Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Watu wengi hawakumbuki kuwa miaka ya 60 Nyerere aliunda Tume ya Chifu Mang'enya ambayo iliundwa kuangalia mojawapo ya matatizo makubwa ya kitaifa. Kuundwa kwa tume ile kulionesha kuwa Nyerere hakuwa na hofu ya kulikabili jambo lolote na ripoti yake iliwekwa hadharani. Wazee wengi ambao wamestaafu katika utumishi na wengine ambao labda walikuwa ndio wanaingia kwenye utumishi wanaweza kuikumbuka tume hii na umuhimu wake kwa taifa.
Hata hivyo watu wengi hawajui hata uwepo wake na umuhimu wake kwani yale yale ambayo Tume ya Chifu Mang'enya iliyashughulikia yanarudia tena leo hii na Rais Kikwete na serikali yake hawana ujasiri wa kufanya kile ambacho Nyerere alikifanya wakati ule. Je, unajua nini kuhusu Tume hii? Je ungependa wanahistoria wetu walikumbushe taifa juu ya matokeo ya tume hii? Je unajua kurudishwa kwa hoja zilizoangaliwa na tume hii zitabadilisha kabisa upepo wa kisiasa ambao unaenezwa sasa hivi kama ilivyokuwa karibu miaka hamsini iliyopita.
Wanasema usipojua historia utajikuta unairudia; well, tumesahau historia yetu na sasa tunairudia wenyewe tukiamini tunafanya kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo watu wengi hawajui hata uwepo wake na umuhimu wake kwani yale yale ambayo Tume ya Chifu Mang'enya iliyashughulikia yanarudia tena leo hii na Rais Kikwete na serikali yake hawana ujasiri wa kufanya kile ambacho Nyerere alikifanya wakati ule. Je, unajua nini kuhusu Tume hii? Je ungependa wanahistoria wetu walikumbushe taifa juu ya matokeo ya tume hii? Je unajua kurudishwa kwa hoja zilizoangaliwa na tume hii zitabadilisha kabisa upepo wa kisiasa ambao unaenezwa sasa hivi kama ilivyokuwa karibu miaka hamsini iliyopita.
Wanasema usipojua historia utajikuta unairudia; well, tumesahau historia yetu na sasa tunairudia wenyewe tukiamini tunafanya kwa mara ya kwanza.