa madai ya kukosa huduma.

Kwa mujibu wa Uchunguzi wa Mwananchi na tume hiyo imeamua kufanya uchunguzi huo ili kufahamu aina ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo katika hospitali hiyo.

Taarifa zilizothibitishwa na tume hiyo kuhusu hatua hiyo, zimeeleza kuwa kazi hiyo ilianza siku chache baada ya mama huyo kufariki dunia na kwamba hivi sasa inaelekea ukingoni.

Chanzo chetu cha habari ndani ya tume hiyo kimesema kuwa maofisa wao walianza kufanya kazi hiyo mara tu walipopata taarifa za kifo cha mama huyo.

Chanzo hicho kilisema wameamua kufuatilia undani wa suala hilo, baada ya kuwepo kwa taarifa mbalimbali za vifo vya watoto na akina mama wajawazito zinazodaiwa kusababishwa na uzembe na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Alisema mbali na vifo hivyo, pia kumekuwepo na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa baadhi ya wagonjwa na ndugu zao wanaofika katika hospitali hiyo kwa lengo la kupata matibabu.

''Maafisa wetu wanaendelea na uchunguzi wa suala hilo ingawa wanakumbana na vikwazo kadhaa kutoka kwa uongozi wa hospitali hiyo, lakini kwa kiasi kubwa wameanza kufanikiwa,'' kilieleza chanzo hicho.

Katika hatua nyingine ndugu wa marehemu, wamemuandikia Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa barua ya kuomba wapewe taarifa ya maandishi kuhusu kifo cha ndugu yao na kwamba aunde tume ya kuchunguza suala hilo.

Kwa muujibu wa nakala ya barua hiyo iliyosainiwa na mjomba wa marehemu Teddy Dimoso, Yokonia Gabriel ilisema wao wanaamini kifo cha ndugu yao ilitokana na uzembe wa wauguzi wa hospitali hiyo.
 
hapa inabidi mmoja wao ajifanye mgonjwa kujua hali halisi ... la sivyo tumeumia .. tume chungu mzima zimeshaundwa kutokana na mapungufu au makosa yanayokea mahospitalini lakini .. i have never heard any action taken against anyone ... let this people be true to the suffering and not only come out with the trueth but also take serious measures against these babberic people and acts inorder to end this.

They should also encourage the use of suggestion boxes ... and have a habbit of atleast opening it once a week inorder to verify some claims if any ... guess this will also act as a displinary action against an mal treatment by doctors and nurses for fear of being exposed.

one such cases must be handled with stern measures to let is serve as a lesson to others
 
hapa inabidi mmoja wao ajifanye mgonjwa kujua hali halisi ... la sivyo tumeumia .. tume chungu mzima zimeshaundwa kutokana na mapungufu au makosa yanayokea mahospitalini lakini .. i have never heard any action taken against anyone ... let this people be true to the suffering and not only come out with the trueth but also take serious measures against these babberic people and acts inorder to end this.

They should also encourage the use of suggestion boxes ... and have a habbit of atleast opening it once a week inorder to verify some claims if any ... guess this will also act as a displinary action against an mal treatment by doctors and nurses for fear of being exposed.

one such cases must be handled with stern measures to let is serve as a lesson to others


Mimi nashangaa sana ukimya wa wizara kuficha info na kuwawekea kifua wale wauguzi na walio kuwa zamu .Hili linatisha sana.
 
hii tume nashangaa kuwa inafanyakazi katika sehemu ambazo hazina masilahi kwa mafisadi tu.
hatujawahi kusikia tume hii inafanyakazi kwa watu wa kwenye migodi ambao kila siku tunasikia kama hawajafyatuliwa risasi, tumesikia wanaingiliwa kwa nguvu. au kule si ukiukaji wa haki za binaadamu madhali anayekiuka ni mwekezaji mzungu?
 
Hii inaitwa ni Tume ya Rais na ndiyo maana iko mlangoni kwa Rais na wateule wengi wa juu ni wa Rais tena wamchunguze Rais ? Maajaby haya ya kusema Hosea aanze kuulizia habari zaidi kabla hajaambiwa fanya .Hawa ni wababaishaji wakuwa .Wamewahi kupewa kesi ya mauaji wakaleta mambo ya ajabu na hata huwezi kuamini majibu yao kwa wale walio enda kulala .Waliandika barua wana waambia waende wakabebe mafaili wawapelekee ofisini yaani mtu abebe file toka Kanda ya Ziwa .Nina nala ya barua ya Tume hii wakibisha nitaweka hapa wazi .
 
Back
Top Bottom